Prince Wiliam akutana na Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu. Aahidi kusaidia katika kuboresha ulinzi wa wanyama pori

ishenga

Senior Member
Jul 8, 2015
162
185
1.jpg

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo amekutana na kufanya mazungumzo na Prince William katika jumba la Kifalme la Buckingham Palace.

Makamu wa Rais alimweleza Prince William kuwa Tanzania inatambua mchango wake katika kuzuia ujangili wa wanyama pori na Serikali ya Tanzania imekuwa ikichukua hatua mbali mbali ya kupambana na kuzuia ujangili ingawa bado hatujawa na tekinolojia yenye uwezo wa wa kutambua na kuona wanyama wote lakini tumeendelea kuimarisha ulinzi wa wanyama pori.

Kwa upande wake Prince Williams alimuahidi Makamu wa Rais kusaidia katika kuboresha ulinzi wa wanyama pori kwa kutumia teknolojia ya hali ya juu na pia Prince William amemualika Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika mkutano unaohusu masuala ya Wanyapori unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu jijini London.


Makamu wa Rais Mhe. Samia yupo nchini Uingereza kumuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa nchi za jumuiya ya Madola.

Chanzo: Mpekuzi

Pia soma >Makamu wa Rais kumwakilisha Rais Magufuli kwenye mkutano wa wakuu wa nchi wa Jumuiya ya Madola
 
Angmwambia hatutaki ulinzi tunataka VIWANDA ............!!

Hivi ahadi kama hizi zikitolewa, kabla ya kukubali huwa wanawasiliana na Mkulu kupata baraka au inakuwaje ...........!!?
 
Nina wasiwasi na huyu Baba alie alikwa iwapo atakubali kwenda, maana naona lugha inamtesa sana ndiomaana anaogopa...... tehteehhh
 
Mmmh....mbali na hiyo technolojia Prince William, tunataka tupewe vifaa vya kisasa vya kugundua namna risasi zinawezaje kupigwa chini Na kwenda kwenye daladala ( R.I.P Akwilina), Na namna hawa watu wanaofanya matukio ya utekaji and political assassination ( watu wasiojulikana) hawapatikani kwann wakati jeshi na TIS wapo!
 
Nina wasiwasi na huyu Baba alie alikwa iwapo atakubali kwenda, maana naona lugha inamtesa sana ndiomaana anaogopa...... tehteehhh
Hapo kwenye mwaliko ndo mtihani kama lowasa kupima dna bora angemwambia huo mkutano waufanyie aicc. Vipi netanyahu keshakubali mwaliko?
 
Tuzungushie ukuta tu huko kwenye hifadhi za Taifa zote ili kudhibiti ujangili.

Hakuna namna kila kwenye mali asili zungusha tu. Hakuna wa kumuamini sasa hata mkulu anapiga madili ya trilioni 1.5 itakuwaje kwa hao walinzi wa TANAPA.
 
Back
Top Bottom