Prof. Baregu azomewa kikao cha ndani Mtama baada kushindwa kupata Suluhu kuhusu mgombea Ubunge

Livejr

JF-Expert Member
Feb 6, 2014
2,068
2,792
Jioni ya leo tarehe 19/09 kumetokea hali ya sintofahamu Jimbo la Mtama baada ya Prof. Beregu kushindwa kupata Suluhu ya nani asimame kugombea Ubunge jimbo la Mtama Kati ya ndg. Selemani Methew Luwongo wa CHADEMA na ndg Mchinjita wa CUF.

Hali hiyo imetokea leo majira ya saa kumi na moja jioni kwenye kikao kilichofanyika mkwajuni - Mtama kwenye kikao cha ndani ambapo kila mgombea alitoa maelezo yake na Prof. Beregu aliona maelezo yote yana mashiko ndipo aliposema kuwa asimame mbunge wa CHADEMA hapo hapo watu wa CUF waliopo ndani ya kile kikao wakasimama na kusema kwa hasira huku wakimuonyeshea kidole Prof. Beregu kuwa amekuja kuua CUF kwani Jimbo linajulikana ni la CUF na kuanza kuzomea na kusababisha kikao hicho kufungwa Bila maridhiano.
 
Kwahio tufanyeje? Hizo si ndio hisia za watu? Huwezi kuzuia hisia za watu kama kweli hakuna mapandikizi ya ccm
 
Hapo tatizo si ukawa, tatizo ni wagombea....suluu ni kwaacha wote wapeperushe bendera za vyama vyao. Ukweli ni kuwa wazee walisahau kipengele hiki ambacho kingelahisisha migogoro hii...binadamu wagumu sana...ktk,mazigira fulani.
 
Hapo tatizo si ukawa, tatizo ni wagombea....suluu ni kwaacha wote wapeperushe bendera za vyama vyao. Ukweli ni kuwa wazee walisahau kipengele hiki ambacho kingelahisisha migogoro hii...binadamu wagumu sana...ktk,mazigira fulani.

hapo ni kuvunja makubaliano yakhe.
wataka wagombee wote ili iwe rahisi kwa mgombea wa ccm kushinda?
nadhani siyo sahihi, ccm twapenda upinzani uwepo ili kuchangamsha genge
 
Hapo tatizo si ukawa, tatizo ni wagombea....suluu ni kwaacha wote wapeperushe bendera za vyama vyao. Ukweli ni kuwa wazee walisahau kipengele hiki ambacho kingelahisisha migogoro hii...binadamu wagumu sana...ktk,mazigira fulani.

Wew ni mjinga ,kweli waogombea ni wa wapi kama sio ukawa ,na hio jimbo kapewa nani kwa nin watu wasiheshimu makubaliano waliyojiwekea ,mbona huku kilimanjaro/arusha amna hicho kituko
 
Yule wa CHADEMA atolewe tu.... sbb hilo jimbo ni la CUF... muda mrefu...!!!
 
Wew ni mjinga ,kweli waogombea ni wa wapi kama sio ukawa ,na hio jimbo kapewa nani kwa nin watu wasiheshimu makubaliano waliyojiwekea ,mbona huku kilimanjaro/arusha amna hicho kituko

Hahaha ukawa ni ikawa
 
Jioni ya leo tarehe 19/09 kumetokea hali ya sintofahamu Jimbo la Mtama baada ya Prof. Beregu kushindwa kupata Suluhu ya nani asimame kugombea Ubunge jimbo la Mtama Kati ya ndg. Selemani Methew Luwongo wa CHADEMA na ndg Mchinjita wa CUF.

Hali hiyo imetokea leo majira ya saa kumi na moja jioni kwenye kikao kilichofanyika mkwajuni - Mtama kwenye kikao cha ndani ambapo kila mgombea alitoa maelezo yake na Prof. Beregu aliona maelezo yote yana mashiko ndipo aliposema kuwa asimame mbunge wa CHADEMA hapo hapo watu wa CUF waliopo ndani ya kile kikao wakasimama na kusema kwa hasira huku wakimuonyeshea kidole Prof. Beregu kuwa amekuja kuua CUF kwani Jimbo linajulikana ni la CUF na kuanza kuzomea na kusababisha kikao hicho kufungwa Bila maridhiano.
Kwenye hicho kikao wewe ni mjumbe?
 
Back
Top Bottom