Prof. Tibaijuka 2015 Muleba una wakati mgumu!

JERUSALEM 2006

JF-Expert Member
Apr 23, 2012
526
583
Natumai hamjambo wana_jamiiforum.

Juma lililopita nilitembelea wilaya ya Muleba mkoani Kagera katika jimbo la uchaguzi la Waziri wa nyumba na maendeleo ya makazi, Prof Anna Tibaijuka. Katika uchaguzi mkuu wa 2010 huyu mama alipita bila kupingwa, hivyo basi kuwafanya wananchi wa muleba Kaskazini kumchagua hata kama walikua hawamtaki. CHADEMA na CUF walimpa heshima ya pekee kwa kutomuwekea mpinzani kwani alikua na uhusiano mzuri na hivi vyama vya siasa na pia alikua anakubalika kwa wananchi.

Wanajamvi sikuamini macho yangu wala masikio yangu kwa yale niliyo yaona na kuyasikia huko vijijini. Wananchi wanasema liwalo na liwe kwani huyu mama amewasahau kabisa tangu apewe uwaziri. Kwa ufupi hajawahi kufanya mkutano wowote wa hadhara unao tathimini shughuli zote za maendeleo ya jimbo lake. Ameshindwa kufanikisha na kutekeleza ahadi zake na kuonekana kuwa ni mzushi.

Wana_muleba wanawaomba CHADEMA kutofanya makosa waliyoyafanya uchaguzi uliopita, na wanaombwa kumsimamisha mgombea katika jimbo hilo la uchaguzi linaloonekana kuwa wazi.
 
Wajinga ndo waliwao, Huwezi kufanya kazi yenye kuonekana ktk kundi la maharamia na mafissadi walio kubuhu, wengi tulitegemea mengi toka kwa huyu mama ccm imemumaliza amekua wa propaganda nae, Masikini Tibaijuka! Ikifika 2015 ni kumpiga Chini 2 na M4C ichue jimbo hawa ccm hawana maana
 
Wajinga ndo waliwao, Huwezi kufanya kazi yenye kuonekana ktk kundi la maharamia na mafissadi walio kubuhu, wengi tulitegemea mengi toka kwa huyu mama ccm imemumaliza amekua wa propaganda nae, Masikini Tibaijuka! Ikifika 2015 ni kumpiga Chini 2 na M4C ichue jimbo hawa ccm hawana maana

Kwani ccm ni baba ama mama yake? Kama wanamzingua kwanini asifanye uamuzi thabiti wa kwenda chama chenye mwelekeo? Chama chenye kuwatumikia wananchi? Ukiona anawang'ang'ania jua basi anaendana nao kwani njiwa wa jamii moja huruka pamoja!
 
Ndiyo maana wengine hatutaki mawaziri waendelee kuwakilisha majimbo ya uchaguzi bora wawe kama Mgimwa na naibu wake maana hawa sasa hawana jimbo, hawana wa kumpendelea labda kitu ninachokihisi kwa hawa mawaziri wasiokuwa na majimbo ni kuwa wataanza harakati za kuwa na jimbo uchaguzi ujao, wameonja pepo.
 
Hapo kwa kweli huyu mama aliingia mkondo mbaya na heshima yake kwa wananchi wake imeshuka sana, jibu hapa huwezi fanikiwa ukiwa kwenye kundi la mbigili ccm.
 
Ndiyo maana wengine hatutaki mawaziri waendelee kuwakilisha majimbo ya uchaguzi bora wawe kama Mgimwa na naibu wake maana hawa sasa hawana jimbo, hawana wa kumpendelea labda kitu ninachokihisi kwa hawa mawaziri wasiokuwa na majimbo ni kuwa wataanza harakati za kuwa na jimbo uchaguzi ujao, wameonja pepo.

nani kakudanganya mgimwa ni mbunge wa viti maalum?mgimwa ni mbunge wa jimbo la kalenga na manaibu wake ndo wakuteuliwa acha kupotosha umma.
 
