MPHINGU
JF-Expert Member
- Oct 6, 2016
- 518
- 613
inawezekana kweli hicho chiwanja sio chake, na inawezekana kiwanja kinamilikiwa na mtu jina lake la ukoo ni TIBAIJUKA, na inawezekana ni ukoo mmoja na PROF.A.TIBAIJUKA au ni mtoto wake au mdogo wake au ndugu wa karibu inawezekana wavuta uzi wamekurupuka, kwa kumpakazia na kumpaka masizi PROF. ili naye aonekane mweusi, pole sana profesa kwa kukurupukiwaTaarifa. Sina plot hata moja Kigamboni. Mwenye ushahidi tofauti aulete. Viwanja vya Kisota ni mali ya ushirika wa wanawake wa nyumba. Viwanja hivyo walipewa na Waziri wa Ardhi aliyenitangulia Mhe John Chiligati. Mimi wakati huo nikiwa UNHABITAT.
Jambo moja linalonishangaza na kunisikitisha. Vijana mnaotakiwa kuwa na elimu na mori wa kujadili mambo/jambo ambalo kimsingi ni zuri. Kwa nini kabla ya kuandika msiyoyajua vizuri hamuendi kwenye sehemu husika kufanya utafiti kidogo? Chairman Mao alisema no research no right to speak. Ukienda Wizara ya Ardhi watakwambia viwanja husika vya Kisota ni vya nani. Lakini uzembe! Mtu anakaa tu kwenye kiti chake anaandika mambo ya kashfa bila hata uchunguzi wowote. Jirekebisheni. Dhambi hizo mbele ya Mwenyezi Mungu kuna siku zitawatafuna. Basi sasa umejua ukweli. Nendeni kawajulishe wananchi unaodai wanadhani viwanja ni vyangu. Si kweli. Mama T