Prof. wa Kenya awaumbua wabunge wa TANZANIA

Bitabo

JF-Expert Member
Sep 27, 2011
1,900
687
Kwenye kikao cha kujadili report ya APRM leo jijini Dar es Salaam, Prof. mmoja wa kenya amewauliza wabunge wetu ni kwa nini wanatunga sheria kwa Kiingereza wakati watekelezaji na wasimamizi wa sheria hizo hawajui Kiingereza wanajua Kiswahili. Na swali limeulizwa kwa Kiswahili lakini cha ajabu Kamati ya sheria na katiba kupitia kwa Mh. Angela Kairuki akajibu kuwa wameshaliona tatizo na sasa wameishauri wizara ya sheria na mambo ya katiba kuhakikisha wanaprint sheria kwa lugha zote mbili, Kiswahili na Kiingereza. japo alitoa jibu hilo kwa Kiingereza.\

Source: Startv News saa mbili usiku

Je, ina maana tatizo hili ndo limeonekana sasa wakati hata wabunge wenyewe Kiingereza kinawapa kazi kujieleza???
Kama Mtanzania nimeona aibu kwa swali hili kutoka kwa majirani zetu
 
..wa-Tanzania tulifanya makosa kutokutilia mkazo lugha ya kiingereza.

..sasa wenetu wanageuzwa wapagazi ktk nchi yao wenyewe.
 
Tukisubiri wabunge (na hasa wabunge wa ccm) kufanya jambo la maana hii nchi itafutika. Hakuna cha lugha mbili, lugha ya Taifa ni Kiswahili na kila mtu anafahamu hii lugha, sasa kwa nini bunge linaongelea habari ya kuchapisha miswada/sheria kwa lugha mbili? Kama Tanzania haitasimamia lugha yake yenyewe nani afanye hivyo?
 
swali zuri mi nachofurahia wakenya ni kwamba wanatuamsha sasa tukiamua kuendelea kulala then we are doomed tukiamka tutaenda nao sawa na hapo sasa ndio watatuelewa na kutusoma. tuamke tuwe watu wakusoma, kuipenda nchi yetu kiukweli, watu wenye maono, na zaidi tuargue na enough heavy points, na kubwa tujae ujasiri kwamba tukisema waziri toka atoke tena siku hiyo hiyo.
 
Tukisubiri wabunge (na hasa wabunge wa ccm) kufanya jambo la maana hii nchi itafutika. Hakuna cha lugha mbili, lugha ya Taifa ni Kiswahili na kila mtu anafahamu hii lugha, sasa kwa nini bunge linaongelea habari ya kuchapisha miswada/sheria kwa lugha mbili? Kama Tanzania haitasimamia lugha yake yenyewe nani afanye hivyo?

FJM,

..hiyo ni kwasababu watoto wa viongozi wa CCM na serikali hawajui kusoma na kuandika Kiswahili.

..Kiswahili wanachokijua wao ni cha kuombea maji tu.
 
FJM,

..hiyo ni kwasababu watoto wa viongozi wa CCM na serikali hawajui kusoma na kuandika Kiswahili.

..Kiswahili wanachokijua wao ni cha kuombea maji tu.

Na hapo ndipo wanapotumaliza hawa wakubwa. Zaidi ya nusu ya wabunge hawaelewi kiingereza. Sasa wanapitishaje miswada iliyoandikwa kwa kiingereza? Hii kwa kweli ni scandal ya karne! Yaani wachina wapitishe miswada iliyoandikwa kwa kifaransa? au hata kiingereza huku nusu wa wajumbe wa baraza lao wakiwa hawaelewi nini kimeandikwa? Haiweze tokea, lakini hapa kwetu wabunge wanasaka posho tu, wameelewa au hawajelewa miswada inasema nini kwao sio kitu!
 
..wa-tanzania tulifanya makosa kutokutilia mkazo lugha ya kiingereza.

..sasa wenetu wanageuzwa wapagazi ktk nchi yao wenyewe.

mkuu kwani kingereza ndo maisha? Nenda kenya uone pamoja na kuongea kingetreza watu wana maisha duni sana

wachina wa kariakoo mbona hawajui kingereza na wanapiga business?
 
Kwenye kikao cha kujadili report ya APRM leo jijini Dar es Salaam, Prof. mmoja wa kenya amewauliza wabunge wetu ni kwa nini wanatunga sheria kwa Kiingereza wakati watekelezaji na wasimamizi wa sheria hizo hawajui Kiingereza wanajua Kiswahili. Na swali limeulizwa kwa Kiswahili lakini cha ajabu Kamati ya sheria na katiba kupitia kwa Mh. Angela Kairuki akajibu kuwa wameshaliona tatizo na sasa wameishauri wizara ya sheria na mambo ya katiba kuhakikisha wanaprint sheria kwa lugha zote mbili, Kiswahili na Kiingereza. japo alitoa jibu hilo kwa Kiingereza.\

Source: Startv News saa mbili usiku

Je, ina maana tatizo hili ndo limeonekana sasa wakati hata wabunge wenyewe Kiingereza kinawapa kazi kujieleza???
Kama Mtanzania nimeona aibu kwa swali hili kutoka kwa majirani zetu

Hahahahaaaa! Mimi hili jambo nimeshalipigia sana kelele. Sheria ni za Watanzania - sasa kwa nini zitungwe katika lugha ya kigeni?

Kwangu haiingii akilini kabisa na ni ujinga na upumbavu wa hali ya juu. Watetezi utawasikia wanasema 'oh eti Kiswahili hakina misamiati ya kutosha' na upuuzi mwingine kama huo.

Nami huwa nawauliza kwani Kiingereza kina misamiati ya kutosha? Ni maneno mangapi ambayo Kiingereza imeazima toka lugha zingine? Kiingereza kimeazima hadi kwenye Kiswahili.

Halafu kwenye misamiati ya sheria Kiingereza hicho hicho kimeazima sana toka kwenye Kilatini sasa iweje Kiswahili kisiwe na misamiati ya kutosha?

Lugha hukuzwa na kupanuliwa na watumiaji wake. Mimi nakataa katakata hiyo dhana ya eti Kiswahili hakijitoshelezi. Kama hakijitoshelezi kwa nini tusitengeneze misamiati mipya? Au kwa nini tusiazime misamiati mingine zaidi?

Hakuna sababu yoyote ile ya msingi zaidi ya uvivu na hali ya kujiona hatuwezi.
 
Hivi Prof maji marefu (mfano) anaelewa kweli Ki English? Hapa juzi wakati wanajadili marekebisho ya sheria ya kutunga katiba mpya, hata sikumuona yeye wala Kibajaji wakichangia. lakini ukienda kwenye hansard za bunge utakuta waliunga mkono hoja kwa 100%
 
hata huku mtaani sign boards na matangazo ni kiingereza tu wakati walengwa ni asilimia 95 hawajui kiingereza. Kimsingi nchi yetu tuna tatizo la kasumba.
 
Kwenye kikao cha kujadili report ya APRM leo jijini Dar es Salaam, Prof. mmoja wa kenya amewauliza wabunge wetu ni kwa nini wanatunga sheria kwa Kiingereza wakati watekelezaji na wasimamizi wa sheria hizo hawajui Kiingereza wanajua Kiswahili. Na swali limeulizwa kwa Kiswahili lakini cha ajabu Kamati ya sheria na katiba kupitia kwa Mh. Angela Kairuki akajibu kuwa wameshaliona tatizo na sasa wameishauri wizara ya sheria na mambo ya katiba kuhakikisha wanaprint sheria kwa lugha zote mbili, Kiswahili na Kiingereza. japo alitoa jibu hilo kwa Kiingereza.\

Source: Startv News saa mbili usiku

Je, ina maana tatizo hili ndo limeonekana sasa wakati hata wabunge wenyewe Kiingereza kinawapa kazi kujieleza???
Kama Mtanzania nimeona aibu kwa swali hili kutoka kwa majirani zetu

sidhani kama ni kuumbua, mimi nimeona ni kuuliza tu
 
mkuu kwani kingereza ndo maisha? Nenda kenya uone pamoja na kuongea kingetreza watu wana maisha duni sana

wachina wa kariakoo mbona hawajui kingereza na wanapiga business?
mkuu.we jipe moyo tu kingereza ndio kiswahili cha dunia, wachina wa kariokoo mkuu ni kama wale wapiga debe wa posta , kujua kingereza kwake haimsaidii chochote
 
Hivi Prof maji marefu (mfano) anaelewa kweli Ki English? Hapa juzi wakati wanajadili marekebisho ya sheria ya kutunga katiba mpya, hata sikumuona yeye wala Kibajaji wakichangia. lakini ukienda kwenye hansard za bunge utakuta waliunga mkono hoja kwa 100%

Halafu sidhani kabisa kama wabunge wetu wana uwezo wa kujadili mijadala yao kwa Kiingereza mwanzo mwisho huko bungeni. Sidhani kabisa aisee.
 
Wapo wabunge wetu hata ulete muswada kwa kiswahili au lugha yao ya kikabila bado hawataelewa.Tunawachagua kwa ushabiki sio uwezo na gharama yake inakula kwetu.Katika EAC sisi ndio mazoba,hata kama neno hilo ni la kuuzi lakini ndio ukweli
 
Hahahahaaaa! Mimi hili jambo nimeshalipigia sana kelele. Sheria ni za Watanzania - sasa kwa nini zitungwe katika lugha ya kigeni?

Kwangu haiingii akilini kabisa na ni ujinga na upumbavu wa hali ya juu. Watetezi utawasikia wanasema 'oh eti Kiswahili hakina misamiati ya kutosha' na upuuzi mwingine kama huo.

Nami huwa nawauliza kwani Kiingereza kina misamiati ya kutosha? Ni maneno mangapi ambayo Kiingereza imeazima toka lugha zingine? Kiingereza kimeazima hadi kwenye Kiswahili.

Halafu kwenye misamiati ya sheria Kiingereza hicho hicho kimeazima sana toka kwenye Kilatini sasa iweje Kiswahili kisiwe na misamiati ya kutosha?

Lugha hukuzwa na kupanuliwa na watumiaji wake. Mimi nakataa katakata hiyo dhana ya eti Kiswahili hakijitoshelezi. Kama hakijitoshelezi kwa nini tusitengeneze misamiati mipya? Au kwa nini tusiazime misamiati mingine zaidi?

Hakuna sababu yoyote ile ya msingi zaidi ya uvivu na hali ya kujiona hatuwezi.

Eti wenyewe munasingizia komoni wesi.
Wanaacha kula kwa usawa pale kamba zao zinaishia wanataka kula anapokula jirani.
 
tahadhari jamani jamani jamani, umetuzunguka huyu msomi wa kikenya
nia yake ataingize mkenge, yaani wabongo tuzidi kukumbatia lugha ya shambani (kiswahili) ili tuzarau lungha ya biashara ya dunia nzima na ambayo nchi zisizo jua kabisa wanatuonea wivu sisi makoloni ya england, tizama nchi ngapi hujiunga na umoja wa madola na kuacha asili yao ya labda ureno mfano msumbiji, au ya ufaranza mfano rwanda? jamani kenya inataka kutufanya shamba lake, ili sisi tulime tu, na mazao yapitie kwa wanaojua lugha ya biashara yaani Kenya. professa hatari!!!
 
tahadhari jamani jamani jamani, umetuzunguka huyu msomi wa kikenya
nia yake ataingize mkenge, yaani wabongo tuzidi kukumbatia lugha ya shambani (kiswahili) ili tuzarau lungha ya biashara ya dunia nzima na ambayo nchi zisizo jua kabisa wanatuonea wivu sisi makoloni ya england, tizama nchi ngapi hujiunga na umoja wa madola na kuacha asili yao ya labda ureno mfano msumbiji, au ya ufaranza mfano rwanda? jamani kenya inataka kutufanya shamba lake, ili sisi tulime tu, na mazao yapitie kwa wanaojua lugha ya biashara yaani Kenya. professa hatari!!!

