Prof. Kabudi aieleza Jumuiya ya Kimataifa kuwa Tanzania haijawahi kushindwa vita ya aina yoyote

kweli wameapa kutumikia watu lakini hawajaapa kudharauliwa na wazungu kwa ajili ya misaada, BORA KUFA UMESIMAMA KULIKO KUISHI UMEPIGA MAGOTI.
Wale pesa za corona makusudi kwa wizi kisha wasingizie ni dharau za wazungu? CCM acheni ujinga wenu acheni dharau kwa watanzania msidhani ni wajinga hivyo
 
Anawafokea mabeberu kisa kasoro za uchafuzi mkuu wa mwaka huu 2020?
Anaongea na watu ambao hawana uwezo hata wa kumuuliza swali pale dodoma ati wanasema anawajibu umoja wa ulaya??? Mbele ya watumishi wa umma mbumbumbu wa Tanzania???? Yule prof wa wapi??
 
Kabudi ni binadamu anayejiita msomi lakini ni binadamu wa kwanza kichwani mwake kufutika vyote anavyojidai alivisomea, kwa sasa kabudi ni level ya Lipumba wote wamesalia na darasa la nne tu kwenye Ubongo hakuna Taaluma wala maarifa tena imesalia mikwara ya kichaa cha dog
 
Anaongea na watu ambao hawana uwezo hata wa kumuuliza swali pale dodoma ati wanasema anawajibu umoja wa ulaya??? Mbele ya watumishi wa umma mbumbumbu wa Tanzania???? Yule prof wa wapi??
Kabudi siyo profesa bali ni yule Profeselii wa Olijino comedy mwenye taaluma ya darasa la nne tu
 
Hahahahaa

Ndio uhuru Kabudi jicho pima anautaka!

EU ifanye fasta kupiga ban hawa vichaa wote,hakuna kwenda hata hapo Kenya yaani.....

Wanadhani kwenye hii dunia unaweza jifanyia lolote bila concequences!Yaani uue,uibe kura,uweke watu jela,uteke watu,etc just free tuuu?

No way!
Kabudi aliingia Serikali akiwa masikini mchovu hohehahe tokea jalalani , lakini ameota mapembe baada ya kutafuna pesa za mkulima wa kizungu aliyekamata Ndege, migao ya 10% ununuzi wa Ndege, mikataba mipya ya siri ya madini, pesa za corona na michongo kibao ya kimataifa, sasa Kabudi ni tajiri ni bilionea ndiyo maana kawa na kiburi cha kishamba mno kutwa kujimwambafy kishetani shetani pasipo kutafakari kabla
 
Unajihesabu nawe ni mjuaji, kwa kurahisisha mambo kihivyo!

Na si ajabu ukawa unashikilia nafasi mhimu ndani ya serikali hii inayopotosha kila jambo mradi tu ionekane inajitutumua.

Haya, hata nyinyi mna jeshi, kama walivyo nalo wamarekani. Unataka tuwape uwanja mkapimane nguvu?

Inawezekana kabisa usielewe maana ya mfano huo niliokuwekea hapo; na hata kama umeelewa utakaza tu shingo mradi uonekane mjuaji.

Watu wa hovyo sana nyinyi.
ID yako inaelezea uhalisia wako. Wewe ni wakutumiwa kuandika tu hata kama ni utopolo. Ndiyo kazi ya Kalamu.
 
Kabudi aliingia Serikali akiwa masikini mchovu hohehahe tokea jalalani , lakini ameota mapembe baada ya kutafuna pesa za mkulima wa kizungu aliyekamata Ndege, migao ya 10% ununuzi wa Ndege, mikataba mipya ya siri ya madini, pesa za corona na michongo kibao ya kimataifa, sasa Kabudi ni tajiri ni bilionea ndiyo maana kawa na kiburi cha kishamba mno kutwa kujimwambafy kishetani shetani pasipo kutafakari kabla
Kumbe wewe ndiyo wale matapeli wa rasilimali zetu mlizokuwa mnaiba kupitia mabeberu?
 
Mkuu JokaKuu
Wiki moja iliyopita tuliongelea ujasiri wa Mwalimu mwaka 1965 kwa Waingereza na 1964 kwa Wajerumani

Profesa anaonekana kuilinganisha Tanzania ya Nyerere na ya leo, kosa! Mwl alikuwa ''super Diplomat''

Hili suala la EU limeifanya serikali ku-panic sana, na ukweli upo wazi wanaogopa vikwazo
Katika kuogopa wamekurupuka sana

1. Kamati za Bunge la EU zinaongea na Bunge lao,ni mambo ya Bungeni kwao. Tanzania haipaswi kujibu maongezi ya Wabunge. Pale Dodoma Wabunge wakiongea EU haiwezi kuwajibu kwasababu wanaongea kama Watanzania

EU wangejibiwa ikiwa tu suala hilo lingetoka Bungeni na kuwa kauli au msimamo rasmi wa EU kuhusu Tanzania.
Hapo ndipo Balozi, Waziri na wahusika wangetafuta mawasiliano ya kuongelea hili jambo.

Kwasababu ya ku-panic hakuna anayefuata taratibu za kidiplomasia, wanakurupuka tu.

2. Hoja iliyopo siyo misaada, ni matumizi ya Euro Milioni 27. Watanzania hawakujua kuna hizo pesa
Iuwajibu EU muda ukitimia (siyo sasa) serikali inapaswa kuwaeleza Watanzania na EU pesa zimekwenda wapi?

Watu hawataki kujibu milioni 27 wanataka tuamini kuna vita ya uchumi! hakuna vita ya uchumi kati ya Wazungu na Waafrika. Tanzania, uchumi wake haupo 'intertwined' na uchumi wa dunia, vita inatoka wapi?

Fuateni taratibu za kidiplomasia, andaeni majibu kuhusu Euro ambazo Watanzania wenyewe hawakujua zipo ingawa leo wanaombwa washikamane !

Mag3 tindo Sky Eclat The Boss
 
Nasema km kuna kiama kweli kama dini zinavotueleza hakuna politician ataekwenda peponi wallah kumbe kuna mahela ya covid tulipewa yalifanya nini na watu karantini walijilipia?NO POLITICIAN WILL GO TO HEAVEN..
 
Nasema km kuna kiama kweli kama dini zinavotueleza hakuna politician ataekwenda peponi wallah kumbe kuna mahela ya covid tulipewa yalifanya nini na watu karantini walijilipia?NO POLITICIAN WILL GO TO HEAVEN..
Hopeless kweli wewe kwani ulikuwa hujui kuwa EU walijipendekeza wakatoa misaada ya corona?
 
Nyerere alishindwa vita gani na mabeberu mpaka akaamua kung'atuka ?.Profesa zima halina linachojua .
 
Kumbe wewe ndiyo wale matapeli wa rasilimali zetu mlizokuwa mnaiba kupitia mabeberu?
CCM mkienda kuomba omba misaada ulaya huwaita wazungu wafadhili wahisani lakini hao hao wazungu wakikataa ujinga upumbavu unyanyasaji uonevu mateso ya CCM kwa wapinzani ndipo CCM hugeuka na kuwaita wanaume wenzenu mabeberu utazani nyinyi CCM ni mbuzi jike
 
CCM mkienda kuomba omba misaada ulaya huwaita wazungu wafadhili wahisani lakini hao hao wazungu wakikataa ujinga upumbavu unyanyasaji uonevu mateso ya CCM kwa wapinzani ndipo CCM hugeuka na kuwaita wanaume wenzenu mabeberu utazani nyinyi CCM ni mbuzi jike
Wazungu si wote mabeberu! Mabeberu ni wale wazungu wezi wakishirikiana na vibaraka kama wewe kuiba rasilimali zetu. Nafikiri utakuwa umeelewa maana ya mabeberu sasa!
 
Kila nchi ina kopa wamarekani wanadaiwa na China mkuu. Hivyo kukopa siyo shida hata hao wanaokopesha wanafanya hivyo ili wapate faida bila kukopesha wanakufa kwa njaa pia. Maana yake tunategemea wote!
Msiwe wajinga. US haijawahi kukopeshwa na China. China huwa inanunua treasury bonds za Serikali ya Marekani ili kutengeneza faida. Watu wenye akili ndogo huwa wanadhani ni mikopo kama hii tunayoichukua sisi.

Kama una hela, hata wewe unaweza kununua treasury bonds za Serikali ya Marekani. Baada ya hapo, kwa ujinga kabisa na meno nje utaweza kutamka kuwa umeikopesha US?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom