Prison Enterprises-Making our Prison System Productive

Masokotz

JF-Expert Member
Nov 26, 2018
3,480
5,506
Sina Takwimu za uhakika za idadi ya Wafungwa Nchini ila nina imani kabisa katika Magereza yetu tunaweza kuwa na idadi ya Wafungwa ambao wanaweza kuzalisha bidhaa mbalimbali na kuchangia katika ujenzi wa uchumi.Natambua kwamba mtu anapokuwa kifungoni anakuwa anatumikia adhabu kwa kosa alilofanya lakini hii haimaanishi kwamba maisha yake hayana maana na kwamba hawezi kufanya shughuli za uzalishaji.

Kama taifa tunaweza kuwa na Mfumo ambao unawawezesha wafungwa kupata malipo kabisa kwa kazi za uzalishaji wanazofanya wanapokuwa gerezani.Kipato hiki kinaweza kutumika kuwasaidi wafungwa pindi wamalizapo kifungo na pia kinaweza kusaidia katika kuwapatia mahitaji wategemezi wao pindi wawapo kifungoni.

Baadhi ya Shughuli zinazoweza kufanywa na wafungwa ni pamoja na shughuli za KILIMO na UFUGAJI,Uchimbaji wa Kokoto na Mchanga,Uzalishaji wa Nguo,viatu na bidhaa za aina hio.Katika kuamua mfumo wa malipo inaweza kutumika kanuni ya minimum wage ya sekta husika.

Ni muhimu sana Walipwe kwa kazi wanazofanya ili kuwajengea utu,hadhi na nidhamu.

Tukifanikiwa katika hili tutajenga jamii ya kipekee sana ambayo inathamini utu na tunaweza kuchangia kushusha kiwango cha uhalifu hapa nchini.

Tujadili hapa kwa kina namna ambavyo tunaweza kuboresha mfumo wetu wa Magereza na kuongeza uzalishaji wenye Tija.
 
"Tujadili hapa kwa kina namna ambavyo tunaweza kuboresha mfumo wetu wa Magereza na kuongeza uzalishaji wenye Tija"

Umejiuliza ni nani atawalipa wafungwa kwa Shughuli za kilimo na ufugaji?
Na mtaji wa shughuli hizo nani atatoa! serikali?

Kwa hiyo tuwafanye kama vibarua walime,na wafuge walipwe na serikali?
 
"Tujadili hapa kwa kina namna ambavyo tunaweza kuboresha mfumo wetu wa Magereza na kuongeza uzalishaji wenye Tija"
Umejiuliza ni nani atawalipa wafungwa kwa Shughuli za kilimo na ufugaji?
Na mtaji wa shughuli hizo nani atatoa! serikali?
Kwa hiyo tuwafanye kama vibarua walime,na wafuge walipwe na serikali?
Sio lazima iwe serikali,Kunaweza kuwa na aina ya ubia kati ya serikali na wawekezaji kuhusu namna ya kutumia hio labour force kwa manufaa ya nchi.Kama serikali ikweza kuwekeza basi itakuwa ni jambo zuri pia.Naamini kuna namna nyingi ya kulifanya hili na kuweza kufikia lengo la msingi.
 
Sio lazima iwe serikali,Kunaweza kuwa na aina ya ubia kati ya serikali na wawekezaji kuhusu namna ya kutumia hio labour force kwa manufaa ya nchi.Kama serikali ikweza kuwekeza basi itakuwa ni jambo zuri pia.Naamini kuna namna nyingi ya kulifanya hili na kuweza kufikia lengo la msingi.
Sawa,em elezea hizo namna nyingi ya kulifanya jambo hili lifanikiwe!
 
Sio lazima iwe serikali,Kunaweza kuwa na aina ya ubia kati ya serikali na wawekezaji kuhusu namna ya kutumia hio labour force kwa manufaa ya nchi.Kama serikali ikweza kuwekeza basi itakuwa ni jambo zuri pia.Naamini kuna namna nyingi ya kulifanya hili na kuweza kufikia lengo la msingi.
Una mawazo mazuri sana sana. Magereza ni sehemu inayoweza kutumika kuzalisha bidhaa za aina nyingi. Kuna vitu kama bustani za mboga, uokaji wa vitafunwa eg mikate, biskuti nk. Vikifanyika kitaalam hata bidhaa zake zinaweza kuuzwa nje ya nchi.

Pia Magereza wanaweza kuwa na chain ya vitu kama SuperMarkets na bidhaa zote zinazouzwa humo zikawa zinatengenezwa nao. Mambo ni mengi: Ufugaji wa samaki, ufugaji wa wanyama na ndege, kilimo, bakeries, etc
 
Ni wazo zuri sana. Tukifikia hapo itabidi vijana watamani kufungwa ili wapate hiyo fursa ya kuzalisha mali na kupata huo ujira kidogo.

Maana huku mtaani wanazunguka tu kama pia, wanazunguka na kalamu na makaratasi kama wasomi kumbe ni kamari tu.
 
Back
Top Bottom