Mama aliingia siasa za bongo bila kujipanga. Sasa imekula kwake! Jana alikua na kikao na wana Muleba waishio Dsm.
Kwani ccm ni baba ama mama yake? Kama wanamzingua kwanini asifanye uamuzi thabiti wa kwenda chama chenye mwelekeo? Chama chenye kuwatumikia wananchi? Ukiona anawang'ang'ania jua basi anaendana nao kwani njiwa wa jamii moja huruka pamoja!
 
Natumai hamjambo wana_jamiiforum.

Juma lililopita nilitembelea wilaya ya Muleba mkoani Kagera katika jimbo la uchaguzi la Waziri wa nyumba na maendeleo ya makazi, Prof Anna Tibaijuka. Katika uchaguzi mkuu wa 2010 huyu mama alipita bila kupingwa, hivyo basi kuwafanya wananchi wa muleba Kaskazini kumchagua hata kama walikua hawamtaki. CHADEMA na CUF walimpa heshima ya pekee kwa kutomuwekea mpinzani kwani alikua na uhusiano mzuri na hivi vyama vya siasa na pia alikua anakubalika kwa wananchi.

Wanajamvi sikuamini macho yangu wala masikio yangu kwa yale niliyo yaona na kuyasikia huko vijijini. Wananchi wanasema liwalo na liwe kwani huyu mama amewasahau kabisa tangu apewe uwaziri. Kwa ufupi hajawahi kufanya mkutano wowote wa hadhara unao tathimini shughuli zote za maendeleo ya jimbo lake. Ameshindwa kufanikisha na kutekeleza ahadi zake na kuonekana kuwa ni mzushi.

Wana_muleba wanawaomba CHADEMA kutofanya makosa waliyoyafanya uchaguzi uliopita, na wanaombwa kumsimamisha mgombea katika jimbo hilo la uchaguzi linaloonekana kuwa wazi.

Hapo kwenye red umekosea ni muleba kusini

Kusema kweli huyu mama hajafnya kitu haadi zote kazitelekeza

alitoa ahadi ya kutengeneza barabara ya muleba-nshamba-rubya-buganguzi

lakini alipokuja akakana kusema hajatoa hiyo ahadi:wink2:
 
Nimegundua kuwa ukiwa waziri usipokuwa makini unaweza sahau kwenu ili liinchi likubwa sana
Katiba mpya mawaziri wasiwe wabunge pls pls
 
Kama Ni kweli hajafanya lolote anastahili adhabu ili ajue sio muhimu na haisaidii kujiunga na propaganda mfu za ccm
 
HAYA NI MAONI YA MWANA MULEBA NILIYOKUTANA NAYO KWENYE GROUP EMAIL YA WANAKAGERA

Kwa sisi wengine tulioko kwenye makampuni binafsi muda mwingi tunakuwa tunawatumikia sana wenzetu waliokuwa na upeo zamani na kuwekeza nchi kwetu na kututumia sisi Watanzania tulio wengi katika kuwazidishia kipato chao huku tukilipa kodi serikalini ambazo nyingi mwisho wa siku zinaishia mikononi mwa wachache.

Tutoke huko, leo nimekaa chini na kusoma email moja baada ya nyingine na kwa umakini kabisa. Nimefurahi sana kukutana na michango mizuri sana yenye lengo la kututoa wanaKagera mahali tulipo na kutusogeza mbele angalua kufikia hatua hata ya kusikia harufu tu ya hili neno "keki ya taifa".

Nimefurahishwa sana na uimara wa mbunge wetu Mh. Mwijage katika kujenga hoja na muda mwingine kuweka evidences mezani ili wote tuwe sawa kimtazamo.

Suala la elimu ndilo hasa lililoniibua huku nilipo na kushawishika kutoa la moyoni. Kusema ukweli mkoa wa Kagera bado tuko nyuma na tunazidi kudidimia.
Nisijue majukumu ya mbunge kama akishateuliwa kuwa waziri uwajibikaji na uteteaji wa wananchi waliomchagua uwa unakuwaje.

Mimi ni mwananchi wa jimbo la Muleba Kusini lakini naomba niseme wazi kabisa kwamba kuna siku najiuliza kwamba labda tatizo la jimbo letu ni kuwapata wabunge ambao baadae wanabahatika kupata nafasi ya uwaziri.

Tulikuwa na mh Masilingi lakini kupitia ubunge wake na uwaziri jimbo la Muleba kusini hatukuona chochote cha maana ambacho kiligusa maisha ya mwananchi moja kwa moja. Wananchi hawakuamasishwa kufanya kazi kwa maendeleo yao wa kuhamasishwa kuchangamkia fursa za kimaendeleo. Ni kipindi hicho jimbo letu lilikuwa ni jimbo lenye watu wa MAJUNGU, watu wa kupigana vijembe majukwaani, jimbo likawa limegawanyika kati ya watawala na watawaliwa maana Mbunge alikuwa akipita kwa wananchi anasema Mtendaji yeyote wa serikali akipita majumbani kuomba pesa za uchangiaji wa shule za Kata au ujenzi wa vyumba vya madarasa, kamata huyo mtendaji na ikiwezekana piga viboko. Mwishowe jimbo likamaliza miaka kumi na tano bila chochote cha maana kufanyika hasa ukilinganisha majimbo mengine.

Sasa tumepata mwingine ambaye naye sijui niseme kwa bahati mbaya au nzuri akachaguliwa kuwa waziri.
Hamuwezi kuamini lakini hakuna jambo la maana la kimaendeleo lenye utofauti tumeweza kuliona kwa wananchi wa jimbo la Muleba Kusini kwa kipindi cha takribani miaka miwili sasa.
Pongezi zimekuwa zikipelekwa kwa Mh mbunge mfano kwa kujenga shule moja nzuri ya watoto wa kike pale Bukoba.

Jamani tukae tukijua hiyo shule ni ya Private na ni kundi chache sana linalosomea pale ukilinganisha na kundi la vijana wa FIV wanaomaliza kwenye shule za Kata.

Ni aibu kubwa sana shule ya mkiani Kimkoa na almost Kitaifa imetoka jimbo la Muleba Kusini hiyo shule inaitwa Gwanseli S/S. Kuna muda nailaumu sana Serikali na hili neno linaloitwa Siasa. Kwa mfano Muleba tulikuwa na shule kama Kishoju Sekondari ya KCU, Biirabo Sekondari ya wazazi, hizi ni shule zilizokuwa mkombozi sana wa Elimu ya watu wa Muleba na Kagera kwa ujumla. Pamoja na kwamba zilikuwa private lakini ada yake ilikuwa affordable na wazazi walihamasika kupeleka watoto wao maana shule zilikuwa zinafanya vizuri.
Tulikuwa na uwezo wa kupata vijana si chini ya ishirini mpaka thelathini kila mwaka kwenda kidato cha tano na wengi wao kupata nafasi za vyuo.
Hii siasa ya Mungai ikaamua kuingilia suala la Elimu, hizi shule zote zikaingia mikononi mwa serikali na kuanzia hapo mambo yakabadilika kabisa.
Tumejenga shule nyingi sana za Kata lakini zote zinatoa wafunzi wachache sana wa kuendelea na kidato cha tano, vyuo vya ualimu na hata kuwa na sifa za kujiunga na vyuo vya ufundi.

Ukiangalia sekta nyingine kama ya kiuchumi; Jimbo la Muleba Kusini tunatia aibu pamoja na kwamba Muleba ni kati ya Wilaya chache Tanzania zenye vyanzo vizuri na rasmi vya mapato.
Maendeleo ya jimbo hili yamebaki ni maendeleo ya mtu binafsi na familia yake huku kundi kubwa la wananchi likitaabika na kusukumizwa shimoni na hali ngumu ya kimaisha.

Wananchi waliahidiwa ahadi kibao lakini hakuna kitu tangible kilichokwisha kufanyika. Ukienda vijijini hasa vijiji vya pembezo utatokwa na machozi. Mafano kuna vijiji vya kata za Kibanga, Mubunda, Kalambi, maeneo ya Kanywangonge, Bweyenza n.k unaweza kulia machozi. Watu wanaishi maisha ya enzi za mawe za kale.
Kuna siku nilitembelea vijiji vya Magata, Karutanga, Gwanseli, Ilemera, Lulanda na Lunazi kwenye pitapita yangu nikaambiwa wakati wa kampeni mbunge aliahidi umeme ungekuwa umefika maeneo ya Lunazi kutoka kijiji cha Magata na kupitia vijiji vingine nilivyotaja baada tu ya miezi sita toka kuchaguliwa kwake. Lakini mpaka sasa si nyaya wala nguzo zinaonekana kwenye maeneo yaliahidiwa.

Ndo maana nafikia hatua nasema labda jimbo letu kupata uwaziri ni mojawapo ya kikwazo cha maendeleo. Waziri anahangaika na Job Description ya uwaziri anasahau JD aliyopewa na wananchi wake.
Mh.Jimbo la Muleba Kusini liko taabani na halina mtu wa kulisemea na bahati mbaya hata ukiangalia kwenye forum hii tuko wachache mno hatuzini watano kutoka jimbo hilo.
Wenzetu wanapigana kila kukicha kwa maendeleo ya watu wao lakini sisi wa Muleba kusini tumelala sana kama si kulala basi kuna kuogopana "KAKITANDUGAO"

Nikipata nafasi nyingine kupitia jukwaa hili nitalisemea jimbo hili maana hali yake kiuchumi,kiafya na kielimu ni MBAYA SANA.

Waitu mabaksinge.
 
Muleba kuna upinzani asilia tatizo amekosekana mpinzani halisi ambaye wananchi wanaweza kumwamini. Tangu Prince Bagenda ahamie CCM wagombea wa CCM hawakuwahi kupata mpinzani mwenye nguvu. Katika uchaguzi wa 1995 upinzani (NCCR-Mageuzi) ulishinda muleba kusikazini na kusini, Kusini wakachakachua mahakama ikatengua. Kutokana na mgogoro uliokuwepo ndani ya NCCR-Mageuzi Bagenda hakuweza kupata idhini ya chama kwa maana ya sahihi ya katibu (Marando) hivyo hakugombea na Masilingi akaweza kupita kirahisi.

Nilisikia 2010 kuna mwanasheria mmoja wa Mazingira alitaka agombee kupitia Chadema lakini kwa kuwa Prof. Anna ni dada yake na inasemekana ndiye aliyemsomesha akaamua kutotangaza nia.

Binafsi naumizwa na hali ya jimbo letu. Nakusanya nguvu sitasita kutangaza nia 2015
 
Kwani ccm ni baba ama mama yake? Kama wanamzingua kwanini asifanye uamuzi thabiti wa kwenda chama chenye mwelekeo? Chama chenye kuwatumikia wananchi? Ukiona anawang'ang'ania jua basi anaendana nao kwani njiwa wa jamii moja huruka pamoja!
Kinachoshangaza sana ni kwamba wala huwezi dhani kuwa anaganga njaa, sasa nini kimemkumba?
 
Kikwazo kikubwa ni unafiki na mazoea,hawazi kama kuna maisha nje ya CCM! Nchi nyingine mtu kama huyu ambaye hana njaa,ambaye hata watawala wakimfanyia fitina ataendelea kupata pensheni yake kubwa ya UN ungetarajia aongoze mageuzi,lakini kinyume chake anashirikiana na wala rushwa!!!
Kinachoshangaza sana ni kwamba wala huwezi dhani kuwa anaganga njaa, sasa nini kimemkumba?
 
Kikwazo kikubwa ni unafiki na mazoea,hawazi kama kuna maisha nje ya CCM! Nchi nyingine mtu kama huyu ambaye hana njaa,ambaye hata watawala wakimfanyia fitina ataendelea kupata pensheni yake kubwa ya UN ungetarajia aongoze mageuzi,lakini kinyume chake anashirikiana na wala rushwa!!!

Sasa ina maana ndiyo tukubali kuwa waTanzania ndivyo tulivyo? Hata tukisoma? hata tukiwa na kila kitu bado hatuwezi kulinda nchi yetu na kuiendeleza ni mpaka tukaite watu waje watufanyie kazi, watuibie waondoke wamevimbiwa na sisi tukibaki maskini vilevile? Nataabika sana kimawazo. Au labda anautaka Uraisi nini ndiyo anakaa kimya illi wasimteme? Maana wakina Mama nao usifanye mzaha Bwana!.
I just want to remain positive, I think she is up to something. I have made up my mind.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom