President Banda insists Lake Malawi is for Malawi not Tanzania

Anawaharibia sana wanawake wenzie wa kiafrika kuja kuwa Rais.........sijui kwa nini hajaenda Liberia kujifunza namna njema ya kuwa Rais mwanamke wa kiafrika
 
Swala siyo kuachia ziwa bali ni kuushughulikia mgogoro kidiplomasia au kisheria. Sheria za kimaitaifa si zipo na Mahakama ya ICJ si ipo tunaogopa nini? au tumeanza kufuatwa na wauza silaha na tumeahidiwa 10%. Na suala siyo kuachia ziwa bali ni kujua kila mmoja ana haki gani?
 
Katika comments za hawa jamaa nimeona matusi ambayo jamaa mmoja kachangia kuwa Tanzania ni taifa la wajinga kwa vile ni nchi pekee yenye wingi wa madini lakini inaongoza kwa umasikini.
Kwa kweli nimeumia sana kwa ukweli huo.Hivi tutaendelea kutukanwa na kebehi kibao kutoka kwa mataifa hata dhaifu kama malawi mpaka lini?
Kwa nini hatuchukui hatua kwa wanaotusababishia tudharaulike duniani kwa sababu ya wao kubebana?
Kwa kweli kama mtu bado anaweza kusimama wima na kutetea utawala huu na wakati huo yeye si sehemu ya utawala basi huyo anamapungufu akilini. Hatuwezi kuendelea kutukanwa katika ukweli tunaoweza kuubadilisha.


Ndo Nyerere legacy hiyo, very unfortunately!!
 
Hii ishu mimi napata picha tofauti kabisa kwa mwendo wa dunia jinsi unavokwenda.Huyu mama kaingia na vishindo na nadhani tayari amepambwa tokea hajakaa urais.Na watu wanaompamba itakuwa hukohuko kwa wazungu.Kuna dalili nyingi zinaonyesha kama anauhusiano wa karibu sana na hawa jamaa na wanampa mpaka nguvu za kijeshi sasa hivi.Hamuoni kama kuna kadili hapa?Sasa hivi ukiangalia kwa makini kila sehemu kuna mgogoro au vita.Kwanini isizuke miaka yoote ikazushwa sasa hivi.Jamani wazungu wamechacha sana wananchi wao hawana kazi makampuni mengi yanafungwa ama kuhamia China.Economy yote sasa hivi ameichukua Mchina mpaka Marekani hawezi hata kumlipa Mchina deni la trilioni za dola.Hawa jamaa hata kama wanaurafiki hapa na wanachota madini lakini kubadilika ni rahisi sana.Hawanaga urafiki wa kudumu hata uwape kisiwa kizima lakini hawaridhiki.Sasa nadhani kunakila sababu ya watanzania kuungana kwa hili suala ila tumuombe mungu yaishe bila vita lakini sio rahisi kama mzungu yupo katikati vita lazima itakuwepo.Kwani ni moja ya kuwauzia silaha na kuanza kuuwana waafrika kwa waafrika.Biashara yao kubwa hivi sasa ni silaha ndio iliyobaki kampuni nyengine nyingi zinakufa mpaka za magari.
 
ICJ ndio mwamuzi wa suala hili. Tulipeleke mahakamani haraka iwezekanavyo.Hatutaki vita sisi wote ni black race. Tusiuwane sisi ni ndugu moja.Pan-africanism itumiwe katika maeneo kama haya na si vita.
No need for war or killing these days, we can sort out our issues diplomatically or legally, if this fails we would need some serious hackers to teach them a lesson or two. if we could hack and paralyses their internet for a day or two, or do something like that in a minor scale, i believe they will come to their senses.
 
Hii ishu mimi napata picha tofauti kabisa kwa mwendo wa dunia jinsi unavokwenda.Huyu mama kaingia na vishindo na nadhani tayari amepambwa tokea hajakaa urais.Na watu wanaompamba itakuwa hukohuko kwa wazungu.Kuna dalili nyingi zinaonyesha kama anauhusiano wa karibu sana na hawa jamaa na wanampa mpaka nguvu za kijeshi sasa hivi.Hamuoni kama kuna kadili hapa?Sasa hivi ukiangalia kwa makini kila sehemu kuna mgogoro au vita.Kwanini isizuke miaka yoote ikazushwa sasa hivi.Jamani wazungu wamechacha sana wananchi wao hawana kazi makampuni mengi yanafungwa ama kuhamia China.Economy yote sasa hivi ameichukua Mchina mpaka Marekani hawezi hata kumlipa Mchina deni la trilioni za dola.Hawa jamaa hata kama wanaurafiki hapa na wanachota madini lakini kubadilika ni rahisi sana.Hawanaga urafiki wa kudumu hata uwape kisiwa kizima lakini hawaridhiki.Sasa nadhani kunakila sababu ya watanzania kuungana kwa hili suala ila tumuombe mungu yaishe bila vita lakini sio rahisi kama mzungu yupo katikati vita lazima itakuwepo.Kwani ni moja ya kuwauzia silaha na kuanza kuuwana waafrika kwa waafrika.Biashara yao kubwa hivi sasa ni silaha ndio iliyobaki kampuni nyengine nyingi zinakufa mpaka za magari.

Kaka,inaonekana bado haujajua vijana kule kusini wanafanya nini kwa sasa. Tuache ushabiki wa kisiasa,tufanye kazi kwa bidii na tuwe wamoja ki fikra na kimatendo,kwani likimegwa eneo lolote halimegwi eneo la CCM,CHADEMA,CUF au NCCR,ni eneo la Tanzania!. Hata hizo nchi za magharibi mnazoziogopa huwa zinaangalia kwanza ni wapi pa kutingisha. Kwa nini siku zote wanaingia na kutoka Goma lakini hawaji Mwanza au Shinyanga ilhali nako kuna madini!. Tuwape moyo vijana wetu wa vyombo vya ulinzi na rest assured,everything will gonna be alright for Tanzania!
 
Kaka,inaonekana bado haujajua vijana kule kusini wanafanya nini kwa sasa. Tuache ushabiki wa kisiasa,tufanye kazi kwa bidii na tuwe wamoja ki fikra na kimatendo,kwani likimegwa eneo lolote halimegwi eneo la CCM,CHADEMA,CUF au NCCR,ni eneo la Tanzania!. Hata hizo nchi za magharibi mnazoziogopa huwa zinaangalia kwanza ni wapi pa kutingisha. Kwa nini siku zote wanaingia na kutoka Goma lakini hawaji Mwanza au Shinyanga ilhali nako kuna madini!. Tuwape moyo vijana wetu wa vyombo vya ulinzi na rest assured,everything will gonna be alright for Tanzania!

Swat....Sijafahamu haya majibu kwako yalikuwa yanalenga nini kutoka ktk comment yangu.Kwasababu mimi nauzungumzia utaifa zaidi kwakuwa sina uhakika na chama chochote hapa TZ naona mizugazuga tu.Nimesema tuwe wamoja ktk hili suala na mungu atuepushe na vita hii ambayo itatuletea umasikini.Nafahamu kama vijana wanajiweka tayari kwa chochote huko mpakani.Tena ninae mtu ambae na yeye yumo kundini mpakani ambapo wamemaliza mazoezi wiki iliyopita.Vita sio lelemama tuwaombee vijana wetu waliopo huko kwani tukimpoteza mmoja tu inaumiza sana.Na mungu atakuwa nasi maana chokochoko nyingi duniani haziishi.
 
Ni rahisi kuiba mali asili za DRC-Kinshasa kuliko URT-Dar es Salaam.Kwa kuona watanzania wamezinduka na sasa wanataka kulinda rasilimali zao kwa ajili ya maendeleo ya nchi yao, lazima wezi hawa waje na mbinu ya kuhakikisha tupigana na Malawi.Maana kwenye vita uporaji ni rahisi.

Bahati mbaya sana wezi hawa wamemkamata vizuri Joyce Banda sina hakika kwa upande wa Tanzania wamemkamata nani hasa kuhakikisha vita inapiganwa ili rasilimali za Tanzania ziporwe kwa urahisi.

Ila bado nina imani kuwa adui atapata kibano anachostahili na watanzania wazelendo watahakikisha aibiwi mtu. Hapa kama wengine walivyosema tuwe wamoja kulinda rasilimali za nchi yetu kwa manufaa ya maendeleo ya watanzania.
 
Kila lakheri ndugu yangu kama wewe una advocate vita. Vita ya Uganda hadi leo makovu yetu hayajapona wewe unafanya ushabiki wa vita au unafikili vita ni mchezo. Halafu lazima ujue Dunia hii ina super nations, Nchi yetu si kubwa kiasi hicho.Tukianza vita kuna baadhi ya viongozi wataanza kutafuta namna ya kuiba.

Haki inatafutwa kwa gharama yeyote ile ikiwa ni pamoja na kupoteza maisha. Kama ule ujasiri wa kumngoa nduli bado tunao na huyu Joyce tusimcheleweshe waliomtangulia walikuwa wastaarabu yeye anataka kumega sehemu yetu? Lazima ashughulikiwe moja kwa moja kama nduli ili iwe fundisho. Kuwa kiongozi wa nchi si kuanza kusogeza mpaka. Tunajua kuna nguvu nyuma yake lakini ni bora kufa ukitetea haki yako kuliko kuporwa ukiwa unaangalia! Na wakifanikiwa kwa hili hawataishia hapo kwani ule ukanda wa madini unaungia nchini na kuna Wachina wanachimba kule usiku na mchana sijui kama wana vibali!
 
Wewe ni mwoga hutufai wa TZ tusikubali haki yetu ipokonywe kwa namna yeyote ile. Ni heri kuwa maskini ukitetea haki.
Wale ambao hajapitia JKT wakae chonjo kwenda mstari wa mbele ni lazima. Mbona baada ya vita vya nduli bado tunaishi? Kupitia Malawi ni wakubwa wanatafuta gear ya kuingia huko kusini kwani ile uranium wanaitaka kwa udi na uvumba!
 
Naliamini sana JWTZ. Nadhani bado hii ni taasisi ambayo imeendelea kuwa imara na makini hadi leo. Ni jeshi imara na lenye uwezo mkubwa wa kulinda vyema mipaka yetu. Hatuna haja ya kuogopa lolote. Huyu mama anatafuta balaa tu, hata kama ana mabwana zake ulaya; akituchezea atakula kichapo cha haja.
 
Malawi haijipendi, Tanzania ni Superpower kwa Africa, wa kupigana sisi ni South Africa, Nigeria, Egypt, sio Malawi
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom