Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,498
- 51,090
PROF. MKUMBO, MWAMBE, POKEENI LAWAMA HIZI KISHA MJIPIME
Na Bollen Ngetti
SIJUI kama kuna ukweli katika usemi huu. Kwamba "kenge hasikii hadi umtoe damu au aone kwa macho". Eti hata kama anaona na kukutazama usoni lakini ni kiziwi asiyesikia hata jambo la hatari.
Naam. Vivyo hivyo katika Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan kuna baadhi ya viongozi pamoja na kelele za kutoboa ngoma ya masikio lakini wao hawasikii chochote. Kundi hili wamo rafiki yangu Prof. Kitila Mkumbo (Waziri wa Viwanda & Biashara) na Geoffrey Mwambe, Waziri katika ofisi ya Rais Uwekezaji. Mkumbo na Mwambe hawasikii!
Siandiki makala haya kuwashambulia Mkumbo na Mwambe, hapana. Naandika kuwatoa damu labda wakaelewa kama kenge.
Rais Samia anapasuka koo kuhamasisha suala zima la Biashara na Uwekezaji nchini ili kupunguza saratani ya ajira hususan kwa vijana. Samia anatamani nchi ipae kiuchumi. Huyu mama halali akiwahangaikia Watanzania ndani na nje ya nchi kusaka wawekezaji kama ilivyo sera mujarab kwa dunia nzima. Kwamba ili kuinuka kiuchumi katika dunia ya sasa ni lazima kuwepo na ndoa halali kati ya Serikali na sekta binafsi. Kwamba isiwepo hata dakika moja ya kupoteza linapokuja suala la uwekezaji na Biashara. Lakini Mkumbo na Mwambe hawasikii. Ni viziwi!
Hebu tazama. Ukienda Bagamoyo mkoa wa Pwani eneo la Budebude-Kitopeni shamba namba 983 lenye ukubwa wa hekari 150 mali halali ya mwekezaji Slim Slim toka miaka ya Tanganyika hadi Tanzania limekaa bila shughuli yoyote.
Hili eneo ni miongoni mwa maeneo ya uwekezaji hususan Viwanda, EPZA miaka 15 iliyopita. Slim Slim ambaye pia ni mmiliki wa Green Park Village Hotel ametaka kujenga viwanda zaidi ya 12 na kutoa ajira za moja kwa moja 500 ili kukidhi kelele anazopiga Rais Samia lakini kwa uziwi wa Mkumbo na Mwambe huyu bwana Slim amewekewa ngumu pamoja na kukidhi vigezo vyote kwa maana ya vyote pale TIC alikotoka Mwambe kabla ya kuwa Waziri. Unajiuliza, iko wapi dhana ya uwekezaji katika viwanda na Biashara? Mnamuelewa Samia?
Slim amekamilisha kujenga nyumba (apartments) watakazoishi wataalamu wake wa ndani na nje lakini mwaka wa pili haijulikani Kati ya EPZA, TIC, Mkumbo na Mwambe nani kambale na nani ni pegere. Yani eneo limetengwa kwa uwekezaji na Ujenzi wa Viwanda, tayari mwekezaji yuko hapa, tena mzawa anataka kujenga viwanda (si dalali), ardhi ni yake anayolipia kodi miaka yote, masharti na taratibu ametimiza lakini anaambiwa "no subiri". Asubiri nini na kelele za Samia kutaka uchumi ukue kwa haraka? Urasimu huu unatoka wapi? Mkumbo na Mwambe mnamsikia Rais Samia au mpaka mkatwe wembe muone damu ndipo muelewe maana uwekezaji "chap-chap"? Tunapoteza muda na pesa kiasi gani kuendelea kuwachelewesha wawekezaji kama kina Slim? Mkumbo na Mwambe mnamwelewa Rais Samia lakini?
Nasema haya maana mwishoni mwa wiki nilifanya ziara ukanda wa Bagamoyo. Viwanda vingi sana vimekufa na kufungwa baada tu ya Magufuli kuingia madarakani. Wawekezaji walitimka. Hata Slim yuko mbioni kutimka kwa urasimu huu. Mkumbo na Mwambe mpigwe na nini utosini msikie anachopigania Rais Samia?
Tunaona baada tu ya Samia kutwaa madaraka Tanzania imechupa kutoka nafasi ya 15 (2019) hadi nafasi ya 10 (2021) kwa nchi zenye masharti nafuu kuwekeza barani Afrika kwa mujibu wa ripoti ya Rand Merchant Bank ya mwezi huu. Lakini kwa makwazo kama haya ya kina Mkumbo na Mwambe tutawezaje kutoka 10 kwenda 7 kama si kurudi 20 na pengine kuburuta mkia? Mkumbo na Mwambe mnamwelewa Rais Samia?
Kituko kingine ni hiki: ukija kuwekeza Tanzania unapitia TIC ambako sasa wameweka "One Stop Facilitation Center". Well and good. Lakini tazama kinachotokea. Mwekezaji anapeleka andiko lake, kama mgeni anathibitisha kuwa na dola 500 au zaidi benki. Kama mzawa ni dola 100. Anapewa ardhi na mahitaji mengine yote. Anajiondokea kwenda kuwekeza. Cha ajabu mwekezaji huyu hatembelewi na TIC kuona na kujiridhisha je, amewekeza alichokiomba?
Matokeo yake, nimekuta aliyeomba kuwekeza usindikaji wa matunda akiuza chuma chakavu. Nimekuta aliyeomba TIC kuwekeza kwenye usindikaji wa samaki akilima tikiti maji nakadhali. Hii ndio maana utasikia Waziri akijigamba "TIC imeandikisha uwekezaji wenye thamani ya Trilioni kadhaa" lakini what is happening in the ground ni hewa. Mkumbo na Mwambe mnamwelewa na Rais Samia?
Mwekezaji anasema biashara yangu itatoa ajira ya vijana 1000 hivi tumeenda huko viwandani tukawapanga vijana hao na kuwahesabu kwa kidole moja hadi 1000? Kwa tunajifungia kwenye viyoyozi eti mambo kwa digitali, upuuzi mtu. Tunapigwa. Tunatapeliwa viwanda vingi ni hewa kwa hisani ya Mkumbo na Mwambe. Tuwe serious basi Kaka zangu Mkumbo na Mwambe. Tuvute wote tusivutane. Hapa tuache mjadala na ushindani wa hoja. Nendeni field mkivaa viatu kazi msiuze sura na maneno mengi kwenye TV. Hapo mtakuwa mmemuelewa Rais Samia na nia ya Watanzania. Tupunguze porojo. Sihitaji utetezi wenu. Pigeni kazi matokeo yaonekane hadharani si kwenye makaratasi. Ova!
#MguseMamaNinuke
Na Bollen Ngetti
SIJUI kama kuna ukweli katika usemi huu. Kwamba "kenge hasikii hadi umtoe damu au aone kwa macho". Eti hata kama anaona na kukutazama usoni lakini ni kiziwi asiyesikia hata jambo la hatari.
Naam. Vivyo hivyo katika Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan kuna baadhi ya viongozi pamoja na kelele za kutoboa ngoma ya masikio lakini wao hawasikii chochote. Kundi hili wamo rafiki yangu Prof. Kitila Mkumbo (Waziri wa Viwanda & Biashara) na Geoffrey Mwambe, Waziri katika ofisi ya Rais Uwekezaji. Mkumbo na Mwambe hawasikii!
Siandiki makala haya kuwashambulia Mkumbo na Mwambe, hapana. Naandika kuwatoa damu labda wakaelewa kama kenge.
Rais Samia anapasuka koo kuhamasisha suala zima la Biashara na Uwekezaji nchini ili kupunguza saratani ya ajira hususan kwa vijana. Samia anatamani nchi ipae kiuchumi. Huyu mama halali akiwahangaikia Watanzania ndani na nje ya nchi kusaka wawekezaji kama ilivyo sera mujarab kwa dunia nzima. Kwamba ili kuinuka kiuchumi katika dunia ya sasa ni lazima kuwepo na ndoa halali kati ya Serikali na sekta binafsi. Kwamba isiwepo hata dakika moja ya kupoteza linapokuja suala la uwekezaji na Biashara. Lakini Mkumbo na Mwambe hawasikii. Ni viziwi!
Hebu tazama. Ukienda Bagamoyo mkoa wa Pwani eneo la Budebude-Kitopeni shamba namba 983 lenye ukubwa wa hekari 150 mali halali ya mwekezaji Slim Slim toka miaka ya Tanganyika hadi Tanzania limekaa bila shughuli yoyote.
Hili eneo ni miongoni mwa maeneo ya uwekezaji hususan Viwanda, EPZA miaka 15 iliyopita. Slim Slim ambaye pia ni mmiliki wa Green Park Village Hotel ametaka kujenga viwanda zaidi ya 12 na kutoa ajira za moja kwa moja 500 ili kukidhi kelele anazopiga Rais Samia lakini kwa uziwi wa Mkumbo na Mwambe huyu bwana Slim amewekewa ngumu pamoja na kukidhi vigezo vyote kwa maana ya vyote pale TIC alikotoka Mwambe kabla ya kuwa Waziri. Unajiuliza, iko wapi dhana ya uwekezaji katika viwanda na Biashara? Mnamuelewa Samia?
Slim amekamilisha kujenga nyumba (apartments) watakazoishi wataalamu wake wa ndani na nje lakini mwaka wa pili haijulikani Kati ya EPZA, TIC, Mkumbo na Mwambe nani kambale na nani ni pegere. Yani eneo limetengwa kwa uwekezaji na Ujenzi wa Viwanda, tayari mwekezaji yuko hapa, tena mzawa anataka kujenga viwanda (si dalali), ardhi ni yake anayolipia kodi miaka yote, masharti na taratibu ametimiza lakini anaambiwa "no subiri". Asubiri nini na kelele za Samia kutaka uchumi ukue kwa haraka? Urasimu huu unatoka wapi? Mkumbo na Mwambe mnamsikia Rais Samia au mpaka mkatwe wembe muone damu ndipo muelewe maana uwekezaji "chap-chap"? Tunapoteza muda na pesa kiasi gani kuendelea kuwachelewesha wawekezaji kama kina Slim? Mkumbo na Mwambe mnamwelewa Rais Samia lakini?
Nasema haya maana mwishoni mwa wiki nilifanya ziara ukanda wa Bagamoyo. Viwanda vingi sana vimekufa na kufungwa baada tu ya Magufuli kuingia madarakani. Wawekezaji walitimka. Hata Slim yuko mbioni kutimka kwa urasimu huu. Mkumbo na Mwambe mpigwe na nini utosini msikie anachopigania Rais Samia?
Tunaona baada tu ya Samia kutwaa madaraka Tanzania imechupa kutoka nafasi ya 15 (2019) hadi nafasi ya 10 (2021) kwa nchi zenye masharti nafuu kuwekeza barani Afrika kwa mujibu wa ripoti ya Rand Merchant Bank ya mwezi huu. Lakini kwa makwazo kama haya ya kina Mkumbo na Mwambe tutawezaje kutoka 10 kwenda 7 kama si kurudi 20 na pengine kuburuta mkia? Mkumbo na Mwambe mnamwelewa Rais Samia?
Kituko kingine ni hiki: ukija kuwekeza Tanzania unapitia TIC ambako sasa wameweka "One Stop Facilitation Center". Well and good. Lakini tazama kinachotokea. Mwekezaji anapeleka andiko lake, kama mgeni anathibitisha kuwa na dola 500 au zaidi benki. Kama mzawa ni dola 100. Anapewa ardhi na mahitaji mengine yote. Anajiondokea kwenda kuwekeza. Cha ajabu mwekezaji huyu hatembelewi na TIC kuona na kujiridhisha je, amewekeza alichokiomba?
Matokeo yake, nimekuta aliyeomba kuwekeza usindikaji wa matunda akiuza chuma chakavu. Nimekuta aliyeomba TIC kuwekeza kwenye usindikaji wa samaki akilima tikiti maji nakadhali. Hii ndio maana utasikia Waziri akijigamba "TIC imeandikisha uwekezaji wenye thamani ya Trilioni kadhaa" lakini what is happening in the ground ni hewa. Mkumbo na Mwambe mnamwelewa na Rais Samia?
Mwekezaji anasema biashara yangu itatoa ajira ya vijana 1000 hivi tumeenda huko viwandani tukawapanga vijana hao na kuwahesabu kwa kidole moja hadi 1000? Kwa tunajifungia kwenye viyoyozi eti mambo kwa digitali, upuuzi mtu. Tunapigwa. Tunatapeliwa viwanda vingi ni hewa kwa hisani ya Mkumbo na Mwambe. Tuwe serious basi Kaka zangu Mkumbo na Mwambe. Tuvute wote tusivutane. Hapa tuache mjadala na ushindani wa hoja. Nendeni field mkivaa viatu kazi msiuze sura na maneno mengi kwenye TV. Hapo mtakuwa mmemuelewa Rais Samia na nia ya Watanzania. Tupunguze porojo. Sihitaji utetezi wenu. Pigeni kazi matokeo yaonekane hadharani si kwenye makaratasi. Ova!
#MguseMamaNinuke