Sikubaliani na wewe kwa sababu unapozungumzia uzalendo wa wananchi unazungumzia mapenzi yao kwa lugha yao na sisi lugha yetu ni kiswahili!! Haingii akilini wakati wajumbe wanaoomba kuwa wabunge wa bunge la Afrika MashAriki wanalazimishwa kuoomba kura kwa kiingereza toka kwa wabunge wa bunge letu wengi wao hawajui lugha ya kiingereza kwa ufasaha; sio hivyo tu hawa wabunge wanapopiga kura kuwachagua wabunge wa bunge la Afrika mashariki waNAFANYA HIVYO KWA NIABA YA WATANZANIA TAKRIBANI MILLIONI 50 WENGI WAO HAWAJUI KIINGEREZA , HIVYO BASI KWAVILE WAKATI WA UCHAGUZI HUO WANANCHI KWA KUPITIA TEKNOLOJIA WATAKUWA WANAWAONA HAO WATAKAOMBA UTUMISHI NI VYEMA WAKAJIELEZA KWA LUGHA YA KISWAHILI ILI WANANCHI WAWEZE KUJUA KAMA WALE WAWAKILISHI WAO WATAPIGA KURA NA KUWACHAGUA WATU WATAKAOWAKISHA MASLAHI YAO NA SIO MASLAHI YA WATU BINAFFSI
 
mkuu kwani kingereza ndo maisha? Nenda kenya uone pamoja na kuongea kingetreza watu wana maisha duni sana

wachina wa kariakoo mbona hawajui kingereza na wanapiga business?
mkuu Chasa ebu acha kujifariji ktk msiba kwamba marehemu ajafariki!
 
Kwenye kikao cha kujadili report ya APRM leo jijini Dar es Salaam, Prof. mmoja wa kenya amewauliza wabunge wetu ni kwa nini wanatunga sheria kwa Kiingereza wakati watekelezaji na wasimamizi wa sheria hizo hawajui Kiingereza wanajua Kiswahili. Na swali limeulizwa kwa Kiswahili lakini cha ajabu Kamati ya sheria na katiba kupitia kwa Mh. Angela Kairuki akajibu kuwa wameshaliona tatizo na sasa wameishauri wizara ya sheria na mambo ya katiba kuhakikisha wanaprint sheria kwa lugha zote mbili, Kiswahili na Kiingereza. japo alitoa jibu hilo kwa Kiingereza.\

Source: Startv News saa mbili usiku

Je, ina maana tatizo hili ndo limeonekana sasa wakati hata wabunge wenyewe Kiingereza kinawapa kazi kujieleza???
Kama Mtanzania nimeona aibu kwa swali hili kutoka kwa majirani zetu

Katika mambo ambayo yamekuwa yakinishangaza ni kusikia kwamba lugha rasmi ya kisheria hapa nchini ni kiingereza, yaani ukienda mahakamani hasa mahakama kuu ni kiinglish tuuu hadi mtu unashindwa kuelewa nini maana ya sisi kama nchi kuwa na lugha yetu ya taifa- Kiswahili.

Kitu kingine cha ajabu sana katika nchi ambayo zaidi ya asilimia 80 hawajui kiingereza, na hata katika hiyo asilimia 20 wanaojua kiingereza ni wachache sana wanaokimudu bado tunaendekeza matumizi ya kiingereza. Serikalini kiingereza, bungeni kiingereza, mahakamani kiingereza, tukihudhuria makongamano/warsha/semiana kiingereza!!
 
Katika mambo ambayo yamekuwa yakinishangaza ni kusikia kwamba lugha rasmi ya kisheria hapa nchini ni kiingereza, yaani ukienda mahakamani hasa mahakama kuu ni kiinglish tuuu hadi mtu unashindwa kuelewa nini maana ya sisi kama nchi kuwa na lugha yetu ya taifa- Kiswahili.

Kitu kingine cha ajabu sana katika nchi ambayo zaidi ya asilimia 80 hawajui kiingereza, na hata katika hiyo asilimia 20 wanaojua kiingereza ni wachache sana wanaokimudu bado tunaendekeza matumizi ya kiingereza. Serikalini kiingereza, bungeni kiingereza, mahakamani kiingereza, tukihudhuria makongamano/warsha/semiana kiingereza!!

Sasa kama mtu hujui Kiingereza huko mahakama kuu utajuaje kama unatendewa haki?

Halafu basi ni afadhali hata wangekuwa wanaongea Kiingereza kizuri na kilichonyooka manake ukiwasikia...hmmmmm
 
Back
Top Bottom