Prof. Palamagamba Kabudi, mtaalamu wa sheria Afrika na duniani

Mkuu siasa ni mchezo mchafu. Kinachozungumzwa hadharani mara nyingi hakuuwakilishi usafi wa mtu kimaadili.

Kuna minong'ono kuwa yule mkuu wa kyela anataka kuachana na nafasi yake kwa sababu binafsi za kifamilia.

Ndio maana JPM ameona bora ampe ubunge Kabudi ili aende akairithi nafasi. Naamini hawezi kwenda kinyume na msimamo wa bosi wake kikazi.

Yapo mengi zaidi ya suala la serikali tatu, ambayo msomi huyu anaweza kuyafanya kwa faida ya Tanzania.
Kwamba siasa ni mchezo mchafu, nakubaliana na wewe na ndio maana I trust no politician... iwe ni wa upinzani au upande wa chama tawala!!

Kuhusu kwamba yapo mengi zaidi ya serikali 3; hilo la serikali 3 nimelitaja tu kwa sababu ndilo ambalo lilitofautisha watu mbalimbali kwa uwazi! Isitoshe, binafsi sio mfuasi wa serikali 3 kwahiyo hata akianza kuhubiri serikali 2 atakuwa tu anahubiri upande ambao mimi nauunga mkono! Lakini kama suala sensitive kama hili anaweza kubadilika, basi atakuwa ananipa mashaka ya kuogofya!
 
Prof Palamagamba Kabudi mtaalam wa sheria Afrika na duniani ambae alikuwa ni Lecturer wa sheria UDSM pia mwanasheria mkuu wa chuo UDSM.

Anaenda kulitumikia Taifa lake ndani ya Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Mimi naweza sema Prof anaenda kuwa mwarobaini kwa wanasiasa wafanya fujo za kisheria.

Rais DR JPM siku zote huwa anafanya maamuzi ya busara sana ya kuchagua watu wenye uweledi mkubwa wa kazi, kwa hilo DR JPM tunampongeza sana.

Ndugu yangu Mh Tundu Lissu natumai umepokea uteuzi huu kwa kuraha sana maana mwalimu wa sheria mmeletewa bungeni, hivyo mtakapo kwama msisite kumwomba ushauri.

UDSM tunakuombea mema Prof Kabudi katika safari yako hii mpya ya kuwatumikia WaTanzania.

Mungu ibariki Tz
Mungu ibariki UDSM.

hamis abeid (mr amazing)View attachment 460802
mtu unaweza kuwa profesa lakini ulifeli mtihani wa Bar examination ili uwe wakili, hivyo haujawahi kupractice sheria mahakamani, ulichonacho ni theory tu, mazingira ya mahakamani unayasikia tu kwasababu hauna mandate kuappear mahakamani....utaitwa mtaalamu wa sheria? mtaalam wa sheria gani? ametunga kitabu gani? kiweke hapa....kitu gani kinachokufanya umwite mtaalam? na, unajua kuwa sheria ni practice na sio theory?
 
Tujiulize
1. Lipumpa
2. Mbarawa
3. Maghembe
4. Muhongo
Wote hawa ni wasomi wa kimataifa but jiulize wamelifanyia nini taifa. Ni aibu sana kutatua matatizo na njia zile ziletufanya tushindwe. Prof kabudi akuna kipya anacholeta zaid atakuwa controlled by system. Hata uwe professor ukishaingia kwenye siasa uwez itwa tena mtahalamu.
We must awake and arise from our beds. Our beds is not physical beds but are CCM, opposition, judicial, parliament, executive
 
Aliturostisha kwenye kesi ya mgombea binafsi alipoitwa kama friend of the court mahakamani akaongea utumbo mpaka tukakosa mgombea binafsi sidhani kama amebakiza jambo la maana kwa wananchi
sasa angeonea nini mtu sio wakili? ukiwa wakili utaizoea mahakama, utazoea namna gani ya kuongea mahakamani, kuna experience fulani unaipata na ni automatic. semeni ni kesi gani alishawahi kuwakilisha mtu mahakamani, hata kama kesi ya kuku. sheria ni practice, theory hata kama ni prof utakuwa sawa tu na fresher anayemaliza chuo na hajaanza kupractice, kwasababu yale wanayotufundisha ni machache sana unayatumia mahakamani, yaliyo mengi tunayotumia mahakamani ni yale tuliyojifunza nje ya chuo kwenye practice...sasa mtu haujapractice sheria, hujui mazingira ya mahakama, utasemaje wewe ni mwanasheria au mtaalam? atatolewa knock out na kina tundu lisu hadi ashangae...na aangalie, atahitaji sana kulinda cheo chake cha uprofesser asije kusambaratishwa na kina tundulisu wenye masters tu hata phd hawana.
 
Mimi naona uwaziri wa mwakyembe kama unawekwa rehani hivi kwa uteuzi huu wa nguli wa sheria nchini.
nguli wa sheria sio huyo mkuu, manguli ni kama hao kina Dr Tenga wenye malawfirm hapa dsm na wengine. heshimuni sheria wandugu.
 
Nilijua hilo lilijadiliwa kwa kina na GT wakaja mwisho kukubali kuwa Kabudi alikuwa sawa. Hata UK ambako sisi tunaiga, Mahakama haiwezi kuiamuru Serikali. Inaweza tu kuiambia ibadili sheria fulani kwa sababu inapishana na sheria za haki za Binadamu. Serikali itasema sawa na tukipata fedha tutalishughulikia.

Kama ulifuatilia kwenye Katiba ya Warioba, hayo yaliingizwa na mengine mengi mazuri. Ila pamoja na yote hayo, Kikwete au Sitta au wote wawili na team yao waliivuruga Katiba pendekezwa na kila kitu kikaishia hapo.

Lazima mkumbuke kuwa Mihimili mitatu huwa haiingiliani kisheria. Mahakama huishia kusema na Serikali ndiyo ntekelesaji. Kabudi alilijua hilo na ndiyo akasema aliyosema.

Kama ni kumhukumu, subiri sasa muda umefika maana utapata mengi tu ya kumhukumu kwani kuitetea Serikali yoyote duniani inabidi uwe kichwa kwelikweli vinginevyo utaishia kutukanwa na kuabishwa hata na wale ambao hawakusoma sheria na hata degree moja hawana. Kibaya zaidi ni kuwa watakuaibisha kwa ushahidi.

Aliturostisha kwenye kesi ya mgombea binafsi alipoitwa kama friend of the court mahakamani akaongea utumbo mpaka tukakosa mgombea binafsi sidhani kama amebakiza jambo la maana kwa wananchi
 
Nauliza tu..Je Profesa Kabudi ana utofauti gani na wasomi wengine walioteuliwa au kuingia kwenye siasa,utofauti ambao utafanya watanzania tusimuone kama wasomi wengine wa Tanzania ambao wametubadilikia baada ya kupata ugali?
 
hawa wataalam wakishaingia CCM akali zao wanaziacha kwenye kabati nyumbani.

refer; Mwakyembe, Dr Rioba, Dr Bana nk.
 
Uteuzi huu umenikumbusha uteuzi wa Prof. Tibaijuka akitokea UN na Muhongo.........
Prof. Shivji alivyotetea katiba pendekezwa.........
Kilichotokea baada ya hapo...............
Karibu Prof. Kabudi na kila la Kheri (Tunaamini ulikuwa na akili ndiyo ukaamua kusoma,usiwe kama BWANA YULE aliyeamua kusoma wakati hana akili)
 
Bingwa alikuwa Juan Mwaikusya
yap, na kuna tetesi aliuawa na kagame baada ya kumtetea adui yake ICTR kule Arusha akatoa maeneno kuwa...kama mteja wangu huyu anashitakiwa basi kagame naye alitakiwa ashitakiwe naye. walimfuata home anapoingia wakamuua mbele ya mtoto wake..saa kumi na mbili jioni. yule alinifundisha, alikuwa mwalimu mzuri sana, comand yake ya kiingereza ilikuwa bora kuliko hao walimu waliopo sasaivi waliosoma bongo darasa la kwanza hadi phd.
 
WanaJF wamekuwa wakiusema uteuzi wa jana wa Prof. Kabudi kama Nguli wa sheria. Naomba kuelimishwa vigezo vya kitaaluma mnavyovitumia. Elimu haina mwisho
 
WanaJF wamekuwa wakiusema uteuzi wa jana wa Prof. Kabudi kama Nguli wa sheria. Naomba kuelimishwa vigezo vya kitaaluma mnavyovitumia. Elimu haina mwisho
Unazi kweli ni NOUMA
Mtu ni profesa wa sheria,
Lecturer wa wanaosomea phd ya Sheria
Amebobea kwa uzoefu wa miaka tele
Bado inakuuma akiitwa NGULI WA SHERIA...
Mbona sijakusikia ukihoji yule dogo anayejiita Wakili MSOMI as if kuna wakili ambaye hajasoma
Au mwanasheria nguli ni LISSU pekee
Teh teh teh teh teh teh teh......
 
Kwani bado hamjajifunza tu kwa yule mwalimu nguli wa tasnia ya habari Dr.Ayubu Rioba? Eti bado munaegesha matumaini yenu kwa msomi nguli wa sheria? Haa wekeni maneno ya akiba kengele ya alam ikifika.
 
Tutaona kama Mbunge wa kuteuliwa na Rais na mwenye weledi wa sheria kama atasimamia hoja yake ya serikali tatu.
Akipinga maandiko yake kama Mwakyembe ndio tutaamua kama anao weledi kama anavyo fikiriwa au laa
Hii Nchi wapumbavu cjui wataisha lini!? Yaani ww unahoji kama atasimamia msimamo wake au laa! Hv msimamo wa CDM yako juu ya serikali tatu unaujua!?

Msimamo wa Lowassa juu ya serikali tatu unaufahamu!? Kaangalie Hansard za bunge! Upo ushahidi was wazi was Lowassa kuvuruga mchakato was katiba!
Hv umesahau kuwa Lowassa ndo aligombea urais kupitia CDM na hakuwahi kuweka hadharani juu ya msimamo wake was serikali mbili! Yaani CDM inayoamini ktk serikali tatu ilimsimamisha mgombea anayeamini ktk serikali mbili na hadi Leo maisha yanaendelea, hv umejiuliza kwanini hawazungumzii katiba mpya SKU hizi!!

We endelea kuwa rofa, wenzako cku nyingi hawachez mbali na matumbo!
Wahoji kwanza hao, then njoo kwa Kabudi!!
 
Hii Nchi wapumbavu cjui wataisha lini!? Yaani ww unahoji kama atasimamia msimamo wake au laa! Hv msimamo wa CDM yako juu ya serikali tatu unaujua!?

Msimamo wa Lowassa juu ya serikali tatu unaufahamu!? Kaangalie Hansard za bunge! Upo ushahidi was wazi was Lowassa kuvuruga mchakato was katiba!
Hv umesahau kuwa Lowassa ndo aligombea urais kupitia CDM na hakuwahi kuweka hadharani juu ya msimamo wake was serikali mbili! Yaani CDM inayoamini ktk serikali tatu ilimsimamisha mgombea anayeamini ktk serikali mbili na hadi Leo maisha yanaendelea, hv umejiuliza kwanini hawazungumzii katiba mpya SKU hizi!!

We endelea kuwa rofa, wenzako cku nyingi hawachez mbali na matumbo!
Wahoji kwanza hao, then njoo kwa Kabudi!!
Wewe ndio mpumbavu kabisa. Unaelewa maana ya chama tawala ni nini? Ndicho kinasimamia serikali na lazima wateule wake wawe na msimamo mmoja.
Huwezi kuendesha serikali na ideology za aina mbili. Chadema au TLP tutawahoji hilo ujinga wako unalofikiri kama wamepewa madaraka.
Kesho mtahojiwa kitu mtaanza mbona Dovutwa yuko hivi au vile.
Kabudi anaweza kuharibu credibility yake kwa kujichanganya na mambo ya kiccm
 
Back
Top Bottom