Prof. Anna Tibaijuka atolea Ufafanuzi sakata la Escrow, agoma Kujiuzulu

ajiuzulu..ndio ajue ukiwa waziri halafu unazungukia matajiri kuomba hela kwa miradi yako binafsi sio maadili. Kwani wanaomchangia anawapa hisa kwenye huo mradi wake wa shule? Alichofanya ni matumizi mabaya ya ofisi yake kama waziri. Kwa mtindo huo rugemalila akitaka hisani yoyote kwa waziri ataweza kumkatalia?

kuwa na nidhamu. Kunadada zako wanasomeshwa na yy bureee. Acha ubinafsi weyeeee
huyu mama anafaa sana ni mchapakazi na nimsomi. Ulionaga wapi msomi akawa mbuzi wa kafara? Hawa wasomi maprofesa ni watendaji wenye uthubutu na ambao huchapa kazi nzuri na nzito. Hatakiwi kujiuzuru maana hizo pesa sio zake bali ni za kuwasaidia wanawake kupata elimu katika shule zake kabambe zenye viwango vya hali ya juu.
 
yuko single unaweza kumapproach kama anakuvutia,tusichotaka ni kutumia rasilimali za taifa kwa manufaa binafsi, kama wewe ni msichana nena babro johnson ukasaidiwe 'bure'!

mimi namtaka mama yako na bibi yako niwawowe kwa pamoja , then badae ntakuwowa wewe
 
huyo ni mwizi tu kama wezi wengine. kwanza kwa mtumishi wa umma kama yeye sheria haziruhusu kupokea zaidi ya 50,000 kama msaada bila kutoa taarifa. yeye kapiga 1,600,000,000,000 kimya.
achilia mbali hizo hela alipewa kwa dili lipi. hiyo ya shule yake ni zuga tu. labda kama atatuambia na hiyo shule haina account.
 
huyu profesa ni mwizi. yeye katika kufanya kazi kwake duniani ni wapi alipoona waziri katika serikali anapewa pesa kwenye akaunti yake binafsi na mfanyabiashara!? je hao anaowataja walimuwekea pesa kwenye akaunti yake binafsi kama Rugemarila? ni msomi mpuuzi!? atuambie na wezi wenzake wamepewa ngapi Werema na Muhongo!
 
Hii nchi bwana mi mpaka naona kama tunafanya maigizo,nchi nyingine mtuhumiwa kama huyu hata kujitokeza barabarani tu ni kimbembe lakini hapa kwetu ndiyo kwanza na press anaandaliwa na wizara kama hela walikula na wizara
 
Safari hii JK anakazi kwerikweri, alizoea wanajiuzulu wenyewe, sasa ngoma anaicheza mwenyewe na inaelekea imemshinda!
 
Nimeamini kwamba tunaviongozi vilaza. Hivi huyu mama ndio utetezi gani huu dhidi ya tuhuma nzito kama hii???uongozi wa kisiasa sio wakung'ang'ania namna hii...aibu Yao na ndio mwanzo wa mwisho wao katika uongozi wa kisiasa. Ref: uchaguzi wa serikali za mitaa. Bado kuipiga chini Katiba na kulinda Kura 2015 tuone watatokea wapi....
 
huyu mama huwa hajui kujitetea sijui ni prof wa aina gani..ndo maana akipigwa maswali sana anakuja juu na kuwa mkali kwa majibu hayo bado ni dhaifu sana kuwaeleza watu wakakwamini.
 
Hii nchi bwana mi mpaka naona kama tunafanya maigizo,nchi nyingine mtuhumiwa kama huyu hata kujitokeza barabarani tu ni kimbembe lakini hapa kwetu ndiyo kwanza na press anaandaliwa na wizara kama hela walikula na wizara
madhara ya ujinga wao na viutetezi vyao ni makubwa mno. Ni kwakukosa akili ndio maana hata hotuba ya raisi inahairishwa
 
Tangia jana nilipoona hotuba yake nimeghairi kwenda kuchumbia kwenye ukoo wao,inaonekana ni wasumbufu na wabishi sana.
 
madhara ya ujinga wao na viutetezi vyao ni makubwa mno. Ni kwakukosa akili ndio maana hata hotuba ya raisi inahairishwa

Msimuonee mama AKJ anasaidia watoto wanaotoka kwenye mazingira magumu kama alivyosaidia makazi bora kwa wasio na uwezo kule Kenya
 
Jamani the donn na rais mtalajiwa ndio mama tibaijuka, hivyo kazi kwenu hizo post anajibu mwenyewe
 
Kwa muda mwingi tanga bunge kutoa mapenedkezo kuhusu watuhumiwa wa account ya ESCROW mama huyu amekua akiongea sana na hata kujisifu kuwa Hela aliazopewa hazina shida ni mchango tu kwa shule yake na wala asingeweza kukataa.Pia jana ameongea na waandishi na kujisifu kua hawezi kujiudhuru kwani haoni kosa lake! Maswali yangu yanakuja hapa , Jeuri ya mama Tibaijuka inatoka na Nini?? Ukimya wa Muheshimiwa Rais na Ikulu yake?? au ana mkataba na Uwaziri kwamba hakuna anayeweza kumtoa hata kama ameshindwa kuwajibika? . kwa nini Prof mohongo yuko kimya lakini yeye kutwa kwenye vyomba vya habari kutaka kuclarify fedha hizo anazosema alipewa kwa ajili ya mchango wa shule yake!!

Mimi kwa kweli Hasira zimepanda na hata cielewi Jeuri ya Huyu mama inatoka api???
 
Acha kuchokonoa mambo? au unataka kuhusisha na Kikwete kulala kwa Tibaijuka akiwa Safarini Bukoba?
 
inatokana na kwamba anajiamini anachokifanya na anachokiongea. Kama unajiamini na na unajua kinachoelekezwa kwako si sahihi huwez tetereka.
 
acheni ushabiki wakijinga. Huyu mama hana kosa hata. Na kwenye chama kama mnataka fitina mkidhani ni ushindi mtaangukia pua. Tuache ushabiki wa kijinga, make a research before.
tujibu alifanya kazi ipi huyu mtumishi wa umma kwa malipo halali ya 1.6b ??
 
Back
Top Bottom