Press ya Mnyika yawavuruga CCM

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Oct 29, 2018
539
3,507
Baada ya John Mnyika kuweka wazi namna Jeshi la Polisi na serikali walivyotumika kubambikia kesi Mbowe huku wakipeleka charge isiyo na sifa CCM kupitia Shaka wameparaganyika na kuanza kuitetea polisi, Mahakama na serikali.

Hatua hii inafuatia Mnyika kueleza utekaji aliofanyiwa Mbowe, ubovu wa hati ya mashtaka na uhusika wa viongozi wa CCM kwenye njama hiyo.

Aidha press ya Mnyika imeweka wazi njama ya msajili wa vyama kutaka kukifuta Chadema kwa maelekezo ya CCM na kwakutumia mbinu matumizi ya sheria iliyofanyiwa marekebisho na bunge kuhusu wanachama wa siasa kufanya vurugu.

Aidha, mtego wa kufutwa chadema unabainishwa na Chadema baada ya Kigogo kusisitiza waandamane Jambo ambalo lingewepa ccm nguvu kupitia msajili wa vyama kutekeleza adhma yao.

Njama hizi zinavuja siku chache baada ya vijana wa CCM kuvalia sare za chadema nakuitisha mkutano na waandiahi wa habari ambapo hata baada ya kufichuliwa kwa uovu huo msajili wa vyama alikaa kimya kuashiria alifahamu au anakubaliana na kitendo hicho.

Kwa Hali ilivyo upo uwezekano vijana wengi zaidi wa CCM wakaendelilea kuvaa sare za chadema na kufanya uhalifu kuthibitisha njama mbovu ya viongoz wa CCM dhidi ya CDm
 
CCM ilishakufa. Kilichopo madarakani ni kikundi cha ukandamizaji na uonevu kinacholindwa na dola.

Maana hata uchaguzi mkuu wa 2020 hakikushinda. Kimewekwa na dola.
Mkuu, umeliweka hili vizuri sana kiasi kwamba asiyeweza kuelewa mistari hii miwili atakuwa ana matatizo kichwani mwake, au atakuwa ni mmoja wa hicho "kikundi cha ukandamizaji."

Naomba ruhusa na mimi niwe natumia nukuu yako hii katika maandiko yangu humu JF, ili kuwekea uzito wa hali tuliyofikia nchini mwetu.
 
Siku bunge lisilo na meno linalokula tu fedha za watanzania na kisha kutunga sheria kandamizi likivunjwa ndio nitarudi Tanzania. Bunge limeshindwa kabisa kuishauri serikali.

Kwa sasa nipo zangu Burundi
Kwani serikali inataka kushauriwa mkuu 'Mega Mind Nyerere'?

Kwan nini usiione serikali kuwa ndiyo inayopenda hali hiyo, na badala yake ulaumu bunge ambalo lenyewe limepewa kazi hiyo ya kutoshauri na kutunga sheria kandamizi?

Inaoneana hata kukaa kwako huko Burundi hakutakusaidia sana kama utaendelea kuwa na mawazo ya kuweka lawama mahali ambapo lawama si mahali pake.

Unaogopa nini kuilaumu serikali ya CCM na viongozi wake kuhusu ubovu wa bunge na mambo mengine? Unamaslahi nako huko serikalini?
 
Tanganyika Huru haijawahi kupata Chama Machachari kabisa cha Upinzani kama Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Chama tawala hakilali wala kupata usingizi kama hapo zamani

Hizi njama za kukifuta Chama chetu ni dalili za kushindwa kwa CCM na vibaraka wake ULIMI NJE😁

Hadi naukumbuka ule Wimbo wa Tundu Lissu wapeleke mchakamchaka😂
 
CHADEMA bado mna mwendo mrefu Sana.
Mtu anapigapiga domo no action mnamsifia. Poor you.
Watu Wale wale mbinu zilezile utegemee maendeleo never.
Mtazoza usiku mtalala CCM ipo tuuu.
 
Baada ya John Mnyika kuweka wazi namna Jeshi la Polisi na serikali walivyotumika kubambikia kesi Mbowe huku wakipeleka charge isiyo na sifa CCM kupitia Shaka wameparaganyika na kuanza kuitetea polisi, Mahakama na serikali.

Hatua hii inafuatia Mnyika kueleza utekaji aliofanyiwa Mbowe, ubovu wa hati ya mashtaka na uhusika wa viongozi wa CCM kwenye njama hiyo.

Aidha press ya Mnyika imeweka wazi njama ya msajili wa vyama kutaka kukifuta Chadema kwa maelekezo ya CCM na kwakutumia mbinu matumizi ya sheria iliyofanyiwa marekebisho na bunge kuhusu wanachama wa siasa kufanya vurugu.

Aidha, mtego wa kufutwa chadema unabainishwa na Chadema baada ya Kigogo kusisitiza waandamane Jambo ambalo lingewepa ccm nguvu kupitia msajili wa vyama kutekeleza adhma yao.

Njama hizi zinavuja siku chache baada ya vijana wa CCM kuvalia sare za chadema nakuitisha mkutano na waandiahi wa habari ambapo hata baada ya kufichuliwa kwa uovu huo msajili wa vyama alikaa kimya kuashiria alifahamu au anakubaliana na kitendo hicho.

Kwa Hali ilivyo upo uwezekano vijana wengi zaidi wa CCM wakaendelilea kuvaa sare za chadema na kufanya uhalifu kuthibitisha njama mbovu ya viongoz wa CCM dhidi ya CDm
Ccm ilishakufa zamani kilichobaki ni kikundi cha watu wanaolinda maslai yao kwa kusaidiwa na plc
 
CHADEMA bado mna mwendo mrefu Sana.
Mtu anapigapiga domo no action mnamsifia. Poor you.
Watu Wale wale mbinu zilezile utegemee maendeleo never.
Mtazoza usiku mtalala CCM ipo tuuu.
nakuonea huruma sana kwakua ujitambti
 
Nimesikitika kuona hata TBC nao wanahusika na hizi propaganda. Hii Hali ina athari kubwa Sana kwa utendaji wa mkuu wa nchi. Bado miaka mitatu kufikia kipindi Cha kuanza propaganda za uchaguzi ila ukianza Leo maana yake lazima uache kuwatumikia wananchi uwatumikie viongozi wa CcM na watoto wao. Si muda wakuangaika kutumia pesa za walipa kodi kulipa watu wafanye propaganda ni muda wakutenganisha urais na shughuli za chama.

Naomba nitabiri na kama Rais akitumia utabiri wangu atakubaliana na Mimi " Ikulu, kwenye chama na ndani ya vyombo vya dola wapo watu wanatajirika kupitia mradi huu wakupambana na upinzani. Watu Hawa wanatumia mwanya huu kupokea fedha serikalini kusafiri nchi nzima kwa mambo yasiyokuwepo na ambayo hayawezi kufanyiwa auditing. Naamini kwa uzoefu wangu kwenye ualimu wapo watu kutoka makao make ya wizara,idara na state wanatengeneza propaganda mikoani then wanajilipa kwenda kuzitatua tuweni makini nao. Naamini hata kwenye dola wanaojenga maghorofa ni wale walioofisi nyeti ya nchi ambao kwa kipindi Cha mwalimu walikuwa hawaruhusiwi kuzikumbatia fedha haramu, wanaotisha watu bar ni watu wa ofisi nyeti, wanaotisha watu wauziwe ardhi ni watu wa ofisi nyeti, wanaofanya anasa ni watu wa nyumba nyeti na si kutoka ofisi zote Bali kutoka makao Dodoma na Dar. Hawa watu wanatoa wapi fedha kipindi hiki? Wanasafiri huko mikoani hakuna watu wakufanya hizo kazi? Hawa ndio wanaelekeza watu wasitolewe mahabusu Hadi wafike wao, Hawa ndio wanaowaelekeza ma RPC wafanye nn? Tusipowadhibiti tukaona wananufaika ipo siku waliopo mikoani watagawanyika kutaka kwenda huko juu kwa kuchoshwa na maelekezo ya watu wapumbavu.

Nchi haina Tena nidhamu, wasimamizi wa nidhamu wamekuwa watovu na nidhamu. Kijana wa Tiss ana few years kazini anapata wapi fedha zakujenga ghorofa? Anapata wapi jeuri yakutisha watu bar kwamba atawafix? Ipo siku wakiendelea kuzoea kupata madili machafu siku wakiyakosa watakuwa waasi, turudishe nidhamu ya jeshi, idara nyeti na taasisi nyingi, tuwajengee uwezo lakini TUKIRUHUSU CONSTABLE WA MAKAO MAKUU AKAWA NA NGUVU KULIKO OCD TUTAVUNA TUNACHOPANDA ALIYASEMA MWALIMU WETU WA JKT MIAKA YA TISINI KWAMBA UKUBWA WA ASKARI SIYO KITUO NI MABEGA.
 
Mimi nawalaumu sana Bavicha kuwaacha hawa mashoga wa uvccm kuendelea kuichafua Chadema. Hao vijana wanafahamika,makazi yao yanafahamika na familia zao zinafahamika,sasa ugumu uko wapi? Lazima kuwashughulikia ili iwe fundisho wasirudie tenda huu umalaya wao.
 
Baada ya John Mnyika kuweka wazi namna Jeshi la Polisi na serikali walivyotumika kubambikia kesi Mbowe huku wakipeleka charge isiyo na sifa CCM kupitia Shaka wameparaganyika na kuanza kuitetea polisi, Mahakama na serikali.

Hatua hii inafuatia Mnyika kueleza utekaji aliofanyiwa Mbowe, ubovu wa hati ya mashtaka na uhusika wa viongozi wa CCM kwenye njama hiyo.

Aidha press ya Mnyika imeweka wazi njama ya msajili wa vyama kutaka kukifuta Chadema kwa maelekezo ya CCM na kwakutumia mbinu matumizi ya sheria iliyofanyiwa marekebisho na bunge kuhusu wanachama wa siasa kufanya vurugu.

Aidha, mtego wa kufutwa chadema unabainishwa na Chadema baada ya Kigogo kusisitiza waandamane Jambo ambalo lingewepa ccm nguvu kupitia msajili wa vyama kutekeleza adhma yao.

Njama hizi zinavuja siku chache baada ya vijana wa CCM kuvalia sare za chadema nakuitisha mkutano na waandiahi wa habari ambapo hata baada ya kufichuliwa kwa uovu huo msajili wa vyama alikaa kimya kuashiria alifahamu au anakubaliana na kitendo hicho.

Kwa Hali ilivyo upo uwezekano vijana wengi zaidi wa CCM wakaendelilea kuvaa sare za chadema na kufanya uhalifu kuthibitisha njama mbovu ya viongoz wa CCM dhidi ya CDm
Kwahiyo jana walilala na viatu?
 
15 Reactions
Reply
Back
Top Bottom