Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,868
Waziri wa Sheria, Prof Kabudi ameikosoa kampeni ya RC wa Dar, Paul Makonda ya kuwasaidia wanawake waliotelekezwa asema ilitakiwa kuwa ya faragha
Aidha kwa upande mwingine Mbunge wa Viti Maluum (Chadema), Sabrina Sungura amemtaka Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Palamagamba Kabudi atakapojibu hoja za wabunge waliochangia mjadala wa bajeti ya wizara hiyo mwaka 2018/19, kueleza sababu za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuvunja sheria mbalimbali za nchi.
Akizungumza katika mjadala huo leo Aprili 18 bungeni, Sabrina amesema moja ya sera zinazovunjwa na mkuu huyo wa mkoa ni pamoja na kuvunja mabaraza ya ardhi ya kata yaliyopo kisheria.
“Huyu mkuu wa mkoa, hivi sasa amesababisha hata hayo mabaraza hayafanyi kazi, ni kwanini anavunja sheria namna hii?” Amehoji Sungura.