Prof. Mussa Assad kumaliza muda wake November, 5 mwaka 2019. Je, Rais Magufuli atamuongezea mkataba wa ajira?

Lord Diplock MR

JF-Expert Member
Mar 16, 2015
1,393
3,234
Waungwana salaam.

Kwa mujibu wa katiba ikisomwa pamoja na Sheria ya ukaguzi wa umma ya mwaka 2008 Rais ndiye mwenye mamlaka ya kumteua mtanzania kuwa mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG. Mbali na sifa za kihasibu na ubobezi na uzoefu sifa nyingine ni lazima awe raia wa Tanzania kwa kuzaliwa.

Kwa mujibu wa kifungu cha 6 cha Sheria ya Ukaguzi wa Umma ya mwaka 2008 mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali atadumu kwa muda wa miaka 5 na anaweza kuongezewa mkataba wa kipindi kimoja tu kingine cha miaka mitano. Kwa maana hiyo sheria inaruhusu mkaguzi kukaa vipindi viwili tu vya miaka mitano mitano.

Kwa kuwa Mheshimiwa sana CAG aliyepo Prof. Assad uteuzi wake ulianza rasmi baada ya kuteuliwa na Rais Kikwete tar 5 November, 2014 basi miaka yake mitano itaisha mwaka huu November 5, 2019.

Kwa kuwa hakuna ubishi kuwa mtu huyu ni mwadilifu na mbobezi. Kwa kuwa hakuna mashaka kuwa CAG aliyepo amefanya kazi iliyotukuka iliyofanya mpaka UN wakampatia sifa, Je Mheshimiwa Rais atakuwa tayari kumuongezea mkataba wa miaka mingine mitano?

Wanajamvi au mnaonaje?
 
Prof. Asad atarudi UDSM kuendelea na ile kazi anayoipenda sana ya kunoa wahasibu wapya kwa maslahi ya taifa. Viva Prof. Asad aka Simba. Wasiompenda hawawezi kumwongezea muda wa kuwa CAG maana Prof. Asad siyo mtu wa kulamba viatu vya bwana mkubwa
 
Prof. Asad atarudi UDSM kuendelea na ile kazi anayoipenda sana ya kunoa wahasibu wapya kwa maslahi ya taifa. Viva Prof. Asad aka Simba. Wasiompenda hawawezi kumwongezea muda wa kuwa CAG maana Prof. Asad siyo mtu wa kulamba viatu vya bwana mkubwa

Ni mwanaume asiyetaka kudhalilisha taaluma yake yaani kutumiwa na mwanaume mwwenzake kama wale wengine wenye njaa
 
Prof. Asad atarudi UDSM kuendelea na ile kazi anayoipenda sana ya kunoa wahasibu wapya kwa maslahi ya taifa. Viva Prof. Asad aka Simba. Wasiompenda hawawezi kumwongezea muda wa kuwa CAG maana Prof. Asad siyo mtu wa kulamba viatu vya bwana mkubwa
Baada ya kustaafu haruhusiwi kufanya shughuri/kazi yoyote ya uma
CAG
DCI
DPP
Sheria ndio inataka hivyo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waungwana salaam.

Kwa mujibu wa katiba ikisomwa pamoja na Sheria ya ukaguzi wa umma ya mwaka 2008 Rais ndiye mwenye mamlaka ya kumteua mtanzania kuwa mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG. Mbali na sifa za kihasibu na ubobezi na uzoefu sifa nyingine ni lazima awe raia wa Tanzania kwa kuzaliwa.

Kwa mujibu wa kifungu cha 6 cha Sheria ya Ukaguzi wa Umma ya mwaka 2008 mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali atadumu kwa muda wa miaka 5 na anaweza kuongezewa mkataba wa kipindi kimoja tu kingine cha miaka mitano. Kwa maana hiyo sheria inaruhusu mkaguzi kukaa vipindi viwili tu vya miaka mitano mitano.

Kwa kuwa Mheshimiwa sana CAG aliyepo Prof. Assad uteuzi wake ulianza rasmi baada ya kuteuliwa na Rais Kikwete tar 5 November, 2014 basi miaka yake mitano itaisha mwaka huu November 5, 2019.

Kwa kuwa hakuna ubishi kuwa mtu huyu ni mwadilifu na mbobezi. Kwa kuwa hakuna mashaka kuwa CAG aliyepo amefanya kazi iliyotukuka iliyofanya mpaka UN wakampatia sifa, Je Mheshimiwa Rais atakuwa tayari kumuongezea mkataba wa miaka mingine mitano?

Wanajamvi au mnaonaje?

Sent using Jamii Forums mobile app

Acha ujinga weww hata UTOUH Alipewa sifa UN,ila assad mwizi alishirikiana na dau kufisadi nssf, ktk ripoti za audit jina lake lipo alinunua nyumba akiwa mjumbe wa board na member wa investment commitee nssf,
Hana uadilifu zaidi ya unafiki wa swala kwa shetani wake.OVER
 
Acha ujinga weww hata UTOUH Alipewa sifa UN,ila assad mwizi alishirikiana na dau kufisadi nssf, ktk ripoti za audit jina lake lipo alinunua nyumba akiwa mjumbe wa board na member wa investment commitee nssf,
Hana uadilifu zaidi ya unafiki wa swala kwa shetani wake.OVER
Boss chuki yako ipo deep sana hutapata bp mkuu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom