Prof Pius Yanda ashinda zawadi ya Nobel

Waliotunukiwa zawadi ya Nobel Peace Prize ya mwaka 2007 ni Al Gore na IPCC. IPCC ilitunikiwa kwa kazi ilizozifanya tangu ilipoanzishwa mwaka 1988. IPCC imekuwa likitoa ripoti kuhusu climate change uhai wake wote. Profesa Pius Yanda ni mmoja ( wako wengi sana) wa contributors katika Working Group II ( ziko WG tatu) Fourth Assessment report. Humo katika WG kuna reviewers wengi tuu ambao nao wanachangia katika hii ripoti. Unaweza kuona majina yao hapa:
http://www.ipcc.ch/pdf/assessment-report/ar4/wg2/ar4-wg2-app.pdf
Mkuu wa IPCC ni Bw. Rajendra Cheuri kutoka India ambaye ni kiongozi wa tatu kuongoza Panel hii. Wote hawa kwa namna moja au nyingine wamechangia katika mafanikio ya IPCC lakini hatuwezi kuwaita 'joint recipients' wa Nobel Peace Prize.
Profesa Yanda anastahili kuheshimiwa na pengine hata kutunukiwa nishani na taifa lake maana aliyoyafanya hata nje ya Panel hii ni makubwa. Tulibidi sisi kama taifa tumuenzi badala ya kujificha nyuma ya hii zawadi. Bila sisi kumvisha hiki kilemba cha ukoka, Profesa Yanda anaweza kutembea kifua mbele kwa yale aliyoishayafanya. Ndio maana nikaweka CV yake humu kuthibitisha hilo.

Fundi Mchundo,

Hilo la kwamba yeye hajashinda hiyo noble prize linajulikana, tatizo kwa watu wengine hapa ni hiyo kujaribu ku negate umuhimu wake kwenye hiyo IPCC kushiinda hiyo prize.

Taifa litamtunikia vipi kama hakuna publicity yoyote anayopata hata anapofanya jambo la maana au kupata fanikio kama alilopata kwa kushiriki kwenye kuandaa reports ambazo zimeifanya IPCC ishinde prize?

Vyombo vya habari havikutakiwa kumtangaza prof. kama mshindi wa nobel peace prize lakini pia vilitakiwa kuongelea contribution yake kwenye hizo reports.
 
Kitila,

Ila pia naona ni mafanikio kwa reports ambazo prof wetu alishiriki kuzitayarisha kushinda hiyo nobel prize. Naamini hilo ni fanikio na ilitakiwa waandishi wetu kuitangaza hiyo habari na hata kumhoji ili aweze kutoa utaalamu wake kwenye mambo ya climate change.


Yes, hii ni sawa kabisa. Lakini this is a bit complex kwa waandishi wetu wa habari, wala hawana huo uwezo wa kutofautisha kunshinda nobel peace prize na kushiriki kuandika an esteemed report. Lakini lazima pia tukiri kwamba hili jambo limepotoshwa sana, maana hata VC wa UDSM alivyomtangaza pale kwenye graduation ni kama vile alishinda Nobel Peace Prize wakiwa yeye na Al Gore. Nimeona hata kwenye discussion fulani ya UDASA somewhere, nimeona wenzake wanampongeza kama vile kashinda Nobele Peace Prize, nao wanashangaa kwa nini hajatangazwa; Surprisingly naye kapokea hizo shukrani bila hata kutoa ufafanuzi au masahihisho! Big confusion.

Halafu lazima tutambue kwamba kuandika ni sehemu ya kazi muhimu ya mwanataaluma, ikiwemo reports na majarida mbalimbali, maarufu na ya kawaida. Sasa tukiamua kupongeza maprofesa kwa kuandika report tutakesha, wameandika sana tena sana.
 
Kitila
Asante kwa maelezo yako safi hapo juu. Nitawapongeza sana maprofesa wetu wakiweza kufanya utafiti, na kutengeza 'models' katika maeneo husika: sayansi, uchumi, siasa, michezo, nk.

Kwa kifupi: maprofesa wetu wana nafasi kubwa sana ya kutuletea heshima watanzania kwa kutuletea kitu 'original' kutoka Tanzania. Huo utakuwa ndio umiliki, ambao ni nguvu, ambayo ni uhuru. Na uhuru huleta heshima.
 
Hapo ndipo mimi ninapopata kizunguzungu! Kwa nini mwenyewe hakuwaambia 'thanks but no thanks'? Au hataki kuwaumbua waliomtangaza? Unaweza kuwakuta hao wasomi wenzake walikuwa wanampaka mafuta kwa mgongo wa chupa! Kwa bahati mbaya jamii yetu imekumbwa na wimbi la kutaka sifa zisizo na msingi. Angalia utiriri wa PH.D zinavyomwagika bila hata mtu kuhoji," hiyo dissertation, mkuu, uliandika lini maana kila siku tuko wote kijiweni?"Ingawa ni muhimu kuwaenzi na kuwapongeza wasomi wetu ni lazima tuwe makini kuwa tunafanya hivyo pale panapostahili kama walivyoeleza wenzangu Kitila na Invisible. Tusipoangalia tutakuwa laughing stock ya ulimwengu! Tuwe wadadisi na tusikubali kila tunacholetewa. Google ipo kwa ajili yetu.
 
Kitila
Asante kwa maelezo yako safi hapo juu. Nitawapongeza sana maprofesa wetu wakiweza kufanya utafiti, na kutengeza 'models' katika maeneo husika: sayansi, uchumi, siasa, michezo, nk.

Kwa kifupi: maprofesa wetu wana nafasi kubwa sana ya kutuletea heshima watanzania kwa kutuletea kitu 'original' kutoka Tanzania. Huo utakuwa ndio umiliki, ambao ni nguvu, ambayo ni uhuru. Na uhuru huleta heshima.

Invicible,

Unajua Profesa wetu aliandika kuhusu nini? Kwenye film ya Gore
ambayo kwa sehemu kubwa alikuwa anatangaza yale yaliyoandikwa na IPCC, kuna mambo ya kuyeyuka kwa ice kutoka mlima Kilimanjaro.

Kikubwa zaidi ni wananchi kutambua mchango wa wana sayansi. Kama wanasiasa hawatoi pesa za research kwenye vyuo, usitegemee wanasayansi kuja na hizo models.

Kwasasa kwenye mazingira kuna pesa za research nyingi, zinatolewa na watu wa Magharibi kwahiyo hata vitu vinavyotakiwa kuchunguzwa kwa vyovyote vitalenga matakwa ya hao wanaotoa pesa.

Priorities zetu kama Watanzania ziko mrama, sitashangaa kama vijana wengi wakakimbilia kusoma arts kama njia rahisi ya kupanda
maisha. Hayo mambo tayari yanatokea nchi za Magharibi ila tu wenzetu wana pesa za kuwezo kuibadili hiyo trend.
 
Halafu lazima tutambue kwamba kuandika ni sehemu ya kazi muhimu ya mwanataaluma, ikiwemo reports na majarida mbalimbali, maarufu na ya kawaida. Sasa tukiamua kupongeza maprofesa kwa kuandika report tutakesha, wameandika sana tena sana.

Lakini ni reports ngapi kati ya hizo zinaishia kwenye kupata prize ya maana kama nobel? Nafikiri hapo unakosea, hatumpongezi profesa kwa kuandika reports maana kwa vyovyote ameshaandika reports nyingi sana. Tunampongeza kwa kushiriki kuandika reports
hizi za IPCC ambazo matokeo yake ni kwa IPCC kushinda nobel peace prize.

Nakumbuka hotuba ya Mwalimu sehemu fulani kuhusu Korea na watengeneza trekta. Siku rais wao kaitwa kuonyeshwa trekta walilolitengeneza, trekta badala ya kwenda mbele likaanza kwenda nyuma, engineers wote wakainama chini kwa aibu na kuanza kuomba msamaha. Rais aliposimama akawapongeza sana kwa hatua waliyofikia na kwamba kama trekta limeweza kwenda nyuma, kazi iliyobakia ni ndogo sana ya kulifanya liende mbele, kweli haikuchukua muda mrefu, trekta likaanza kufanya kazi. Ingelikuwa Tanzania, naona hao engineers wangechekwa na kila mtu, hilo ndilo tatizo, hatuwapi sifa zinazotakiwa wataalamu wetu pale wanapofanya la maana. Ni mabingwa wa kucheka na kukebehi, utafikiri sisi tumefanya makubwa zaidi ya hayo.
 
Mtanzania
Hilo la priorities nakuunga mkono kabisa. Kwa nchi yetu isiyo na dira; na inayoongozwa na wasanii, huko mbele giza tupu. Nchi za magharibi wanapotoa fedha zao, lengo lao kubwa ni kutawala zaidi, au kuwa na ushawishi mkubwa zaidi katika eneo husika.

Sasa hivi naangalia press conference ya Al gore hapa Norway kwenye channel ya TV2 Nyhetskanalen. Yupo pamoja na mtaalamu mmoja kutoka India...Pachaura.
 
Mtanzania: hamna anayekebehi hapa, tunachosema mtu apewe sifa anayostahiki na anayostahili. Ukiona wameongeza chumvi hasa kwenye mambo serious kama haya, unasema, kama alivyosema Fundi, jamani ahsanteni lakini sifa zingine sio zangu. Huyu Profesa namjua na uwezo wake nautambua maana nafanya naye kazi katika taasisi moja wala sina sababu ya kumkejeli. Ninachosema na ambacho wengine pia wanasema ni kwamba hakushinda Nobel Peace Prize, isipokuwa report iliyoshida Nobele Peace Prize alishriki kuiandika. Sasa hili la pili ni kubwa lakini nafikiri utakubali kwamba sio kubwa kwa kiwango cha kubebea bango kama wengine wanavyotaka na kuwalaumu waandishi wa habari au serikali. Kuna wengine wanataka apewe heshima kama ile Prof Maathai, nami nasema ushindi alioupata haufikii wa Prof Maathai au Wole Soyinka na hivyo hakuna sababu ya kutaka vyombo vya habari vilikuze jambo hili au serikali itoe tamka rasmi. That is said, tunasema kudos Prof Yanda and keep up, who knows the real Nobel Peace Prize could be on your way. He is only 47 and already has done quite noticeable and prestigious achievements.
 
Nashukuru nyote mliochangia mada hii, mmetuwezesha kuelewa ukweli hasa ulivyokuwa na hasa mchango halisi wa huyu Prof Yanda kwenye hiyo kamati iliyoshinda zawadi ya Nobel pamoja na Al Gore. Nakiri pia hata mie nilipoanzisha mjadala huu, sikuwa na taarifa zote hizi zilizotolewa na wote mliochangia, na hii ndio faida ya kuwa na mtandao wenye watu wenye taarifa kama huu. Nilipokuwa naanzisha mjadala huu, reference yangu pekee ilikuwa hotuba iliyotolewa na VC wa UDSM, Prof Mukandara siku ya mahafali, nayo niliisoma sehemu tu waliyonukuu waandishi wa habari nasi tukapata kuona kwenye mtandao. Ndipo nikawa nashangaa, kama huyu Prof kapata tuzo kubwa hivi, iweje iishie tu hapo kutamkwa na VC kwenye mahafali? Sasa nimeelewa, na ninakushukuruni nyote. Zaidi nampongeza Prof Yanda kwa hatua hiyo, kwani kwa umri wake (bado ni umri "mbichi" katika anga za kitaaluma) ninaamini bado anayo nafasi kubwa sana ya kufanya mambo makubwa zaidi. Namsihi na kumtia moyo azidi kufanza bidii, ili hii tuzo ya Nobel tuliyoanza "kumchulia" leo, ifikie siku aipate kweli, inshaallah kabla hajastaafu.
 
CV ya Profesa hii hapa:
Utaona anastahili kupongezwa tena sana kwa achievements zake bila ya hii tunayotaka kumvisha. Kama anasoma naamini kabisa yeye mwenyewe atajisikia vibaya kuona kuwa tunamtangaza kuwa mshindi wa Nobel Peace Prize!

Ahsante Mchundo kwa hii CV ya nguvu ya huyu muungwana ila mimi banafsi imenitatiza kidogo kwani naona kisomo chake na unri wake haviendani, labda tu kama wazee wake walikuwa vigogo au wana pesa hivyo akasoma akiwa mdogo sana!

Kwa wale tulosoma na wenzetu toka kona za kasulu tutakumbuka kuwa wengi walikuwa wana umri mkubwa kuliko wengine darasani kutokana na family backgraound zao etc.

Pia miaka aloanza mlimani Wanaume walikuwa wanaenda Jeshini halafu baada ya jeshi lazima watekeleze Azimio la Musomo ( ilikuwa lazima wafanyekazi miaka kama miwili au mitatatu kabla ya kwenda Chuo kikuu, hakuna cha mtoto wa nani au nani) Ina maana baada ya A level, alienda jeshini halafu kazi si chini ya miaka mitatu hiyo tayari, je alimaliza "A" level na "O" level na pia darsa la saba akiwa na umri gani?,
 
Hakuhusika hata kuandaa report ila sehemu tu ya mojawapo ya publication yake ilitumika.
 
This is what the mainstream media reported....

Amekuwa joint-recepient... mshindi-mwenza! Ameshinda au hajashinda?

Kalaghabaho!

--------------------------------------------



UDSM don becomes a joint recipient of Nobel Peace Prize

2007-12-01 08:43:14
By Hellen Nachilongo

The University of Dar es Salaam has announced that one of its dons, Prof Pius Yanda, was among co-authors who on October 12 this year jointly received the prestigious Nobel Peace Prize.

In a statement released in Dar es Salaam on Thursday, the university�s public relations office said Yanda was a joint recipient of the world`s top prize with former US vice-president Al Gore for co-authoring the Inter-Government Panel for Climate Change (IPCC) report.

Yanda, according to the statement, is a professor of Physical Geography specialising in natural resources management and environment and is currently engaged in a research project that provides high resolution information on predicted future climate change and associated impact on natural and social systems in various parts of Tanzania.

The project is conducted in collaboration with Michigan State University of the US and the Livestock Research Institute of Nairobi.

However, in the IPCC report, the statement said, Prof Yanda participated in the project, entitled `Climate Change Impacts, Adaptation and Vulnerability, ` with specific focus on Africa.

Findings presented in the report include that of vulnerability of Africa to climate change and climate variability, a situation aggravated by the interaction of multiple stresses occurring at various levels and law adaptive capacity, noted the statement.

Another finding states that climate change could result in low-lying lands being inundated, with resultant impacts on coastal settlements.

The report also notes that human health, already compromised by a range of factors, could further be impacted by climate change and climate vulnerability.

* SOURCE: Guardian
 

Attachments

  • Pius Yanda.jpg
    Pius Yanda.jpg
    16.7 KB · Views: 73
Hakuhusika hata kuandaa report ila sehemu tu ya mojawapo ya publication yake ilitumika.

Hakushiriki kuandika, una maana hakuwa karani? Kwi kwi kwi Watanzania bwana!

Kama sehemu ya findings zake au research zake ilitumika ndio kushiriki kwenyewe huko!
 
Ahsante Mchundo kwa hii CV ya nguvu ya huyu muungwana ila mimi banafsi imenitatiza kidogo kwani naona kisomo chake na unri wake haviendani, labda tu kama wazee wake walikuwa vigogo au wana pesa hivyo akasoma akiwa mdogo sana!

Kwa wale tulosoma na wenzetu toka kona za kasulu tutakumbuka kuwa wengi walikuwa wana umri mkubwa kuliko wengine darasani kutokana na family backgraound zao etc.

Pia miaka aloanza mlimani Wanaume walikuwa wanaenda Jeshini halafu baada ya jeshi lazima watekeleze Azimio la Musomo ( ilikuwa lazima wafanyekazi miaka kama miwili au mitatatu kabla ya kwenda Chuo kikuu, hakuna cha mtoto wa nani au nani) Ina maana baada ya A level, alienda jeshini halafu kazi si chini ya miaka mitatu hiyo tayari, je alimaliza "A" level na "O" level na pia darsa la saba akiwa na umri gani?,

Prof hakutoka familia ya kitajiri ni kati ya wale waliosoma kama watoto wengi wa watanzania maskini tena kijijini...Kilichomwezesha kufanikiwa akiwa na umri huo alionao ambao kwa watanzania ni "mbichi" kama walivyo viongozi wetu "vijana" ni kichwa. Wote tunakubaliana kwamba walikuwepo vichwa waliotoka maeneo mbalimbali ya nchi wakapelekwa shule za bweni mbali na makwao na walionekana kama waliotumwa na vijiji kwa namna walivyokuwa wanasoma kwa bidii! Yanda ni mmoja kati ya walioonekana wakati ule ametumwa na kijiji...lakini alikuwa na malengo. Hakuwa kati ya wale waliopelekwa shule ukubwani lakini alifanya vizuri siku zote. Alitumwa toka kwao Kasulu.
Hata ikiwa mafanikiwa hayo yametoka na publications alizowahi kufanya bado amechangia kupatikana kwa ushindi huo...na yeye mwenyewe anashangaa sana kwanini watu wanalifanyia gumzo hili.
 
Ahsante Mchundo kwa hii CV ya nguvu ya huyu muungwana ila mimi banafsi imenitatiza kidogo kwani naona kisomo chake na unri wake haviendani, labda tu kama wazee wake walikuwa vigogo au wana pesa hivyo akasoma akiwa mdogo sana!

Kwa wale tulosoma na wenzetu toka kona za kasulu tutakumbuka kuwa wengi walikuwa wana umri mkubwa kuliko wengine darasani kutokana na family backgraound zao etc.

Pia miaka aloanza mlimani Wanaume walikuwa wanaenda Jeshini halafu baada ya jeshi lazima watekeleze Azimio la Musomo ( ilikuwa lazima wafanyekazi miaka kama miwili au mitatatu kabla ya kwenda Chuo kikuu, hakuna cha mtoto wa nani au nani) Ina maana baada ya A level, alienda jeshini halafu kazi si chini ya miaka mitatu hiyo tayari, je alimaliza "A" level na "O" level na pia darsa la saba akiwa na umri gani?,


Choveki,

Nafikiri hiyo miaka ni halali kabisa kuingia chuo kikuu kwa wakati huo. In facts alitutangulia wengine kwa miaka kama mitatu wakati kwa umri yuko zaidi yangu kwa miaka 5.

Kwenye intake yetu mimi sikuwa katika wadogo kabisa pale mlimani, nilikuwa katikati, kulikuwa na wadogo wengi tu. Average
ya kuingia mlimani wakati huo ilikuwa 21, 22. Wengi wetu tulikuwa watoto wa wakulima.

Pia hiyo sheria unayoisema nafikiri ilikuwa imeondolewa. Nina uhakika mwaka 1986 haikuwepo na huenda hata 1983 ilikuwa tayari imeondolewa.

Ukiangalia CV yake hakuna mahali anaonyesha alifanya kazi kabla ya kuingia mlimani.

Nafikiri nimesaidia kuondoa wasiwasi wako.
 
Mbona tunashabikia kuwaponda Watanzania wanaojitahidi kuhangaika, kujitoa muhanga, hatimaye kufanikiwa, badala ya kuwapongeza?

Tunawapongeza zaidi wale wanaotuibia na kutunyima haki zetu, na kusema hawapaswi kujadiliwa, ati kwa kuwa ni watawala wa nchi?

Jamani mnashangaza! Yanda anapaswa kuungwa mkono kwa jitihada zote! Zote!
 
Back
Top Bottom