Prof. Kabudi aieleza Jumuiya ya Kimataifa kuwa Tanzania haijawahi kushindwa vita ya aina yoyote

Hii dunia ni ngumu sana kuielewa, kina Pompeo wanahubiri katika mataifa mengine free and fair election, viongozi wakubali matokeo ya uchaguzi wakati huo Pompeo hamtambui na kumkubali Biden kama mshindi halali wa USA, hii inatuambia nini ndugu zangu?
 
Lakini kwa kauli hizi za paniki tutakaoumia ni sisi Watanzania wa kawaida.

Halafu sioni Kabudi akimaliza miaka mitano ya Uwaziri, mbinyo ukizidi yeye ndio atakaetolewa kafara.
...🤔🤔🤔...
 
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi amesema Tanzania haitakubali kudhalilishwa utu na heshima yake kama nchi huru, kupigishwa magoti kupata misaada na mikopo kutoka katika nchi yoyote duniani.
Safi sana japo Lissu na Zitto watakuwa na hasira za sisi kukataa ushoga ila habari ndiyo hiyo. Tuwaachie wao wenyewe huo ushoga.
 
Huyu jamaa alinifanya nihairishe kusomea PHD pamoja na kuchaguliwa kusomea kozi hiyo Mlimani.

Yaani ukimuangalia unaona kabisa anaongea aliyotumwa akaseme Prof mzima unalazimishwa kuongea pumba kwa ajili ya kulinda nafasi yako
Kipi bora kulinda taaluma au kulinda tumbo
 
Hii dunia ni ngumu sana kuielewa, kina Pompeo wanahubiri katika mataifa mengine free and fair election, viongozi wakubali matokeo ya uchaguzi wakati huo Pompeo hamtambui na kumkubali Biden kama mshindi halali wa USA, hii inatuambia nini ndugu zangu?
Wao mawazo binafsi sio mawazo ya wote sisi mawazo binafsi ya mtawala ndiyo sheria.Wao uongozwa kwa katiba na sheria sisi uongozwa na maagizo
 
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi amesema Tanzania haitakubali kudhalilishwa utu na heshima yake kama nchi huru, kupigishwa magoti kupata misaada na mikopo kutoka katika nchi yoyote duniani...
Hii wizara naona Prof Kabudi imeshampwaya kabisa, pengine wamjaribu sasa January Makamba ama Emmanuel Nchimbi ambaye pia anaweza kuteuliwa kuwa mbunge

Sent from my Nokia 2.1 using JamiiForums mobile app
 
Huyu ana ukichaa.

Kila siku anapigiwa simu na Magufuli usiku na kuambiwa mpumbavu (Rais Magufuli aliwaeleza Watanzania wote, ikiwa ni oamoja na wake na watoto wa Kabudi ja Mpango), naye anakenua meno. Kama angekuwa ni mtu anayejali heshima yake, si angejiuzulu siku hiyo alipoambiwa mpumbavu kwa mara ya kwanza.

Kila siku, yeye na Mpango wanaambiwa wapumbavu, wanakenua meno, halafu leo atuambie eti analinda utu na heshima ya Taifa. Ameshindwa kulinda utu na heshima yake binafsi, halafu anaongelea Taifa!!

Na Magufuli kawateua wao wawili tu ili apate wa kuwaambiwa wapumbavu kila siku, akijua kwa ujuha wao watafurahia. Nadhani wasipotukanwa huwa wanachanganyikiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
.......Ningependa kujua hao wapiga makofi ni akina nani. Bila shaka watakuwa ni akina Bia yetu, Johnthebaptist, magu2016, Jane Lowassa, mama D.... Nchi yaani ina watu wengi sana wasiojitambua. Wako kama mbwa. Wakipata chakula tu basi kazi yao ni kutikisa mkia tu kila wanapomwona anayewapa chakula!
Hawa watu ni wachumia tumbo hatari, hawana utu kabisaa. Labda hata siyo Watanzania
 
Niwakumbusheni tuu izo fedha za misaada zinatoka kwa wananchi walipa kodi barani ulaya. Wana haki ya kuhoji inakuwaje zinapewa serekali ambazo hazi heshimu haki za binaadamu.

Kuanza kutishia kama umeshinda vita ya Iddi Amini na kuanza kukimbilia kama TZ ni taifa huru. Nadhani ni yale yalioolezwa na hao wabunge namnukuu mmoja wao "..the relation with Tanzania has been difficult". Hii inatoa picha kamili kama uongozi wa Tanzania haufahamu kinachojadiliwa na kupelekea uhusiano wake kuwa mgumu kimataifa. Ukipewa msaada wa kukabiliana na covid na kupewa muongozo na WHO, halafu ukafanya tofauti sasa utarajie nini kutoka kwa mfadhili ? Ataridhishwa tuu na kuanza kupiga makofi ?

Nadhani uongozi wa Tanzania ujitafakari hususan katika masuala ya haki za binadaamu, demokrasia na uhusiano wa kimataifa.Prof. Kabudi na wenzake waache kuwa defensive na badala yake watumie mapungufu hayo kuboresha hali ilivyo. Huu ndio mtazamo wa mtu anaependa maendeleo.
 
Wakati tunajipanga kujidhatiti kutopokea mikopo toka nchi wahisani,tujipange kurudisha fedha zao Eu 27M,nadhani huo ndio uungwana na utu wenyewe ambao Kabudi anasisitiza
 
21 November 2020

WAZIRI WA MAMBO YA NJE TANZANIA PROFESA PALAMAGAMBA KABUDI AWAJIBU MABEBERU, HATUJAWAHI KUPIGISHWA MAGOTI, UCHAGUZI ULIKUWA HURU NA HAKI

Waziri wa Mambo ya Nje Prof. Palamagamba Kabudi aijibu EU - Umoja wa Ulaya kufuatia kikao cha bunge hilo la ulaya huko makao makuu ya EU kutishia uwezekano wa vikwazo kupitia Kamati yake Mambo ya Nje ya Bunge la Umoja wa Ulaya kujadili uwezekano wa kuibana Tanzania kwa vikwazo vya aina mbalimbali ikiwemo kusitisha msaada wa kuifadhili bajeti ya Maendeleo ya Tanzania.

Prof. Palamagamba Kabudi ameomba msaada wa vyombo vya habari nchini kuisaidia serikali ya Tanzania kwa kujitokeza na kuieleza Jumuiya ya Kimataifa ukweli wa mambo. Na kueleza Nyerere aliwahi kuwadindia Germany na United Kingdom na kukataa misaada na fedha zao. Prof. Palamagamba Kabudi anashangaa waTanzania kuanza kutetemeka ktk mitandao ya kijamaii kuhusu nchi yetu kuwekewa vikwazo.

Prof. Palamagamba Kabudi amesema Tanzania haifuati sera za kidiplomasia za kujitenga kufanya kazi na Jumuiya za Kimataifa. Hivyo waziri Prof. Kabudi amesema Tanzania ipo tayari kukaa ktk meza moja na wadau wa kimataifa kuzungumzia mapungufu yaliyopo lakini si kwa kuburuzwa na mabeberu bila kuwa na facts mezani.

Prof. Palamagamba Kabudi amesema kuwa watu wahuni wachache wa Kamati ya Mambo ya Nje ya Bunge la Ulaya EU hawawezi kuitisha na kuidhalilisha Tanzania na watambue Tanzania ni nchi huru.

Prof. Palamagamba Kabudi amesema maneno hayo mazito akiongea na Wafanyakazi wa Wizara hiyo muhimu ya Mambo ya Nje akatumia fursa hiyo kujibu uvumi kuwa Tanzania itanyimwa misaada na kuwakumbusha wafanyakazi hao kutembea vifua mbele kwani Tanzania siyo nchi ndogo kidiplomasia, kimsimamo, kiji-Geopolitiki na kiushawishi kimataifa.

.....................................................

EU Parliament Committee on Foreign Affairs discussion on Tanzania​

Tujikumbushe walioitwa "wahuni wachache" na Prof. Kabudi, tarehe 19 November 2020 jijini Brussels kwa dakika 45 mfululizo walisema nini kuhusu Tanzania ktk kikao cha Kamati ya Mambo ya Nje cha Bunge la Jumuiya ya EU
Tazama / sikiliza dakika 45 za mjadala ktk kamati hiyo:

Waziri kabudi hafai kabisa.
 
Huyu mzee atavuliwa nguo na hatoamini kama nyeti anazoziona ni zake.

Beberu atamuuliza ulipata kura ngapi kwenye jimbo lako, atajibu demokrasia ililkua safi nilipita bila kupingwa mana wapinzani wangu 12 wote walikosea kuandika majina yao kwenye fomu.
 
Back
Top Bottom