johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 82,754
- 139,562
Kwanza sielewi kiitifaki imekaaje pale mteule wa Rais anapoamua kujibu kwa niaba ya Rais pasipo kuagizwa tena Rais mwenyewe akiwepo mahali hapo.
Pili, Prof Lipumba alitoa ombi/ kumbusho na siyo swali kwamba ikimpendeza Rais Magufuli atuachie katiba mpya.
Tatu, Jaji Mutungi amemtaka Prof Lipumba ahakikishe wabunge wa upinzani hawasusii vikao vya bunge ili kutokwamisha utendaji wa bunge. Kwani wapinzani wako wangapi bungeni kwamba wakisusa shughuli za bunge zitasimama?
Leo niamini CCM iko kila kona kwakweli.
Maendeleo hayana vyama!
=============
Leo Rais Magufuli alikuwa kwenye maadhimisho ya miaka 100 ya mahakama na alipomaliza hotuba yake alimkaribisha Profesa Ibrahimu Lipumba,Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) kusalimia, ifatayo ni sehemu ya salamu yake.
MAGUFULI: Mwenyekiti Lipumba, njoo usalimu hapa kidogo professa, tukae tu tumsikilize kidogo apige lugha, hatujamuona halafu amenenepa kweli baada ya uchaguzi. Mzee Lipumba njoo usalimu hapa angalau dakika moja tafadhali. Kwa ruhusa yako mheshimiwa Jaji mkuu naomba asalimu kidogo.
LIPUMBA: Mheshimiwa Rais, Mheshimiwa Jaji mkuu, itifaki imezingatiwa. Mimi nikialikwa na majaji lazima nifike, mahakama inaponialika siku ya sheria najitahidi kuja kwa sababu hujui IGP Sirro anaweza akakupeleka huko. Kwahiyo wakiwa wanakuonaona wanajua kabisa kwamba huyu ni mtu wetu.
Jaji mkuu ameeleza vizuri kazi ambayo Rais umeifanya ya kuweza kuisaidia mahakama kujenga miundombinu, nakumbuka ulipoingia madarakani 2016 palikuwa na tatizo ya bajeti ya maendeleo, kwenye siku ya mahakama ulipokwenda Dar es Salaam ukasema bajeti yote ya maendeleo ya mahakama naipitisha hapa na kwa mara ya kwanza fedha yote ya bajeti ya maendeleo wakaipata idara ya mahakama kama ilivyopangwa.
Ulipokuwa unatoa hotuba tarehe 20 Novemba 2015 ulisema kwamba pana kiporo kiliachwa cha kukamilishwa swala ambalo watanzania wengi walishiriki kutoa maoni yao ili iweze kupatikana katiba mpya, ukasema kwenye hotuba hiyo, hilo umelipokea na wewe utalitekeleza.
Na vilevile ulipokuwa unapokea ripoti ya tume ya uchaguzi 2016 ulisema kabisa kwamba, masuala yale ambayo yamo kwenye katiba iliopendekezwa na kama kuna watu wana maoni mengine, serikali yako iko wazi itapokea.
Kwahiyo mimi nashukuru kwa kusema kwamba vile viporo vyote ulivyovitoa ambavyo havijatekelezwa 2015 alivyovieleza katika, miaka hii mitano utavitekeleza.
Na natoa wito na nakuombea kwa Moyo wa dhati kabisa, mwenyezi Mungu akupe nguvu, hivi viporo vyote katika kipindi hiki uweze kuvitekeleza, unapomaliza kipindi chako watu watakaoweza kuyalinda mafanikio uliyoyaleta katika nchi yetu ni kuwa na Katiba inayotokana na mapendekezo ya wananchi wa Tanzania.
Natoa wito na kwa bahati wewe mwenyewe ulikuwa mjumbe wa Bunge maalum la Katiba na mama Samia ndio alikuwa makamu mwenyekiti wa Bunge maalum la katiba, kuna wazee wazito kina Prof. Kabudi, huyu bado kijana lakini ndio walikuwa wajumbe wa Tume ya Jaji Warioba, kuna vijana wako, Polepole ndio alikuwa mjumbe wa Tume ya katiba, kuna watu wamekuzunguka wajumbe, Naibu Spika tena tulikuwa nae kwenye kamati moja na yeye ndio aliongoza kamati ya Chuo Kikuu.
JAJI MUTUNGI: Mimi nimesimamishwa hapa kama Msajili wa Vyama vya Siasa, bila kigugumizi chochote naweza nikasema hata vyama vya siasa vimekuwa na imani kubwa na mahakama zetu ndio maana unaona kila nikitoa maamuzi wanakimbilia mahakama.
Ninachowaomba kama alivyosema mheshimiwa Rais, msitumie mahakama kwenda kupaki kesi za msajili ila mzidi kuonyesha imani yenu kwa mahakama, kitendo ambacho naomba tuwapigie tena makofi kwasababu vyama vya siasa mpaka kuiamini mahakama kuleta kesi zao kwako, mheshimiwa Jaji mkuu mahakama mnastahili kupigiwa makofi.
Kwasababu sikupewa nafasi kubwa ya kuhutubia, nirudi kwa ndugu yangu mwenyekiti wa chama cha CUF, mheshimiwa Rais nimesikia anakuomba kuhusiana na Katiba, nilijua lazima wanasiasa watakumbushia mambo ya katiba lakini naomba kumuambia mheshimiwa mwenyekiti akawaambie wenzanke ule mchezo wa kutokatoka kwenye mabunge kukwamisha shughuli ya haya masuala muhimu ya kitaifa basi wayapunguze, mwaka 2021 tuwe ni watu wenye uzalendo tukiwa na masuala ya kitaifa, mambo ya kuinuka inuka kutoka kwenye Bunge hayo tuyaache. asanteni sana.
Pili, Prof Lipumba alitoa ombi/ kumbusho na siyo swali kwamba ikimpendeza Rais Magufuli atuachie katiba mpya.
Tatu, Jaji Mutungi amemtaka Prof Lipumba ahakikishe wabunge wa upinzani hawasusii vikao vya bunge ili kutokwamisha utendaji wa bunge. Kwani wapinzani wako wangapi bungeni kwamba wakisusa shughuli za bunge zitasimama?
Leo niamini CCM iko kila kona kwakweli.
Maendeleo hayana vyama!
=============
Leo Rais Magufuli alikuwa kwenye maadhimisho ya miaka 100 ya mahakama na alipomaliza hotuba yake alimkaribisha Profesa Ibrahimu Lipumba,Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) kusalimia, ifatayo ni sehemu ya salamu yake.
MAGUFULI: Mwenyekiti Lipumba, njoo usalimu hapa kidogo professa, tukae tu tumsikilize kidogo apige lugha, hatujamuona halafu amenenepa kweli baada ya uchaguzi. Mzee Lipumba njoo usalimu hapa angalau dakika moja tafadhali. Kwa ruhusa yako mheshimiwa Jaji mkuu naomba asalimu kidogo.
LIPUMBA: Mheshimiwa Rais, Mheshimiwa Jaji mkuu, itifaki imezingatiwa. Mimi nikialikwa na majaji lazima nifike, mahakama inaponialika siku ya sheria najitahidi kuja kwa sababu hujui IGP Sirro anaweza akakupeleka huko. Kwahiyo wakiwa wanakuonaona wanajua kabisa kwamba huyu ni mtu wetu.
Jaji mkuu ameeleza vizuri kazi ambayo Rais umeifanya ya kuweza kuisaidia mahakama kujenga miundombinu, nakumbuka ulipoingia madarakani 2016 palikuwa na tatizo ya bajeti ya maendeleo, kwenye siku ya mahakama ulipokwenda Dar es Salaam ukasema bajeti yote ya maendeleo ya mahakama naipitisha hapa na kwa mara ya kwanza fedha yote ya bajeti ya maendeleo wakaipata idara ya mahakama kama ilivyopangwa.
Ulipokuwa unatoa hotuba tarehe 20 Novemba 2015 ulisema kwamba pana kiporo kiliachwa cha kukamilishwa swala ambalo watanzania wengi walishiriki kutoa maoni yao ili iweze kupatikana katiba mpya, ukasema kwenye hotuba hiyo, hilo umelipokea na wewe utalitekeleza.
Na vilevile ulipokuwa unapokea ripoti ya tume ya uchaguzi 2016 ulisema kabisa kwamba, masuala yale ambayo yamo kwenye katiba iliopendekezwa na kama kuna watu wana maoni mengine, serikali yako iko wazi itapokea.
Kwahiyo mimi nashukuru kwa kusema kwamba vile viporo vyote ulivyovitoa ambavyo havijatekelezwa 2015 alivyovieleza katika, miaka hii mitano utavitekeleza.
Na natoa wito na nakuombea kwa Moyo wa dhati kabisa, mwenyezi Mungu akupe nguvu, hivi viporo vyote katika kipindi hiki uweze kuvitekeleza, unapomaliza kipindi chako watu watakaoweza kuyalinda mafanikio uliyoyaleta katika nchi yetu ni kuwa na Katiba inayotokana na mapendekezo ya wananchi wa Tanzania.
Natoa wito na kwa bahati wewe mwenyewe ulikuwa mjumbe wa Bunge maalum la Katiba na mama Samia ndio alikuwa makamu mwenyekiti wa Bunge maalum la katiba, kuna wazee wazito kina Prof. Kabudi, huyu bado kijana lakini ndio walikuwa wajumbe wa Tume ya Jaji Warioba, kuna vijana wako, Polepole ndio alikuwa mjumbe wa Tume ya katiba, kuna watu wamekuzunguka wajumbe, Naibu Spika tena tulikuwa nae kwenye kamati moja na yeye ndio aliongoza kamati ya Chuo Kikuu.
JAJI MUTUNGI: Mimi nimesimamishwa hapa kama Msajili wa Vyama vya Siasa, bila kigugumizi chochote naweza nikasema hata vyama vya siasa vimekuwa na imani kubwa na mahakama zetu ndio maana unaona kila nikitoa maamuzi wanakimbilia mahakama.
Ninachowaomba kama alivyosema mheshimiwa Rais, msitumie mahakama kwenda kupaki kesi za msajili ila mzidi kuonyesha imani yenu kwa mahakama, kitendo ambacho naomba tuwapigie tena makofi kwasababu vyama vya siasa mpaka kuiamini mahakama kuleta kesi zao kwako, mheshimiwa Jaji mkuu mahakama mnastahili kupigiwa makofi.
Kwasababu sikupewa nafasi kubwa ya kuhutubia, nirudi kwa ndugu yangu mwenyekiti wa chama cha CUF, mheshimiwa Rais nimesikia anakuomba kuhusiana na Katiba, nilijua lazima wanasiasa watakumbushia mambo ya katiba lakini naomba kumuambia mheshimiwa mwenyekiti akawaambie wenzanke ule mchezo wa kutokatoka kwenye mabunge kukwamisha shughuli ya haya masuala muhimu ya kitaifa basi wayapunguze, mwaka 2021 tuwe ni watu wenye uzalendo tukiwa na masuala ya kitaifa, mambo ya kuinuka inuka kutoka kwenye Bunge hayo tuyaache. asanteni sana.