Bitabo
JF-Expert Member
- Sep 27, 2011
- 1,900
- 687
Kwenye kikao cha kujadili report ya APRM leo jijini Dar es Salaam, Prof. mmoja wa kenya amewauliza wabunge wetu ni kwa nini wanatunga sheria kwa Kiingereza wakati watekelezaji na wasimamizi wa sheria hizo hawajui Kiingereza wanajua Kiswahili. Na swali limeulizwa kwa Kiswahili lakini cha ajabu Kamati ya sheria na katiba kupitia kwa Mh. Angela Kairuki akajibu kuwa wameshaliona tatizo na sasa wameishauri wizara ya sheria na mambo ya katiba kuhakikisha wanaprint sheria kwa lugha zote mbili, Kiswahili na Kiingereza. japo alitoa jibu hilo kwa Kiingereza.\
Source: Startv News saa mbili usiku
Je, ina maana tatizo hili ndo limeonekana sasa wakati hata wabunge wenyewe Kiingereza kinawapa kazi kujieleza???
Kama Mtanzania nimeona aibu kwa swali hili kutoka kwa majirani zetu
Source: Startv News saa mbili usiku
Je, ina maana tatizo hili ndo limeonekana sasa wakati hata wabunge wenyewe Kiingereza kinawapa kazi kujieleza???
Kama Mtanzania nimeona aibu kwa swali hili kutoka kwa majirani zetu