Invisible
Robot
- Feb 11, 2006
- 9,075
- 7,878
Prof. Safari kajiunga RASMI na CHADEMA na hivi sasa yupo Live anajaribu kutoa ufafanuzi wa kwanini kajiunga CHADEMA.
Tutaendelea kujuzana kinachoendelea, fuatilia updates hapa chini:
=============
UPDATES:
1) Kuna mvua sana jijini Dar, vyombo vya habari kadhaa vimeomba kupewa muda walau ili waandishi waweze kuwasili. Ieleweke kuwa HABARI HII bado itakuwa TETESI, jina na nani anahamia CHADEMA tutafahamu baadae.
2) We are now LIVE. Mvua nafahamishwa imepungua jijini Dar
3) Sasa anaongea Dr. Slaa, anamkaribisha rasmi Prof. Safari na anamkabidhi katiba ya CHADEMA
4) Baada ya kutoka CUF nilitafakari kwa kina, nilishauriwa kuandika vitabu. Mke wangu na wanangu tumetafakari na tukafikia muafaka! - Prof. Safari
5) Kuna masuala matatu muhimu ambayo si ya kufumbia macho; suala la ununuzi wa nyumba za serikali, analitolea ufafanuzi. Kuna suala la UKANDA, nalo analitolea ufafanuzi. Na kuna suala la UDINI ambalo pia anajaribu kulitolea ufafanuzi kwa mapana kwa kuangalia historia tangu uhuru wa Tanganyika na ule wa Zanzibar - Prof. Safari
6) Anawashangaa waislam wanaoburuzwa na wadini kuendekeza udini na anadai kinachosisitizwa katika uislam ni uadilifu. Anasema CCM wametumia fursa hii kujaribu kuuvuruga upinzani hasa wanapoona chama cha upinzani wanapoona kinakuwa na nguvu. Walianzia CUF kwa kudai ni chama cha waislam na sasa wanadai CHADEMA ni chama cha wakatoliki - Prof. Safari
7) Tumepewa vitu tulivyo navyo Tanzania ili vitunufaishe sote si wachache tu- Prof. Safari
8) Saa ya Ukombozi imefika sasa! Tujiunge na CHADEMA kuleta ukombozi huo - Prof. Safari
MUDA WA MASWALI NA MAJIBU:
Bahati mbaya sisikii vema maswali, majibu nitayaweka hapa.
Kwanini anayaongelea yanayohusu ufisadi baada ya kujiunga CHADEMA? Ni propaganda za kisiasa au aelewekeje?
- Nyumba za serikali anapendekeza twende mahakamani lakini anasikitika majaji wengi wameshanunuliwa! Anasema njia nyingine itumike falsafa ya People's Power. Hoja ya kuuzwa nyumba za serikali haikupita bungeni na ni haramu
- Slaa anaongezea kuwa kati ya vitu ambavyo CHADEMA ingefanya within 100 days ingepewa madaraka ingerejesha nyumba hizo kwakuwa ilikuwa ni batili.
- Anasema kitu kibaya ni kibaya, haijalishi upo CHADEMA ama CUF si propaganda.
- Mbowe anaongelea kuwa kazi ya uamsho imefanyika Kanda ya Ziwa tu, si kama Zanzibar haijafikiriwa na wala Prof hajaja kwa ajili ya hili, suala si kujenga ukanda bali kujenga taifa. Rukwa bado, Kilimanjaro wala Arusha bado hivyo Lindi watafika na hata Zanzibar
- Mbowe anasema kwanza wanamkaribisha Prof. ndani ya chama na wanaamini ni mtu muhimu na ana historia safi. Masuala mengine ya kiuongozi yatafuatia baada ya vikao vya chama vya kimaamuzi kufanyika
- Anaulizwa kadi ya CUF ataiweka wapi? Kasema technically ndani ya CUF kama hutoi michango maanake umeshajiondoa rasmi na alishatoa taarifa CUF kuwa kaachana nao. Kasema wakiihitaji atawapelekea.
- Anafafanua juu ya CCM kutumia UDINI kuwagawa watanzania, anasema hawana utofauti na wakoloni walivyotumia mbinu za kuwagawa waafrika ili kuwatawala
- Dr. Slaa anasema yeye binafsi anayo kadi ya CCM kwakuwa aliinunua na wala si mali ya Makamba, hajairudisha na wala hawapi kamwe!
- Prof. Safari anahitimisha kwa kuwakaribisha wanasiasa wengine MAKINI kuhamia CHADEMA kwani ndicho chama makini na anasisitiza wale MAKINI TU.
MWISHO
====================
WASIFU WA PROF. SAFARI:
KUZALIWA (UMRI):
Profesa Safari alizaliwa June 3, 1951.
ELIMU YAKE:
1972- Secondari,
1979- University of Dar es salaam shahada ya sheria (LLB),
1985- Masters (LLM),
1995- (PhD) University of Sussex England. Baada ya kupata shahada hiyo alibaki England akawa anafundisha,
2000- Alitunukiwa u Profesa.
UZOEFU WA KAZI
1972-1974 Matafiti msaidizi katika taasisi ya Institutes of Kiswahili Research
1974-1976 Mhariri katika kampuni ya Tanzania Publishing House
1979-1986 Wakili wa serikali katika wizara ya sheria
1988-1991 Afisa Mtafiti na uchapishaji katika kituo cha Uhisiano wa nje kisha Mhadhiri mwandamizi wa sheria katika kituo hicho Nyadhifa (Vyeo) alivyowahi kushika;
1978-1986 Mwenyekiti wa Chama cha wanasheria wa chuo Kikuu cha Dar es Salaam
1982-1984 Mhadhiri wa sheria university of Dar es Salaam
1983-1986 Mkuu wa Kitengo cha sheria, wizara ya sheria
1984-1986 Mwakilishi wa wizara ya sheria katika baraza la elimu ya sheria Afrika Mashariki
1990-1991 Kaimu Mkurugenzi wa masomo na program katika kituo cha mahusiano ya kimataifa
1996-Hadi sasa, Mwenyekiti wa chama cha wandishi wa Vitabu Tanzania (UWAVITA), pia Mkurugenzi wa Masomo na programu wa kituo cha uhusiano wa Kimataifa
1999-Hadi sasa, Katibu Mkuu wa Tanzania Center for Conflict Resolution, pia Mkurugenzi wa bodi ya hakimiliki (COSOTA)
Makongamano:
1978-Alihudhuria mikutano kadhaa ya Kimataifa kuhusiana na mambo ya sheria barani Afrika huko Nairobi (All African Law Students Association) Aidha,amewahi kuhudhuria makongamano mbalimbali yaliyohusu mambo ya sheria katika sehemu zifuatazo, Afrika Kusini, Sweden, Geneva, Botswana, Uganda na Marekani.
Tuzo alizowahi kupata:
1991-alitunukiwa tuzo iitwayo Ford Foundation Scholarship for Doctor of Philosophy programme
1999-2001, Shaaban Robert Literary
Maisha yake:
Ameoa na ana watoto wawili.
Tutaendelea kujuzana kinachoendelea, fuatilia updates hapa chini:
=============
UPDATES:
1) Kuna mvua sana jijini Dar, vyombo vya habari kadhaa vimeomba kupewa muda walau ili waandishi waweze kuwasili. Ieleweke kuwa HABARI HII bado itakuwa TETESI, jina na nani anahamia CHADEMA tutafahamu baadae.
2) We are now LIVE. Mvua nafahamishwa imepungua jijini Dar
3) Sasa anaongea Dr. Slaa, anamkaribisha rasmi Prof. Safari na anamkabidhi katiba ya CHADEMA
4) Baada ya kutoka CUF nilitafakari kwa kina, nilishauriwa kuandika vitabu. Mke wangu na wanangu tumetafakari na tukafikia muafaka! - Prof. Safari
5) Kuna masuala matatu muhimu ambayo si ya kufumbia macho; suala la ununuzi wa nyumba za serikali, analitolea ufafanuzi. Kuna suala la UKANDA, nalo analitolea ufafanuzi. Na kuna suala la UDINI ambalo pia anajaribu kulitolea ufafanuzi kwa mapana kwa kuangalia historia tangu uhuru wa Tanganyika na ule wa Zanzibar - Prof. Safari
6) Anawashangaa waislam wanaoburuzwa na wadini kuendekeza udini na anadai kinachosisitizwa katika uislam ni uadilifu. Anasema CCM wametumia fursa hii kujaribu kuuvuruga upinzani hasa wanapoona chama cha upinzani wanapoona kinakuwa na nguvu. Walianzia CUF kwa kudai ni chama cha waislam na sasa wanadai CHADEMA ni chama cha wakatoliki - Prof. Safari
7) Tumepewa vitu tulivyo navyo Tanzania ili vitunufaishe sote si wachache tu- Prof. Safari
8) Saa ya Ukombozi imefika sasa! Tujiunge na CHADEMA kuleta ukombozi huo - Prof. Safari
MUDA WA MASWALI NA MAJIBU:
Bahati mbaya sisikii vema maswali, majibu nitayaweka hapa.
Kwanini anayaongelea yanayohusu ufisadi baada ya kujiunga CHADEMA? Ni propaganda za kisiasa au aelewekeje?
- Nyumba za serikali anapendekeza twende mahakamani lakini anasikitika majaji wengi wameshanunuliwa! Anasema njia nyingine itumike falsafa ya People's Power. Hoja ya kuuzwa nyumba za serikali haikupita bungeni na ni haramu
- Slaa anaongezea kuwa kati ya vitu ambavyo CHADEMA ingefanya within 100 days ingepewa madaraka ingerejesha nyumba hizo kwakuwa ilikuwa ni batili.
- Anasema kitu kibaya ni kibaya, haijalishi upo CHADEMA ama CUF si propaganda.
- Mbowe anaongelea kuwa kazi ya uamsho imefanyika Kanda ya Ziwa tu, si kama Zanzibar haijafikiriwa na wala Prof hajaja kwa ajili ya hili, suala si kujenga ukanda bali kujenga taifa. Rukwa bado, Kilimanjaro wala Arusha bado hivyo Lindi watafika na hata Zanzibar
- Mbowe anasema kwanza wanamkaribisha Prof. ndani ya chama na wanaamini ni mtu muhimu na ana historia safi. Masuala mengine ya kiuongozi yatafuatia baada ya vikao vya chama vya kimaamuzi kufanyika
- Anaulizwa kadi ya CUF ataiweka wapi? Kasema technically ndani ya CUF kama hutoi michango maanake umeshajiondoa rasmi na alishatoa taarifa CUF kuwa kaachana nao. Kasema wakiihitaji atawapelekea.
- Anafafanua juu ya CCM kutumia UDINI kuwagawa watanzania, anasema hawana utofauti na wakoloni walivyotumia mbinu za kuwagawa waafrika ili kuwatawala
- Dr. Slaa anasema yeye binafsi anayo kadi ya CCM kwakuwa aliinunua na wala si mali ya Makamba, hajairudisha na wala hawapi kamwe!
- Prof. Safari anahitimisha kwa kuwakaribisha wanasiasa wengine MAKINI kuhamia CHADEMA kwani ndicho chama makini na anasisitiza wale MAKINI TU.
MWISHO
====================
WASIFU WA PROF. SAFARI:
KUZALIWA (UMRI):
Profesa Safari alizaliwa June 3, 1951.
ELIMU YAKE:
1972- Secondari,
1979- University of Dar es salaam shahada ya sheria (LLB),
1985- Masters (LLM),
1995- (PhD) University of Sussex England. Baada ya kupata shahada hiyo alibaki England akawa anafundisha,
2000- Alitunukiwa u Profesa.
UZOEFU WA KAZI
1972-1974 Matafiti msaidizi katika taasisi ya Institutes of Kiswahili Research
1974-1976 Mhariri katika kampuni ya Tanzania Publishing House
1979-1986 Wakili wa serikali katika wizara ya sheria
1988-1991 Afisa Mtafiti na uchapishaji katika kituo cha Uhisiano wa nje kisha Mhadhiri mwandamizi wa sheria katika kituo hicho Nyadhifa (Vyeo) alivyowahi kushika;
1978-1986 Mwenyekiti wa Chama cha wanasheria wa chuo Kikuu cha Dar es Salaam
1982-1984 Mhadhiri wa sheria university of Dar es Salaam
1983-1986 Mkuu wa Kitengo cha sheria, wizara ya sheria
1984-1986 Mwakilishi wa wizara ya sheria katika baraza la elimu ya sheria Afrika Mashariki
1990-1991 Kaimu Mkurugenzi wa masomo na program katika kituo cha mahusiano ya kimataifa
1996-Hadi sasa, Mwenyekiti wa chama cha wandishi wa Vitabu Tanzania (UWAVITA), pia Mkurugenzi wa Masomo na programu wa kituo cha uhusiano wa Kimataifa
1999-Hadi sasa, Katibu Mkuu wa Tanzania Center for Conflict Resolution, pia Mkurugenzi wa bodi ya hakimiliki (COSOTA)
Makongamano:
1978-Alihudhuria mikutano kadhaa ya Kimataifa kuhusiana na mambo ya sheria barani Afrika huko Nairobi (All African Law Students Association) Aidha,amewahi kuhudhuria makongamano mbalimbali yaliyohusu mambo ya sheria katika sehemu zifuatazo, Afrika Kusini, Sweden, Geneva, Botswana, Uganda na Marekani.
Tuzo alizowahi kupata:
1991-alitunukiwa tuzo iitwayo Ford Foundation Scholarship for Doctor of Philosophy programme
1999-2001, Shaaban Robert Literary
Maisha yake:
Ameoa na ana watoto wawili.