Prof. Mwandosya: Kuuliza si Ujinga, kamati za Bunge kutowasilisha ripoti bungeni kwanza, Je kanuni zimebadilika?

Acha porojo bwana mdogo rudi kwenye kanuni za utendaji wa mihimili yetu inavyoelekeza. Usipende kuamini anayoyaongea rais wetu mpendwa, ayaongeayo mengi yana matatizo ya kiufundi na kiafya..
Kuhusu kumuangalia Lipumba ni bora niangalie nzi walivyo kizunguka kinyesi.
Mimi nimeamini maneno ya Kub Mbowe wakati wakimkabidhi ripoti Waziri Mkuu, kwamba anaishukuru serikali kwa kuliamini bunge na kuwa mambo yote yameenda vizuri. Labda wewe mkuu unazijua kanuni za bunge kumpita Mbowe, Silinde na wakili msomi Ole Milya!!!!!
 
View attachment 584627

Mwanasiasa mkongwe na waziri mwandamizi wa zamani,Prof Mark Mwandosya ameandika katika "tweet" akihoji kuwa,huu utaratibu wa kamati ya Bunge kuundwa na Spika kuchunguza jambo fulani,na baadae badala ya kuliwasilisha bungeni na wabunge kupata muda wa kujadili,safari hii kamati zimewasilisha taarifa zao nje ya bunge lakini katika viwanja vya bunge,na baadae taarifa hiyo kukabidhiwa kwa Rais.

Prof Mwandosya anahoji anasema "Je Kanuni za Bunge zimabadilika?"...Maana ilivyozoeleka na kwa mujibu wa kanuni,kamati kama hizi huwasilisha taarifa zao ndani ya bunge,bunge hujadili na baadae kutoa maazimio ambayo Serikali hupaswa kuyafuata na kuyatekeleza.

Hivi ndivyo ilivyofanya kamati ya Mwakyembe juu ya suala la Richmond,Kamati ile ya Operesheni Tokomeza na hata kamati hizi mbili za kuchunguza Tanzanite na Almasi zilipaswa kufanya hivyo kwa mujibu wa kanuni za kudumu za Bunge.

Nami niungane na Prof Mwandosya kuuliza "JE KANUNI ZA BUNGE ZIMEBADILIKA"
barafu wa JF
Ripoti ilikua kwenye flash mzee. Ile ya dom ilikua funika kombe tu, rimoti iko ferry
 
Kanuni hazijabadilika na wala hazijavunjwa. Tofauti na kamati hizo nyingine alizotaja prof Mwandosya ambazo ziliundwa kwa utashi wa bunge lenyewe, hizi za juzi ziliundwa kwa ombi la Rais. Kama ulimsikia Spika Ndugai wakati anawasilisha alisema wazi aliunda kamati zile kutokana na ombi la Rais kwamba bunge limsaidie kuchunguza. Kimsingi kamati ya bunge ndio bunge lenyewe na taarifa hii ilikuwa ni hitaji la serikali so hakukuwa na haja ya mjadala wa bunge zima kwani si wao walioagiza uchunguzi. Ahsante!
Mnajitahidi sana kutetea maovu, na actually nyie ni sehemu ya maangamizi yanayoelekezwa kwa taifa hili. Baada ya awamu hii utawala utakaoingia madarakani(kama waliopo hawatajigeuza akina Kagame, M7 na Mugabe) kazi kubwa ya kwanza itakuwa kuanza upya kuirejesha nchi katika kuheshimu mihimili (mgawanyo wa madaraka).

Yaani, awamu hii Bunge limegeuzwa kuwa chombo cha kupangiwa kazi na muhimili mwingine? Unataka kutuambia kwa mwelekeo huu Bunge litaendelea na majukumu yake ya kuisimamia serikali? Ambacho huelewi ni kwamba, wenzako wanatumia ripoti hizo kama milestone za kisiasa, huku wakiwalinda watu wao wasiguswe japokuwa kwenye ripoti wameguswa. Wasubiri akina Dk Kalemani kama watang'oka au kung'olewa? Ripoti hizo zilitakiwa zijadiliwe bungeni then Bunge litoe maazimio yake kwa serikali, na kupitia mijadala hiyo ya bungeni ndipo ya akina Kalemani yangewekwa wazi zaidi. Hapo ndipo heshima kidogo ya Bunge iliyobakia ingeendelea kuonekana!
 
Naona Wazee yamewafika shingoni,wanaanza kuuliza maswali "indirect" ya juu ya uvunjwaji wa sheria na katiba.

Tundu Lissu alishasema sana...Wakati anasema wengi tulikuwa kimya,sasa naona hata waliokuwa kimya nao wameanza kusema yaleyale ambayo Lissu alianza kuyasema miaka miwili iliyopita.

Mwisho wa siku,wazee wote wataibuka na kuanza kurudia kusema yale ambayo Lissu alishayasema huko nyuma,akaishia kuitwa mchochezi!!

Duuuh....A Novice has been given a task of his/her Senior!!No doubt he/she will never meet a target
Na ipo siku mawe yataongea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
View attachment 584627

Mwanasiasa mkongwe na waziri mwandamizi wa zamani,Prof Mark Mwandosya ameandika katika "tweet" akihoji kuwa,huu utaratibu wa kamati ya Bunge kuundwa na Spika kuchunguza jambo fulani,na baadae badala ya kuliwasilisha bungeni na wabunge kupata muda wa kujadili,safari hii kamati zimewasilisha taarifa zao nje ya bunge lakini katika viwanja vya bunge,na baadae taarifa hiyo kukabidhiwa kwa Rais.

Prof Mwandosya anahoji anasema "Je Kanuni za Bunge zimabadilika?"...Maana ilivyozoeleka na kwa mujibu wa kanuni,kamati kama hizi huwasilisha taarifa zao ndani ya bunge,bunge hujadili na baadae kutoa maazimio ambayo Serikali hupaswa kuyafuata na kuyatekeleza.

Hivi ndivyo ilivyofanya kamati ya Mwakyembe juu ya suala la Richmond,Kamati ile ya Operesheni Tokomeza na hata kamati hizi mbili za kuchunguza Tanzanite na Almasi zilipaswa kufanya hivyo kwa mujibu wa kanuni za kudumu za Bunge.

Nami niungane na Prof Mwandosya kuuliza "JE KANUNI ZA BUNGE ZIMEBADILIKA"
barafu wa JF
Hili jambo nami niliuliza hapa jamvini katika mtindo wa kuomba mwongozo kwa Mhe. Spika. Bunge letu lijitathmini kweli ama la, linatekeleza matakwa ya Kikatiba, Kisheria na Kikanuni.
 
Hawa wazee wakishatoka madarakani ndo akili zinawarudia. Strange indeed!
Dah! Afadhali yeye zimemrudia. Bunge lote kimya wao wanavuta posho tu na mishahara. Wao ndo walitakiwa kuidai ripoti. Ni muhimu mihimili iweze kuwa independent kama katiba inavyotaka.
 
Huyu ni mpumbavu sana. Ushenzi wao ndo umetugarimu leo anauliza unafiki. Prof wa Tz wengi ni matahila.

Sent using Jamii Forums mobile app

Nyie vijana wasengerema,kumalija na nyegezi mnahasira watu wakihoji tofauti na mata kwa ya mjomba enu. Wenzenu wa pwani mbona walikuwa barida show yote alisimamia mwenyewe JK na kutusua, nyie matusi na sasa bunduki mnafikiri mtaweza zuia waTZ wasifikiri tofauti.
 
Maprof wengi wapi huko sawa lakini sio Mark,uliza historia ukijifanya kumpeleka peleka anakurushia brief case ya document zako n.a. kukuachia offisi
Wahenga wanaokua.
 
Kanuni hazijabadilika na wala hazijavunjwa. Tofauti na kamati hizo nyingine alizotaja prof Mwandosya ambazo ziliundwa kwa utashi wa bunge lenyewe, hizi za juzi ziliundwa kwa ombi la Rais. Kama ulimsikia Spika Ndugai wakati anawasilisha alisema wazi aliunda kamati zile kutokana na ombi la Rais kwamba bunge limsaidie kuchunguza. Kimsingi kamati ya bunge ndio bunge lenyewe na taarifa hii ilikuwa ni hitaji la serikali so hakukuwa na haja ya mjadala wa bunge zima kwani si wao walioagiza uchunguzi. Ahsante!
Anachosema mkuu ni sawa, lakini kwanini raisi asingeunda kamati kama ile ya Prof.Mruma badala yake akatumia bunge? Hapo ndipo panaleta shida kwa sababu kamati ikishakuwa ya bunge hata kama raisi ndiye aliomba iundwe lazima kikanuni repoti ya kamati hiyo iwasilishwe kwenye bunge na kujadiliwa na bunge, na mapendekezo ya bunge yapelekwe serikalini kwa utekelezaji.

Sasa kinachoonekana hapa ni huu mhimili uliojichimbia zaidi kuagiza bunge nini cha kufanya badala ya bunge kuagiza huo mhimili nini cha kufanya. Mambo yamebadilika, serikali ndiyo inasimamia bunge. Tukubali tu kwamba baada ya kuambiwa kuwa katiba inawekwa pembeni, tumebakiwa na mhimili mmoja tu.

Hoja kwamba kuna tofauti ya kuundwa kwa kamati haina nguvu, maadamu inaitwa kamati ya bunge na bunge liliiunda, hata kama ni raisi aliagiza bado kanuni za bunge zingefuatwa mpaka report imfikie raisi.
 
Back
Top Bottom