Prof. Joseph Mbele: Nimewabaini wanaomkwamisha Rais Magufuli

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
Mimi ni raia ambaye sina chama, na daima ninaongea kile ninachoamini. Rais Magufuli anahitaji watu wa kumsaidia afanikiwe, si watu wa kumwunga mkono na kumsifia kwa kila kitu. Wapambe na watendaji ndio wanamkwamisha. Ninamsikia akilalamika kila anapopita hadi akasema kuwa saa nyingine anakuwa na "frustrations."

Watendaji na wanaCCM waache hii jadi ya kumsifia tu Rais na kumwuunga mkono. Wawe wanamsaidia kufanikisha yale mazuri anayotaka kufanya, na papo hapo wawe wanamshauri na hata kumzuia mengine ambayo anataka. Yeye ni binadamu, na ana mapungufu. Watendaji wanapaswa wamsaidie kufanikiwa yale mazuri, vinginevyo wanamwangusha. Napenda nitoe mfano.

Wakati ndege yetu ilipokamatwa Canada kwa amri ya mahakama ya kule, Rais Magufuli aliamua kupeleka ujumbe kwa waziri mkuu wa Canada kuomba atusaidie. Waziri mkuu alijibu kwamba hangeweza kufanya lolote na kwamba alikuwa na imani na mahakama. Taarifa hii niliisoma katika gazeti la Toronto:
...
Huu ni mfano wa ninachomaanisha. Ilitakiwa watendaji wa Rais wamwambie kwa dhati kabisa kwamba ombi lake kwa waziri mkuu wa Canada halingetekelezwa kwa kuwa kuna suala la mihimili kujitegemea. Nina hakika kuwa serikali ya awamu ya tano ina wanasheria ambao wanategemewa kujua hili suala la mihimili kutoingiliana.

Sasa kwa kuwa jadi iliyopo katika awamu ya tano ni ya kuunga mkono na kusifia kila anachowazia au kufanya Rais Magufuli, watendaji wamemsababishia Rais Magufuli dosari kimataifa. Taarifa hizi zilizochapishwa zitawafanya watu waulize inakuwaje Rais wa Tanzania akaomba msaada kwa suala lililokuwa mahakamani. Wanaweza kujiuliza ni nchi ya namna gani hiyo.
Je, huku ndiko kumwunga mkono Rais Magufuli? Yaani hata akiwa anaelekea kwenye kichaka cha simba, watu wasimzuie? Wahusika wajirekebishe.
 
Fikra na mawazo huru ni utajiri mkubwa sana! Prof ameeleweka! Unajua kuongoza watu walionyamaza tuu wanasubiri ww ndio uwe kila kitu yaani kazi yao kusifia tuu ni sawa na kuongoza maiti. Tz inatia huruma sana
 
Mbona hajataja directly hao wasaidizi wake, wako wengi mno..!!
 
Kuzungukwa na lundo la watendaji na wapambe wanaosifia tu bila ya kukosoa wala kuelekeza au kutoa ushauri,ni janga kubwa.Ni bora kuwa na mbwa ambaye mara zote habweki bila ya sababu kuliko kuwa na watu wa namna hii.
 
Mimi ni raia ambaye sina chama, na daima ninaongea kile ninachoamini. Rais Magufuli anahitaji watu wa kumsaidia afanikiwe, si watu wa kumwunga mkono na kumsifia kwa kila kitu. Wapambe na watendaji ndio wanamkwamisha. Ninamsikia akilalamika kila anapopita hadi akasema kuwa saa nyingine anakuwa na "frustrations."

Watendaji na wanaCCM waache hii jadi ya kumsifia tu Rais na kumwuunga mkono. Wawe wanamsaidia kufanikisha yale mazuri anayotaka kufanya, na papo hapo wawe wanamshauri na hata kumzuia mengine ambayo anataka. Yeye ni binadamu, na ana mapungufu. Watendaji wanapaswa wamsaidie kufanikiwa yale mazuri, vinginevyo wanamwangusha. Napenda nitoe mfano.

Wakati ndege yetu ilipokamatwa Canada kwa amri ya mahakama ya kule, Rais Magufuli aliamua kupeleka ujumbe kwa waziri mkuu wa Canada kuomba atusaidie. Waziri mkuu alijibu kwamba hangeweza kufanya lolote na kwamba alikuwa na imani na mahakama. Taarifa hii niliisoma katika gazeti la Toronto:
...
Huu ni mfano wa ninachomaanisha. Ilitakiwa watendaji wa Rais wamwambie kwa dhati kabisa kwamba ombi lake kwa waziri mkuu wa Canada halingetekelezwa kwa kuwa kuna suala la mihimili kujitegemea. Nina hakika kuwa serikali ya awamu ya tano ina wanasheria ambao wanategemewa kujua hili suala la mihimili kutoingiliana.

Sasa kwa kuwa jadi iliyopo katika awamu ya tano ni ya kuunga mkono na kusifia kila anachowazia au kufanya Rais Magufuli, watendaji wamemsababishia Rais Magufuli dosari kimataifa. Taarifa hizi zilizochapishwa zitawafanya watu waulize inakuwaje Rais wa Tanzania akaomba msaada kwa suala lililokuwa mahakamani. Wanaweza kujiuliza ni nchi ya namna gani hiyo.
Je, huku ndiko kumwunga mkono Rais Magufuli? Yaani hata akiwa anaelekea kwenye kichaka cha simba, watu wasimzuie? Wahusika wajirekebishe.
Wangeshauri utakavyo wangeendaje Ulaya? Let people get per diems!
 
Mkuu wa mkoa anasifia mpaka mshahara mnene anaolipwa na rais kuwa unamuwezesha kuwa hata na kamchepuko tena anaongea mbele ya rais!!! Hapa hatuko salama kabisa kabisa kwa viongozi wetu waliopewa dhamana kuiongoza jamii..
 
Tatizo kubwa la serikali ya awamu ya TANO ni kutokana na kujaza MAKADA wa Chama cha CCM kwenye serikali tena waliowengi hawana weredi kwenye nafasi walizopo huku akiacha watendaji wenye weredi nje ya ulingo, mnajua sababu za kuwaacha watalaam weredi ni nini?
1. Sababu za kisiasa kwa kuhisi ni
wanachama wa upinzani
2. Ushauri kutoka kwa wanasiasa
waliomzunguka Rais
3. Fadhila za Rais kwa wana CCM
wenzake baada ya kumpigania
kwenye uchaguzi uliopita
4. Ubovu wa KATIBA yetu inayomfanya
Rais kuwa mwamuzi wa kila kitu
hata kama hakina maslahi kwa nchi
5. Watanzania tulio wengi hatuna utamaduni wa kumwambia kiongozi wetu pale anapokosea
 
Bado kitambo kidogo tu, maiti watafufuka na jambo kubwa litatokea kwa ajili ya mustakabali mzuri kwa taifa.
Fikra na mawazo huru ni utajiri mkubwa sana! Prof ameeleweka! Unajua kuongoza watu walionyamaza tuu wanasubiri ww ndio uwe kila kitu yaani kazi yao kusifia tuu ni sawa na kuongoza maiti. Tz inatia huruma sana
 
Tatizo kubwa la serikali ya awamu ya TANO ni kutokana na kujaza MAKADA wa Chama cha CCM kwenye serikali tena waliowengi hawana weredi kwenye nafasi walizopo huku akiacha watendaji wenye weredi nje ya ulingo, mnajua sababu za kuwaacha watalaam weredi ni nini?
1. Sababu za kisiasa kwa kuhisi ni
wanachama wa upinzani
2. Ushauri kutoka kwa wanasiasa
waliomzunguka Rais
3. Fadhila za Rais kwa wana CCM
wenzake baada ya kumpigania
kwenye uchaguzi uliopita
4. Ubovu wa KATIBA yetu inayomfanya
Rais kuwa mwamuzi wa kila kitu
hata kama hakina maslahi kwa nchi
5. Watanzania tulio wengi hatuna utamaduni wa kumwambia kiongozi wetu pale anapokosea
Kwamba kwenye mikutano ya hadhara wanaona kama wako kwenye vikao vya ndani vya chama 🙆🏽‍♂️🙆🏽‍♂️🙆🏽‍♂️🙆🏽‍♂️
 
You can't believe this article is from a proffessor! !!
Nyerere alikuwa mwandishi mzuri sana, kaandika hata vitabu. Kwa maandishi yake yale wananchi walijua rais wao anawazaje kiuchumi, kijamii na kisiasa. Wananchi walijua hata upeo wake wa kufikiri. Imagine kiongozi wetu wa sasa hajawahi kuandika hata sentensi mbili kwenye gazeti la uhuru au la habarileo achilia mbali daily news paper. Tutajuaje anawazaje juu ya mustakabali was nchi hii? Tutapimaje upeo wake juu ya masuala kadhaa kitaifa na kimataifa?
Ni heri huyu profesa ameondoka hako ka-articlea na watu wamemwelewa ikiwemo wewe.
 
Kwamba kwenye mikutano ya hadhara wanaona kama wako kwenye vikao vya ndani vya chama 🙆🏽‍♂️🙆🏽‍♂️🙆🏽‍♂️🙆🏽‍♂️
Ziara za kiserikali badala ya kuongelea matatizo ya nchi tunahangaika na vyama,,, utasikia CCM hoyeeeeee
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom