Prof. Kabudi kama huwezi kujibu hoja, kaa kimya

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
48,776
102,134
EU wametoa hoja zao ambazo ni kukosekana demokrasia kwenye uchaguzi mkuu, polisi kuhujumu uchaguzi, na kupokea pesa za Corona wakati tulisema hatuna Corona. Hizi ndio hoja za EU ambazo kaka Msando amekwepa kuzijibu badala yake amemshambulia mtoa hoja (McAllister) na chama chake.

Lakini tujiulize je madai ya EU ni ya uongo? Je vyombo vya dola havikutumika kuvuruga uchaguzi? Je, watu hawakukamatwa? Je hakuna walioripotiwa kuuawa? Je hatukuchukua pesa za corona? Kwanza kuchukua pesa za Corona wakati tulisema hatuna Corona ni utapeli. Serikali imejipatia pesa kwa njia za udanganyifu. Hii ni jinai, na ni uhujumu uchumi.

Kwanini tunaacha kujadili hoja za EU tunawashambulia watoa hoja? Urafiki wa McAllister na Lissu haundoi ukweli kwamba tumetapeli hela za Corona. Wala urafiki wa Chadema na CDU hauondoi ukweli kwamba uchaguzi ulivurugwa na vyombo vya dola.

Hata kama McAllister angekuwa rafiki wa CCM bado hoja za kamati yake haziwezi kupuuzwa. Kaka Msando ni rafiki mkubwa wa kaka yangu mwingine Ally Bananga japo wanatofautiana vyama. Je, ikitokea Msando akafanya kosa huko CCM, halafu CCM wakamhukumu kwa sababu ya urafiki wake na Bananga ataridhika?

Tujadili hoja za EU na kuzitolea majibu bila kuwashambulia viongozi wake. Hoja za EU hata zingetolewa na mwanafunzi wa darasa la 3B kule Manda Ludewa, bado zingehitaji majibu. Tuhadili hoja, tusiwajadili watoa hoja.!

Msando Alberto aliandika kuhusu mjadala unaoendelea bunge la Ulaya kuhusu Tanzania kupokea pesa za Corona, pamoja na mapendekezo ya kamati ya mambo ya nje kutunyima msaada kwa sababu ya udanganyifu kwenye uchaguzi, wizi wa kura, watu kuuawa na wengine kutupwa jela. Wanahoji kama kuna haja ya kuendelea kuipa msaada nchi isiyoheshimu demokrasia.

Msando amedai tishio la EU kutunyima msaada ni kutokana na ushirika uliopo kati ya Chadema, CDU, Konrad Adenauer Stiftung na David McAllister.

Anadai kwa kuwa CHADEMA na chama cha CDU cha Ujerumani (anachotoka McAllister) ni wajumbe wa shirikisho la vyama vya kidemokrasia duniani (IDU), basi Chadema itakua imetumia nafasi hiyo "kuiharibia" Tanzania, hasa kwa kuwa McAllister ndiye Makamu Mwenyekiti wa IDU.

Ukivuliwa nguo chutama

Credit: G. Malisa
 
Katika maisha ata kama unacho kidogo jitahid kukisimamia hicho hicho, lakin pale unapo acha mwanya afu mtu mwingine anataka akutawale kifikra apo unaweza jikuta unapoteza kila kitu

Sasa pro. Kabudi yeye alichokifanya ni kusimama katika kile anachokiamini kama kiongonzi mwenye maono ya mbali katika nchii hi ya Mh JPM
 
Mwambie huyo Bwana yako Malisa uwezo wake wa kujua mambo ni mdogo sana! Sawa na kulinganisha Kichuguu (Malisa) na Mlima Kilimanjaro (Prof. Kabudi)
 
Tena ushukuru Mungu wewe hajakuumba kuwa Kabudi, lakini katika mazingira ya utendaji wa serikali za kiafrika hususani ukiwa chini ya Rais wa aina ya Magufuli aliyoyasema Kabudi ni mwanzo mzuri wa kukabili mashambulizi.

Boss anapenda Kabudi awe vile, maana ndio kwake ndio tafsiri ya kuchapa kazi.

Kabudi amenena vizuri kwasbabu maneno aliyoyasema yanampendeza Boss na sio wewe wala mabeberu.
 
Hopeless ni wewe unaetetea kila utumbo
Hata wakina mambosasa na sirro hawakuwa hivi.
Na imewabidi wawe hivi kulinda vyeo vyao ,kwa kumplease mkuu.
Ukweli awamu kuna nakosa mkubwa ya waziwazi,lakini ni nani mwenyewe ubavu wa kusimama hadharani na kukosoa?
Wewe unawatetea wakina Amsterdam na vibaraka wao au?
 
Katika maisha ata kama unacho kidogo jitahid kukisimamia hicho hicho, lakin pale unapo acha mwanya afu mtu mwingine anataka akutawale kifikra apo unaweza jikuta unapoteza kila kitu

Sasa pro. Kabudi yeye alichokifanya ni kusimama katika kile anachokiamini kama kiongonzi mwenye maono ya mbali katika nchii hi ya Mh JPM
wale wale tu,eti kusimamia ubachokiamini
 
13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom