Prof. Makame Mbarawa: Wizara ya Maji hakuna uadilifu na hatuwapendi Watanzania

bagamoyo

JF-Expert Member
Jan 14, 2010
21,293
24,173
January 23, 2020

Profesa Makame Mbarawa - ''Wizara ya Maji Hakuna Uadilifu na Hatuwapendi Watanzania, Changamoto za Maji Tanzania wizarani Wakurugenzi, ma-Consultant, Wahandisi hawazijui'




Prof. Makame Mbarawa amesema watalaamu wake walioko wizarani hawajui miradi iliyopo bali wanakaa ofisini sana.

Alisema hayo alipokutana na Bodi ya Maji na Waziri kutoa mrejesho wa ziara zake Tanzania nzima. Ziara ya Mh. Makame Mbarawa imegundua na kumfundisha kuwa serikali inapoteza mabilioni ya shilingi kwa wakandarasi kutoa makadirio yaliyo zaidi ya gharama halisi kwa zaidi ya 100% na kuendelea.

Mfano mmoja Mh. Mbarawa Makame alitumia case study halisi kutokana na ziara zake, ni mradi mmoja ulikadiriwa na wataalamu kugharamia shilingi bilioni 16.

Lakini baada ya kukaa na mkandarasi na kupitia upya gharama zake ziliteremka mpaka shilingi bilioni 10 yaani serikali katika mradi huu mmoja ilikuwa inapoteza zaidi ya bilioni 6 kutokana na kuzidishwa makadirio ya mradi huo.

Waziri amesema hata kama serikali ikiipa wizara trilioni ya shilingi matatizo ya maji hayawezi kutatuliwa na kumalizia maana makadirio (estimation) hayana uhalisia na ni ya juu mara 4 ya gharama halisi.

Mh. Mbarawa alisema miradi mingi ya maji inayoteketeza pesa zaidi kuliko uhalisia ni iie iliyopo pembezoni mwa nchi yetu kama mikoa ya Mtwara , Ruvuma, Rukwa na Kigoma kwa kutaja kwa uchache.

Miradi hii mingi haitembelewi na wataalamu wa wizara waliopo makao makuu. Mh. Mbarawa kutaka kuthibitisha hilo aliutaja mradi mmoja wa majina kuwataka wanabodi kuutaja mradi huo upo wapi na unagharimu kiasi gani.

Hakuna aliyeweza kujibu swali la Mh. Mbarawa na waziri akasema hilo ni thibitisho kuwa wataalamu wanakaa sana ofisini na hawaelewi nini kinaendelea katika miradi ya maji nchini.

Mwisho Mh. Makame Mbarawa akasema dhuminu ya ziara yake kila kona ya nchi ilikuwa kujifunza changamoto za miradi ya maji nchini na hilo litamsaidia kutimiza wajibu wake vizuri.

Hivyo ametoa rai kwa wataalamu wa maji kutoka ofisini na kukagua miradi ili kuhakikisha fedha za umma wazipotei bure kwa wakandarasi kukadiria bajeti isiyo halisi.

Waziri anamalizia wataalamu wakitimiza wajibu wao kama alivyo-share alichojifunza katika ziara zake basi kwa bajeti iiliyopo wananchi wengi zaidi watapata huduma ya maji na tatizo la maji nchini kuwa kumalizika na kuw historia.

Source: Millard Ayo
 
Deceber 22, 2019



MKANDARASI ALIYEJENGA OFISI YA MABATI KWA MILIONI 100, AJENGA TENA KIBANDA KWA MILIONI 30


Waziri wa Maji Mh. Makame Mbarawa ameahidi kufuta usajili wa kampuni ya MBESA iliyopewa kandarasi ya maji katika mji wa moshi ambapo waejenga Kibanda ambacho kimegharimu kiasi cha shilingi Milioni 30 bila kuwa na thamani ya Fedha ambapo kampuni hiyo ndiyo iliyojenga Ofisi ya mabati kwa shilingi milioni 100



Source: Muungwana TV
 
December 22, 2019

"TAKUKURU MCHUNGUZE" Waziri wa Maji, Prof Makame Mbarawa,

ameeleza kusikitishwa na mradi wa maji wa Arusha ambao bado haujakamilika kuwa na mapungufu mengi yanayosababishwa kwa kiasi kikubwa na utendaji kazi mdogo wa Injinia Wa Mradi huo .. Moja kati ya Madudu yaliyowahi kuibuliwa na Waziri Mbalawa ni Mabomba mabovu yaliyotakiwa kuwekwa kwenye mradi huo na sasa ni Gharama kubwa za ujenzi wa majengo, hali iliyo mlazimu kuwataka TAKUKURU Kumchunguza injinia huyo. Mradi huo endapo utakamilika utaondoa kero ya upungufu wa maji kwani uboreshaji wa huduma utaongezeka kutoka wastani wa lita 40,000,000 hadi lita..



Source:Global TV online
 
Boss bagamoyo Haya yote ni Matokeo tu, Shida na Tatizo kubwa linaanzia na hayo Ma Kampuni na Viongozi.

MaKampuni (Contractor) na Wasimamizi (Consultant), Tatizo ni hizi tenda kupewe Kampuni zisizo kuwa na uwezo, kwenye Bidding tender Kampuni inayoshinda tender haipewi kazi, anayepewe asiyeshinda kwa kutoa 10% au kujuana.

Wasimamizi (Consultant), hawa nao ni kama Contractor (Wajenzi) wanapewa kazi kwa kujuana na kulindana tu, Washindi hawapewi kazi ila kazi anapewa hawa wapigaji.

Ushauri wangu, Kazi wapewe Makampuni na Watu wenye sifa na walioshinda Tender za kazi. Pili hili suala la mtu au kampuni kushindwa kazi na bado analindwa iishe. Pia nafasi za kazi wapewe watu wenye elimu na uzoefu wa kazi.

Otherwise kila siku tutakuwa ni kuwalalamikia hawa Wajenzi (Contractor) na Wasimamizi (Consultant) bure na hawa Washenzi kutuharibia sisi Ma Engineer na Consultant Wazalendo na waadilifu.
 
Nimefurahi sana kuwa anatumia mitandao kupata maoni, sasa wanataka kuifungia hayo maoni watapata wapi?
 
Huyu Prof mkumbo nae bure tu, alivyokuwa act wazalendo taralila nyiiingi, walewale kopo la chooni,

Haya majitu yaliyotoka upinzani keep tupu mkumbo waitara, afadhali kidogo mama ngwira.
 
Boss tilburg1 Wanaotaka kuifungia ni wale wapigaji, wanaogopa kuanikwa Madudu yao, Kiongozi clean aka Msafi hawezi kuogopa Maoni na Ushauri wa Wananchi ambao ndio Boss wao. Ni kama vile Makelele ya Chura hayamzuii Tembo kunywa maji. Upinzani na Mitandao ikitumiwa vizuri ni Afya kwa Taifa.



Nimefurahi sana kuwa anatumia mitandao kupata maoni, sasa wanataka kuifungia hayo maoni watapata wapi?
 
Boss tilburg1 Wanaotaka kuifungia ni wale wapigaji, wanaogopa kuanikwa Madudu yao, Kiongozi clean aka Msafi hawezi kuogopa Maoni na Ushauri wa Wananchi ambao ndio Boss wao. Ni kama vile Makelele ya Chura hayamzuii Tembo kunywa maji. Upinzani na Mitandao ikitumiwa vizuri ni Afya kwa Taifa.
Sasa ni nani huyo kiongozi clean aka msafi???
 
December 22, 2019

"TAKUKURU MCHUNGUZE" Waziri wa Maji, Prof Makame Mbarawa,

ameeleza kusikitishwa na mradi wa maji wa Arusha ambao bado haujakamilika kuwa na mapungufu mengi yanayosababishwa kwa kiasi kikubwa na utendaji kazi mdogo wa Injinia Wa Mradi huo .. Moja kati ya Madudu yaliyowahi kuibuliwa na Waziri Mbalawa ni Mabomba mabovu yaliyotakiwa kuwekwa kwenye mradi huo na sasa ni Gharama kubwa za ujenzi wa majengo, hali iliyo mlazimu kuwataka TAKUKURU Kumchunguza injinia huyo. Mradi huo endapo utakamilika utaondoa kero ya upungufu wa maji kwani uboreshaji wa huduma utaongezeka kutoka wastani wa lita 40,000,000 hadi lita..



Source:Global TV online
Kwa majengo cost per square meter inahusu makadirio ya gharama sio gharama halisi za ujenzi. Gharama halisi inapatikana baada ya jengo kukamilika.
Serikali
1. Imulike na isimamie bodi za wataalamu ujenzi ERB, CRB, A&QS-RB, na wengine. Hawa watu ni bogus.
2. Watoaji vibali vya miradi ya ujenzi eg jiji, manispaa, na wengine; ni wababaishaji tu, rejea saga la maghorofa 200+- yaliyotakiwa kubomolewa Kariakoo DSM miaka kadha iliyopita yalipataje vibali vya ujenzi?
3. Nani awajibike kwa vyuo vyetu kuzalisha wataalamu wasioiva?
4. Nani awajibike kwa shule zetu kupasisha wahitimu wasiokidhi viwango?
5. Nini hatma ya miradi inayoendelea kutekelezwa katika mfumo mzima wa ubunifu mpaka utekelezaji unaofanywa na taasisi na watu wasioiva kitaaluma lakini ndio wenye mamlaka na hawapendi ushauri?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu Prof mkumbo nae bure tu, alivyokuwa act wazalendo taralila nyiiingi, walewale kopo la chooni,

Haya majitu yaliyotoka upinzani keep tupu mkumbo waitara, afadhali kidogo mama ngwira.

Huyo profesa Mkumbo kipindi amehongwa cheo kila siku alikuwa anapanda majukwaani kufanya siasa za majitaka, ila baada ya kuambiwa ukweli wake akacha hiyo tabia.
 
Boss bagamoyo Haya yote ni Matokeo tu, Shida na Tatizo kubwa linaanzia na hayo Ma Kampuni na Viongozi.

MaKampuni (Contractor) na Wasimamizi (Consultant), Tatizo ni hizi tenda kupewe Kampuni zisizo kuwa na uwezo, kwenye Bidding tender Kampuni inayoshinda tender haipewi kazi, anayepewe asiyeshinda kwa kutoa 10% au kujuana.

Wasimamizi (Consultant), hawa nao ni kama Contractor (Wajenzi) wanapewa kazi kwa kujuana na kulindana tu, Washindi hawapewi kazi ila kazi anapewa hawa wapigaji.

Ushauri wangu, Kazi wapewe Makampuni na Watu wenye sifa na walioshinda Tender za kazi. Pili hili suala la mtu au kampuni kushindwa kazi na bado analindwa iishe. Pia nafasi za kazi wapewe watu wenye elimu na uzoefu wa kazi.

Otherwise kila siku tutakuwa ni kuwalalamikia hawa Wajenzi (Contractor) na Wasimamizi (Consultant) bure na hawa Washenzi kutuharibia sisi Ma Engineer na Consultant Wazalendo na waadilifu.
Wanawalipa wakandarasi kwa wakati? riba wanazodaiwa na wakopeshaje watazilipaje?

Ili kupata suluhu ya kweli timely payment haitakiwi iachwe isiangaliwe, mfano mtu anadai kwa miaka miwili hizo riba pia nazo zinapandisha gharama za mairadi
 
Actual building construction cost unategemea material specifications na quality and cost of labor.
Bei ya beer Tanzania unategemea brand, ujazo, na mahali ulipo. Ukiwa Buguruni, Airport, jeshini, Kilimanjaro hotel nk bei ni tofauti.
Kwahiyo tusichukulie kuwa cost per unit in area kama ni standard. Tutakosea sana!
Quality na bei za materials na labor haziwezi kuwa sawa kila siku kila mahali.
Mifano:
Bati. Zipo za material, size, gauge na bei tofauti. Vivyohivyo na mbao, misumari, nondo, mchnga, maji, kokoto, cement, rangi, tiles, wire za umeme, bomba, nk.
Pili mafundi na vibarua wako wenye ujuzi na uzoefu tofauti kwahiyo hulipwa kutegemea na uwezo wa mwajiri, sheria zenu za kazi na mshahara wa kima cha chini; narudia: SHERIA ZENU ZA KAZI NA KIMA CHA CHINI CHA MISHAHARA.
Tatu mahali linapojengwa hilo jengo: mjini, kijijini, juu au chini ya maji au barafu eg bandari nk. Halafu majira gani! Kiangazi, masika, kwa Tanzania unaweza kuambiwa ghafla ujenge usiku na mchana!
Nne muda na mazingira yasiyotabirika: Mfano mzuri ni hivi sasa tuko mwanzo wa mwaka tunasubiri Bajeti ya Serikali ya 2020-21. Nani anajua kama gharama za maisha zitapanda au kushuka?
Mjuwe kwamba mkipandisha kodi tu, na bei za vitu zitapanda. Sukari ikipanda bei, chai itapanda bei, maandazi na vitumbua vitapanda bei, la sivyo vitakuwa vidogo zaidi. Mikate hali kadhalika! Kwasababu bei za mchele, mafuta na mkaa vyote vitapanda bei! Dawa hospitalini zitapanda bei, gharama za usafiri, na UJENZI zitapanda bei!
Lakini haiishii hapo. Majengo yakijengwa chini ya kiwango yanasababisha gharama za ujenzi kupanda. Kwasababu yatalazimika kurudiwa ujenzi au kukarabatiwa kwa gharama za ziada. Hasara katika ujenzi maana yake ni gharama kwa mlipaji (Serikali) ambaye ni sisi wananchi.
Kwahiyo MH Waziri kama una uchungu na wananchi anzia bungeni kwenye Bajeti ya Serikali. Punguzeni matumizi ya Serikali kwenye utawala bila kuzingatia sheria na taratibu za tenda na sheria za manunuzi.
Mkiendelea na utaratibu wa miradi ya papo kwa papo mnakaribisha hayo mnayokemea. Kwasababu kama wewe Mkuu wa mkoa au Waziri ukitoa amri "nataka darasa lijengwe hapa kwa wiki mbili kwa shillings kadhaa, watu watajenga watakupakia rangi nzuri utalizindua kwa vigelegele na mapicha! Baada ya mwaka jengo linameguka vipande vipande! Utalaumu wataalamu?



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanawalipa wakandarasi kwa wakati? riba wanazodaiwa na wakopeshaje watazilipaje?

Ili kupata suluhu ya kweli timely payment haitakiwi iachwe isiangaliwe, mfano mtu anadai kwa miaka miwili hizo riba pia nazo zinapandisha gharama za mairadi


Boss Ndalama Mapungufu na Changamoto ni nyingi uliyotaja nayo ni Changamoto moja wapo, natumaini kupitia humu, Wahusika wamekusikia na wanazidi kulifanyia kazi, mimi nimetaja machache, na mimi sipo Jikoni aka Serikalini. Hata na mimi naidai Jamhuri na Serikali pesa nyingi, na barua wananitumia kujua deni langu.
 
Back
Top Bottom