Prof. Maghembe afungua mkutano wa kimataifa wa nchi 21 Duniani kujadili upandaji wa miti kibiashara

Hamza Temba

R I P
Feb 10, 2017
20
4

Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe akizungumza mkoani Morogoro jana wakati wa ufunguzi wa mkutano wa pili wa Mashirika yanayohamasisha upandaji wa miti kibiashara na uzalishaji wa mazao ya misitu barani Afrika, mkutano huo wa siku mbili umewashirikisha wajumbe kutoka nchi 21 duniani kwa lengo la kubadilishana mawazo juu ya kuboresha uzalishaji na upatikanaji wa masoko. Aliwataka wajumbe hao kujadili namna ya kuwawezesha wakulima wa miti wakati wanasubiri kuvuna mazao yao waweze kujishuulisha na kilimo cha mazao ya muda mfupi kwa kutumia mbinu bora za kisayansi ili waweze kujikimu kimapato.

Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe akizungumza mkoani Morogoro jana wakati wa ufunguzi wa mkutano wa pili wa Mashirika yanayohamasisha upandaji wa miti kibiashara na uzalishaji wa mazao ya misitu barani Afrika, mkutano huo wa siku mbili umewashirikisha wajumbe kutoka nchi 21 duniani kwa lengo la kubadilishana mawazo juu ya kuboresha uzalishaji na upatikanaji wa masoko.

Baadhi ya wajumbe kutoka nchi 21 duniani wakifuatilia mkutano huo. Nchi hizo ni Burkina Faso, Chad, Ethiopia, Gambia,Ghana, Italy, Mali, Niger, Nigeria, Senegal, Sudan, Liberia, Cameroon, Swaziland, Finland, Zambia, Canada,Mozambique, Zimbabwe, Kenya na Tanzania.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Steven Kebwe akizungumza katika mkutano huo. Aliwataka wajumbe wa mkutano huo kujadili na kuishauri dunia namna bora ya kutunza na kuendeleza misitu kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho ikiwemo utekelezaji wa sheria za usimamizi wa misitu.

Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Ezekiel Mwakalukwa akizungumza katika mkutano huo ambapo aliwataka wajumbe kujadili kwa uwazi kuhusu mikakati mbalimbali ya kukabiliana na changamoto za sekta ya misitu na kwamba Serikali kupitia Wizara itapokea maoni na mapendekezo yao kwa ajili ya kuyafanyia kazi ili kuimarisha ustawi wa sekta hiyo.

Waziri Maghembe akieleza jambo kwenye ka mkutano huo ambapo aliwataka wajumbe wajumbe wajadili namna bora ya kuwafundisha wakulima wa miti kufanya kilimo bora ikiwa ni pamoja na mafunzo uvunaji wa hewa ukaa ili kuwainua kimapato. Aliwataka pia kusaidia wakulima wa miti katika upatikanaji wa masoko ya uhakika.

Prof. Maghembe akisisitiza jambo kwenye mkutano huo.
DSC_2047.JPG
Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe akizungumza mkoani Morogoro jana na baadhi ya viongozi waliondaa mkutano wa pili wa Mashirika yanayohamasisha upandaji wa miti kibiashara na uzalishaji wa mazao ya misitu barani Afrika muda mfupi kabla ya kufungua mkutano huo wa siku mbili uliowashirikisha wajumbe kutoka nchi 21 duniani kwa lengo la kubadilishana mawazo juu ya kuboresha uzalishaji na upatikanaji wa masoko.

Baadhi ya wajumbe walishiriki mkutano huo kutoka nchi 21 duniani.

Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe (kushoto) akizungumza na Mbunge kutoka Kenya, Chariti Katambi mkoani Morogoro jana baada ya kufungua mkutano wa pili wa Mashirika yanayohamasisha upandaji wa miti kibiashara na uzalishaji wa mazao ya misitu barani Afrika, mkutano huo wa siku mbili umewashirikisha wajumbe kutoka nchi 21 duniani kwa lengo la kubadilishana mawazo juu ya kuboresha uzalishaji na upatikanaji wa masoko.

Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe akizungumza na waandishi wa habari mkoani Morogoro jana baada ya kufungua mkutano wa pili wa Mashirika yanayohamasisha upandaji wa miti kibiashara na uzalishaji wa mazao ya misitu barani Afrika, mkutano huo wa siku mbili umewashirikisha wajumbe kutoka nchi 21 duniani kwa lengo la kubadilishana mawazo juu ya kuboresha uzalishaji na upatikanaji wa masoko.


Picha ya pamoja na washiriki wa mkutano huo.

Source: www.wizarayamaliasilinautalii.blogspot.com
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom