Prof. Muhamad Yunus: Umasikini mtauona makumbusho

OLS

JF-Expert Member
Oct 12, 2019
419
669
Muhamad Yunus Muasisi wa mfumo wa kisasa wa mikopo midogo midogo, Micro-finance na Micro-Credit, alizaliwa Juni 28, 1940

Profesa huyu alitamani kuupeleka umasikini wa India kwenye makumbusho, yani kumfanya kila mtu kuwa tajiri na umasikini ukabaki kwenye makumbusho na akaamini vizazi vijavyo vitasimuliana kuhusu umasikini bila kuujua umasikini wenyewe.

Kwa kipindi chake aliangalia namna ya kuwasaidia masikini kwa mikopo, kwa kuwa mikopo ya awali ilikuwa inataka dhamana kubwa kama nyumba, shamba kiwanja au mali yoyote.

Muhamad aliona kwa watu masikini ambao wanauhitaji mkubwa wa mikopo hawana mali ila IMANI, ‘trust’ kati yao, na akatumia Imani hiyo kama kigezo cha kutoa mikopo kwa masikini.

Ndipo kukaja mfumo wa kuwakopesha watu wakiwa katika vikundi, ili kila mtu awe mlinzi wa mwenzie kwa Imani ya kwamba wote hawawezi kukimbia na pia wenyewe wanajuana kwamba nani anafaa kuaminiwa na asiyefaa kuaminiwa.

Mwaka 1983 ndipo muhamad yunus alianzisha Gramen Bank ili kuwakomboa wahindi kutoka kwenye umasikini.

Miaka ya mwanzo mfumo huo ulionyesha kufanikiwa kwa azma ya yunus ya kuuona umasikini ukielekea makumbusho, lakini ghafla hali ikabadilika baada ya Micro Finances kuvamiwa na mafisi wabinafsi walitaka faida Zaidi na sio kuwaondolea umasikini watu walio wengi.

Tafiti zimeonyesha umasikini ulipungua kwa kasi tangu kuanzishwa kwa Gramen bank, pia maeneo mbalimbali ambayo yali-adapt mfumo huo wa ukopeshaji na umasikini ukapungua.

Lakini ghafla kuanzia mwaka 2000 kuja juu, mafisi hao wakafanya umasikini wa masikini kuongezeka badala ya kupungua kama ambavyo Muhamad Yunus alivyowaza awali.

NB: Dhumuni la Makala haya sio kujadili kufeli au kufaulu kwa MicroFinance bank, lakini ni kuiangazia ndoto kubwa ya Muhamad Yunus ya kuupeleka umasikini kwenye makumbusho.

Je na sisi tuna wachumi/bankers wenye mawazo ya kuupeleka umasikini kwenye makumbusho?



Signed

Oedipus
 
Umechanganya mambo mengi kwenye mada moja, sijajajua unataka watu wajadili lipi ?

Anyway Prof Mohammed Yunus ni raia wa Bangladesh na hata Grameen Bank iliasisiwa Bangladesh siyo INDIA
 
Umechanganya mambo mengi kwenye mada moja, sijajajua unataka watu wajadili lipi ?

Anyway Prof Mohammed Yunus ni raia wa Bangladesh na hata Grameen Bank iliasisiwa Bangladesh siyo INDIA
Ukisoma utaelewa nini naongea, hiyo ya Bangaladesh, Bombay sijui wapi mimi naweka kapu moja
 
Kuna sehemu nilisoma mifumo hii ilianzia ujerumani, huenda nachanganya mambo.
Nitarudi tena nikisoma ile nyaraka.
 
Kuna sehemu nilisoma mifumo hii ilianzia ujerumani, huenda nachanganya mambo.
Nitarudi tena nikisoma ile nyaraka.
Mfumo wa micro finance una phases,

Classical ilianza kitambo, ila huu wa kutumia imani, Modern micro finance model ameandika huyu mwamba
 
Muhamad Yunus Muasisi wa mfumo wa kisasa wa mikopo midogo midogo, Micro-finance na Micro-Credit, alizaliwa Juni 28, 1940

Profesa huyu alitamani kuupeleka umasikini wa India kwenye makumbusho, yani kumfanya kila mtu kuwa tajiri na umasikini ukabaki kwenye makumbusho na akaamini vizazi vijavyo vitasimuliana kuhusu umasikini bila kuujua umasikini wenyewe.

Kwa kipindi chake aliangalia namna ya kuwasaidia masikini kwa mikopo, kwa kuwa mikopo ya awali ilikuwa inataka dhamana kubwa kama nyumba, shamba kiwanja au mali yoyote.

Muhamad aliona kwa watu masikini ambao wanauhitaji mkubwa wa mikopo hawana mali ila IMANI, ‘trust’ kati yao, na akatumia Imani hiyo kama kigezo cha kutoa mikopo kwa masikini.

Ndipo kukaja mfumo wa kuwakopesha watu wakiwa katika vikundi, ili kila mtu awe mlinzi wa mwenzie kwa Imani ya kwamba wote hawawezi kukimbia na pia wenyewe wanajuana kwamba nani anafaa kuaminiwa na asiyefaa kuaminiwa.

Mwaka 1983 ndipo muhamad yunus alianzisha Gramen Bank ili kuwakomboa wahindi kutoka kwenye umasikini.

Miaka ya mwanzo mfumo huo ulionyesha kufanikiwa kwa azma ya yunus ya kuuona umasikini ukielekea makumbusho, lakini ghafla hali ikabadilika baada ya Micro Finances kuvamiwa na mafisi wabinafsi walitaka faida Zaidi na sio kuwaondolea umasikini watu walio wengi.

Tafiti zimeonyesha umasikini ulipungua kwa kasi tangu kuanzishwa kwa Gramen bank, pia maeneo mbalimbali ambayo yali-adapt mfumo huo wa ukopeshaji na umasikini ukapungua.

Lakini ghafla kuanzia mwaka 2000 kuja juu, mafisi hao wakafanya umasikini wa masikini kuongezeka badala ya kupungua kama ambavyo Muhamad Yunus alivyowaza awali.

NB: Dhumuni la Makala haya sio kujadili kufeli au kufaulu kwa MicroFinance bank, lakini ni kuiangazia ndoto kubwa ya Muhamad Yunus ya kuupeleka umasikini kwenye makumbusho.

Je na sisi tuna wachumi/bankers wenye mawazo ya kuupeleka umasikini kwenye makumbusho?



Signed

Oedipus
Hivi wenzetu mnatolea wapi hizi mada , maana mpaka nchi mnazokosea au ndio hivyo Jiografia haikua kipaumbele kwako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom