Prof. Baregu aanza kazi SAUT

Paschal Matubi

JF-Expert Member
Sep 15, 2008
235
302
**********************************************************

Waweza kusoma habari hii hapa chini au attachment niliyoambatanisha humu ambayo ni scan ya gazeti la TUMAINI LETU.

**********************************************************

{Prof. Baregu aanza kazi SAUT}

Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine Tanzania (SAUT) kinachomilkiwa na Kanisa Katoliki nchini kimeingia mkataba na Profesa Mwesiga Baregu ambapo atafundisha katika chuo hicho kulingana na mkataba huo.

Hatua hiyo ya Profesa Baregu kujiunga na SAUT inkauja baada ya suala lake na Chuo Kikuu cha D'Salaam kumalizika na kwamba ujio wa profesa huyo unaleta changamoto katika maendeleo ya taaluma ya uandishi wa habari na mawasiliano nchini.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa Profesa Baregu tayari amekwishaanza kufundisha katika kampasi ya D'Salaam ya SAUT ambako kuna wanafunzi wa shahada ya uzamili (MA) na uzamivu (PhD).

Akizungumza na TUMAINI LETU kwa njia ya simu, mkuu wa idara ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano ya Umma, Padri (Dk.) Joseph Matumaini alithibitisha tarifa hiyo na kwamba tayari wameingia mkataba na Profesa Baregu na atakuwa akifundisha katika kampasi ya D'Salaam na Mwanza yaliko makao makuu ya SAUT.

Dk. (Padri) Matumaini alisema kuwa kuwepo kwa profesa huyo hapo chuoni SAUT kunaleta matumaini mapya na changamoto katika tasnia ya habari kwa kuwa ana uzoefu mkubwa katika fani mbalimbali kitaaluma.

"Ni kweli Prof. Baregu amekwishaanza kazi SAUT kwa sababu tunatambua mchango wake na tunaamini ataongeza nguvu katika kukiimarisha chuo chetu katika utoaji wa elimu bora", alisema Dk. (Padri) Matumaini ambaye pia ni mhadhiri katika chuo hicho.

Alifahamisha kuwa ni matumaini ya SAUT kuwa Profesa huyo atatumia uwezo na ujuzi wake kitaaluma kuwanufaisha wanafunzi wanaosoma katika chuo hicho kinacholenga kuleta mapinduzi ya tasnia ya habari na mawasiliano ya umma nchini.

"Sisi tunafahau kuwa Profesa bareu ana mchango mkubwa sana kitaaluma, hivyo tunategemea tutabadilishana naye mawazo kitaaluma katika nyanja tofauti ili kusaidia utoaji wa elimu ukizingatia kwamba chuoa chetu ni ca kwanza kutoa shahada ya uzamili na uzamivu katika tasnia ya habari na mawasiliano", alisisitiza Dk. (Padri) Matumaini.

Alifahamisha kuwa mkataba alioingia profesa huyo ni wa miaka mitatu ambao hata hivyo unaweza kupitiwa upya kila unapomalizika.

**********************************************************
Chanzo: Gazeti la TUMAINI LETU
Mmiliki wa gazeti: Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la D'Salaam
Toleo la Gazeti: Namba 00298, February 19, 2010
Sehemu ya Gazeti yenye habari: Ukurasa wa 04

**********************************************************
 

Attachments

  • Baregu aanza kazi SAUT.pdf
    261 KB · Views: 114
Safi sana, acha SAUT wamtumie mwanazuoni huyo mahiri. Ila tu Prof. Baregu utulie uheshimu kazi yako, shughuli binafsi na zile za kisiasa zisimeze (outweight) vipindi vyako. Hongera, tunategemea matunda mazuri ya kazi.
 
Safi sana, aachane na wakina Hawa Ghasia wasiojua faida ya Wahadhiri wetu na uhaba tulio nao
 
. Ila tu Prof. Baregu utulie uheshimu kazi yako, shughuli binafsi na zile za kisiasa zisimeze (outweight) vipindi vyako. Hongera, tunategemea matunda mazuri ya kazi.
unachosahau ni sawa na kile ambacho serikali imejisahau kuwa Prof.Baregu ili abaki kuwa mwalimu mzuri ni lazima ajishughulishe na siasa kiundani hasa, maana yeye amebobea ktk siasa , na anawafunza watoto wetu siasa, hivyo lazima awe muelewa kiasi cha kutoosha.
ni sawa na bwana shamba asie na shamba, anaonekana kupwaya mbele ya macho ya Pinda[PM]
vilevile ni sawa na kina Prof Shaba , ingawa yeye ni daktari wa kuchunguza maiti na amekuwa mwalimu pale Muhimbili UNiversity kwa miaka zaidi ya 25,
elimu ya chuo kikuu inahitaji watu waliobobea hasa, sasa utabobeaje kama utendi kile ambacho taaluma yako inakutaka utende.?
kumbuka chuma kisichotumika huota kutu kwa kasi....
 
Safi sana, acha SAUT wamtumie mwanazuoni huyo mahiri. Ila tu Prof. Baregu utulie uheshimu kazi yako, shughuli binafsi na zile za kisiasa zisimeze (outweight) vipindi vyako. Hongera, tunategemea matunda mazuri ya kazi.

Yeye ni mwalimu wa siasa ataachaje siasa Prof. Baregu na siasa ni kama chanda na kidole havitenganishwi kwa urahisi.
 
Wote ni Watanzania na kazi ya SAUT ni nzuri sana katika ujenzi wa Taifa letu, hivyo kwa Prof Baregu anaweza kuwa chachu ya wanafunzi kubwa sana
 
Ila tu Prof. Baregu utulie uheshimu kazi yako, shughuli binafsi na zile za kisiasa zisimeze (outweight) vipindi vyako.

SAUT waliomchukua walisema mapema kabisa kwamba wanajua Prof. Baregu ni mwanasiasa na wanajua haitamzuia kutoa elimu yake pale. Kumbuka ilitamkwa vile siku mbili tu UDSM walivyomtupa Baregu kwa kujidhani bado ni chuo cha kubabaikiwa na kunyenyekewa kana kwamba utandawazi haujakifunika kwa kuleta vyuo vikuu tele.

Wewe Maane ungekuwa unamiliki University yako basi ungesubiri Baregu aje kuomba kazi kwako na umueleza hiyo kauli yako ambayo naamimi Baregu angeachana na wewe kabla hujamalizia sentensi yako. Hata mimi ukinieleza hayo sina haja ya kunyenyekea kufundisha au hata kusoma katika chuo chako!
 
Wote ni Watanzania na kazi ya SAUT ni nzuri sana katika ujenzi wa Taifa letu, hivyo kwa Prof Baregu anaweza kuwa chachu ya wanafunzi kubwa sana
ni kweli Josh, SAUT inaweza kutoa funzo kwa watendaji dhalili wa sekta za umma,
mimi naamini SAUT wamelamba dume kwa kupata hicho kichwa na inaweza ikawaongezea hadhi na heshima.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom