Prof. Lipumba: Rais Samia hawezi kukwepa lawama kuhusu kukamatwa kwa Mbowe

Shujaa Mwendazake

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
3,735
6,292
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba, amesema Rais Samia Suluhu Hassan hawezi kukwepa lawama kufuatia tukio la kukamatwa kwa Mwenyekiti wa CHADEMA Mh Freeman Mbowe.

"Jeshi la Polisi lingeweza kumkamata Freeman Mbowe popote hata alipokuwa msibani, kama kweli kuna tuhuma zozote dhidi yake.Kumkamata kufuatia kongamano lao la Mwanza na kisha kudai kwamba anatuhumiwa kwa ugaidi, ni jambo linaloibua maswali mengi bila majibu.......CUF kinatoa wito kwa Serikali kupitia Jeshi la Polisi, kuwaachia viongozi wote wa CHADEMA wanaoshikiliwa kufuatia Kongamano la Mwanza" . Aliongeza Prof. Lipumba"

Pia Lipumba ameiomba Serikali imuachie huru Freeman Mbowe na wenzake, waliokamatwa jijini Mwanza, wakijiandaa kufanya kongamano la kudai Katiba Mpya.
 
Marais ambao hawakujiandaa kushika madaraka wataitesa hii Nchi, kinachotokea kwa Samia ndicho kilichotokea kwa Marehemu aka Shujaa Magufuli, wote hawa U - rais wameupata kwa kukutana nao kwenye kona, hawakujiandaa na stress za upinzani, stress za uchumi wala stress za Jamii, hasa katika dunia hii ya utandawazi.

Rais Samia anakosea sana anapodhani Bunge au Polisi watamsaidia kupata ahueni ya Stress, asipojipanga vizuri atakuwa Rais wa hovyo sana, bila shaka kusababisha Watanzania au Africa kutokuwa na imani juu ya uongozi wa mwanamke katika nafasi kubwa, tuliodhani tumepata, sasa tunaanza kudhani tumepatikana, Mungu atusaidie.

MBOWE SIO GAIDI........
 
Mimi team Marehemu Magufuli nilipanga kushauri Raisi Samia jamii forums amteue Proffesor Lipumba kuwa mbunge na waziri wa fedha nimegairi naomba ampe ubunge wa kuteuliwa Dr Idris Rashid na ampe uwaziri wa fedha akikataa ampe ubunge na amteue Rished Bade aliyekuwa kamishina wa TRA kuwa waziri wa fedha they are highly capable. TEAM Samia wako weak hawawajui watu wazuri

Kwa rank Proffesor Lipumba ndio namba one afaaye kuwa waziri wa fedha akifuatiwa na Namba mbili Dr Idris Rashid aliyekuwa gavana wa benki kuu wa Tatu ni Rished Bade aliyekuwa kamishina wa TRA hao wako fit hasa kwa post ya waziri wa fedha
 
True mkuu wa nchi kila kitu kinachotokea na kinachokuwa kimetoke kipo mezani kwake

Sasa anakwepaje lawama?
Kwani ametoa kauli yoyote?
Licha ya maswali mengi hivi tunachukuliaje Ugaidi,halafu tunasema tz sio kisiwa.
Tumejivua nguo
 
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba, amesema Rais Samia Suluhu Hassan hawezi kukwepa lawama kufuatia tukio la kukamatwa kwa Mwenyekiti wa CHADEMA Mh Freeman Mbowe.

"Jeshi la Polisi lingeweza kumkamata Freeman Mbowe popote hata alipokuwa msibani, kama kweli kuna tuhuma zozote dhidi yake.Kumkamata kufuatia kongamano lao la Mwanza na kisha kudai kwamba anatuhumiwa kwa ugaidi, ni jambo linaloibua maswali mengi bila majibu.......CUF kinatoa wito kwa Serikali kupitia Jeshi la Polisi, kuwaachia viongozi wote wa CHADEMA wanaoshikiliwa kufuatia Kongamano la Mwanza" . Aliongeza Prof. Lipumba"

Pia Lipumba ameiomba Serikali imuachie huru Freeman Mbowe na wenzake, waliokamatwa jijini Mwanza, wakijiandaa kufanya kongamano la kudai Katiba Mpya.
Ila ni endapo tu,hayo yanatoka moyoni,kwani yaweza kuwa ni namna yake ya kuwapongeza watesi na wabambikaji.
 
Ifikie wakati tuondokane na hili jeshi la kikoloni. Tunatakiwa tuwe na jeshi la kulinda raia na mali zao! Na siyo kuilinda ccm kwa gharama yoyote ile, hata kama haikubaliki kwa Watanzania walio wengi.
Kama hili au ?
images - 2021-07-24T170401.860.jpeg
 
Nasubiri vile vyama ambavyo kazi yao kuongeza idadi ya wagombea. Navyenyewe vinasemaje?
 
Back
Top Bottom