Prof. Mbele: Tundu Lissu haichafui nchi, kumsema Spika wa Bunge na Serikali sio kuichafua nchi. Hata Nyerere alisema CCM ni kansa

Ngaliba Dume

JF-Expert Member
Oct 6, 2010
1,710
3,669
Anaandika Profesa Joseph Mbele

Mimi ninaufahamu vizuri utamaduni wa vyuo vikuu vya Marekani, kwa sababu nilisomea kule na ninafundisha kule. Nimeshatoa mihadhara katika vyuo vingi, sio Marekani tu bali sehemu mbali mbali za dunia.

Ninavyosikiliza mahojiano na hotuba za Tundu Lissu ninafahamu fika kwamba ataamsha fikra za wasikilizaje wake kwa kiwango cha juu. Ninafahamu pia kwamba katika vyuo vya Marekani, hawamwaliki mtu kwa ajili ya kumsikiliza tu, bali pia kwa ajili ya kumpiga masuali. Mtu anatoa hotuba halafu anakalishwa kitimoto.

Tundu Lissu ni hodari kwa yote hayo. Wanaombeza hapa Tanzania wanajisumbua. Kwa kusema hivyo, simaanishi kwamba mawazo yangu ni sawa na ya Tundu Lissu. Kuna ambayo ninatofautiana naye.

Lakini kutofautiana mitazamo ndio utamaduni wa watu wanaofikiri. Ndio utamaduni wa watu walioelimika. Vyuo vikuu ni mahali ambapo tunatofautiana na kulumbana muda wote. Ni uhai wa vyuo vikuu. Ni uhai wa taaluma. Tunawajibika sisi waalimu kujenga tabia hiyo miongoni mwa wale tunaowafundisha.

Kuna haya madai kwamba Tundu Lissu anaichafua nchi. Binafsi, sijawawahi kuona popote au siku yoyote ambapo Tundu Lissu ameichafua nchi. Anazilalamikia mamlaka za nchi, kama vile serikali na Bunge. Lakini serikali si nchi. Bunge si nchi. Anapomshutumu Spika, haichafui Tanzania. Spika si Tanzania.

Ingekuwa vinginevyo, basi kwa jinsi Mwalimu Nyerere alivyoandika kitabu cha "Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania" tungesema kwamba ameichafua nchi. Mwalimu anaiponda CCM na serikali yake, hadi kutamka kwamba kuna kansa katika CCM. Hadi akasema kwamba alitamani kitokee chama cha upinzani kilicho bora kuliko CCM ili kishike nchi badala ya CCM. Lakini itakuwa ni upuuzi kusema kuwa Mwalimu Nyerere aliichafua nchi.

Binafsi, siku nitakapoona Tundu Lissu anaichafua nchi, sitamlazia damu. Lakini sijaona. Badala yake, nimemsikia akitangaza kwamba yuko tayari kuitumikia nchi katika nafasi ya uongozi, iwapo atapata ridhaa. Ameelezea kuwa akishika uongozi, ataweka utawala wa sheria, haki za binadamu, na demokrasia. Kila mwenye kuwania uongozi wa nchi ana haki na wajibu wa kutueleza ana malengo gani. Kwa hayo malengo yake, sioni mantiki yoyote ya kusema kuwa Tundu Lissu anaichafua nchi.
 
Hizi ndizo hoja za kisomi.
Prof.Mbele hongera sana.
CCM na wafuasi wao pamoja na vibaraka wengine rudieni kusoma huu uzi mara nyingi kadri inavyowezekana mpaka liwakae vichwani mwenu..
Balozi wetu kule Ujerumani naye alielewe hili jambo ni jambo la msingi sana na aache kukurupuka.
 
Anaandika Profesa Joseph Mbele

Mimi ninaufahamu vizuri utamaduni wa vyuo vikuu vya Marekani, kwa sababu nilisomea kule na ninafundisha kule. Nimeshatoa mihadhara katika vyuo vingi, sio Marekani tu bali sehemu mbali mbali za dunia.

Ninavyosikiliza mahojiano na hotuba za Tundu Lissu ninafahamu fika kwamba ataamsha fikra za wasikilizaje wake kwa kiwango cha juu. Ninafahamu pia kwamba katika vyuo vya Marekani, hawamwaliki mtu kwa ajili ya kumsikiliza tu, bali pia kwa ajili ya kumpiga masuali. Mtu anatoa hotuba halafu anakalishwa kitimoto.

Tundu Lissu ni hodari kwa yote hayo. Wanaombeza hapa Tanzania wanajisumbua. Kwa kusema hivyo, simaanishi kwamba mawazo yangu ni sawa na ya Tundu Lissu. Kuna ambayo ninatofautiana naye.

Lakini kutofautiana mitazamo ndio utamaduni wa watu wanaofikiri. Ndio utamaduni wa watu walioelimika. Vyuo vikuu ni mahali ambapo tunatofautiana na kulumbana muda wote. Ni uhai wa vyuo vikuu. Ni uhai wa taaluma. Tunawajibika sisi waalimu kujenga tabia hiyo miongoni mwa wale tunaowafundisha.

Kuna haya madai kwamba Tundu Lissu anaichafua nchi. Binafsi, sijawawahi kuona popote au siku yoyote ambapo Tundu Lissu ameichafua nchi. Anazilalamikia mamlaka za nchi, kama vile serikali na Bunge. Lakini serikali si nchi. Bunge si nchi. Anapomshutumu Spika, haichafui Tanzania. Spika si Tanzania.

Ingekuwa vinginevyo, basi kwa jinsi Mwalimu Nyerere alivyoandika kitabu cha "Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania" tungesema kwamba ameichafua nchi. Mwalimu anaiponda CCM na serikali yake, hadi kutamka kwamba kuna kansa katika CCM. Hadi akasema kwamba alitamani kitokee chama cha upinzani kilicho bora kuliko CCM ili kishike nchi badala ya CCM. Lakini itakuwa ni upuuzi kusema kuwa Mwalimu Nyerere aliichafua nchi.

Binafsi, siku nitakapoona Tundu Lissu anaichafua nchi, sitamlazia damu. Lakini sijaona. Badala yake, nimemsikia akitangaza kwamba yuko tayari kuitumikia nchi katika nafasi ya uongozi, iwapo atapata ridhaa. Ameelezea kuwa akishika uongozi, ataweka utawala wa sheria, haki za binadamu, na demokrasia. Kila mwenye kuwania uongozi wa nchi ana haki na wajibu wa kutueleza ana malengo gani. Kwa hayo malengo yake, sioni mantiki yoyote ya kusema kuwa Tundu Lissu anaichafua nchi.
Tatizo ma ccm ni kondoo yamezoea ndiyo mzee hawathubutu kuhoji
 
Anaandika Profesa Joseph Mbele

Mimi ninaufahamu vizuri utamaduni wa vyuo vikuu vya Marekani, kwa sababu nilisomea kule na ninafundisha kule. Nimeshatoa mihadhara katika vyuo vingi, sio Marekani tu bali sehemu mbali mbali za dunia.

Ninavyosikiliza mahojiano na hotuba za Tundu Lissu ninafahamu fika kwamba ataamsha fikra za wasikilizaje wake kwa kiwango cha juu. Ninafahamu pia kwamba katika vyuo vya Marekani, hawamwaliki mtu kwa ajili ya kumsikiliza tu, bali pia kwa ajili ya kumpiga masuali. Mtu anatoa hotuba halafu anakalishwa kitimoto.

Tundu Lissu ni hodari kwa yote hayo. Wanaombeza hapa Tanzania wanajisumbua. Kwa kusema hivyo, simaanishi kwamba mawazo yangu ni sawa na ya Tundu Lissu. Kuna ambayo ninatofautiana naye.

Lakini kutofautiana mitazamo ndio utamaduni wa watu wanaofikiri. Ndio utamaduni wa watu walioelimika. Vyuo vikuu ni mahali ambapo tunatofautiana na kulumbana muda wote. Ni uhai wa vyuo vikuu. Ni uhai wa taaluma. Tunawajibika sisi waalimu kujenga tabia hiyo miongoni mwa wale tunaowafundisha.

Kuna haya madai kwamba Tundu Lissu anaichafua nchi. Binafsi, sijawawahi kuona popote au siku yoyote ambapo Tundu Lissu ameichafua nchi. Anazilalamikia mamlaka za nchi, kama vile serikali na Bunge. Lakini serikali si nchi. Bunge si nchi. Anapomshutumu Spika, haichafui Tanzania. Spika si Tanzania.

Ingekuwa vinginevyo, basi kwa jinsi Mwalimu Nyerere alivyoandika kitabu cha "Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania" tungesema kwamba ameichafua nchi. Mwalimu anaiponda CCM na serikali yake, hadi kutamka kwamba kuna kansa katika CCM. Hadi akasema kwamba alitamani kitokee chama cha upinzani kilicho bora kuliko CCM ili kishike nchi badala ya CCM. Lakini itakuwa ni upuuzi kusema kuwa Mwalimu Nyerere aliichafua nchi.

Binafsi, siku nitakapoona Tundu Lissu anaichafua nchi, sitamlazia damu. Lakini sijaona. Badala yake, nimemsikia akitangaza kwamba yuko tayari kuitumikia nchi katika nafasi ya uongozi, iwapo atapata ridhaa. Ameelezea kuwa akishika uongozi, ataweka utawala wa sheria, haki za binadamu, na demokrasia. Kila mwenye kuwania uongozi wa nchi ana haki na wajibu wa kutueleza ana malengo gani. Kwa hayo malengo yake, sioni mantiki yoyote ya kusema kuwa Tundu Lissu anaichafua nchi.
Sawa unaeleweka kabisa isipokuwa siku hizi misamiati imebadirika siku hizi inategemea unaongea toka upande upi,hawa wazungu-
Lissu akipngea nao =MABEBERU
CCM/SERIKALI wakiongea nao = WASHIRIKA WA MAENDELEO.
NCHI YA WANAFIKI Ole nchi yangu!!!
 
Anaandika Profesa Joseph Mbele

Mimi ninaufahamu vizuri utamaduni wa vyuo vikuu vya Marekani, kwa sababu nilisomea kule na ninafundisha kule. Nimeshatoa mihadhara katika vyuo vingi, sio Marekani tu bali sehemu mbali mbali za dunia.

Ninavyosikiliza mahojiano na hotuba za Tundu Lissu ninafahamu fika kwamba ataamsha fikra za wasikilizaje wake kwa kiwango cha juu. Ninafahamu pia kwamba katika vyuo vya Marekani, hawamwaliki mtu kwa ajili ya kumsikiliza tu, bali pia kwa ajili ya kumpiga masuali. Mtu anatoa hotuba halafu anakalishwa kitimoto.

Tundu Lissu ni hodari kwa yote hayo. Wanaombeza hapa Tanzania wanajisumbua. Kwa kusema hivyo, simaanishi kwamba mawazo yangu ni sawa na ya Tundu Lissu. Kuna ambayo ninatofautiana naye.

Lakini kutofautiana mitazamo ndio utamaduni wa watu wanaofikiri. Ndio utamaduni wa watu walioelimika. Vyuo vikuu ni mahali ambapo tunatofautiana na kulumbana muda wote. Ni uhai wa vyuo vikuu. Ni uhai wa taaluma. Tunawajibika sisi waalimu kujenga tabia hiyo miongoni mwa wale tunaowafundisha.

Kuna haya madai kwamba Tundu Lissu anaichafua nchi. Binafsi, sijawawahi kuona popote au siku yoyote ambapo Tundu Lissu ameichafua nchi. Anazilalamikia mamlaka za nchi, kama vile serikali na Bunge. Lakini serikali si nchi. Bunge si nchi. Anapomshutumu Spika, haichafui Tanzania. Spika si Tanzania.

Ingekuwa vinginevyo, basi kwa jinsi Mwalimu Nyerere alivyoandika kitabu cha "Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania" tungesema kwamba ameichafua nchi. Mwalimu anaiponda CCM na serikali yake, hadi kutamka kwamba kuna kansa katika CCM. Hadi akasema kwamba alitamani kitokee chama cha upinzani kilicho bora kuliko CCM ili kishike nchi badala ya CCM. Lakini itakuwa ni upuuzi kusema kuwa Mwalimu Nyerere aliichafua nchi.

Binafsi, siku nitakapoona Tundu Lissu anaichafua nchi, sitamlazia damu. Lakini sijaona. Badala yake, nimemsikia akitangaza kwamba yuko tayari kuitumikia nchi katika nafasi ya uongozi, iwapo atapata ridhaa. Ameelezea kuwa akishika uongozi, ataweka utawala wa sheria, haki za binadamu, na demokrasia. Kila mwenye kuwania uongozi wa nchi ana haki na wajibu wa kutueleza ana malengo gani. Kwa hayo malengo yake, sioni mantiki yoyote ya kusema kuwa Tundu Lissu anaichafua nchi.
Na Mimi nasema hawa faru wawili ni wa hovyo sana katika nchi yetu, mimi nasema ukweli, msemakweli ni mpenzi wa Mungu naomba mniamini
 
Anaandika Profesa Joseph Mbele

Mimi ninaufahamu vizuri utamaduni wa vyuo vikuu vya Marekani, kwa sababu nilisomea kule na ninafundisha kule. Nimeshatoa mihadhara katika vyuo vingi, sio Marekani tu bali sehemu mbali mbali za dunia.

Ninavyosikiliza mahojiano na hotuba za Tundu Lissu ninafahamu fika kwamba ataamsha fikra za wasikilizaje wake kwa kiwango cha juu. Ninafahamu pia kwamba katika vyuo vya Marekani, hawamwaliki mtu kwa ajili ya kumsikiliza tu, bali pia kwa ajili ya kumpiga masuali. Mtu anatoa hotuba halafu anakalishwa kitimoto.

Tundu Lissu ni hodari kwa yote hayo. Wanaombeza hapa Tanzania wanajisumbua. Kwa kusema hivyo, simaanishi kwamba mawazo yangu ni sawa na ya Tundu Lissu. Kuna ambayo ninatofautiana naye.

Lakini kutofautiana mitazamo ndio utamaduni wa watu wanaofikiri. Ndio utamaduni wa watu walioelimika. Vyuo vikuu ni mahali ambapo tunatofautiana na kulumbana muda wote. Ni uhai wa vyuo vikuu. Ni uhai wa taaluma. Tunawajibika sisi waalimu kujenga tabia hiyo miongoni mwa wale tunaowafundisha.

Kuna haya madai kwamba Tundu Lissu anaichafua nchi. Binafsi, sijawawahi kuona popote au siku yoyote ambapo Tundu Lissu ameichafua nchi. Anazilalamikia mamlaka za nchi, kama vile serikali na Bunge. Lakini serikali si nchi. Bunge si nchi. Anapomshutumu Spika, haichafui Tanzania. Spika si Tanzania.

Ingekuwa vinginevyo, basi kwa jinsi Mwalimu Nyerere alivyoandika kitabu cha "Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania" tungesema kwamba ameichafua nchi. Mwalimu anaiponda CCM na serikali yake, hadi kutamka kwamba kuna kansa katika CCM. Hadi akasema kwamba alitamani kitokee chama cha upinzani kilicho bora kuliko CCM ili kishike nchi badala ya CCM. Lakini itakuwa ni upuuzi kusema kuwa Mwalimu Nyerere aliichafua nchi.

Binafsi, siku nitakapoona Tundu Lissu anaichafua nchi, sitamlazia damu. Lakini sijaona. Badala yake, nimemsikia akitangaza kwamba yuko tayari kuitumikia nchi katika nafasi ya uongozi, iwapo atapata ridhaa. Ameelezea kuwa akishika uongozi, ataweka utawala wa sheria, haki za binadamu, na demokrasia. Kila mwenye kuwania uongozi wa nchi ana haki na wajibu wa kutueleza ana malengo gani. Kwa hayo malengo yake, sioni mantiki yoyote ya kusema kuwa Tundu Lissu anaichafua nchi.
Nakubaliana na Prof

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom