"Iwapo nia ni kuunda mkoa unaosogeza huduma jirani na wananchi ni busara mkoa huu kuundwa kwa kuweka makao makuu Biharamulo.

Hara hivyo sioni maana/mantiki ya wakazi wa wilaya za Ngara na Kakonko kuvuka wilaya ya Biharamulo wakienda Chato ambayo ni wilaya itakayokuwa pembeni mwa mkoa huu mpya.

Mkoa huu badala ya kunufaisha wakazi wake wengi, utawaumiza.

Pia sioni manufaa atakayoyapata mkazi wa Buseresere na Katoro kwa kuwa ataongeza umbali wa kwenda makao makuu ya mkoa.

Hata hivyo nashauri serikali badala ya kuwaza kuongeza mikoa, ijikite kupunguza ukubwa wa vijiji na kata.
Hili liende sambamba na kuwarahisishia utendaji wa kazi zao viongozi wa vijiji na kata kwa kuwapa usafiri, vifaa vya kazi kama kompyuta mpakato, simu zinazoweza kupata matukio [picha] vema.

Hapa Ngara kwenye kata ya Muganza, umbali kutoka Kitongoji cha Nyakafandi hadi makao makuu ya Kijiji chao cha Mukubu ni km.15.
Kutoka kitongoji hicho hadi makao makuu ya kata ni zaidi ya km.30.

Mtendaji wa kata na kijiji hawana usafiri wowote.
Huko hakuna umeme.
Wangeweza kusaidiwa kupewa umeme wa jua kwenye ofisi zao ili wachaji simu zao ambazo Kwa sehemu kubwa zinafanya kazi za ofisi.

Wananchi hatuna hitaji la mikoa na wilaya.
Tunahitaji zaidi huduma bora za vijiji na kata.

Ikumbukwe miaka michache iliyopita ukubwa wa vitongoji uliongezwa badala ya kupunguzwa.
Kuna sehemu mitaa/vitongoji vitatu viliungwa kuwa kimoja.
Mzigo uliongezeka."
Buseresere iko wilaya ya chato na Katoro iko wilaya ya Geita. Hapo umechanganya
 
Angalia hii

Chato wakaazi 365,127, Geita 1,739,530, Manyara 1,425,131, Kagera 2,458,022, Arusha 1,288,088, Kilimanjaro 1,640,087, Tabora1,717,908, Katavi 564,504. Sensa 2012
IMG-20210530-WA0063.jpg

Kisha jiulize kwa Nini tunataka kugawa Geita na sio mikoa mingine. Kigezoni kipi
 
"Katika mazishi Wazee Chato walimuomba Rais Samia mkoa wakidai ni ahadi ya mtangulizi wake.kwa hekima akasema ataangalia vigezo.Kama Mbunge Mstaafu jirani Muleba Kusini najua vigezo havipo.Wazo halitekelezeki. Wazee jirani na sisi naamini tutapewa nafasi kushauri"Anna Tibaijuka

---
Anaandika PROF. ANNA K. TIBAIJUKA

Ramani inaonyesha Chato ni sehemu ya Wilaya ya Biharamulo Mkoa wa Kagera. Kiuhalisia. Na kihistoria. Mengine ni kulazimishalazimisha tu.

Naendelea kusisitiza hakuna hoja yoyote ya kiuchumi kuunda mkoa wa Chato. La sivyo basi tuelimishwe.

Ila kama mnapenda siasa za upendeleo wa sehemu fulani ama kwa kuwa mkubwa aliwahi kuzaliwa pale au mtu apewe nafasi kwa sababu ni mtoto wa kiongozi endeleeni kuwabebesha wananchi mizigo ya kulipa kodi kusudi wateule wajichane. Period.

Kwanza ikumbukwe Mkoa wa Geita ulianzishwa kusudi Chato iwe Makao Makuu. Ikakosa vigezo. Geita mjini ikaonekana ndiyo yenye sifa za kuwa Makao Makuu ya Mkoa mpya wa Geita. Hii ilikuwa 2010. Sasa 11 years later Chato ati ina vigezo kuwa Makao Makuu ya Mkoa wake wenyewe? Are we serious with our development? Really? Na Rais wetu mpendwa SSH tunataka kweli kumtwisha zigo la kuamua jambo hili na controversy zake? Elimu haina mwisho. Mimi kama kuna vigezo naomba viorodheshwe. Labda ndiye sina taarifa. Ila so far Hoja ya kuwaletea maendeleo Kakonko, Biharamulo, Ngara na Muleba inayokatwa vipande ninazikataa. Mkoa unaweza kuleta maendeleo gani kwa Wilaya yake wakati Mkoa unategemea bajeti ya Serikali Kuu. Mkoa una mapato gani zaidi ya kutumia kodi? Lets be serious. Maendeleo yanatokana na uwekezaji na uwezeshaji kwa wananchi. Siyo watumishi wa Serikali tena baadhi bila maadili wanaweza kuishia kuwabugudhi wananchi badala ya kuwa msaada.

Njia pekee kumuenzi Hayati Magufuli ni kurekebisha mambo ambayo kama binadamu hakufanya vizuri. Mengine yote ni ubinafsi. Na kufifisha sifa zake katika historia ya nchi hii. Tumuache apumzike.

Miundombinu iliyowekwa Chato siyo kigezo kuunda mkoa hapo. Tuikamilishe na kuitafutia matumizi mbadala ya kitaifa. Mfano Airport ya Chato inaweza kufanywa Hub ya kilimo cha contract floriculture na horticulture...(kilimo mkataba cha maua na mboga) ili tuwe na ndege za mizigo kuja kubeba. Na maziwa .

Hospitali ya Kanda Chato.... naomba tutathmini kwanza maendeleo ya hospitali ya Mloganzila. State of the Art buildings only 40km away from Dar City Centre na Muhimbili. Mojawapo ya mafanikio makubwa ya Awamu ya nne. Lakini Angalia changamoto zake. Uhaba wa madaktari hadi leo. Sasa hao specialist doctors watakaokubali kuishi Chato mtawalipa fedha kiasi gani?. A hospital is not just buildings. Its manpower resources and the economy surrounding it. Katika dhana ya mipango miji na maendeleo ya makazi lazima vigezo vyote hivyo kuangaliwa. Kwa uelewa wangu Chato haina vigezo. Tusidanganyane.
Well said bi Kidude, zaidi ya hapo vigezo vya kijiografia na idadi ya watu imezidiwa zaidi ya mara 6 na Mkoa wa Morogoro. No Chato Region, Sukuma Gang sasa mtulie rasilimali zigawanywe sawa. Ova
 
Hivyo vigezo ni vipi?.Kuna mtu yeyote anavifahamu?
Rais Samia alipoombwa Mkoa wa Chato aliwajibu kwa busara kabisa kuwa serikali haitakuwa na kigugumizi kama Chato itakidhi vigezo!!! Sasa huko mkoani wanasema eti wamekidhi vigezo vya kuwa mkoa ; sawa imebakia kwa serikali kuu sasa kutafakari na kuona kama kweli hivyo vigezo vimefikiwa na kama kuna ulazima wa chato kuwa mkoa kwa mzingira ya kiuchumi tuliyonayo!! Hao wa mikoa ambayo sehemu zao zitamegwa kuletwa huko Chato wamehusishwa katika huo uamuzi? Isije ikawa kila Rais inayekuja anataka kulazimisha kijiji alikozaliwa kiwe mkoa kwa mtindo huo nchi itadumaa bila maendeleo!!!
 
Chato tayari ni mkoa wananchi kupitia madiwani wao wameshamaliza kutoa mawazo yao na wengi wameshapendekeza wilaya za mkoa wao sasa huyo Prof. alikuwa wapi wakati wa kutoa maoni? Haturudi nyuma tunasonga mbele. Tarehe 14/10/2021 wakati wa sherehe za kuzima Mwenge hapa Chato tunategemea Rais wetu mpendwa Samia atangaze rasmi kuwa Chato ni mkoa. Sasa wasiotaka wajiandae kisaikorojia wasije wakafa na stress bure.
Bado sio mkoa mtu wa mwisho kutoa au kutotoa hadhi ya mkoa ni Rais,kumbuka hilo ni wazo lililotoka kwa wanachato lakini Kuna mikoa inaathirika Kama kagera,kigoma na Geita yenyewe ambayo inaathirika kwa mipaka yake kubadilika lazima Rais pia ashauriane na wenye mipaka pia.Chato inatuleta hapa ni kwa sababu mtu alikua akipambania na ilipokosa vigezo ndio hiyo Geita.
 
Kama vigezo vipo kwa nini hili suala limekuwa mjadala mkali hadi kumuibua mama wa hela ya mboga ?

Kwa nini Chato wasiambiwe vigezo ambavyo hawajakidhi kuweza kuwa mkoa?
Ofisi ya Waziri mkuu TAMISEMI wanavyo hivyo vigezo!!! Hata kupandisha hadhi ya miji pia hufanywa kwa kutumia vigezo maalum!!
 
Kama vigezo vipo kwa nini hili suala limekuwa mjadala mkali hadi kumuibua mama wa hela ya mboga ?

Kwa nini Chato wasiambiwe vigezo ambavyo hawajakidhi kuweza kuwa mkoa?

Bila shaka watakapopeleka hayo maombi yao huko mbele watafahamishwa!
 
"Katika mazishi Wazee Chato walimuomba Rais Samia mkoa wakidai ni ahadi ya mtangulizi wake.kwa hekima akasema ataangalia vigezo.Kama Mbunge Mstaafu jirani Muleba Kusini najua vigezo havipo.Wazo halitekelezeki. Wazee jirani na sisi naamini tutapewa nafasi kushauri"Anna Tibaijuka

---
Anaandika PROF. ANNA K. TIBAIJUKA

Ramani inaonyesha Chato ni sehemu ya Wilaya ya Biharamulo Mkoa wa Kagera. Kiuhalisia. Na kihistoria. Mengine ni kulazimishalazimisha tu.

Naendelea kusisitiza hakuna hoja yoyote ya kiuchumi kuunda mkoa wa Chato. La sivyo basi tuelimishwe.

Ila kama mnapenda siasa za upendeleo wa sehemu fulani ama kwa kuwa mkubwa aliwahi kuzaliwa pale au mtu apewe nafasi kwa sababu ni mtoto wa kiongozi endeleeni kuwabebesha wananchi mizigo ya kulipa kodi kusudi wateule wajichane. Period.

Kwanza ikumbukwe Mkoa wa Geita ulianzishwa kusudi Chato iwe Makao Makuu. Ikakosa vigezo. Geita mjini ikaonekana ndiyo yenye sifa za kuwa Makao Makuu ya Mkoa mpya wa Geita. Hii ilikuwa 2010. Sasa 11 years later Chato ati ina vigezo kuwa Makao Makuu ya Mkoa wake wenyewe? Are we serious with our development? Really? Na Rais wetu mpendwa SSH tunataka kweli kumtwisha zigo la kuamua jambo hili na controversy zake? Elimu haina mwisho. Mimi kama kuna vigezo naomba viorodheshwe. Labda ndiye sina taarifa. Ila so far Hoja ya kuwaletea maendeleo Kakonko, Biharamulo, Ngara na Muleba inayokatwa vipande ninazikataa. Mkoa unaweza kuleta maendeleo gani kwa Wilaya yake wakati Mkoa unategemea bajeti ya Serikali Kuu. Mkoa una mapato gani zaidi ya kutumia kodi? Lets be serious. Maendeleo yanatokana na uwekezaji na uwezeshaji kwa wananchi. Siyo watumishi wa Serikali tena baadhi bila maadili wanaweza kuishia kuwabugudhi wananchi badala ya kuwa msaada.

Njia pekee kumuenzi Hayati Magufuli ni kurekebisha mambo ambayo kama binadamu hakufanya vizuri. Mengine yote ni ubinafsi. Na kufifisha sifa zake katika historia ya nchi hii. Tumuache apumzike.

Miundombinu iliyowekwa Chato siyo kigezo kuunda mkoa hapo. Tuikamilishe na kuitafutia matumizi mbadala ya kitaifa. Mfano Airport ya Chato inaweza kufanywa Hub ya kilimo cha contract floriculture na horticulture...(kilimo mkataba cha maua na mboga) ili tuwe na ndege za mizigo kuja kubeba. Na maziwa .

Hospitali ya Kanda Chato.... naomba tutathmini kwanza maendeleo ya hospitali ya Mloganzila. State of the Art buildings only 40km away from Dar City Centre na Muhimbili. Mojawapo ya mafanikio makubwa ya Awamu ya nne. Lakini Angalia changamoto zake. Uhaba wa madaktari hadi leo. Sasa hao specialist doctors watakaokubali kuishi Chato mtawalipa fedha kiasi gani?. A hospital is not just buildings. Its manpower resources and the economy surrounding it. Katika dhana ya mipango miji na maendeleo ya makazi lazima vigezo vyote hivyo kuangaliwa. Kwa uelewa wangu Chato haina vigezo. Tusidanganyane.
Mungu mbariki Tibaijuka
 
Sijaona popote mtu alipotaja vigezo mahususi vya kisheria, taratibu au sera katika kugawa mikoa. Labda uniambie ni posti namba ngapi.
Mkuu Yoda, mada yote hii hujaona popote palipozungumziwa "taratibu na vigezo" ambavyo hutumika (vilikuwa vikitumika) kuanzisha mikoa mipya, kweli?

Hivi mikoa imeanza lini kuanzishwa sehemu mbalimbali Tanzania tokea tupate uhuru? Huwa inafikiriwa tu na mtu mmoja na kuamuru pawepo na mkoa mpya?

Kwenye mada hiihii, ulianzia mwanzo wa mada yenyewe hadi hapa uliponi'quote', na ukakuta kuna baadhi ya mabandiko yakieleza sababu zinazochangia kuanzisha mkoa mpya?
Au unatafuta bandiko maalum linalo orodhesha vigezo vyote kwa pamoja, ndipo ukubali kwamba vimekwishazungumziwa kwenye jukwaa hili?

Sijui kama kuna "sheria" ilitokwisha tungwa kusimamia jambo hilo, lakini najua kuna "taratibu na vigezo" ambavyo hufuatwa katika kukidhi mahitaji ya mahali fulani kuundwa mkoa.

Miaka hii ya karibuni, kama ilivyoelezwa sehemu, hasa katika kuunda mikoa kama Katavi, ndipo taratibu hizo zilikiukwa, na sasa inataka kujirudia na hii Chato.
 
Mkuu umepewa hizo sifa/vigezo/taratibu/sheria zinazotumika kuyafanya maeneo mikoa?
Ukipewa unitag.
Tunaomba orodha ya sifa zinazotakiwa kwa sehemu ya Jamhuri ya Muungano Tanzania kufuzu kuitwa mkoa. Tukizipata hizo sifa itaturahisishia kujua kama Chato inakidhi vigezo kwa sasa ama la!
 
Sijaona popote mkuu, labda wewe uniambie posti mmojawapo.
Mkuu Yoda, mada yote hii hujaona popote palipozungumziwa "taratibu na vigezo" ambavyo hutumika (vilikuwa vikitumika) kuanzisha mikoa mipya, kweli?

Hivi mikoa imeanza lini kuanzishwa sehemu mbalimbali Tanzania tokea tupate uhuru? Huwa inafikiriwa tu na mtu mmoja na kuamuru pawepo na mkoa mpya?

Kwenye mada hiihii, ulianzia mwanzo wa mada yenyewe hadi hapa uliponi'quote', na ukakuta kuna baadhi ya mabandiko yakieleza sababu zinazochangia kuanzisha mkoa mpya?
Au unatafuta bandiko maalum linalo orodhesha vigezo vyote kwa pamoja, ndipo ukubali kwamba vimekwishazungumziwa kwenye jukwaa hili?

Sijui kama kuna "sheria" ilitokwisha tungwa kusimamia jambo hilo, lakini najua kuna "taratibu na vigezo" ambavyo hufuatwa katika kukidhi mahitaji ya mahali fulani kuundwa mkoa.

Miaka hii ya karibuni, kama ilivyoelezwa sehemu, hasa katika kuunda mikoa kama Katavi, ndipo taratibu hizo zilikiukwa, na sasa inataka kujirudia na hii Chato.
 
Sijaona popote mkuu, labda wewe uniambie posti mmojawapo.
Kuna kurasa 1 hadi 18 sasa hivi. Najuwa ni shida sana kupekuwa moja moja.

Basi tukubali tu kwamba huwa hakuna "taratibu na vigezo" vya aina yoyote ambavyo hutumika ili sehemu ipewe hadhi ya kuwa mkoa!
 
"Katika mazishi Wazee Chato walimuomba Rais Samia mkoa wakidai ni ahadi ya mtangulizi wake.kwa hekima akasema ataangalia vigezo.Kama Mbunge Mstaafu jirani Muleba Kusini najua vigezo havipo.Wazo halitekelezeki. Wazee jirani na sisi naamini tutapewa nafasi kushauri"Anna Tibaijuka

---
Anaandika PROF. ANNA K. TIBAIJUKA

Ramani inaonyesha Chato ni sehemu ya Wilaya ya Biharamulo Mkoa wa Kagera. Kiuhalisia. Na kihistoria. Mengine ni kulazimishalazimisha tu.

Naendelea kusisitiza hakuna hoja yoyote ya kiuchumi kuunda mkoa wa Chato. La sivyo basi tuelimishwe.

Ila kama mnapenda siasa za upendeleo wa sehemu fulani ama kwa kuwa mkubwa aliwahi kuzaliwa pale au mtu apewe nafasi kwa sababu ni mtoto wa kiongozi endeleeni kuwabebesha wananchi mizigo ya kulipa kodi kusudi wateule wajichane. Period.

Kwanza ikumbukwe Mkoa wa Geita ulianzishwa kusudi Chato iwe Makao Makuu. Ikakosa vigezo. Geita mjini ikaonekana ndiyo yenye sifa za kuwa Makao Makuu ya Mkoa mpya wa Geita. Hii ilikuwa 2010. Sasa 11 years later Chato ati ina vigezo kuwa Makao Makuu ya Mkoa wake wenyewe? Are we serious with our development? Really? Na Rais wetu mpendwa SSH tunataka kweli kumtwisha zigo la kuamua jambo hili na controversy zake? Elimu haina mwisho. Mimi kama kuna vigezo naomba viorodheshwe. Labda ndiye sina taarifa. Ila so far Hoja ya kuwaletea maendeleo Kakonko, Biharamulo, Ngara na Muleba inayokatwa vipande ninazikataa. Mkoa unaweza kuleta maendeleo gani kwa Wilaya yake wakati Mkoa unategemea bajeti ya Serikali Kuu. Mkoa una mapato gani zaidi ya kutumia kodi? Lets be serious. Maendeleo yanatokana na uwekezaji na uwezeshaji kwa wananchi. Siyo watumishi wa Serikali tena baadhi bila maadili wanaweza kuishia kuwabugudhi wananchi badala ya kuwa msaada.

Njia pekee kumuenzi Hayati Magufuli ni kurekebisha mambo ambayo kama binadamu hakufanya vizuri. Mengine yote ni ubinafsi. Na kufifisha sifa zake katika historia ya nchi hii. Tumuache apumzike.

Miundombinu iliyowekwa Chato siyo kigezo kuunda mkoa hapo. Tuikamilishe na kuitafutia matumizi mbadala ya kitaifa. Mfano Airport ya Chato inaweza kufanywa Hub ya kilimo cha contract floriculture na horticulture...(kilimo mkataba cha maua na mboga) ili tuwe na ndege za mizigo kuja kubeba. Na maziwa .

Hospitali ya Kanda Chato.... naomba tutathmini kwanza maendeleo ya hospitali ya Mloganzila. State of the Art buildings only 40km away from Dar City Centre na Muhimbili. Mojawapo ya mafanikio makubwa ya Awamu ya nne. Lakini Angalia changamoto zake. Uhaba wa madaktari hadi leo. Sasa hao specialist doctors watakaokubali kuishi Chato mtawalipa fedha kiasi gani?. A hospital is not just buildings. Its manpower resources and the economy surrounding it. Katika dhana ya mipango miji na maendeleo ya makazi lazima vigezo vyote hivyo kuangaliwa. Kwa uelewa wangu Chato haina vigezo. Tusidanganyane.
Tuongelee Takwimu za ukubwa wa Mikoa.
Tanzania ina Mikoa 26.
Mkoa mkubwa kuliko yote ni Tabora, wenye ukubwa wa kilomita za mraba, (sq km) 76,171
Wa pili ni Rukwa (75,240 sq km). Wa tatu ni Morogoro (74,139 sq km).
Mkoa wa Geita, wenye ukubwa wa kilomita za mraba 19,592 ni wa 23 kwa ukubwa Nchini mwetu, ukiipita Mikoa ya Mtwara (16,707 sq km), Kilimanjaro (13,209 sq km) na Dar es Salaam (1,393 sq km).
Mwendazake alikuwa Mkabila aliyepitiliza.
Profesa Tibaijuka kasema ukweli.
Hoja ya kuugawa Mkoa wa 23 kwa ukubwa Tanzania, kati ya Mikoa 26, NI YA UKABILA
Kwa nini asiugawe Mkoa wa Tabora, ambao ni mkubwa zaidi ya mara 3 na robo tatu ya Mkoa wa Geita?
Rais wangu Mama SSH ninaamini ataitendea haki Nchi yetu.
Kama kuna haja ya Mkoa Mpya, basi utokee Tabora
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom