Prof Euphrase Kezilahabi: Mwanazuoni anayehitajika kwenye ujenzi wa taifa hili

Nimefika ukerewe kipindi flani hivi na kusema kweli kizazi hicho kiliibeba sana ukerewe. Wengine ni kina Profesa Machunda(rip), Yupo Askofu Lukanima (sina kumbukumbu sahihi sana), Pius Msekwa, Getruda Mongela kwa kutaja wachache. Ni kabila lenye watu wa IQ kubwa na ni wasiri sana ndo maana waliaminiwa sana na mwalimu hasa kwenye mambo nyeti hapo namkumbuka Mpambe/Close bodyguard wa mwl nadhani aliitwa Mkanzabi. Wana msemo wao mkelebhe ni mpelhe
Mkuu Ukabila huo
 
You are very very wrong! Prof. Kezilahabi is living. Kulikuwa na Kezilahabi mwingine akiwa Mapato, sijui kama yuko hai. Yaonekana wote ni wakerewe. Kabla ya kukujibu imebidi nimtafute. Wikipedia ina maelezo kidogo lakini muhimu ni update ya May 2015. Kezilahabi yuko hai, ktk umri wa kutosha maana yaonekana amezaliwa 1944. he must be at 71.

btw. Hawa wakerewe siyo ajabu kuwa na ubora wa kiwango hicho. Ni kabila ambalo wako poetic. Bila kujali majivuno ya kila kabila, hawa tuwasifu pale wanapostahili. Yupo mkerewe mwingine alishatoa kitabu chenye juzuu mbili ambacho pia ukikisoma kinatisha! Kinaitwa Myombekere na Bugonoka na Ntulanalwo na Bulihwali . Ni kitabu cha mwaka 1945 na kikachapishwa 1981! Fantastic book. Ongeza na mwingine Gabriel Ruhumbika ambaye nadhani yuko based US. Wote wakitokea kisiwani Ukerewe!
Namkumbuka sana mwalimu wangu wa shule ya msingi castam mrs mkama ni mkerewe pia naye alikuwa na kipaji cha kutunga mashairi kwa kiwango cha juu
 
Mkuu Ukabila huo
Unanikumbusha tabia za viongozi wa Afrika. Ukimwambia ana akili kuliko raia wote, hufurahi sana ingawa siyo ukweli. Ukisema kweli kwamba anaongoza vibaya au ni dhaifu, nguvu za dola zinakuangukia.

Tukubali, kuna watu wana talents za ziada kuliko wengine.
 
Unanikumbusha tabia za viongozi wa Afrika. Ukimwambia ana akili kuliko raia wote, hufurahi sana ingawa siyo ukweli. Ukisema kweli kwamba anaongoza vibaya au ni dhaifu, nguvu za dola zinakuangukia.

Tukubali, kuna watu wana talents za ziada kuliko wengine.
kweli, lakini sio kabila fulani
 
Juzi kati nimesoma kitabu chake cha 'Nagona'. Ni kitabu ambacho kimebeba lugha nzito na yenye picha. Huwezi kuelewa kama umetokea shule zetu pendwa za (kata?)....

Zama hizi zimeishiwa watu wa aina yake, naungana na wewe kwamba angekuwepo nchini angeweza kurithisha ujuzi wake kwa kizazi za leo.
mkuu jinsi ulivyoandika inaonesha wewe sio bora kuliko hao wa shule zetu za kata. hebu angalia ulipoweka hizo brackets zako kama kweli umeelimika.
 
Dah! Jamaa angekua padri sahivi,ila ndo alishatimuliwa bahada ya hapo ikabidi alipize kisasi kwa kutoa kitabu cha Rosa Mistika


Yap, Jamaa angekua padri ila kusoma soma sana kulimfanya akutane na maandishi ya Albert Camus ambayo kwa kiasi kikubwa yalimfanya aanze kujiuliza upya ju ya dhana ya maisha na maana yake.

Lakini kufukuzwa kwake upadri kukawa ni mwanzo wa hisia mpya za kifalsafa.

Ni watu wachache sana wanaothubutu kujaribu kutafuta maana ya maisha, wengi huogopa kwa kushiriki kifo cha kifalsafa.
 
You are very very wrong! Prof. Kezilahabi is living. Kulikuwa na Kezilahabi mwingine akiwa Mapato, sijui kama yuko hai. Yaonekana wote ni wakerewe. Kabla ya kukujibu imebidi nimtafute. Wikipedia ina maelezo kidogo lakini muhimu ni update ya May 2015. Kezilahabi yuko hai, ktk umri wa kutosha maana yaonekana amezaliwa 1944. he must be at 71.

btw. Hawa wakerewe siyo ajabu kuwa na ubora wa kiwango hicho. Ni kabila ambalo wako poetic. Bila kujali majivuno ya kila kabila, hawa tuwasifu pale wanapostahili. Yupo mkerewe mwingine alishatoa kitabu chenye juzuu mbili ambacho pia ukikisoma kinatisha! Kinaitwa Myombekere na Bugonoka na Ntulanalwo na Bulihwali . Ni kitabu cha mwaka 1945 na kikachapishwa 1981! Fantastic book. Ongeza na mwingine Gabriel Ruhumbika ambaye nadhani yuko based US. Wote wakitokea kisiwani Ukerewe!
Ukerewe ni kisiwa ambacho kilikuwa na Maprofesa wengi ,akina Prof.Machunda,Prof Makene,Prof Bwahato,hao niliwasikia nikiwa primary
 
[h=1]Euphrase Kezilahabi[/h]
euphrase-kezilahabi_285x0.jpg
Euphrase Kezilahabi, Tanzanian poet, novelist, and scholar, is perhaps the most widely known and acknowledged contemporary Swahili author. He was one of the first African writers to publish a collection of free verse poetry in Swahili, and he has had a great impact on the development of the genre of the novel in Swahili.
Najua wengi mnaikumbuka riwaya ya 'Rosa Mistika' au ile 'Kichwa maji' zilizoandikwa na Profesa Euphrase Kezilahabi.
Mmenikumbusha mbali, enzi za Roza Mistika!. Primari, nilisoma darasa moja na binti yake Regina Kezirahabi, sijui siku hizi yuko wapi?.

Paskali
 
Hahahhhhaaa
Mbele ya Hukumu: ROSA MISTIKA kwanini umejiua?
Rosa Mistika: Ni kwasababu ya maudhi ya Baba yangu....
Mungu: Nitauuliza Ulimwengu

Hahahhhahaaaaaaaa kitabu kizuri sana sana kiliwahi kupigwa marufuku Tanzania, ukikisoma hutakaa ukiache daima
Nilikisoma mkuu Rosa alichaguliwa kujiunga na chuo cha ualimu
 
Siyo kwamba ni kwa sababu ya kanisa katoliki? Maana kanisa lilimjia juu kwa kutumia jina la Rosa Mistika ambalo linamafungamano na Bikira Maria na kwa Tabia za Rosa Mistika wa kitabuni kanisa liliona limechafuliwa na kitabu husika.

Waandishi wa Tanzania hawapo huru hasa wakiligusa tabaka tawala
 
Juzi kati nimesoma kitabu chake cha 'Nagona'. Ni kitabu ambacho kimebeba lugha nzito na yenye picha. Huwezi kuelewa kama umetokea shule zetu pendwa za (kata?)....

Zama hizi zimeishiwa watu wa aina yake, naungana na wewe kwamba angekuwepo nchini angeweza kurithisha ujuzi wake kwa kizazi za leo.
Waandishi wengi wamekimbilia huko kwenye lugha ya picha kuukwepa mkono wa dola siyo Kezilehabi peke yake
 
Siyo kwamba ni kwa sababu ya kanisa katoliki? Maana kanisa lilimjia juu kwa kutumia jina la Rosa Mistika ambalo linamafungamano na Bikira Maria na kwa Tabia za Rosa Mistika wa kitabuni kanisa liliona limechafuliwa na kitabu husika.

Waandishi wa Tanzania hawapo huru hasa wakiligusa tabaka tawala
Yah kwenye litanies ya Bikira Maria Rosa Mistika ni Waridi lenye Fumbo
 
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom