Prof. Baregu apinga ripoti ya Twaweza. Adai Rais Magufuli anaminya demokrasia

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
Leo Septemba 15, 2016 Taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya Twaweza imetoa matokeo ya utafiti uitwao "Rais wa Watu" tathimini na matarajio ya wananchi kwa serikali ya awamu ya tano, ambapo wamesema kuwa wananchi wanakubali hatua zinazochukuliwa na serikali mpya inayoongozwa na Rais Dk. John Magufuli, hususani kuhusu uondoaji wa wafanyakazi hewa, sera ya elimu bure na usimamishwaji wa watumishi wa Serikali kutokana na makosa mbalimbali.

Kufuatia ripoti hiyo, Profesa Mwesiga Baregu ameeleza kukosa uhakika na matokeo hayo ya utafiti kwani ulifanyika mwezi wa 6 huku mambo mengi yakitokea ndani ya miezi mitatu iliyopita, ambayo yamewabadilisha mtazamo wa watanzania kuhusu Rais.

Profesa Baregu, pia amesema kuwa utafiti huo umeonyesha asilimia 70 ya watanzania hawakuwa na uelewa wa kisiasa.


Chanzo: Dar24
 
Lakini ukipitapita huku mitaani wananchi wajinga bado wengi wanamkubali jamaa. Tatizo la msingi ni kwamba wanaomkubali magu kwa sasa ni wale walozoea shida yani kwao kulala njaa, kufa kwa magonjwa yanayotibika, kukosa umeme, maji ,elimu ni jambo la kawaida. Kama watu wa huko Dodoma. Hivyo utafiti unaweza kuwa sahihi.
Na ndio wapo wengi kuliko malofa katiba ubora wao
 
Leo Septemba 15, 2016 Taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya Twaweza imetoa matokeo ya utafiti uitwao "Rais wa Watu" tathimini na matarajio ya wananchi kwa serikali ya awamu ya tano, ambapo wamesema kuwa wananchi wanakubali hatua zinazochukuliwa na serikali mpya inayoongozwa na Rais Dk. John Magufuli, hususani kuhusu uondoaji wa wafanyakazi hewa, sera ya elimu bure na usimamishwaji wa watumishi wa Serikali kutokana na makosa mbalimbali.

Kufuatia ripoti hiyo, Profesa Mwesiga Baregu ameeleza kukosa uhakika na matokeo hayo ya utafiti kwani ulifanyika mwezi wa 6 huku mambo mengi yakitokea ndani ya miezi mitatu iliyopita, ambayo yamewabadilisha mtazamo wa watanzania kuhusu Rais.

Profesa Baregu, pia amesema kuwa utafiti huo umeonyesha asilimia 70 ya watanzania hawakuwa na uelewa wa kisiasa.


Chanzo: Dar24


Profesa wa Siasa anakosoa kuhusu statistics ambapo ni sehemu ya Hisabati? Tangu lini Mwanasiasa akajua Hesabu?
 
Afanye utafiti wake atuwekee data mezani. Professor akipiga blah blah, Form Six Leaver atakuwaje?
Subiri vijana wa kitengo cha sera na utafiti CHADEMA watakuwekea data mezani!

Ukiingia kwenye kitengo cha propaganda lazima fani uiweke pembeni. Prof. Baregu ameingia kwenye kitengo cha propaganda CHADEMA!

Ukimsoma vizuri siyo kwamba hakubaliani na matokeo ya utafiti ila amejishikiza kwenye muda ambalo utafiti ulifanyika. Yeye anadhani kwa sasa Rais Magufuli hakubaliki kwa asimilia zilizotolewa na TWAWEZA kwa sababu kuna miezi imepita tokea utafiti ufanyike. Kwa maana nyingine anataka hisia zake ziwe ndiyo matokeo ya utafiti. This is fun to say the least!
 
Ni nani anafadhili hii taasisi ya TWAWEZA?
Kla baada ya miei mitatu wanatoka na matokeo ya tafiti,nani anawawezesha?
Research inahitaji uwekezaji mkubwa kwasababu sio kutoka ndani ya week mbl unakuja na report eti umefanya research!!
 
Back
Top Bottom