Press za John John Mnyika mwezi huu zinafikirisha sana

Wiki iliyopita Katibu mkuu wa CHADEMA J J Mnyika aliitisha kikao cha waandishi wa habari na kuhoji alipo Rais Magufuli na kama yupo salama. Waziri mkuu mh Majaliwa alijibu siku hiyo hiyo akiwa mkoani Njombe kikazi.

Jana J J Mnyika alitangaza kikao kingine cha waandishi wa habari ambacho kingefanyika leo lakini usiku wa jana alikiahirisha kufuatia tangazo la msiba wa Rais Magufuli lililotolewa na makamu wa Rais Mama Samia.

Huyu J J Mnyika anaonekana kuanza kukomaa kisiasa.

Maendeleo hayana vyama!
Unaweweseka tu hata huelweki sasa! Poleni kwa musiba
 
Mawazo yangu yapo mbaaali.
Mie nasubiri May Mosi tu Bi mkubwa atangaze nyongeza ya mishahara serekalini
 
Ukitafakari tena matukio yote ya nyuma kuanzia kwa Tundu Lissu mpaka Chahali kututangazia kifo it all adds up.

Huko serikalini sio wapuuzi hivyo kama tunavyodhani. Inavyoonekana mambo yalienda mrama haraka sana kwenye kudhoofika kwa afya ya Magufuli kuliko walivyotegemea.

Baada ya kuona Magufuli yupo kwenye life support na achomoki tena njia sahihi wavujishe habari zenye nusu ukweli kuandaa watu kisaikolojia kupitia kwa Lissu na baadae Chahali kututangazia.

Naamini walijua walichokuwa wanakifanya from the time wanavujisha habari kwa Lissu, mpaka Chahali anatangaza kwa kujiamini; yalikuwa ni maandalizi yetu ya kisaikolojia mjomba kavuta tayari ghafla ghafla watu waanze kukubali hizo possibility’s.
 
Yaani kila nikifikiria miradi ya JPM nashikwa na huzuni. Sijui nani anaweza kuiendeleza. Maana mwisho wa siku ni kodi zetu.

Maana yote ilikuwa inafanyika kwa utashi wa mtu mmoja!
Gbadolite za chato zitakufa! SGR nk itaendelea
 
Back
Top Bottom