Prof. Tibaijuka: Mbunge Lusinde ana elimu ya Uzamili (Masters) lakini hana cheti

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,975
Prof. Anna Tibaijuka ameyasema hayo wakati akichangia mjadala bungeni kuhusu wananchi waliokumbwa na zoezi la uhakiki wa vyeti kwa watumishi wa Umma huku akitoa mfano wa Mbunge wa Mtera (CCM) Livingston Lusinde kwamba licha ya elimu yake ya darasa la saba lakini uwezo wake ni zaidi ya mtu mwenye shahada mbili.

‘’Tukiangalia humu bungeni, Lusinde huwa anapenda kujiita darasa la saba lakini mimi ninamjua huyu ana masters (Shahada ya Uzamili) ni kwamba hana cheti tu. Sasa unaona kwamba ni perspective, Lusinde hawezi kusema ni darasa la saba, sio darasa la saba, elimu yake huyu mtu ana masters tena zaidi lakini sasa sababu ya certification, sisi tumekwama kwenye certification kwa hiyo tunashindwa kwenda mbele kama taifa. Kwa hiyo hilo naomba tuliweke kuwa ni muhimu sana’’.

Prof. Tibaijuka amesema kuna wafanyakazi wengi ambao walikuwa na uwezo mkubwa katika maeneo yao lakini wamejikuta wakifukuzwa kazi kutokana na ukosefu wa vyeti.

Amesema ni vizuri serikali ikaangalia pia uwezo wa mtu kuliko kuangalia vyeti peke yake kwa sababu kutokuwa na cheti hakumfanyi mtu kutokuwa na uwezo katika eneo lake la kazi.

Chanzo: Gazeti la Mwanachi,

Angalizo:
Kwa kiwango kikubwa ninakubaliana na hoja ya Prof. Tibaijuka kwa sababu pia kuna watu wengine kama Mbunge John Mnyika ambaye elimu yake ni kidato cha sita lakini uwezo wake ni zaidi ya mtu mwenye cheti cha Uzamili.

Ninakumbuka tuliwahi kujadili sana uwezo wa Lusinde baada ya mdau mmoja hapa Jamiiforums ( Pascal Mayalla ) kuleta mada (Thread) kuhusu uwezo wa Mbunge Lusinde kwenye Mada hii;

 
Kuna hoja gani ya maana na yenye maslahi kwa nchi imewai kuwasilishwa na Lusinde?
kwa kifupi bunge letu limejaa viazi na wavivu wa kusoma, hata miswaada inayopelekwa pale wengi wao hawasomi, enzi hizo walikua wanategea Tundu Lissu asome kisha aibue jambo ndipo wote waanze kuvutana kwa hoja za kipuuzi. Huyo Tibaijuka ni walewale wanaoishi kwa fikra za mwenyekiti. DHAIFU wakubwa hawa
 
Kuna hoja gani ya maana na yenye maslahi kwa nchi imewai kuwasilishwa na Lusinde?
kwa kifupi bunge letu limejaa viazi na wavivu wa kusoma, hata miswaada inayopelekwa pale wengi wao hawasomi, enzi hizo walikua wanategea Tundu Lissu asome kisha aibue jambo ndipo wote waanze kuvutana kwa hoja za kipuuzi. Huyo Tibaijuka ni walewale wanaoishi kwa fikra za mwenyekiti. DHAIFU wakubwa hawa
''Hoja ya maana yenye maslahi kwa nchi'' ni dhana ambayo inategemea na upeo wako.

Badhani uwezo wa mtu sio lazima upimwe kwa kuleta hoja.
 
Mkuu;
Umetumia kigezo/vigezi gani kuujua ujinga, upumbavu na taahira kwa watu wanaoingia na kutoka CCM?

Naomba unielimishe!
Nimefanya tu hesabu nyepesi kwa kuzingatia vigezo vya kawaida tu na kugundua kuwa Mh Cyril Chami alikuwa genious toka akiwa shule za awali hadi elimu za juu!! Sasa hivi amekuwa kama class 3 student wa st kayumba!! Sidhani kama Mh Gharib bilal anakumbuka hata alichosomea!! Hivi leo ukiambiwa kuwa Eti Mwigulu Nchemba ni 1st class economist utakubali? Au uambiwe kibaka Chenge ni Graduate wa Havard university si utashangaa? Kibajaji wa darasa la saba anaonekana smart kuliko Havard graduate! Si utaahira huu? Na Tibaijuka ni Proffesor!!!?
 
Back
Top Bottom