Prof.Benno Ndullu kafanya maajabu BOT!!

JokaKuu

Platinum Member
Jul 31, 2006
30,442
55,007
..Haya jamani waziri wetu wa fedha katuletea changamoto hapa...

Mkulo: Ndullu kafanya maajabu BoT

na Salehe Mohamed na Kulwa Karedia

SERIKALI imesema kuimarika kwa shilingi dhidi ya dola na kushuka kwa mfumuko wa bei, vimetokana na uongozi mpya wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na sera zilizowekwa na Gavana mpya Profesa Beno Ndullu.

Uuzaji bidhaa za Tanzania nje ya nchi, umesaidia kwa kiasi kikubwa kuimarika kwa uchumi wa nchi na bidhaa za nje kuuzwa hapa kwa bei ya chini ndani ya soko letu.

Hayo yalibainishwa Dar es Salaam jana na Waziri wa Mipango na Fedha, Mustafa Mkulo, alipokuwa akifunga semina ya wabunge kuhusu mwongozo wa kutayarisha mipango na bajeti ya serikali kwa kipindi cha mwaka 2008/2009.

Utoaji mikopo wa benki kwa watu mbalimbali, kutokukopa ndani kwa serikali na mfumuko wa bei kuwa asilimia sita kwa sasa, ni miongoni mwa chachu za ukuaji wa uchumi wa nchi.

Alisema, hadi sasa mfumuko wa bei ni chini ya asilimia sita na benki mbalimbali zimeshusha riba ya mikopo yao na kubainisha kuwa mambo hayo yameimarisha uchumi.

Mkulo alisema, maajabu hayo katika uchumi wetu yametokana na mabadiliko yaliyofanyika BoT baada ya kuondolewa kwa Gavana wa zamani, Daudi Ballali.

Alisema miaka mitano hadi sita iliyopita, benki hazikukopesha watu kwa kasi kama ilivyo sasa na riba zimeshuka kulingana na taratibu walizojiwekea, lakini lengo likiwa ni kuimarisha uchumi na kuwawezesha wananchi.

"Mabadiliko yaliyofanywa na Ndullu pale BoT yamesaidia kwa kiasi kikubwa kuboresha uchumi wa Tanzania, na hivi sasa shilingi ya Tanzania inapambana na dola," alisema Mkulo na kuongeza kuwa, uchumi wa nchi yeyote hauendelei bila wananchi hasa wa tabaka la chini kupata mikopo itakayowawezesha kufanya shughuli za kuwaongezea kipato.

Alisema, ni vigumu kwa wananchi kugundua ukuaji wa uchumi, lakini njia ya kuthibitisha hilo ni kukamilika kwa miradi mbalimbali huku akiainisha miradi hiyo kuwa ni ujenzi wa shule, zahanati na maeneo mbalimbali ambayo yamesaidia kuboreka kwa uchumi wa Tanzania.
 
Huyu sasa anataka kutuburuza yaani hata miezi mitatu hajamaliza tayari analeta kali ya mwaka ,maana naamini kabisa hata mafaili mingine bado hajayafungua ,lakini amekurupuka na kusema mamabo yaliyofanywa kwa muda mfupi aliokuwepo hapo pangoni yamesababisha watu kukopeshwa zahanati,mashule kujengwa na kumalizika kwa wakati ,hivi hajui kama uchumi wa dunia umebadilika na thamani ya dola kila siku inaanguka kutokana na mauza uza ya huko kwenye dunia ya kwanza ,halafu anakuja hapa kusema ni kutokana na mabadiliko ya BOT ,jamani punguzeni kidogo ,kwa kasi hii naona hatufiki mbali tutaanza kutoka bearings.
 
The height of stupidity.

Everybody who understands the basics of economics must understand the repercussions of a falling / tumbling dollar to other currencies.

Kilichotokea hapa is not so much kwamba shilingi ya Tanzania imepanda thamani sana na hivyo kusababisha exchange rate ya shilling/dollar kuimaikawith the shilling gaining, what happenned is that the dollar was falling faster than the shilling was falling.

Kwa mfano, ukiwa na magari mawili yanakimbizana, USD liko mbele lilikuwa linakwenda 100 km/ hr, na Tanzania Shiling linakwenda 90 km/ hr, halafu like gari la USD likaanza kupunguza mwendo liwe linaenda kwa 50 km/ hr na lile la TZ shilling lipunguze pia liwe linakwenda kwa 70 km /hr, overall outcome ni kuwa lile la TZSh litalipita lile la USD sio kwa sababu limezidisha mwendo, bali kwa sababu ingawa limepunguza mwendo, lile lenzake la USD limepunguza mwendo zaidi na hivyo ukiweka mahesabu ya relativity unakuta kuwa lile la TZSh lina gain over lile la USD.

Hiki ndicho kinachotokea, exchange rate ya shilingi haiimariki kwa sababu uchumi wetu unakua wala kwa sababu shilingi inapanda dhidi ya dola, ni kwa sababu dola inashuka kwa kasi kubwa zaidi kuliko shilingi inavyoshuka thamani.

This tumbling of the dollar is apparent the world over, kuanzia kwenye Japanese Yen mpaka Canadian dollar.

Sasa wanataka kutuifanya sisi wajinga na kuchukua credit hapa.Tena hawajui hata ku spin.

Thats what an Ameida MBA coupled with ufisadi will do to you.
 
..sasa tuseme Waziri Mkullo hafahamu kinachoendelea?

..au labda anajua kinachoendelea, lakini kaamua kuwapiga-fix hao wabunge.

..reaction ya wabunge kuhusu hizi taarifa za Waziri Mkullo ni nini?

..WHY??!!
 
..Haya jamani waziri wetu wa fedha katuletea changamoto hapa...

Mkulo: Ndullu kafanya maajabu BoT

na Salehe Mohamed na Kulwa Karedia


SERIKALI imesema kuimarika kwa shilingi dhidi ya dola na kushuka kwa mfumuko wa bei, vimetokana na uongozi mpya wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na sera zilizowekwa na Gavana mpya Profesa Beno Ndullu.
...
“Mabadiliko yaliyofanywa na Ndullu pale BoT yamesaidia kwa kiasi kikubwa kuboresha uchumi wa Tanzania, na hivi sasa shilingi ya Tanzania inapambana na dola,”

Wote tunafahamu kuwa US$ imekuwa ikiporomoka thamani yake kutokana na matatizo ya uchumi wa USA na wala isiwe kigezo cha kumsifia mtu baada ya muda mfupi wa kukaa kazini

Suala la kushuka kwa mfumuko wa bei linaweza kuhusishwa zaidi na "ukapa" baada ya pesa kuondolewa kwanye mzunguko; aidha kutokana na baadhi ya nchi wafadhili kuchelewesha kutoa pesa ya misaada waliyoahidi au sana sana ni hili la "mafisadi" kurejesha baadhi yapesa waliyotuibia.

Hebu acheni ubabaishaji! Fanyeni kazi na matunda yaonekane; mwenye macho haambiwi tazama.
 
Kutokana na yale yaliomtokea Balali na viongozi wa siasa kuwa karibu sana na BOT naona kuna uwezekano mkubwa data zingine zinapikwa kwa ajili ya public consumption.

Ikibidi vipimo vya maendeleo ya nchi vianze kuangalia uwezo wa maisha wa mtanzania wa kawaida kumudu maisha yake ya kila siku. Je ni milo mingapi mtanzania wa kawaida anapata kwa siku?
 
Ndiyo maana watu werevu hupenda kutafuta taarifa kutoka vyanzo mbalimbali vilivyo huru na independent...na hapa JF ni mahala sahihi kwa watu wanaohitaji kuelimika.

Nashauri kwa wana JF mliokaribu na wabunge wapasheni ili wafunguliwe bongo zao hapa JF.

Cha ajabu ni kuwa wabunge wengi wanaelewa ila wanaoneana aibu kuelezana ukweli wanapokuwa kwenye mikutano yao.

Bila kuelezana ukweli nchi itaendelea kuwa maskini.

Inashangaza na kusikitisha sana.
 
The height of stupidity.....................Thats what an Ameida MBA coupled with ufisadi will do to you.

Absolutely...........hii MIJITU MINGINE SIJUI inawezaje kukaa chini na kudscuss issues za uchumi wanapokutana na watu smart (investors).........yaani ni kichekesho tu...............ndio yale yale aliyokuwa akisema Mwl JKN (RIP).......................mijitu kama hii (Mkullo Type) hata ikiambiwa Ujinga inabaki kucheka cheka tu na kusema YES YES.......YAH YAH.......kumbe haijui kuwa inaonyesha UPUMBAVU WAO.......and the smart guys always take an advantage of such idiots
 
BOT: EXCHANGE RATES:
Effective on 17 Mar 2008 TSh
Currency
Australian $ 1095.81
Swedish Kronor 198.19
UAE Dirham 322.44
[Kenya S 17.00 ]
Uganda Shs 0.71
S. Africa Rand 144.00
USD 1183.77
Pound STG 2383.81
EURO 1876.21
Switz. Franc 1213.31

Hizi ni rates kutoka BOT kwenyewe. Ebu angalia Euro inavyokaribia shilingi 2000, mwezi January ilikuwa takribani shs.1600 tu. Paund ya mwingereza ndio usiseme!
Au chunguza what is happening to kenyan money against our shilling
 
BOT: EXCHANGE RATES:
Effective on 17 Mar 2008 TSh
Currency
Australian $ 1095.81
Swedish Kronor 198.19
UAE Dirham 322.44
[Kenya S 17.00 ]
Uganda Shs 0.71
S. Africa Rand 144.00
USD 1183.77
Pound STG 2383.81
EURO 1876.21
Switz. Franc 1213.31

Hizi ni rates kutoka BOT kwenyewe. Ebu angalia Euro inavyokaribia shilingi 2000, mwezi January ilikuwa takribani shs.1600 tu. Paund ya mwingereza ndio usiseme!
Au chunguza what is happening to kenyan money against our shilling

Shukrani sana Mkuu,

Sasa ukiangalia hizi figures ndiyo utajua appreciation ya TSh ni bilateral, meaning shilingi inapata thamani dhidi ya dollar tu, kwa sababu actually shilingi yenyewe haigain kitu per se, ila ina gain kutokana na kuanguka kwa dollar.

Kama shilingi ingekuwa ina gain kutokana na kukua kwa uchumi na kazi nzuri ya Ndulu basi gains zingekuwa across the boards, which is not the case presented here.
 
..Haya jamani waziri wetu wa fedha katuletea changamoto hapa...

Mkulo: Ndullu kafanya maajabu BoT

na Salehe Mohamed na Kulwa Karedia

Unajua wakati mwingine hawa jamaa hata aibu hawana ya kusema uwongo ili kujionesha kwamba wanaifanyia mazuri Tanzania. Anataka kutufanya Watanzania wote ni wapumbavu hatuelewi kwamba dollar ya Marekani inayumba katika soko la dunia na hivyo kuzifanya currencies nyingi za nchi mbali mbali duniani kuongezeka thamani ukilinganisha na dollar ya Marekani. Mkullo acha unafiki wa kusema uwongo mchana kweupe. Ndulu hajafanya chochote pale BoT kilichoimarisha shilingi ya Tanzania
 
Ona sasa gharama ya ujinga wa Mustafa Mkullo tunaibeba wote.

This is Shame for Kikwete, shame for SISIEMU and is shame for all Tanzania to allow this Nut to drag us like bunch of fools
 
Shukrani sana Mkuu,

Sasa ukiangalia hizi figures ndiyo utajua appreciation ya TSh ni bilateral, meaning shilingi inapata thamani dhidi ya dollar tu, kwa sababu actually shilingi yenyewe haigain kitu per se, ila ina gain kutokana na kuanguka kwa dollar.

Kama shilingi ingekuwa ina gain kutokana na kukua kwa uchumi na kazi nzuri ya Ndulu basi gains zingekuwa across the boards, which is not the case presented here.


We can only measure our economy growth by using the term

Balance of Trade.Did he utter a word on this ama anatuona sisi wote wapuuzi kama hao anao wapa taarifa ? Mkandara hili ni eneo lako Bob mwaga vitu .
 
1. Siamini kwamba Prof. Ndulu hata angekuwa malaika angeweza badilisha mambo ndani ya muda mfupi huu... tukiwa bado tunafanya kazi masaa matatu kwa siku.

2. Kama kweli Mkullo amesema hivyo hapa kuna hatari.

3. Hata hivyo nina mashaka na waamandishi zaidi hata kuliko Mkullo... for sure mimi nimekuwa nawaogopa waandishi kuliko hata hao mawaziri wetu...

4. Kwa Tanzania ili uwe na uhakika wa habari ni aidha uone kwenye vyombo kama vya lungina au usome magazeti/source kuanzia 2 na kuendelea na zikiwa zinashabihiana basi amini na pelekea wenzako
 
1. Siamini kwamba Prof. Ndulu hata angekuwa malaika angeweza badilisha mambo ndani ya muda mfupi huu... tukiwa bado tunafanya kazi masaa matatu kwa siku.

2. Kama kweli Mkullo amesema hivyo hapa kuna hatari.

3. Hata hivyo nina mashaka na waamandishi zaidi hata kuliko Mkullo... for sure mimi nimekuwa nawaogopa waandishi kuliko hata hao mawaziri wetu...

4. Kwa Tanzania ili uwe na uhakika wa habari ni aidha uone kwenye vyombo kama vya lungina au usome magazeti/source kuanzia 2 na kuendelea na zikiwa zinashabihiana basi amini na pelekea wenzako

Mkuu matamshi haya alianza nayo Gavana mwenyewe some few days kama si a week or 2 weeks ago.Then karudia Mkullo hili ndiyo lao wewe jadili matamshi wa waziri then linganisha hali halisi kama alivyosema Mkullo .
 
Hahaha, kumbe Waziri wetu wa fwedha kasoma Almeda University - USA.... Masalaleeee... Aibu tupu. Inakuaje sisi wadanganyika tukubali kutambua qualifications za watu wanaosomea uko US wakati serikali ya US imetoa tamko la wazi kwamba hawakitambui hiki chuo? Ama kweli sisi wadanganyika wote ni mambumbumbu.

Mimi naomba niwaulize wana jamboforums... Hivi hawa ndugu zetu wa usalama wa taifa huwa hafafanyi background checks kabla mtu hajapewa madaraka makubwa kama haya? Ni aibu sana kuona kwamba mtu anapewa madaraka ya uwaziri wa pesa wakati ana degrees za uongo.. Je mtamwaminije mtu kumpa madaraka yote hayo wakati yeye vyeti vyake ni bomu? This automatically Disqualifies him for his current post. Hayohayo yalijitokeza kwa waziri wqetu wa zamani wa Sheria. Hivi hadi waziri wa Sheria naye haoni aibu kubandika qualifications feki? Hivi haoni aibu kuitwa "DR" wakati yeye anafahamu kwamba she doesn't deserve to be called a Dr?

Hii Almeda University (according to Wikipedia - http://en.wikipedia.org/wiki/Almeda_University) ni unaccredited American University founded in 1997.

In Connecticut: According to the Connecticut Department of Higher Education, Almeda was ordered to cease operating in Connecticut in October, 2001. After an investigation in 2002 indicated that Almeda was continuing to advertise its programs in Connecticut, the Department of Higher Education sent Almeda a second cease and desist letter and referred the issue to the Connecticut Attorney General for possible legal action.

In Florida: In 2003 the Florida Department of Education made an agreement with Almeda to cease operating in the state. Although Floridians can still get a degree from the online university, Almeda warns Floridians that its degrees may not be valid for public employment in Florida.

In Texas: Almeda is also on the Texas list of "Fraudulent or Substandard Institutions", making it illegal to use an Almeda degree in Texas in an advertisement; to get a job, promotion, raise, license, or to get admitted to an educational program or to gain many positions in government.

Other states: Almeda's website also warns Almeda degrees may not be valid for public employment in Illinois, Oregon, New Jersey, North Dakota, Washington and Idaho.

Hivyo basi, mimi nafikiri waziri wetu wa fedha alitoa tamko la namna ile sio kwamba kafanya makusudi kuwadanganya wadanganyika ila ni kwa sababu haelewi what he was talking about. Mimi sio mchumi, ila mtu aliyeenda Almeda University kujifunza MBA hawezi kunidanganya kirahisi kwa kutumia materials za Almeda.

Duh!!!!
 
Hahaha, kumbe Waziri wetu wa fwedha kasoma Almeda University - USA.... Masalaleeee... Aibu tupu. Inakuaje sisi wadanganyika tukubali kutambua qualifications za watu wanaosomea uko US wakati serikali ya US imetoa tamko la wazi kwamba hawakitambui hiki chuo? Ama kweli sisi wadanganyika wote ni mambumbumbu.

Mimi naomba niwaulize wana jamboforums... Hivi hawa ndugu zetu wa usalama wa taifa huwa hafafanyi background checks kabla mtu hajapewa madaraka makubwa kama haya? Ni aibu sana kuona kwamba mtu anapewa madaraka ya uwaziri wa pesa wakati ana degrees za uongo.. Je mtamwaminije mtu kumpa madaraka yote hayo wakati yeye vyeti vyake ni bomu? This automatically Disqualifies him for his current post. Hayohayo yalijitokeza kwa waziri wqetu wa zamani wa Sheria. Hivi hadi waziri wa Sheria naye haoni aibu kubandika qualifications feki? Hivi haoni aibu kuitwa "DR" wakati yeye anafahamu kwamba she doesn't deserve to be called a Dr?

Hii Almeda University (according to Wikipedia - http://en.wikipedia.org/wiki/Almeda_University) ni unaccredited American University founded in 1997.

In Connecticut: According to the Connecticut Department of Higher Education, Almeda was ordered to cease operating in Connecticut in October, 2001. After an investigation in 2002 indicated that Almeda was continuing to advertise its programs in Connecticut, the Department of Higher Education sent Almeda a second cease and desist letter and referred the issue to the Connecticut Attorney General for possible legal action.

In Florida: In 2003 the Florida Department of Education made an agreement with Almeda to cease operating in the state. Although Floridians can still get a degree from the online university, Almeda warns Floridians that its degrees may not be valid for public employment in Florida.

In Texas: Almeda is also on the Texas list of "Fraudulent or Substandard Institutions", making it illegal to use an Almeda degree in Texas in an advertisement; to get a job, promotion, raise, license, or to get admitted to an educational program or to gain many positions in government.

Other states: Almeda's website also warns Almeda degrees may not be valid for public employment in Illinois, Oregon, New Jersey, North Dakota, Washington and Idaho.

Hivyo basi, mimi nafikiri waziri wetu wa fedha alitoa tamko la namna ile sio kwamba kafanya makusudi kuwadanganya wadanganyika ila ni kwa sababu haelewi what he was talking about. Mimi sio mchumi, ila mtu aliyeenda Almeda University kujifunza MBA hawezi kunidanganya kirahisi kwa kutumia materials za Almeda.

Duh!!!!

Duh !!! Umeua lakini hawa ndiyo chaguo hasa la Mwenyekiti wa Chama Chetu cha kuleta amani Tanzania na raia wa jamhuri ya washinda hoi akina ndivyo tulivyo .
 
1. Siamini kwamba Prof. Ndulu hata angekuwa malaika angeweza badilisha mambo ndani ya muda mfupi huu... tukiwa bado tunafanya kazi masaa matatu kwa siku.

2. Kama kweli Mkullo amesema hivyo hapa kuna hatari.

3. Hata hivyo nina mashaka na waamandishi zaidi hata kuliko Mkullo... for sure mimi nimekuwa nawaogopa waandishi kuliko hata hao mawaziri wetu...

4. Kwa Tanzania ili uwe na uhakika wa habari ni aidha uone kwenye vyombo kama vya lungina au usome magazeti/source kuanzia 2 na kuendelea na zikiwa zinashabihiana basi amini na pelekea wenzako

Kasheshe,
Usilete mambo ya kuamini ndugu yangu kwenye mambo ya utawala.Hapa Afrika mengi yanaharibika kutokana na kuweka imani kwa hawa viongozi wetu.... sina haja ya kurudia kashfa mbalimbali zilizotokea katika muda mfupi uliopita, ila moja mhimu ambayo naweza kukutajia ni jinsi vile ndugu Balali, gavana aliyeng'olewa alivyokuwa anaenda Maelezo na kuwapa waandishi wahabari mambo chungu mzima ya kupanda kwa uchumi wetu.... wengi walimwamini wakiwemo viongozi...ghafla, mtu anakimbia nchi. Na huyo ni Dr. mzima na amefanya kazi kwenye benki ya dunia tayari..... ndugu yangu, usiendekeze imani hata kidogo.... sidhani kama mwandishi wa habari anaubabe wa kuspin taarifa kwa kiwango hicho.


SteveD.
 
Kasheshe,
Usilete mambo ya kuamini ndugu yangu kwenye mambo ya utawala.Hapa Afrika mengi yanaharibika kutokana na kuweka imani kwa hawa viongozi wetu.... sina haja ya kurudia kashfa mbalimbali zilizotokea katika muda mfupi uliopita, ila moja mhimu ambayo naweza kukutajia ni jinsi vile ndugu Balali, gavana aliyeng'olewa alivyokuwa anaenda Maelezo na kuwapa waandishi wahabari mambo chungu mzima ya kupanda kwa uchumi wetu.... wengi walimwamini wakiwemo viongozi...ghafla, mtu anakimbia nchi. Na huyo ni Dr. mzima na amefanya kazi kwenye benki ya dunia tayari..... ndugu yangu, usiendekeze imani hata kidogo.... sidhani kama mwandishi wa habari anaubabe wa kuspin taarifa kwa kiwango hicho.


SteveD.

Chukua tano kisha baada ya NEC na uozo wao Butiama nitakupa 3 jumla 8 .Mara JF inaanza kajambo baadaye linakuwa jambo jambo .Ndiyo maana tunaitwa JF .
 
Pundit, heshima kubwa kwako...wape darasa hawa akina mkullo and the likes...naona huyu hana tofauti na meghji...
 
Back
Top Bottom