Prof Sospeter M. Muhongo - A suitable candidate for the position of DG of UNESCO

Nyani Ngabu ina maana huoni alichokiandika Kuhani
First Lady,

Hata mimi ningefurahi kama angekuwa amefungua hiyo branch ya ICSU Tanzania badala ya ugenini. (By the way, ukisema "...was the first and founding Director of ..." maana yake nini?)

Na anaweza kutokea opponent wa Kiafrika huko anaejua yanayoendelea Tanzania akam corner ajieleze:

Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi wa STAMICO kwa miaka kumi sasa, kwa hiyo madudu yoooote ya ufanisi mbovu, ufisadi lukuki, vifo vya wachimbaji, unyuma wa jamii zilizo karibu na migodi, hasara kwa Taifa ziletwazo na misamaha ya kodi, na ufukara wa wachimbaji wadogo wadodo, yooooote haya yametokea chini ya usimamizi wa bodi ya Wakurugenzi wako, au?

Utakwendaje wewe mkurugenzi wa bodi ya Wakurugenzi wa STAMICO kuchunguza vifo vya migodini wakati ajali zenyewe inawezekana zinatokea kutokana na uzembe fulani wa STAMICO?

Na hiyo tume yako ya uchunguzi iligundua nini, na nini kimebadilika?

Wakati ukiishi nje ya nchi, kwa nini hujiuzulu majukumu yako yanayohusiana na STAMICO, idara ya nyanja muhimu ya uchumi, iliyofeli kazi kwa kila aina ya vipimo?

Mkeo anaitwa Bertha, ana shahada tatu. Bertha who? Kuliko kuweka shahada za mkeo weka jina lake kamili. Unaionyesha dunia kwamba bado una mfumo dume! Na kijana wako mwenye shahada mbili huyu, info nzuri zaidi hapa ni majina ya hao yatima uwaleao, sio shahada za non-candidate family members!

La mwisho, kwa sehemu nyingine, mfano USA (na hawa ndo vinara wenye influence ya nani anakuwa nani na nini kinafanyika United Nations na matawi yake), unapo ji-introduce kama professor unajulikana kama ni mwalimu. Hiyo inakushushia executive profile yako kwa sababu unaonekana unajiuza kama mtu wa academia ambae hana executive credentials. Ondoa hiyo professor weka title ya Doctor!

BTW Kumbe kijana ni mshika pembe wengine wanakamua maziwa.....cupcake wako leo.......
 
Sina muda kusoma anayoandika bibie Ku Who.....

Na skip bandiko zake....

Safari ijayo nisomee bandiko zake kwa niaba yangu....
 
Keynote speeches nyingi huwa zinaandikwa. Unakuwa unaisoma hiyo keynote speech. Hukumbuki Sarah Palin alivyo deliver speech yake ktk convention...

Ni kweli na hasa kwa wanasiasa, isipokuwa kuna tofauti kidogo Kwenye scientific conferences/symposiums, kama academician, keynote speech anaiandika na anaitoa in a form of presentation.
 
Huyu mzee wa structural Geology!kwa kujieleza hapo ndo umefika!...any way na yeye ana mapungufu yake kama binadamu wengine!ila ana nafasi ya kushinda anayo!

Ana mapungufu kama binadamu wengine? Unacheza wewe! Kwa hiyo?

Hata the most unsophisticated voter wa Tarime huwezi kumshawishi kwa kumwambia nina mapungufu lakini nipe kura kwa maana binadamu wote wana mapungufu. Mtarime atakufukuza na mapanga!

"Ana nafasi ya kushinda," unajua wasifu wa opponents? Huyu candidate amepungukiwa na executive résume and or high profile international credence, halafu anazidi kujiharibia kwa kujinadi kama ticha!

Na kwenye kujieleza kwake labda tungeanza na pale aliposema "...the first and founding Director of..."
Maana yake nini hapo?

Halafu résume yake ni kama Curriculum Vitae ya kutafutia kazi kufundisha Geology. Anaenda kushindana na waziri mmoja wa Egypt mwenye international prominence, na kuna Mbulgaria balozi wa Ufaransa ambae kesha anza campaign tour duniani, na watakuja wengi na international profile ndefu. Ndugu yetu ange ditch hii geological talk hii akaongeza "international." I mean, kaandika "geological" up the wazoo..:

"...Vice President of the Commission of the Geological Map… Head of the Department of Geology… Honorary Professor of Geology… profile of the Geological Society… on the Precambrian Geology of Africa… in 2007 The Geological Society… Honours Degree in Geology… founded and chaired the Geological Association… and chaired the Geological… his association with geological societies… a Fellow and a Chartered Geologist of the Geological Society of London… a recognized European Geologist… Academy of Geological Sciences… of the Gondwana Institute for Geology… and a Member of the Geological… the highly acknowledged geological… Group of Experts on Geological Heritage… of the International Union of Geological… of the Geological Map… of Experts on Geological… of the Geological… dealing with the geology and mineral… Geology for Economic Development… and Belgian geologists..."
 
Woh, sure the man's 'CV' is beyond the borders. I wish him success and surely he is marketable for this very post.

Great!
 
Ni kweli na hasa kwa wanasiasa, isipokuwa kuna tofauti kidogo Kwenye scientific conferences/symposiums, kama academician, keynote speech anaiandika na anaitoa in a form of presentation.

Mimi sizungumzii prepared remarks/ speeches. Mimi nazungumzia off the top of the dome....hapo ndo itadhihirisha kama huyo mtu amekariri tu au kweli mavituz yanapanda....

Kama hunielewi tafuta speech ya Bill Clinton mwaka sijui '93 au '94 ule...akizungumzia kuhusu NAFTA......yaani hadi predecessor wake uzalendo ulimshinda na kumwaga sifa kama hana akili nzuri vile....
 
Kuhani, asante sana kwa mtazamo wako wa kina wa mapungufu ya Prof. Kwa kuwa binafsi namfahamu Prof. Muhongo kwa kiasi fulani, basi napenda kutoa maoni juu ya uliyoyaandika:

Kuhani;

Hata mimi ningefurahi kama angekuwa amefungua hiyo branch ya ICSU Tanzania badala ya ugenini. (By the way, ukisema "...was the first and founding Director of ..." maana yake nini?)

ICSU Afrika: Uamuzi wa kuashinza ofisi ya ICSU South Africa haukuwa wa Professor Muhongo. Nafahamu pia Prof. hakuwepo wakati uamuzi unafanywa wa nchi wanachama wa Afrika wa ICSU mwaka 2004. Pia ikumbukwe kuwa Tanzania wakati huo haikuwa Mwanachama.

Hivyo Prof. hakuwa na ubavu wa kuamua kuanzishwa ofisi ya ICSU Tanzania. Pia nafahamu kuwa Prof hakupeleka maombi kutafuta kazi hii bali aliombwa (akiwa Dar Es Salaam anaitumikia Nchi) na ICSU kuchukua nafasi ya Ukurugenzi.

First and Founding could mean . . . Mkurugenzi wa kwanza na muanzilishi kwa maana ya kuset-up office na mfumo mzima wa uendeshaji.

Na anaweza kutokea opponent wa Kiafrika huko anaejua yanayoendelea Tanzania akam corner ajieleze:

Suala la kuwa na opponent si geni katika post kama hizi. Na siku zote katika usaili kuna maswali ya kila namna yakiwepo ya kumcorner mhusika. Una maana huyo Opponent atakayemcorner naye atakuwa anagombea hiyo post au atakuwa tu hamtaki Prof.?

Kwa maoni yangu, ni vizuri tukajenga utaifa na uzalendo kwa kupigia debe vilivyo vyetu. Kwa wale walio katika nafasi nzuri na network ya UNESCO ni vizuri tukasaidiana kumpigia kampeni mtu wetu.

Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi wa STAMICO kwa miaka kumi sasa, kwa hiyo madudu yoooote ya ufanisi mbovu, ufisadi lukuki, vifo vya wachimbaji, unyuma wa jamii zilizo karibu na migodi, hasara kwa Taifa ziletwazo na misamaha ya kodi, na ufukara wa wachimbaji wadogo wadodo, yooooote haya yametokea chini ya usimamizi wa bodi ya Wakurugenzi wako, au?

Kuhani; STAMICO kisheria haina uwezo wa kusimamia mikataba na migodi wala usimamizi wa kodi za madini. Nafahamu moja ya jitihada ya Prof. Muhongo ilikuwa kuzuia STAMICO isiuzwe na nadhani mpaka leo STAMICO ipo.

Utakwendaje wewe mkurugenzi wa bodi ya Wakurugenzi wa STAMICO kuchunguza vifo vya migodini wakati ajali zenyewe inawezekana zinatokea kutokana na uzembe fulani wa STAMICO?

Kuhani, ni uwezekano gani wa uzembe wa STAMICO unaouhusianisha na ajali za migodini? Ndugu zangu, wakati mwingine tusipende kuongelea vitu mabavyo havija hakikiwa.

Na hiyo tume yako ya uchunguzi iligundua nini, na nini kimebadilika?

Kuhani, hivi ni jukumu la nani kutoa Report ya "Merelani Tanzanite Mine's Accident in 2002". Wao walipewa kazi wameifanya na kukabidhi report. Sasa nini cha ziada Prof. angefanya? Na kama ni mabadiliko, Je ni Prof wa kuyaleta au Wizara au Idara husika?

Wakati ukiishi nje ya nchi, kwa nini hujiuzulu majukumu yako yanayohusiana na STAMICO, idara ya nyanja muhimu ya uchumi, iliyofeli kazi kwa kila aina ya vipimo?

Kuhani, bodi nyingi zinakuana mara nne kwa mwaka unless kama kuna extra-ordinary board meeting. Kazi ya board si ya kiutendaji bali ni ya kisera zaidi. Je, unafahamu vipimo ambavyo STAMICO imefeli ni vipi na Prof. alihusika vipi?

Mkeo anaitwa Bertha, ana shahada tatu. Bertha who? Kuliko kuweka shahada za mkeo weka jina lake kamili. Unaionyesha dunia kwamba bado una mfumo dume! Na kijana wako mwenye shahada mbili huyu, info nzuri zaidi hapa ni majina ya hao yatima uwaleao, sio shahada za non-candidate family members!

Du! Ndugu yangu kweli ipo kazi. Ndiyo binafsi na kuheshimu sana kwa uchambuzi wako yakinifu katika masuala mbalimbali, lakini nashindwa kupata picha ni nini hasa unachojaribu kusema. Kama wewe ni Kuhani, nilidhani kuwa mke wako definetely atakuwa Mrs Kuhani na kuwa muhimu zaidi ni kutambulisha jina lake kama mhusika atapenda. Sasa Prof. amependa ku-highlight juu ya family yake kwa maana kiongozi ni vema akitambulisha familia yake pia. Sasa critics zingine zina tija kweli Kuhani?


La mwisho, kwa sehemu nyingine, mfano USA (na hawa ndo vinara wenye influence ya nani anakuwa nani na nini kinafanyika United Nations na matawi yake), unapo ji-introduce kama professor unajulikana kama ni mwalimu. Hiyo inakushushia executive profile yako kwa sababu unaonekana unajiuza kama mtu wa academia ambae hana executive credentials. Ondoa hiyo professor weka title ya Doctor

Ndugu yangu Kuhani; si vema kupotosha uma. Uamuzi wa nafasi hii utapigiwa kura na Nchi Wanachama wa UNESCO na si taifa moja lenye mizengwe. Prof. Muhongo amekuwa mkweli katika CV yake bila kuweka chumvi. Ni Maprofessor wangapi tuionao duniani mbao wanatumikia nchi zao nje ya academia? Si kweli kuwa ukijiuza kwa ukitumia tittle ya Prof. unakuwa huna Executive Credentials. Kama hizo ndizo unazozitafuta mbona Muhongo anazo? Au mpaka aitoe hiyo Prof?

Nafasi za UN siyo zote za quota: zipo za kuchaguliwa na zipo za kuteuliwa (quota) ambazo nchi kama marekani ndiyo huwa wanaleta sana mizengwe.

Kuna ambao wamedai eti Prof. Muhongo hajaifanyia kitu Nchi. Ni uongo mkubwa kwamba hajaifanyia cho chote Tanzania. Mnaodai hivyo, je mnajua kazi zote ambazo nimeifanyia nchini? Ameondoka Nchini Tanzania Juni 2005 kwenda South Africa. Muda mwingi kabla ya hapo ailikuwa Tanzania.

Mantiki ya mimi kuweka post hii hapa ni kuomba watu wenye nafasi za kuweza kushawishi watu wanaowafahamu katika serikali nyingine duniani wazipigie kura Tanzania. Nina imani majibu mazuri ni mengi sana. Siyo busara kwa Watanzania badala ya kutiana moyo na kuonyesha umoja tunaanza kukandiana na kuleta malumbano yasiyo na tija.

Mtanzania mwenye nia ya kusaidia afanye hivyo, na yule ambae anaona Sospeter Muhongo hafai, basi awe na msimamo wake huo na nadhani bado tu tutamheshimu sana. Ila ni vema na yeye vilevile aheshimu uamuzi na msimamo wa wengine.
 
Last edited:
.........I have read between lines for post by Kuhani, really what is expressed should not be taken for granted. Of course based on CV the man is shining. but on grounds of Kuhani's analysis, the man may be terribly not a good manager.
 
Sanctus,

.........ninamfahamu vizuri sana Prof., ni family friend wetu wa karibu sana, naomba usome maoni ya Kuhani with an open mind........nafikiri maoni ya Kuhani kwa kiasi fulani yatamsaidia Prof.

.....sidhani kama Kuhani hamtakii mema Prof.
 
Sanctus,

.........ninamfahamu vizuri sana Prof., ni family friend wetu wa karibu sana, naomba usome maoni ya Kuhani with an open mind........nafikiri maoni ya Kuhani kwa kiasi fulani yatamsaidia Prof.

.....sidhani kama Kuhani hamtakii mema Prof.

mmmmhhhhh......
 
Sanctus,

.........ninamfahamu vizuri sana Prof., ni family friend wetu wa karibu sana, naomba usome maoni ya Kuhani with an open mind........nafikiri maoni ya Kuhani kwa kiasi fulani yatamsaidia Prof.

.....sidhani kama Kuhani hamtakii mema Prof.

Ogah, ahsante.

Unajua mara nyingi tumetofautiana katika mambo mengi humu, tena wakati fulani kwa hisia kali mno, lakini kama mwisho wa yote tunarudi kukumbuka kwamba wote letu moja au linategemewa liwe moja basi kwa kweli nafurahi. Moja lenyewe nadhani ni kuwezeshana kwa vyovyote tunavyoweza ili kujaribu kupunguza kasi ya kurudi nyuma kwa gurudumu la maendeleo ya Taifa letu. Nashukuru, Ogah, unatambua hivyo.

Naomba, basi, tuendelee kukubali na kupingana, kubisha na kujengana, kusaidia na kuwajibishana, almuradi kipaumbele kiwe ni kujenga. Kujenga ya nchi yetu. Huo nadhani ndio uzalendo. Sidhani kama uzalendo ni kuimbiana mapambio kwa vile tu ni Watanzania wenzako, wawe sahihi au wamekosea. Kama unapenda nchi yako, kama unanipenda, nionyeshe njia, na kama ni kwa kukandia ninakoelekea basi kwangu mimi sawa. Kwani unanikandya mimi au unaikandya njia mbovu ninayoelekea? Kama unanisaidia Mtanzania mwenzako kujua pa kuelekea basi we kandya siku nzima! Ndivyo ninavyo define uzalendo.

Professor Muhongo ni rafiki wa ukoo wako, tena wa karibu sana unasema. Lakini hiyo haikukuzuia kuona kwamba kwa machache yasiyoliwaza niliyokuwa nayo kumhusu, sikuwa na nia fidhuli na mtu ambae simjui! Nadhani, Ogah, wewe ni mzalendo wa kweli, mhenga. Uzidishiwe. Ahsante tena.
 
Dang...whats up with this love fest btn these two...?

I'm not sure who has a man-crush who....Lol
 
Sanctus,

.........ninamfahamu vizuri sana Prof., ni family friend wetu wa karibu sana, naomba usome maoni ya Kuhani with an open mind........nafikiri maoni ya Kuhani kwa kiasi fulani yatamsaidia Prof.

.....sidhani kama Kuhani hamtakii mema Prof.

Ogah;

Nimesoma maoni ya Kuhani kwa uangalifu mkubwa sana. Na kwa kuwa namfahamu Kuhani hasa kwenye constructive arguments (alitusaidia sana TPN). Namfahamu pia Prof. Muhongo ingawa si family friend. Lakini nimemwfahamu kama Lecturer wangu, Researcher, Kiongozi na Professionals.

Kama ukisoma majibu yangu kwa makini bila kuwa biased, utanielewa nina maana gani. Kama hujaona tofauti yoyote katika maoni yangu, basi pia ni sawa.

Binafsi naheshimu sana critics za Kuhani, lakini pia kwa hili, nitamwona ni Mwuungwana sana akipima majibu yangu na kama ataona kweli amepotoka he should stand up and be a man kwa kukubali amekosea. Atajiongezea heshima sana na kwa upande wetu wengine tutamwona ni resource ya ukweli kwa nchi yetu. Maana halisi ya Uzalendo, wote tunafahamu.

Sitaki ampambe Professor wala kumwimbia nyimbo za "Zidumu Fikra za Mwenyekiti . . ." Lakini azipime hoja na kuangalia issue iliyopo mbele yetu ni ipi na kama inahitaji critics alizotoa. Au tunaongelea UFISADI katika maada hii?
 
Ogah, ahsante.

Unajua mara nyingi tumetofautiana katika mambo mengi humu, tena wakati fulani kwa hisia kali mno, lakini kama mwisho wa yote tunarudi kukumbuka kwamba wote letu moja au linategemewa liwe moja basi kwa kweli nafurahi. Moja lenyewe nadhani ni kuwezeshana kwa vyovyote tunavyoweza ili kujaribu kupunguza kasi ya kurudi nyuma kwa gurudumu la maendeleo ya Taifa letu. Nashukuru, Ogah, unatambua hivyo.

Naomba, basi, tuendelee kukubali na kupingana, kubisha na kujengana, kusaidia na kuwajibishana, almuradi kipaumbele kiwe ni kujenga. Kujenga ya nchi yetu. Huo nadhani ndio uzalendo. Sidhani kama uzalendo ni kuimbiana mapambio kwa vile tu ni Watanzania wenzako, wawe sahihi au wamekosea. Kama unapenda nchi yako, kama unanipenda, nionyeshe njia, na kama ni kwa kukandia ninakoelekea basi kwangu mimi sawa. Kwani unanikandya mimi au unaikandya njia mbovu ninayoelekea? Kama unanisaidia Mtanzania mwenzako kujua pa kuelekea basi we kandya siku nzima! Ndivyo ninavyo define uzalendo.

Professor Muhongo ni rafiki wa ukoo wako, tena wa karibu sana unasema. Lakini hiyo haikukuzuia kuona kwamba kwa machache yasiyoliwaza niliyokuwa nayo kumhusu, sikuwa na nia fidhuli na mtu ambae simjui! Nadhani, Ogah, wewe ni mzalendo wa kweli, mhenga. Uzidishiwe. Ahsante tena.

Kuhani; japo hujanijibu mimi, lakini nimekusoma vizuri tu ndugu yangu. Na sina lakuongeza. Ila natumaini na wewe umeyasoma mabandiko yangu kwa umakini wa hali ya juu.

Kama tunayo imani na Uzalendo, basi sasa tumsaidie Prof kwa kumwombea na kufanya Networking. Mambo yake sasa hivi yamefika mbali na sidhani kama kubadili CV kwa sasa itasaidia kitu. Feedback zinazokuja out of 193 members countries ni nzuri. Tusaidiane wote ili afanikiwe . . . kwangu mimi huu ndiyo Uzalendo.
 
"As a specialized agency of the United Nations, UNESCO contributes to the
building of peace, the eradication of poverty, sustainable development and intercultural dialogue through education, the sciences, culture, communication and information."
In facing the challenges of the new millennium, it is important to highlight the personal qualities required for the UNESCO Director-General. The point of departure is that the General Conference, in the interests of all Member States, should appoint the best person for the post who should have
the following qualities:
• leadership and proven administrative and management skills;
• a strong commitment to all the objectives of the Organization;
• a visionary and active approach to the role of UNESCO in the community of nations;
• good knowledge of the United Nations system;
• commitment to the highest moral and ethical standards;
• strong communication skills so as to develop effective internal and external
communication strategies, vision and objectives for the Organization;
• empathy and sensitivity to civil society as an important UNESCO constituency by utilizing, as appropriate, the existing structures and in particular the National Commissions for UNESCO.


The above reflects the duties and responsibilities of the Director-General as envisaged in Article VI of UNESCO's Constitution. It should be noted that, according to the Constitution, "the responsibilities of the Director-General and of the staff shall be exclusively international in character. In the discharge of their duties they shall not seek or receive instructions from any government or from any authority external to the Organization. They shall refrain from any action which might prejudice their positions as international officials. Each State Member of the Organization undertakes to respect the international character of the responsibilities of the Director-General and the staff, and not to seek to influence them in the discharge of their duties".

naamini hizi sifa Muhongo anazo, kama kuna mapungufu basi ni angalizo la kuboresha, ni vema tukajenga hoja kwa substance on the main issue rather than personal issues! kuboresha
 
“As a specialized agency of the United Nations, UNESCO contributes to the
building of peace, the eradication of poverty, sustainable development and intercultural dialogue through education, the sciences, culture, communication and information."
In facing the challenges of the new millennium, it is important to highlight the personal qualities required for the UNESCO Director-General. The point of departure is that the General Conference, in the interests of all Member States, should appoint the best person for the post who should have
the following qualities:
• leadership and proven administrative and management skills;
• a strong commitment to all the objectives of the Organization;
• a visionary and active approach to the role of UNESCO in the community of nations;
• good knowledge of the United Nations system;
• commitment to the highest moral and ethical standards;
• strong communication skills so as to develop effective internal and external
communication strategies, vision and objectives for the Organization;
• empathy and sensitivity to civil society as an important UNESCO constituency by utilizing, as appropriate, the existing structures and in particular the National Commissions for UNESCO.


The above reflects the duties and responsibilities of the Director-General as envisaged in Article VI of UNESCO's Constitution. It should be noted that, according to the Constitution, “the responsibilities of the Director-General and of the staff shall be exclusively international in character. In the discharge of their duties they shall not seek or receive instructions from any government or from any authority external to the Organization. They shall refrain from any action which might prejudice their positions as international officials. Each State Member of the Organization undertakes to respect the international character of the responsibilities of the Director-General and the staff, and not to seek to influence them in the discharge of their duties”.

naamini hizi sifa Muhongo anazo, kama kuna mapungufu basi ni angalizo la kuboresha, ni vema tukajenga hoja kwa substance on the main issue rather than personal issues! kuboresha

Very well written and referenced Mzalendo Sabasaba . . .

Also as written in my initial post, after the closing date in May 2009 Prof. Muhongo will provide a statement on his implementation strategy for the mandated and expected functions and strategies of UNESCO for the benefit of the global society that lives in peace, cultural and economic prosperity through the utilization of education, science, technology and innovation.

We wish him all the best . . . .
 
Kwa hakika mambo mazuri hatuna budi kuyakubali na kuyafagilia kwa sana,Prof,Muhongo CV yake tuu inajiuza hata mpige makelele hapa yeye ni Intn'l Figure (IF)Hata tukikaa naye hapa tutam underutilise kwa kiasi kikubwa kufanya akanywe changaa kule Tarime bure.!!!!Mwacheni Mzalendo aonyeshe kwamba hata wa bongo nasi tumo JAMANI.
 
Kwa hakika mambo mazuri hatuna budi kuyakubali na kuyafagilia kwa sana,Prof,Muhongo CV yake tuu inajiuza hata mpige makelele hapa yeye ni Intn'l Figure (IF)Hata tukikaa naye hapa tutam underutilise kwa kiasi kikubwa kufanya akanywe changaa kule Tarime bure.!!!!Mwacheni Mzalendo aonyeshe kwamba hata wa bongo nasi tumo JAMANI.
 
Kwa hakika mambo mazuri hatuna budi kuyakubali na kuyafagilia kwa sana,Prof,Muhongo CV yake tuu inajiuza hata mpige makelele hapa yeye ni Intn'l Figure (IF)Hata tukikaa naye hapa tutam underutilise kwa kiasi kikubwa kufanya akanywe changaa kule Tarime bure.!!!!Mwacheni Mzalendo aonyeshe kwamba hata wa bongo nasi tumo JAMANI.
 
Back
Top Bottom