kabanga
JF-Expert Member
- Dec 12, 2011
- 37,191
- 18,457
alijitekenya....Kwani wa sasa ni "Presidential material" au "alisukumiziwa" na Waliomtaka tu?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
alijitekenya....Kwani wa sasa ni "Presidential material" au "alisukumiziwa" na Waliomtaka tu?
Tunajua bavicha kila kitu ni bora jana.Huyu wa sasa sio kabisa....na hata washauri wanashindwa kumshape.
Ndio maana umekuja na justification ndefu.
Hata Msekwa alikataa hoja ya Nkamia kwa kusema kuwa miaka kumi inatosha kuvumilia a none presidential person (kama huyu wa sasa)
Daah
Ha ha ha ha haaaa... Huyu mama anazeeka vibaya.
Lowassa ndo hafai kabisa, in fact, chadema ya sasa haina mtu ambaye ni president material.Umelipwa bei gani ? Wewe ni mmoja wa waliowadanganya Watanzania kwamba Magufuli anafaa , sasa sema ukweli wako na Mungu akusamehe , Magufuli anafaa kweli kama ulivyodanganya ?
Muulize mumeoUliyemuongelea simfahamu.
Lisu huku anatembelea magongo? Acha utani.Bora maana haya mambo ya kukurupuka ndio sababu tunalia sasa.
Mbarawa or Lissu. Utanzania kwanza.
Muulize mumeo
Tangu hujueeEeeeeh tangu hujue nina mume basi huchoki kumtaja taja eeeeeh... jione kwanza.. kwani ndiye ananiambia ya kuandika humu!!!
Awe waziri wa foreign affairs Kwani ni mvaa Kaunda?watu wa bara wameitawala zanzibar mfululizo,mkapa,kikwete,magu
natarajia mpambano mkali na mtoto wa mwinyi ambaye ni waziri wa ulinzi
pia mbarawa ajiepushe na kundi la kipara,maana linapingwa sana
pia nashauri apewe muda awe waziri wa mambo ya nje akapate uzoefu,tunaona wa sasa anavyoyumba katika siasa za kimataifa
Huyo Makonda anafaa kuwa rais wa ukoo wenu tu!Na Makonda naye atafaa sana sanaaaaa.. tena katika kuendeleza hapa kazi tu.. na pia bila kumsahau Majaliwa
Hawa wawili wakishika vyeo vya juu baada ya 2025 nchi itazidi kunoga.
Wanabodi,
Hili ni bandiko la swali,
Naanza kwa swali la msingi, Jee Tanzania, Tuanze Utamaduni wa Kuwaspoti Watanzania Presidential Materials, na KuwaGroom ili Tupate Rais Bora, Au Tuendelee Kuwaacha Tuu Yoyote Anayeutaka Urais, Awe Hata Kama Sio Presidential Material?.
Sifa za Urais wa Tanzania.
Nafasi ya urais wa JMT, inashikwa na raia yoyote wa JMT mwenye sifa na vigezo. Tangu JMT imezaliwa mwaka 1964, hadi leo Zaidi ya miaka 53, ni Mtanzania mmoja tuu kutoka Zanzibar, aliyekidhi sifa na vigezo hadi kuweza kuwa rais wa JMT, Wazanzibari wengine wote wenye sifa waliojaribu, hawakuweza kupata kutokana na kuzidiwa sifa na vigezo na wagombea kutoka bara, matokeo yake hadi leo sisi bara ni 4 kwa 1 Zanzibar. Hali hii ilipelekea nikashauri
Je, kunahitajika affirmative action ili Mzanzibari aweze tena kuwa Rais wa JMT?
Lakini leo, baada ya kumsikiliza Mtanzania huyu ambaye ni Mzanzibari, kiukweli kabisa, nimemkubali sana kuwa ana kidhi sifa na vigezo hadi sifa za ziada za nationalism ya Utanzania kwanza, na ni mzalendo wa kweli, kwa sababu kwa kauli na matendo, amethibitisha pasi shaka kuwa yeye kwanza ni Mtanzania, kisha ni Mzanzibari, wakati kiukweli kabisa, kwa Wanzanzibari walio wengi, wao kwanza ni Wazanzibari kwanza, kisha ndio Watanzania.
Hebu msikilize Prof. Mbarawa.
Tuwachagize Presidential Materials Wagombee?.
Kuna Watanzania wengi wenye sifa za kutuletaa rais bora kabisa, lakini wengine hawana vyama, wengine wala hawauwazi urais, hivyo wanapotokea watu wenye sifa kama Prof. Mbarawa, unaweza kukuta ndio wale type ya watu hawauwazii hata huo urais, lazima wachagizwe, hata katika hao wagombea Zaidi ya 40 wa CCM ile 2015, sio wote waliutaka urais, kuna baadhi walifuatwa na kuchagizwa kwenda kuchukua fomu na kugombea, hivyo mnaonaje wale wote wenye presidential personalities, or presidential materials, tuwachagize waanze kufikiria kugombe.
Hitimisho, Tusisubiri Marais Wajitokee Tuu, Tuanze Kutengeneza Marais.
Kuna kauli isemayo, leaders are born and not made, Mimi ni muumini wa good leaders are made, besides kuwa born, hivyo lets start making our leaders by grooming them to be good leaders. Kwa upande wangu kwa 2020, nimeishamspoti mmoja kutoka upinzani,
Tundu Lissu ndiye asimame na Magufuli 2020? ...Ameonyesha ...
Na kwa 2025, niliishamspoti mmoja.
Baada ya Magufuli, 2025 Makonda atatufaa ... - jamiiforums.com
huyu Prof. Mbarawa ni wapili, tuendelee kuwaibua presidential materials ili kufikia 2025, tupate viongozi bora, japo mimi binafsi niko kwenye lile kundi tunaotaka 2025 katiba ibadilishwe Magufuli aendelee kama nilivyouliza hapa.
Kwa Kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa ...
Namalizia kwa lile lile swali la msingi, Jee Tanzania, Tuanze Utamaduni wa Kuwaspoti Watanzania Presidential Materials, na KuwaGroom ili Tupate Rais Bora, Au Tuendelee Kuwaacha Tuu Yoyote Anayeutaka Urais, Awe Hata Kama Sio Presidential Material?.
Jumamosi Njema,
Paskali[/QU
Prof ametisha