Prof. Lipumba anafaa kuwa Rais?

Penguini

JF-Expert Member
Apr 24, 2013
377
293
Prf Ibrahim Haruna Lipumba, amekuwa mwanasiasa aliyevuma miaka ya nyuma kdg, licha ya kuwa alikuwa mwenyekiti wa CUF amewahi kugombea nafasi ya kuwa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Na hilo wote tunajua,

Mwaka Jana (2015) katika harakati za kuelekea uchaguzi Lipumba alikuwa mwenyekiti mwenza katika umoja wa katiba ya wananchi, (UKAWA) ulioundwa chini ya ushirikiano wake na viongozi wa vyama vingine vya upinzani, sina haja ya kulielezea sana hili najua linafahamika, ulipofika wakati wa kugombea u Rais ukawa walikubaliana kumsimamisha mgombea mmoja;

Edward Lowassa aliyekuwa mgombea u Rais mwana CCM baada ya kukatwa kule akahamia kwenye umoja wa UKAWA kisha wakampa nafasi ya kugombea u Rais na viongozi wanaounda umoja huo prf. Alikuwa mmoja wao.

Muda mfupi mbele Lipumba aliandika barua ya kujivua uenyekiti na kukiacha chama chake alichokiunga kwenye ukawa (kama mwenyekiti mwenza), katika hali ya sintofahamu, lakini pia alipotea kabisa katika medani za siasa.

Sasa ni miezi kadhaa kuelekea mwaka, amerudi katika medani za siasa

na si tu kurudi kama mwanachama Bali kwa kuutaka uenyekiti aliojivua katika muda wa kuelekea uchaguzi na kukiacha chama katika hali ya taharuki.

Baada ya viongozi waliopo "kumkata" (katika uchaguzi wa viongozi wapya) anatangaza ubavu wa uwepo wake kama kiongozi.

Je CUF, wanaweza kumpokea vyema na kumpa madaraka tena?

Na je, kiongozi wa aina hii kama akipewa majukumu ya kuliongoza Taifa si hatari hii?
Je kama wakati alipogombea urais kura zingetosha kumpa ushindi, Tanzania ingekuwa katika hali gani?

Nadhani sasa ufike wakati vyama vya siasa viongeze mbinu za kuchuja au kutafuta wagombea. Ni afadhali uchaguzi ufanyike bila chama kuweka mgombea kuliko kuteua mgombea wa sampuli hiyo.
 
Akalime sasa, kaanza kugombea urais nipo chekechea leo nshamaliza hadi chuo Kikuu yeye ni mgombea tu....
Profesa gani hajielewi labda profesa wa mazingaombwe
 
Ha ha ha ha!
Sasa kama alikuwa CUF, pia katika ukawa chadema watampokeaje?
 
Prf Ibrahim Haruna Lipumba, amekuwa mwanasiasa aliyevuma miaka ya nyuma kdg, licha ya kuwa alikuwa mwenyekiti wa CUF amewahi kugombea nafasi ya kuwa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Na hilo wote tunajua,

Mwaka Jana (2015) katika harakati za kuelekea uchaguzi Lipumba alikuwa mwenyekiti mwenza katika umoja wa katiba ya wananchi, (UKAWA) ulioundwa chini ya ushirikiano wake na viongozi wa vyama vingine vya upinzani, sina haja ya kulielezea sana hili najua linafahamika, ulipofika wakati wa kugombea u Rais ukawa walikubaliana kumsimamisha mgombea mmoja;

Edward Lowassa aliyekuwa mgombea u Rais mwana CCM baada ya kukatwa kule akahamia kwenye umoja wa UKAWA kisha wakampa nafasi ya kugombea u Rais na viongozi wanaounda umoja huo prf. Alikuwa mmoja wao.

Muda mfupi mbele Lipumba aliandika barua ya kujivua uenyekiti na kukiacha chama chake alichokiunga kwenye ukawa (kama mwenyekiti mwenza), katika hali ya sintofahamu, lakini pia alipotea kabisa katika medani za siasa.

Sasa ni miezi kadhaa kuelekea mwaka, amerudi katika medani za siasa

na si tu kurudi kama mwanachama Bali kwa kuutaka uenyekiti aliojivua katika muda wa kuelekea uchaguzi na kukiacha chama katika hali ya taharuki.

Baada ya viongozi waliopo "kumkata" (katika uchaguzi wa viongozi wapya) anatangaza ubavu wa uwepo wake kama kiongozi.

Je CUF, wanaweza kumpokea vyema na kumpa madaraka tena?

Na je, kiongozi wa aina hii kama akipewa majukumu ya kuliongoza Taifa si hatari hii?
Je kama wakati alipogombea urais kura zingetosha kumpa ushindi, Tanzania ingekuwa katika hali gani?

Nadhani sasa ufike wakati vyama vya siasa viongeze mbinu za kuchuja au kutafuta wagombea. Ni afadhali uchaguzi ufanyike bila chama kuweka mgombea kuliko kuteua mgombea wa sampuli hiyo.
kwahili analolifanya Lipumba nachelea kumuita prof, hili limekuja ili watanzania tujue ni jinsi gani ccm imeweza kucheza na akili zetu katika kila chaguzi kwa kupitia viongozi kama Lipumba, Mrema, Dovutwa nk, wakituaminisha kuwa ni wagombea wa upinzani ilihali ni wagombea wenza wa ccm, angalia jinsi leo Lipumba anavyoivuruga cuf kwa maksudi kabisa, na bado kuna kundi nyuma yake ambalo limesahau alivyoivuraga cuf tena kwa maksudi kabisa miezi micjache iliyopita. ukitaka kujua anafanya kazi kwa niaba ya nani fikiria jinsi alivyohamisha agenda ya cuf kudai wanachokidai zanzibar mpaka kuanza kujadili mtu. hali hii inawanufaishi wenzetu wa ccm na ndomaana wao ndio wanaomsapoti mitandaoni na kwengineko, "haya mahaba ya ccm na lipumba hayajaanza juzi ila tumechelewa tu kuyajua". Hatuna jinsi tutaendelea kuvumilia tu na kuwaangalia wanasiasa mnavyotuburuza maana mmeshajua udhaifu wa watanzania waliowengi, na wala tusiwalaumu ccm kwenye hili maana ni sayansi ya siasa.
 
Prof.Lipumba kwa sasa hana sura ya kuwa mpinzani,hana sura ya kuwa Mwenyekiti wa CUF,hana sura ya kulipigania Taifa kama prof.mwanasiasa.
Kuna tofauti kubwa sana katika siasa ya vyama vyetu nchini kwa mfano: CCM ni chama tawala chenye misingi na mbinu nyingi sana za kisiasa,CHADEMA ni chama cha kiharakati kilichojificha katika siasa za Tanzania hali kadhalika CUF ni chama cha Kikombozi ambacho kinahitaji HAKI SAWA KWA wote kama kinavyojieleza,chama hiki (CUF) kinaamini kuwa Tanzania hakuna haki hususani kule visiwani.

Prof.Hawezi kuongoza chama cha kikombozi kama CUF.Ingefaa zaidi kwa Mh.Edward Lowassa mwenye kila aina ya sifa ya kuwa kiongozi bora katika UKOMBOZI wa Taifa kukiongoza chama cha CUF kama mwenyekiti na huku nyuma yake kukiwa na mtu makini kama James Mbatia mwanasiasa mwenye maono yenye mashiko sana.

Mbowe na wenzake wakina Lissu,Mnyika na wengine wangeendelea kuja na opresheni zao za KIHARAKATI za kuiongia barabarani kila siku kudai uhuru wa kuzungumza.Lipumba kwa sasa angepumzika tu na kuwaacha wenye fikra zao kusonga mbele,Kama mh.rais wetu ni dikteta je anachokifanya huyu Prof.Lipumba kutaka kuendelea kuwa mwenyekiti wa CUF bila uchaguzi kinaimarisha DEMOKRASIA?

Moja kati ya sababu ambazo alianisha wakati akijiuzulu ni kuhusu mchakato wa upatikanaji wa mgombea urais wa UKAWA kwamba haukuwa wa kidemokrasia,vipi yeye leo hii?

Anasema yeye ndio mwenyekiti wa CUF na hautambui mkutano uliokaa hivi juzi na kuharibiwa na wafuasi wake,Je kuna mtu ambaye anajiuzulu na kuendelea kupewa fursa ya kiuongozi katika taasisi hiyo?
Anasema mkutano ule haukuwa na uhalali hali ya kuwa yeye si kiongozi wa CUF,amepata wapi mamlaka za kuharamisha mkutano wa viongozi wakuu ngazi ya TAIFA?

kwa jinsi nilivyo Mchovu Wa Fikra nawaza kuwa prof.Lipumba halitakii mema taifa hili.CCM wameshamtumia na hakuna manufaa katika utumiwaji wake anataka chance nyingine ya kukibomoa chama hapo 2020.
CUF kuna maslahi yanayomkosesha raha prof.?
 
Wewe sio tu ni mchovu wa fikra lakini mvivu na doro wa kufikiri. Rais wa nchi anatakiwa mtu mwenye msimamo, mwenye maono , kujiamini na mwenye maamuzi. Huyu mtu unaempigia upatu hana sifa hizo za msingi. Mwana siasa huyu ni mzuri kumtumia kunenepesha matumbo ya watu.

Rais akiona kuna tatizo kubwa katika nchi kama vile la uhaba wa sukari tu,siku ya pili anajiuzulu. Akitokezea fisadi na kuingiza sukari kwa wingi anazinduka na kudai kwa ukali urais wake!Nchi haiongozwi kama hivyo.

Haiwi ngoma ya beni bati, inasheria na taratibu zake. Wachezaji hawafuati tu midundo lakini na kiranja mwenye usinga,akipinda kulia wachezaji wote huelekea kulia. Sio ngoma ya kumbwaya wachezaji hucheza na kuhemkwa wapendavyo. Nchi inahitaji kiongozi mwenye kuheshimu uamuzi wake, sio Rais wa kukurupuka.
 
Wewe sio tu ni mchovu wa fikra lakini mvivu na doro wa kufikiri. Rais wa nchi anatakiwa mtu mwenye msimamo, mwenye maono , kujiamini na mwenye maamuzi. Huyu mtu unaempigia upatu hana sifa hizo za msingi. Mwana siasa huyu ni mzuri kumtumia kunenepesha matumbo ya watu.

Rais akiona kuna tatizo kubwa katika nchi kama vile la uhaba wa sukari tu,siku ya pili anajiuzulu. Akitokezea fisadi na kuingiza sukari kwa wingi anazinduka na kudai kwa ukali urais wake!Nchi haiongozwi kama hivyo.

Haiwi ngoma ya beni bati, inasheria na taratibu zake. Wachezaji hawafuati tu midundo lakini na kiranja mwenye usinga,akipinda kulia wachezaji wote huelekea kulia. Sio ngoma ya kumbwaya wachezaji hucheza na kuhemkwa wapendavyo. Nchi inahitaji kiongozi mwenye kuheshimu uamuzi wake, sio Rais wa kukurupuka.
Umesoma kichwa cha habari na ku comment, kisha umeniita mvivu, na mchovu, ila kwa mujibu wa maelezo ya comment yako inadhihirisha kabisa hukusoma maudhui yaliyomo ndani "mkuu" wewe ndiyo mvivu soma uone uvivu wako ulipo!!
 
Back
Top Bottom