Prof. Muhongo kutoka si suluhisho: Tatizo mikataba ikoje?

CCM tuache kuzuga kusahau. Tuache kuzuga kusifu uamuzi wa Rais uliochelewa na kuuita wa uthubutu bila ya kuona soni ya historia. Tuache kuzuga kuwa kuweka sawa uchimbaji wa madini ni sera za CCM.

Kwa anachofanya sasa Rais,kila mpendanchi anakipongeza. Kila mpendanchi anamuunga mkono Rais katika kusafisha sekta ili nchi ifaidike. Nchi inatamani kubaki na maendeleo kupitia uchimbaji. Kwa uamuzi wa Rais,wapendanchi tupo pamoja naye na kumtia shime.

Uwazi na uhalali katika sekta ya madini imekuwa ajenda ya wapinzani miaka nenda rudi. Wapinzani,pamoja na kuwa wachache Bungeni,wameshupalia uwazi wa mikataba ya madini na namna nchi inavyofaidika. Wapinzani wa enzi hizo Bungeni wakiongozwa na Dr. Slaa walishikia bango suala hilo

Wapinzani walibezwa na kutwezwa.CCM ikatumia wingi wetu Bungeni kukejeli,kuponda bila kupenda na kuchanachana kwa laana hoja za haja za wapinzani kuhusu madini. Zitto akalipua Buzwagi. Akasakamwa nusu ya kuhama. Wabunge wa CCM wakasema kwa kuhema kutetea usiri wa mikataba ya madini

Leo,wanampongeza Rais bila soni. Lahaula! Inashangaza na kuduwaza. Kwanini wapinzani wasipongezwe? WanaCCM wenzangu,tunaposhabikia sasa kauli na uamuzi wa Rais na Mwenyekiti wetu,tuwe na soni na kiasi. Mwaka 1997,sheria kuhusu uwekezaji na madini zilipitishwa kwa Hati ya Dharura. Upesiupesi bila wasiwasi. Leo,zinatugharimu.Tunachekesha kujifanya tunafanya mema sasa kwa taifa.

Hakika,opposition deserves credits for what is happening now nchini. Aibu na lawama na iwe kwetu wanaCCM!

Bastola ya nini tena jamani!?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Songea,Ruvuma)

Rafiki inaonyesha jinsi CCM ilivyojaza kizazi cha kusifia bila kuhoji.Kizazi cha Chuki na ubaguzi.Kizazicha kufikiria tumbo kwanza mengine baadaye.

Lakini cha kushangaza tuansikia yule aliyekuwa Mwanasheria nguli wa wizara hiyo ambaye ndiye Naibu waziri leo anapewa ufull Naibu,halafu wale akina wakurugenzi wametumbuliwa hii nayo naona ni Changa la Macho.Naona ni mahali tu Mwenyekiti anatafutia kick.

Au yawezekana na yeye anatafuta mahali pakupiga mirahaba yake kama wenyeviti waliopita,maana ndiyo ADA na HULKA ya Chama chetu kikongwe kabisa kisicho na haya aka CCM
 
Nchi hii ni mojawapo ya nchi barikiwa sana duniani.imekua na kila kitu chakumfanya binadam na vilivyomo viweze kuishi raha mstarehe ila kuna jambo moja najiuliza sipati majibu.Hivi binadam wanaoishi kwenye hii nchi tuna shida gani.Toka ripoti ya makanikia ya mchanga kutolewa nimekua nikisikia nakusoma maoni ya watu mbali mbali toka vyanzo tofauti tofauti.Na maoni mengi yamekua yakipongeza hatua zilizochukuliwa na mheshimiwa raisi ila wanaonishangaza ni wale wanaowaita kampuni ya acacia majina ya ajabu kua ni majizi makubwa.sasa mimi najiuliza kua je hiyo kampuni ilikuja hapa kwetu kuchimba ayo madini wakiwa na bunduki na vifaru vyakijeshi.bila shaka jibu ni hapana,sasa kama jibu ni hapana imekuaje tukaibiwa kwa kipindi chote hicho wakati serikali na vyombo vyake vyote vya ulinzi na usalama vilikuwepo,bunge lilikuwepo,mahakama ilikuepo,vikao vya baraza la mawaziri vilikuepo na wananchi tulikuepo tena kwenye nchi yenye amani yakutosha.Mimi nadhani kuwashambulia acacia nikujisahaulisha tu mapungufu yetu kwa muda kwasababu katika mazingira kama hayo inaonyesha wazi waliotuibia ni waswahili wenzetu na tuko nao hapa hapa nchini.Kwaiyo badala yakupiga vigele gele nakuishutum acacia lazima tujiulize na sisi kama watanzania tumeshiriki kiasi gani kuwasaidia hao acacia kutuibia uku tukiona.Kwaiyo hebu tubadilike.Linapokuja swala la kitaifa tuache porojo za vyama na tulishughulikie kwa pamoja kwasababu haya mambo tunayoangaika nayo leo hayakuanza leo wala jana na wako watanzania wenzetu waliopaza sauti zao ila hatukuwasapot kwasababu vichwa vyetu vilikua vinawaza vyama badala ya taifa matokeo yake ndo haya kuja kuangaika na mchanga baada ya miaka 17 kupita.Kwaiyo pamoja na mheshimiwa rais kuthubutu kulianzisha ili swala sisi kama wananchi inatakiwa tupaze sauti zetu ili tupate mifumo bora yakusimamia rasilimali zetu na huko hatuwezi kufika bila kwanza kufukua makaburi.Tafakari.
 
Sikatai kuwa tatizo yawezekana ni mikataba. Lakini sidhani katika hiyo mikataba, ni pamoja na waziri kushindwa kusimamia vyombo vyake kama TMAA kutimiza wajibu wake. Sidhani sera ingetaja mwaka 2009 kuwa ijengwe Smelta Tanzania akazuiliwa asifanya. Sidhani kama ni mkataba kukaaa na skana isiyoona chochote bandarini, Sidhani kama ni mkataba TMAA kuchukua sampuli kuondoka na kuwaacha wageni wakifanya watakalo. Sidhani kama ni mkataba kuwa wawe na makontainer ya tan 22 lakini waandike tan 20. Sidhani kama ni mkataba kuwa na madini ya chuma, n,k isiyolipiwa. Jamani tuache uchuro kwenye hii ishu. Unless wewe ni wale wanufaika au umetumwa kudhoofisha jitihada za mheshimiwa raisi.
Ona walichokuwa wanafanya jana, wanamzuia mkuu wa mkoa kuingia mgodini Bulyanhulu, jee hiyo jeuri iko kwenye mkataba. Kama ndio, mbona alipoenda mgodi mwingine Buzwagi wa kampuni hiyohiyo amepelekwa hadi strong room na waandishi wa habari wakapiga picha dhahabu. Mwaka huu mtanyooka tu. Hamjui power ya kiongozi wa nchi.
 
Nimefatilia hili sakata la mchanga na ripoti iliyotolewa.

Nina maswali mengi sana ya kujiuliza;

1) Kwani Muhongo akitoka ndo suluhisho la kutoibiwa rasilimali zetu? Je, mikataba inasemaje kuhusu kusafirisha michanga nje ya nchi?

2) Hivi haya yanayoendelea kwenye hii nchi hasa katika masuala ya madini na rasilimali zetu hawa viongozi wa CCM waliopo walikuwa hawayajui?

3) Hivi ni Muhongo ndo alisaini hii mikataba ya madini na wawekezaji?

4) Aliesaini hii mikataba ya madini yupo nchini? Au alishatangulia mbele ya haki? Mi nadhani hapa mheshimiwa chonde chonde usimtoe huyu jamaa.

Suluhisho la hii wizara, na chanzo chote cha yanayotokea ni ubovu wa mikataba iliyopo. Nadhani turudi kwenye tatizo bila kumwajibisha yeyote.
Lakini tume itakayowasilisha ripoti kuhusu mikataba na sheria bado ipo kazini.
 
Mkuu huu sio muda wa kumtafuta mchawi maana we all know that toka nchi ipate uhuru ni chama kimoja tu kipo madarakani CCM. They didn't do it out of their senses. Urasimu uliokithiri uliojengeka kama utamaduni wetu ndo uliotufikisha hapa. Leo hii ukienda tu pale emigration ukapata passport kwa bei ya kawaida 50,000 utaona kama ni muugiza. Hii ni kutokana na utamaduni ambao tuliuishi kwa kutojali nchi na kuzidisha ubinafsi. JPM nisiseme CCM, kwa sasa anatutoa huko.
Kwa hali hiyo huoni kama tatizo ni mfumo?
Mambo yote hayo yalishapigiwa kelele sana bungeni na bunge hilo hilo ambalo mh alikuwemo!
Bila weledi wa bunge,kwa kupitisha mambo yao kwa maelekezo ya vikao vyao vya ndani,mhimu wabunge wa CCM waamke ili waisimamie serikali na ninaamini tutakuwa tunalijenga taifa.
 
Kama kuna watu wamepigwa za uso na JPM basi ni wabunge wa CCM maana hawa ndiyo walikuwa wanapitisha sheria mbovu za madini ambazo ndiyo zimezaa mikataba hii ya kinyonyaji, wewe kwa vile ni wa ukoo wa panya akili zimehifadhiwa kwenye kibuyu pale Lumumba ndiyo maana bila aibu unaandika upuuzi huu.
Acha hasira.
 
huwa unaiweka wapi?

Hivi unawezaje kuzungumzia hali ya sasa bila kumtaja Sumaye,? Je, nmeshamchukulia hatua gani mpaka sasa zaidi ya kumuonhezea vyeo
Mkuu umenikumbusha kitu.. Kweli sumaye si ndo alikuwa waziri mkuu kipindi mikataba hii inapitishwa? Dah, chadema wamefanya faulu kuokota hawa jamaa
 
Muhongo katolewa kama mbuzi wa kafara tu., mimi naona kama vile serikali either haimjui adui au chanzo cha haya yote au inamjua na inapretend kutokumjua kwa sababu inayozijua yenyewe.. tutafukuza mawaziri kila awamu ila bila upitiaji wa mikataba hii inayotukandamiza hatutabadilisha chochote., sidhani kama kuna nia ya dhati huku raisi mwenyewe alishasema marais waliopita waachwe wapumzike huku tukijua fika wana mengi sana ya kujibu kuhusu usainishaji wa mikataba hii., I don't see any seriousness hapa
 
Sizonje sasa hivi anaanzisha matukio ili kupoteza muda ili 2020 ifike, maana ameshafail, tumaini lake liko kwenye kuiba kura tu, ukawa msilale maana pia anataka kuwasahurisha ili msije na mbinu za kukabiliana naye muda ukifika
Atashinda. Tatizo kule lowasa na sumaye pia wamechangia kutufikisha hapa.
 
Rafiki inaonyesha jinsi CCM ilivyojaza kizazi cha kusifia bila kuhoji.Kizazi cha Chuki na ubaguzi.Kizazicha kufikiria tumbo kwanza mengine baadaye.

Lakini cha kushangaza tuansikia yule aliyekuwa Mwanasheria nguli wa wizara hiyo ambaye ndiye Naibu waziri leo anapewa ufull Naibu,halafu wale akina wakurugenzi wametumbuliwa hii nayo naona ni Changa la Macho.Naona ni mahali tu Mwenyekiti anatafutia kick.

Au yawezekana na yeye anatafuta mahali pakupiga mirahaba yake kama wenyeviti waliopita,maana ndiyo ADA na HULKA ya Chama chetu kikongwe kabisa kisicho na haya aka CCM
Sina jibu la hilo mkuu. Hiyo ni dhana tu.
 
Nimefatilia hili sakata la mchanga na ripoti iliyotolewa.

Nina maswali mengi sana ya kujiuliza;

1) Kwani Muhongo akitoka ndo suluhisho la kutoibiwa rasilimali zetu? Je, mikataba inasemaje kuhusu kusafirisha michanga nje ya nchi?

2) Hivi haya yanayoendelea kwenye hii nchi hasa katika masuala ya madini na rasilimali zetu hawa viongozi wa CCM waliopo walikuwa hawayajui?

3) Hivi ni Muhongo ndo alisaini hii mikataba ya madini na wawekezaji?

4) Aliesaini hii mikataba ya madini yupo nchini? Au alishatangulia mbele ya haki? Mi nadhani hapa mheshimiwa chonde chonde usimtoe huyu jamaa.

Suluhisho la hii wizara, na chanzo chote cha yanayotokea ni ubovu wa mikataba iliyopo. Nadhani turudi kwenye tatizo bila kumwajibisha yeyote.
Udanganyifu nao unasingizia mikataba?
 
Tundu Lisu anaongea kama mwanasiasa zaidi kuliko kuwa mwanasheria. Kisheria mkataba wowote ule unaweza kuwa reviewed na ku waive baadhi ya mashsrti na vigezo baada ya kugundulika na pande husika kuwa uko UNFAIR kwa upande moja wapo. Mkataba ni makubaliano ya pande husika.Hivyo makubaliano hayo yanaweza kuboreshwa muda wowote na pande husika. Kuhusu mikataba mibaya kama ya uchimbaji madini iliyopo, nchi inaweza kuamua kuivunja kwa MASILAHI YA UMMA ikiwa upande wa wawekezaji haupo tayari kuboresha terms and conditions ambazo ni unfair. Na hii ipo in practice dunia nzima. Vitisho anavyotoa Tundu Lisu ni vya kipuuzi na kisiasa zaidi kuliko uhalisia na kishetia.Kwani mikataba hiyo ikivunjwa watatufanya nini? Nothing.Ni hofu tu. Tz ni DOLA huru kama ilivyo nchi nyingine. Hao wazungu sasa wako busy kupambana na UGAIDI. Attentition yao yote iko huko siyo Afrika tena. Zimbabwe ilifanya maamuzi magumu hayo mpaka leo bado ipo na Mgabe yupo.Hofu hizo zilikuwa relevant ZAMANI.Siyo leo.Kumbuka kuna nchi kama China,India,Russia nk ambazo zinapenda kuwekeza Afrika. Wanasiasa acheni kuwatisha na kuwarubuni wanachi.Magufuli chapa kazi kulinda masilahi mapana ya nchi. Usiyumbishwe na empty propaganda za akina Lissu waliochakaa kisiasa na kuamua kuunga mkono uporaji na uharamia wa kiwango cha juu namna hii.God bless JPM, God bless TZ. By the learned counsel.
 
New-Doc-2017-05-27_21.jpg



Ripoti fake


Swissme
 
Kwa hiyo hali iliyoko Zimbabwe wewe unaona iko sawa? Usiombee ya Zimbabwe yafike Tanzania, utakosa hata uwezo wa kuandika upuuzi wako humu.
 
Tundu Lisu anaongea kama mwanasiasa zaidi kuliko kuwa mwanasheria. Kisheria mkataba wowote ule unaweza kuwa reviewed na ku waive baadhi ya mashsrti na vigezo baada ya kugundulika na pande husika kuwa uko UNFAIR kwa upande moja wapo. Mkataba ni makubaliano ya pande husika.Hivyo makubaliano hayo yanaweza kuboreshwa muda wowote na pande husika. Kuhusu mikataba mibaya kama ya uchimbaji madini iliyopo, nchi inaweza kuamua kuivunja kwa MASILAHI YA UMMA ikiwa upande wa wawekezaji haupo tayari kuboresha terms and conditions ambazo ni unfair. Na hii ipo in practice dunia nzima. Vitisho anavyotoa Tundu Lisu ni vya kipuuzi na kisiasa zaidi kuliko uhalisia na kishetia.Kwani mikataba hiyo ikivunjwa watatufanya nini? Nothing.Ni hofu tu. Tz ni DOLA huru kama ilivyo nchi nyingine. Hao wazungu sasa wako busy kupambana na UGAIDI. Attentition yao yote iko huko siyo Afrika tena. Zimbabwe ilifanya maamuzi magumu hayo mpaka leo bado ipo na Mgabe yupo.Hofu hizo zilikuwa relevant ZAMANI.Siyo leo.Kumbuka kuna nchi kama China,India,Russia nk ambazo zinapenda kuwekeza Afrika. Wanasiasa acheni kuwatisha na kuwarubuni wanachi.Magufuli chapa kazi kulinda masilahi mapana ya nchi. Usiyumbishwe na empty propaganda za akina Lissu waliochakaa kisiasa na kuamua kuunga mkono uporaji na uharamia wa kiwango cha juu namna hii.God bless JPM, God bless TZ. By the learned counsel.
Tatizo nyinyi mabashite hamwezi kumwelewa Lissu kwa sababu akili zenu ni ndogo kama punje ya haradali!
 
Tundu Lisu anaongea kama mwanasiasa zaidi kuliko kuwa mwanasheria. Kisheria mkataba wowote ule unaweza kuwa reviewed na ku waive baadhi ya mashsrti na vigezo baada ya kugundulika na pande husika kuwa uko UNFAIR kwa upande moja wapo. Mkataba ni makubaliano ya pande husika.Hivyo makubaliano hayo yanaweza kuboreshwa muda wowote na pande husika. Kuhusu mikataba mibaya kama ya uchimbaji madini iliyopo, nchi inaweza kuamua kuivunja kwa MASILAHI YA UMMA ikiwa upande wa wawekezaji haupo tayari kuboresha terms and conditions ambazo ni unfair. Na hii ipo in practice dunia nzima. Vitisho anavyotoa Tundu Lisu ni vya kipuuzi na kisiasa zaidi kuliko uhalisia na kishetia.Kwani mikataba hiyo ikivunjwa watatufanya nini? Nothing.Ni hofu tu. Tz ni DOLA huru kama ilivyo nchi nyingine. Hao wazungu sasa wako busy kupambana na UGAIDI. Attentition yao yote iko huko siyo Afrika tena. Zimbabwe ilifanya maamuzi magumu hayo mpaka leo bado ipo na Mgabe yupo.Hofu hizo zilikuwa relevant ZAMANI.Siyo leo.Kumbuka kuna nchi kama China,India,Russia nk ambazo zinapenda kuwekeza Afrika. Wanasiasa acheni kuwatisha na kuwarubuni wanachi.Magufuli chapa kazi kulinda masilahi mapana ya nchi. Usiyumbishwe na empty propaganda za akina Lissu waliochakaa kisiasa na kuamua kuunga mkono uporaji na uharamia wa kiwango cha juu namna hii.God bless JPM, God bless TZ. By the learned counsel.
Umenena vyema kitaaluma.
 
Back
Top Bottom