Infantry Soldier
JF-Expert Member
- Feb 18, 2012
- 15,893
- 16,317
Habari zenu JamiiForums.
Ninaomba kuanza kwa kunukuu maneno ya Balozi Mkuu wa lugha ya Kiswahili Mh. J.P Magufuli alipokuwa kwenye hafla moja jijini Dodoma. Mheshimiwa Rais alisema hivi “Nimefanya PHD bado wanasema sijui Kiingereza, na nikakaa mwaka mzima Uingereza, sijui nilikuwa nazungumza Kisukuma kule!, wakasema sijui Kiingereza, niliamua kuzungumza Kiswahili na kuki-promote kwasababu ni lugha iliyoachwa na Baba wa Taifa"
Picha hapo juu ni Mh. Rais Dk. JP Magufuli akiwa na Waziri wa mashauri ya kigeni Prof. Kabudi wakikabidhi vitabu vya kiswahili kwa Rais wa Jamuhuri ya Afrika ya Kusini Mh. Ramaphosa katika harakati ya kuhakikisha lugha hii tamu inakuwa na kuenea kwa haraka zaidi nje ya mipaka ya Tanzania na Afrika ya Mashariki.
Kitabu cha Kiingereza cha Mzee Mkapa: My Life, My Purpose: A Tanzanian President Remembers
Mheshimiwa, hayati Benjamin William Mkapa ndiye aliyekuwa rais wa tatu wa Tanzania, aliyechaguliwa chini ya mfumo wa kwanza wa vyama vingi hapa nchini. Kitabu chake kinafafanua kumbukumbu zake kutokea utotoni, wakati bado akiwa rais, na kuendelea kwake kujihusisha (hata baada ya kustaafu) kwenye masuala ya kimataifa yahusuyo maendeleo na upatanishi wa amani.
Kitabu hiki kinavutia sana kwa wasomaji wanaopenda kujua kuhusiana na, kadhia aliyoipitia mwafrika katika kipindi cha ukoloni hususan eneo zima la Afrika Mashariki na mapambano ya uhuru na harakati za ukombozi wa nchi kadhaa za kusini mwa Afrika.
Mheshimiwa Mkapa ameandika pia kuhusu utoto wake, kukomaa kwake kisiasa, mabadiliko ya kimfumo/kiutawala na kisiasa nchini Tanzania, na vile vile machafuko ya kisiasa katika nchi jirani.
Kitabu hiki kimejaa maoni yake juu ya uongozi na ushauri kwa viongozi wanaochipukia kama dada yangu mama D. Baada ya Mwalimu Julius Nyerere, ni vitabu vichache sana vimeandikwa na viongozi wakuu wa Tanzania juu ya mageuzi ya nchi; kwa kweli bila kuwa mnafiki vitabu vingi vinavyosomwa hapa nchini vimeandikwa na wageni kuliko watanzania, kwa hivyo kitabu cha Mh. Mkapa ni mfano bora wa kuigwa.
I Can, I Must, I Will written by Dr. Reginald Mengi
=====
OMBI LANGU: Itapendeza sana kama Rais Magufuli ataandika kitabu cha maisha yake kwa kutumia lugha ya wazalendo ya KISWAHILI.
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Ninaomba kuanza kwa kunukuu maneno ya Balozi Mkuu wa lugha ya Kiswahili Mh. J.P Magufuli alipokuwa kwenye hafla moja jijini Dodoma. Mheshimiwa Rais alisema hivi “Nimefanya PHD bado wanasema sijui Kiingereza, na nikakaa mwaka mzima Uingereza, sijui nilikuwa nazungumza Kisukuma kule!, wakasema sijui Kiingereza, niliamua kuzungumza Kiswahili na kuki-promote kwasababu ni lugha iliyoachwa na Baba wa Taifa"
Picha hapo juu ni Mh. Rais Dk. JP Magufuli akiwa na Waziri wa mashauri ya kigeni Prof. Kabudi wakikabidhi vitabu vya kiswahili kwa Rais wa Jamuhuri ya Afrika ya Kusini Mh. Ramaphosa katika harakati ya kuhakikisha lugha hii tamu inakuwa na kuenea kwa haraka zaidi nje ya mipaka ya Tanzania na Afrika ya Mashariki.
Kitabu cha Kiingereza cha Mzee Mkapa: My Life, My Purpose: A Tanzanian President Remembers
Mheshimiwa, hayati Benjamin William Mkapa ndiye aliyekuwa rais wa tatu wa Tanzania, aliyechaguliwa chini ya mfumo wa kwanza wa vyama vingi hapa nchini. Kitabu chake kinafafanua kumbukumbu zake kutokea utotoni, wakati bado akiwa rais, na kuendelea kwake kujihusisha (hata baada ya kustaafu) kwenye masuala ya kimataifa yahusuyo maendeleo na upatanishi wa amani.
Kitabu hiki kinavutia sana kwa wasomaji wanaopenda kujua kuhusiana na, kadhia aliyoipitia mwafrika katika kipindi cha ukoloni hususan eneo zima la Afrika Mashariki na mapambano ya uhuru na harakati za ukombozi wa nchi kadhaa za kusini mwa Afrika.
Mheshimiwa Mkapa ameandika pia kuhusu utoto wake, kukomaa kwake kisiasa, mabadiliko ya kimfumo/kiutawala na kisiasa nchini Tanzania, na vile vile machafuko ya kisiasa katika nchi jirani.
Kitabu hiki kimejaa maoni yake juu ya uongozi na ushauri kwa viongozi wanaochipukia kama dada yangu mama D. Baada ya Mwalimu Julius Nyerere, ni vitabu vichache sana vimeandikwa na viongozi wakuu wa Tanzania juu ya mageuzi ya nchi; kwa kweli bila kuwa mnafiki vitabu vingi vinavyosomwa hapa nchini vimeandikwa na wageni kuliko watanzania, kwa hivyo kitabu cha Mh. Mkapa ni mfano bora wa kuigwa.
I Can, I Must, I Will written by Dr. Reginald Mengi
=====
OMBI LANGU: Itapendeza sana kama Rais Magufuli ataandika kitabu cha maisha yake kwa kutumia lugha ya wazalendo ya KISWAHILI.
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.