Prof. Mafwenga, mtanzania anayedai kuwa na shahada saba, Masters na PhD kadhaa si mkweli, hajamaliza baadhi ya kozi za LLM na PhD. UDSM imuumbue!

Nimetazama hii business card nimekosa majibu.

View attachment 235850




======
View attachment 1306143
Dar es Salaam. Akiwa na shahada tatu za uzamivu (PhD) na tatu nyingine za uzamili (masters), huenda Profesa Handley Mwafwenga ni miongoni mwa wasomi wenye shahada nyingi zaidi nchini hata duniani.

Tangu alipojiunga na Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) na kuhitimu diploma ya juu ya kodi (advanced diploma) mwaka 1987, Profesa Mwafwenga hajawahi kuacha kusoma kiasi cha watu wake wa karibu kumshauri apumzike kidogo.
“Askofu (Alex) Malasusa na Waziri (Palamagamba) Kabudi walinishauri nipunguze kusoma. Napenda kusoma kama wengine wapendavyo kusali, michezo au muziki,” anasema Profesa Mwafwenga ambaye hadi sasa ana digrii (shahada) saba tofauti za chuo kikuu na vyeti vingi vya kozi fupi alizosoma na kumpa mamlaka kitaaluma kuwa mchumi, mwanasaikolojia, mwanasheria na mshauri wa kodi.

Safari ya elimu ya Mwafwenga (52) ilianzia Shule ya Msingi Mwananyamala kabla hajajiunga Shule ya Sekondari Sangu na kumaliza kidato cha nne mwaka 1975.
Tangu akiwa mdogo, anasema baba yake alikuwa anamwita profesa na wakati wote alimsisitiza kusoma kwa bidii.

“Mimi ni mtoto wa mwisho. Baba yangu alikuwa mwalimu shule ya msingi. Ndiye aliyetujengea ari ya kupenda kusoma. Ndani ya nyumba yetu kuna maprofesa zaidi yangu na madokta wengi,” anasema.

Moyo wa kusoma
Mitandaoni, India ilitikisa mwaka 2017 ilipokuwa na habari kuhusu Profesa VN Parthiban mwenye digrii tofauti 145. Huenda akawa ndiye mtu mwenye digrii nyingi zaidi duniani. Prosefa huyu alitumia miaka 30 kupata shahada hizo.

Kabla yake, mwaka 2012, Michael Nicholson alikuwa Mmarekani mwenye elimu ya juu zaidi akiwa na digrii 30 alizozipata ndani ya miaka 55 ya kusoma. Akiwa na miaka 75 wakati huo, alikuwa anatamani kufikisha digrii 33 au 34.
Ukiachana na Mmarekani huyo kutoka Jimbo la Michigan, mwaka 2010 China kulikuwa na Profesa Zhou Baokuan (74) kutoka Jimbo la Shenyang aliyekuwa na shahada tisa tofauti zikiwamo PhD tatu na shahada mbili za uzamili alizozipata ndani ya miaka 35. Katika kipindi hicho, alikuwa anafanya PhD yake nyingine Chuo Kikuu cha Fudan.

Lakini nchini Tanzania, akitumia miaka 32, Profesa Mwafwenga ameshatunukiwa digrii nyingi tofauti. Anasema muda wake wa kupumzika anautumia kusoma. Wakati wengine wanafanya mengine, yeye anasoma kitabu au chochote kitakachomuongezea maarifa.
Anasema kusoma ndio kitu anachokipenda zaidi kama ilivyo kwa wanaopenda kunywa pombe, kushabikia mpira au kuwa na wapenzi wao. Ni mapenzi haya yanayompa ujasiri wa kuendelea kusoma kila kukicha na hafikirii kuacha.

“Kwa sasa nina digrii saba. Natamani niwe nazo 10. Mara nyingi, huwa nasoma kila ninapokutana na changamoto. Sipendi kuacha kinachonishinda bila kukitafutia suluhu ya kudumu,” anasema.
Jukumu kubwa la wasomi wa ngazi za juu ni kuandika machapisho na vitabu. Yeye anasema tayari ameandika vitabu vitatu na kutoa machapisho zaidi ya 43.

Shahada alizonazo
Alipomaliza kidato cha nne, alisoma cheti cha uhasibu (National Certificate of Bookkeeping) na akaajiriwa kwa sifa hiyo.
Baada ya kufanya kazi kwa muda alijiunga na chuo cha IFM alikosoma stashahada ya juu (advanced diploma) ya kodi akigharamiwa na Wizara ya Fedha kisha akachukua diploma ya uzamili (PGD) ya kodi, akilipiwa na Wizara ya Mambo ya Ndani.

Baada ya hapo alifanya shahada ya uzamili katika usimamizi wa fedha akilipiwa na Wizara ya Mambo ya Ndani halafu akamaliza na shahada ya uzamivu (PhD) katika fedha kwa gharama za Wizara ya Fedha.
“Baada ya kuona nafanya kazi nyingi zinazohusu sheria…fedha ni sheria na kodi ni sheria pia, nilirudi shule kusoma sheria,” anasema.

Sheria alisoma kuanzia digrii ya kwanza hadi PhD. Zote akijilipia mwenyewe. Kwenye sheria, anayo digrii ya kwanza, digrii mbili za uzamili na mbili za uzamivu.
Kwenye orodha hiyo pia ana shahada ya uzamili katika usimamizi wa biashara (MBA). Ingawa kwa wengi si kazi rahisi kupata shahada zote hizo, Profesa Mwafwenga anasema wakati mwingine alilazimika kusoma digrii mbili kwa pamoja.

“Wakati nasoma MBA ndio kipindi nilichosoma (shahada ya uzamili ya sheria) LLM. Digrii zote nimezipata hapa nchini. Sijaenda nje ya nchi hata mara moja,” anasema.

Familia na siasa
Msomi huyu ni baba wa watoto wanne, wote wa kiume na yupo karibu sana na watoto wake waliorithi tabia ya kupenda kusoma.

Anasema kutokana na kufanana tabia, wanapata muda wa kutosha kusoma pamoja na watoto wake.
“Watanzania wengi wanasoma ili kupata cheti, mpaka waone changamoto ndio wataenda kusoma ‘masters’ kama anayo digrii ya kwanza baada ya hapo, akishapandishwa cheo, haendelei tena. Mimi nasoma ili nipate maarifa,” anasema.

Wakati mwingine, anasema huwa anachukua wasifu wake na kuutathmini na akiona kuna upungufu wowote basi anaenda kusoma.
Hata akiwa kazini na kukawa na kitu kinamsumbua, hurudi shule kunoa uwezo wake.
“Nilipohitimu masomo ya kodi muda mwingi nilikuwa nakutana na wanasheria, niliona kuna vitu haviko sawa hivyo nikarudi shule kusoma sheria ili nizungumze nao lugha moja,” anasema.

“Nilipokuwa Wizara ya Nishati na Madini nikaona nisome ‘masters ya accounting in oil and gas’ kwa kuwa ndivyo vitu vilikuwa vinaleta changamoto wakati huo.”
Profesa Mwafwenga anayevutiwa na siasa pia anasema ameshagombea ubunge wa Afrika Mashariki mara mbili kupitia CCM bila mafanikio.

Hasomi tu, hufanya mambo mengine pia kila apatapo wakati. Kwa nyakati tofauti anasema ameshakuwa mshereheshaji na mchangiaji kwenye magazeti mbalimbali.
“Nimekuwa MC, nimepiga muziki nikiwa na Zahiri Ally Zorro na wengineo. Nimekuwa mwandishi wa habari pia nikiandikia gazeti la Majira. Kati ya mwaka 1997 na 2001 nikahamia Mwananchi. Nimeandikia Uhuru pia,” anasema.

About
Prof (Dr.Juris) Handley Mpoki Mafwenga is a Macro-Fiscal Policy Psychologist who has enthusiastically been involved in International negotiations pertaining to Investment and Fiscal policy. His Taxation, Evaluation of Illicit Financial Flows, Financial Risks Management, Anti-money laundering, Anti-Terrorism Measures, Investigation of Tax Crimes, and PPP projects Mgt, are considered his Magnum Opus.

He is a father of Revenue Forecasting Modeling, Financial programming, and Fiscal Psychology empiricism. He is a Supernumerary Fellow who served as a Professor at the Tumaini University Makumira (TUDARCO), Iringa University, Teofilo Kisanji University(TEKU) and IFM. Being a renowned Budget advocacy expert under the auspices of Treasury, he has been a Member of SADC Sub-Committee on Tax matters, SADC Trade Negotiating Forum (TNF) on trade services under UNCTAD, and Curriculum Validation Committee of the NACTE.

He is a versatile resource person of the NBAA, Natural Resources Governance Institute (NRGI) and Commonwealth Secretariat (COMSEC). He has been given awards (23 by the NBAA, 2 by the NRGI, 2 by the JET, 1 by the COMSEC, 1 by UN-ESCAP, and 2 by the TUDARCO. He is a Certified Tax Practitioner with wealthy of experience in Tax Laws, International Legal Practice, Investment Laws, and Mining, Oil and Gas. Handley is an icon of reforms of Anti-drugs Unit, VAT, PPP Center, Gold Audit Program, and Tanzania Minerals Audit Agency.

He has vigorously been an artery in the formulation of the Income Tax Act, EMA Act, Mineral Policy, 2009; Mining Act, VAT Act; Income Tax (Transfer Pricing) Regulations, Tax Administration Act, The Oil and Gas Revenues Management Act, SADC Protocol on the Exchange of Information in Mineral sector, SADC-MoU on the Exchange of Information on Tax Matters, and Treaties.

Handley, has made 60 vetted publications, 4 Books including “Mineral Tax Clinic-A reflection of Old and New Fiscal Regime for Effective Tax Auditing in Tanzania ISBN: 978 9976 60 552 6:” Co-authored a Book edited by Professor Sijbren Cnossen “The Excise Tax Policy “Administration in the Southern African Countries ISBN 1-86888-366-3”.

He is an Associate Editor of the EAJR of Iringa University, a regular contributor and peer reviewer of the NBAA Journals and the Teofilo Kisanji University Journal.

Handley holds a Ph.D.(Inter. Economic Law), Ph.D(finance), Ph.D (Business Studies), MA(M&E), LL.M(Taxation), LL.M(Procedural & Intern-legal practice), MSc (finance), MBA(Mg-Economics), PGDip(Tax Mgt), LL.B, ADDip(Tax Mgt), ICSA(UK), ACCPA(AML), P3PCertified
Hongera zake kwa kipaji na bidii za kufanikisha hayo yote, he is a daring person. Big up Professor H. Mafwenga
 
Hyo logo ya CCM tu ndio imemuharbia CV
I don't think so. CCM ndiyo imetengeneza Serikali iliyopo madarakani. How do you segregate government performance from the ruling party. Unless you are ignorant of the facts
 
Naona kuna shida kidogo katika uelewa hapa; huyu Prof Mafwenga hajaonesha kwenye Business card yake kuwa amesoma Chuo gani naona watu hukurupuka tu na kushambulia na kumuita tapeli; Mimi namfahamu sana sana; huyu kasoma IFM, Tumaini University, ESAMI/Maastricht, Chuo Kikuu UDSM na anasoma Open University; Lazima tukubali kuwa huyu Bwana ni Icon kwenye elimu; Nina taatifa za kina za yeye kupigwa vita sana hata ndani ya Taasisi za Serikali na watu ambao wana penda vyeo; Huyu Bwana hana tabia ya kujikweza kihivyo ni mtu wa kujishusha sana, mcheshi na hajapandishwa wala kupata teuzi au kuwa na hamu ya kufanyiwa hivyo; Ninachojiuliza mbona hii business card miaka ya nyuma alituhumiwa kuweka nembo ya Chama cha Mapinduzi? Wabaya nyie mkashindwa; kwa hofu tu kuwa anagombea nafasi za kisiasa; Nakumbuka ilikuwa karibu na Uchaguzi na sasa ni Karibu na Uchaguzi; so far kama hakuna hila mbona nembo hiyo imefutwa kwanini Business Card yake isionekane kwa uhalisia wake? Lazima Watanzania tukiri kuwa na Watanzania wapenda elimu hapa angekuwa na ngozi nyeupe au anatoka familia ya vigogo angesifiwa; Ninavyomfahamu ana Advanced Diploma ya Tax kutoka IFM, ana Postgraduate Diploma ya Tax toka IFM, ana LL.B toka Tumaini University, ana MSc ya finance toka Strathclyde University ya Scotland Uingereza, ana MBA kutoka ESAMI/Maastricht ya Uholanzi ana LL.M ya Tax toka UDSM ana LL.M ya Procedural and International Legal Practice toka UDSM ana Ph.D toka Commonwealth University, na nasikia ana Ph.D kutoka Israel chuo na fani yake nahifadhi na sasa anasoma University of Dodoma na slip ya CRDB mmeonesha hapa ina maana nayo ni fake? Watesi wa huyu BWANA mrudieni Mungu anawaona huyu ni geneus nyie elimu za kwenu ziko wapi? Ninachofahamu ni kweli hakumaliza Ph.D UDSM kwa kukosa supervisors na kwa utafiti wanguu alikosa supervisors wa kwanza alikuwa Prof Asad akachomoa kumsupervise, wa pili alikuwa Dr Mariam Nchimbi akachomoa kumsupervise wa tatu alikuwa Dr Masoud akachomoa kumsupervise; Kijana wa watu akasajili MFA ya Oil and Gas UDSM chuo kikabadili ghafla course kutoka Executive Program kuwa full time akaamua kusajili LL.M ya Procedural Law and International Legal Practice ya Jioni na taarifa nilizofuatilia za huyu bwana ada yake ya MFA in Oil and Gas ilihamishiwa School of Law; Hao Staff mnaosema wanakataa kumaliza course kwa huyu bwana waulizeni hizi facts ambazo nimepewa na mmoja ya Dean wa Faculties hapo UDSM; Ebu tujiulize ni Mtanzania gani ana hizi sifa kwa sasa? Halafu Business Card yake ina simu zake lukuki kwanini asiulizwe ila tunakimbilia kumdhihaki Mtanzania Mwenzetu bure? Nilisoma Magazeti na baadhi ya groups kuwa yeye hapendi ulevi wala uzinzi ; Je wazinzi tumewadhihaki hapa? Tunahoji kama ana nyumba nimefuatilia ana ghorofa analoishi Bunju Mabwepande na anajenga lingine kwao Tukuyu fuatilieni; huyu hata katika kufuruku kimaisha mtamshangaa sana ni kiumbe wa ajabu sana; Kabla ya kuhuhumu na kutukana mpigieni simu muda wote yupo hewani hajikwezi; mengine mimi nimemuuliza direct na nime confirm huko UDSM mnakosema; halafu mnamtuhumu professorial status jamani Tumaini ipo hapa, Iringa University ipo hapa na Teofilo Kisanji ipo Hapa kaulizeni maana mmoja ya Wanafunzi kwenye group yetu amekiri kufundishwa naye, mmoja wa Wahasibu amekiri kuwa ni resource persons wa muda mrefu NBAA mpaka alipofika kiongozi mmoja hapo aliyefundisha naye IFM kuanza kumpiga vita ya ajabu sana; tunaenda wapi Watanzania? Badala ya kumpa moyo na support tunamtwanga twanga tu Mafwenga why? Mmoja wa Deans za Fcaulty au Schools hapo UDSM nilipomuuliza kuhusu Mafwenga kwanini alikosa Supervisions alikimbia mita mia kujibu ila akasema tulimlazimisha afanye deregistration ya PH.D ili afanye MFA ya Oil and Gas kwa vile Mwanafunzi hawezi kuwa na registration mbili, Nikamtafuta mmoja ya Wanafunzi ambao Mafwenga alisema alisoma nao akajibu kuwa Mzee wetu anapigwa vita sana angekuwa na roho ndogo angejinyonga; Mzee wetu tulisoma naye Semester nzima na alifanya tests zote kasoro semester exams course ikabadilishwa mzee wetu hatukumuona tena tuakasikia anafanya LL.M nyingine School of Law; Sasa najiuliza kwanini tusiamini elimu ya huyu mtu; Nashauri kuwa yeyote aliye kuwa injured na Mafwenga aende Mahakamani badala ya kumchafua;
Kwa maelezo haya huyu omar said kibwende ndiye Handley Mwafwenga Simba Malema. Huwezi kuwa details za maisha ya mtu ambazo ziko so detailed kama alvyoweka huyu

RIP Mafwenga
 
Muandishi hebu weka sawa hapa.Ana umri wa miaka 52 maana yake 2023-52=1971 kwa hiyo amezaliwa mwaka 1971.
Mwaka 1975 alimaliza kidato cha nne.Wakati huo alikuwa na umri wa miaka 5. Hebu weka sawa kwanza kwa jambo hili kabla hujaendelea habari za huyu mwamba.
Mimi mwenyewe ni kaka yake mwaka 1975 nilikuwa na umri wa miaka 10 lakini nilikuwa darasa la tatu.
No research no permission to talk or write.
Hata hivyo ni ubidamu labda umekosea kuandika.
 
Muandishi hebu weka sawa hapa.Ana umri wa miaka 52 maana yake 2023-52=1971 kwa hiyo amezaliwa mwaka 1971.
Mwaka 1975 alimaliza kidato cha nne.Wakati huo alikuwa na umri wa miaka 5. Hebu weka sawa kwanza kwa jambo hili kabla hujaendelea habari za huyu mwamba.
Mimi mwenyewe ni kaka yake mwaka 1975 nilikuwa na umri wa miaka 10 lakini nilikuwa darasa la tatu.
No research no permission to talk or write.
Hata hivyo ni ubidamu labda umekosea kuandika.
Kwenye umri huyu marehemu Mafwenga alitubagaza. Sidhani kama alizaliwa mwaka 1971. Angalia picha yake ya mwaka 2015 hapa
IMG-20230919-WA0033.jpg
 
Back
Top Bottom