Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,564
- 7,973
Mkuu Mkandara kwanza kabisa nikiri kwamba wewe ni mmoja kati ya watu ninaowaheshimu sana hapa JF kwa comments zilizo na ujazo na tena uko objective sana on issues of our national interests. Na kwahakika najifunza mengi sana toka kwako na maandiko yako hapa JF.
Samahani lakini mkuu, unaonaje ukitumia kipaji chako, taaluma yako, uzoefu wako, ujuzi wako na nguvu zako kujaribu kutoa suluhisho la matatizo/maswaibu/malalamiko ya waislamu ili kuwasaidia wale wasiofahamu exactly ni mambo gani yanayodaiwa na waislamu ambayo yanahitaji kuungwa mkono na wazalendo wote.
Nadhani ni muhimu sana usikwame kwenye tope la kuwa mlalamikaji, kama walivyo viongozi wetu; DC analalamika, RC analalamika, Waziri analalamika, Waziri mkuu analalamika na Raisi naye analalamika! Naomba utusaidie kutoa/kupendekeza suluhu ya matatizo hayo ili tupate pa kuanzia.
Kwa sasa naomba kuishia hapa kiongozi wangu.
Samahani lakini mkuu, unaonaje ukitumia kipaji chako, taaluma yako, uzoefu wako, ujuzi wako na nguvu zako kujaribu kutoa suluhisho la matatizo/maswaibu/malalamiko ya waislamu ili kuwasaidia wale wasiofahamu exactly ni mambo gani yanayodaiwa na waislamu ambayo yanahitaji kuungwa mkono na wazalendo wote.
Nadhani ni muhimu sana usikwame kwenye tope la kuwa mlalamikaji, kama walivyo viongozi wetu; DC analalamika, RC analalamika, Waziri analalamika, Waziri mkuu analalamika na Raisi naye analalamika! Naomba utusaidie kutoa/kupendekeza suluhu ya matatizo hayo ili tupate pa kuanzia.
Kwa sasa naomba kuishia hapa kiongozi wangu.
Last edited by a moderator: