Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Klabu ya Simba SC ambao ni Mabingwa wa Tanzania, katika mwendelezo wao wa kujiandaa na msimu mpya wa TPL, 2019/2020 na michuano ya Kimataifa, pamoja na kuwapa burudani ya kweli kwa Wanasimba wote, na katika kuelekea tamasha la Simba Week, leo Julai 30 2019, walisafiri kutoka mjini Rustenburg kuelekea Johannesburg kwa ajili ya kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Orlando Pirates ya Afrika Kusini.
Katika mchezo huo ambao ulimalizika kwa sare ya goli 1-1 ambapo Simba SC, ndio walikuwa wa kwanza kuandika bao kipindi cha kwanza kupitia kwa Clatous Chota Chama 'Triple C' kunako dakika ya 33' Kabla Orlando Pirates hawajasawazisha dakika ya 40' kabla ya mapumziko kupitia kwa Mulenga.
Katika mchezo huo ambao ulimalizika kwa sare ya goli 1-1 ambapo Simba SC, ndio walikuwa wa kwanza kuandika bao kipindi cha kwanza kupitia kwa Clatous Chota Chama 'Triple C' kunako dakika ya 33' Kabla Orlando Pirates hawajasawazisha dakika ya 40' kabla ya mapumziko kupitia kwa Mulenga.