Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Timu ya Tanzania Prisons imepewa ushindi wa alama tatu na mabao matatu kwenye mchezo uliokuwa ufanyike February 11, 2020 baada ya timu ya Ruvu Shooting ambao ni wenyeji wa mchezo kushindwa kuleta gari la wagonjwa (Ambulance) uwanjani.
Taarifa iliyotolewa leo na Shirikisho la soka la TFF imeeleza kuwa uamuzi huo ni kwa mujibu wa kanuni ya 14 (2|) jambo lililosababisha mchezo kuvunjwa na mwamuzi baada ya kusubiri dakika 30 bila gari hilo kutokea.
Mchezo huo ulikuwa wa ligi kuu Tanzania, Vodacom Premier League (VPL), namba 205, kati ya Tanzania Prisons FC na Ruvu Shooting.
Taarifa iliyotolewa leo na Shirikisho la soka la TFF imeeleza kuwa uamuzi huo ni kwa mujibu wa kanuni ya 14 (2|) jambo lililosababisha mchezo kuvunjwa na mwamuzi baada ya kusubiri dakika 30 bila gari hilo kutokea.
Mchezo huo ulikuwa wa ligi kuu Tanzania, Vodacom Premier League (VPL), namba 205, kati ya Tanzania Prisons FC na Ruvu Shooting.