Tatizo la ufisadi ndani ya PPF limechukua sura mpya na mbaya.
Miezi ya January hadi March, kulikuwa na mjadala mrefu sana hapa jamvini juu ya tabia mbaya za uongozi wa PPF wa kutumia madaraka vibaya.
Tuhuma zilizo anikwa hapa ni pamoja na;
1. Wakurugenzi kujilipa zaidi shilingi milioni 220 kila mmoja za Group Endowment (GES) ambayo sio stahili yao mwaka 2008 na kurudia kujilipa tena mwaka huu mwezi wa tatu kiasi hicho hicho tena. Kwa utaratibu wa PPF kama mwajili, wafanyakazi wa mikataba hulipwa GRATUITY TU na imekuwa miaka yote na wafanyakazi wa kudumu wanapostaafu au kufa hulipwa group endowment. Cha kusikitisha na kwa kutumia madaraka vibaya, wakaamua na hiyo GES wajilipe walipo maliza mkataba. Mhasibu Mkuu wa PPF akakataa kuwa sio sahihi, wafanyakazi wakachachamaa kuzuia lakini wapi, wakachukua mwaka 2008 na wamelipwa tena 2011 licha ya kamati ya fedha ya Bunge kuzuia.
2. Mwaka 2010, Mkurugenzi Mkuu wa sasa baada ya kumaliza miaka mitatu akalipwa GES isivyo halali Milioni 520, hizi ni nje ya 25% ya mishahara yake kwa kipindi cha mkataba kama gratuity, na ni nje ya 15% anayochangiwa kwenye pension na PPF amabyo nayo ni kinyume na waraka wa Wizara ya utumishi unaokataza watumishi wa umma wanaolipwa gratuity kuchangiwa tena na mwajili michango ya pension
3. Mkurugenzi wa Fedha na Mkurugenzi wa ukaguzi wa ndani kujichukulia viwanja vya PPF Bahari Beach vilivyonunuliwa mwaka 1996 kwa milioni 56 lakini wao wakavichukua kwa milioni 16 tu mwaka 2004 kwa kisingizio kuwa vinalitia hasara shirika.
4. Uzinzi ndani ya mfuko uliokithiri. Mkurugenzi Mkuu akiongoza kwa ngono na wafanyakazi ( vibinti vidogo vilivyoajiliwa kama vibarua), Mkurugenzi wa utawala na Mkaguzi wa ndani wakimfuatia.
5. Uizi kupitia miradi ya uwekezaji, hasa ule wa Bunge na wa UDOM ( vyote vimeanza kuvuja na nyufa mmeziona)
6. Unyanyasaji wa wafanyakazi wenye msimamo tofauti nao hasa wakipinga udokozi na uzinzi.
YALIYOTOKEA BAADA YA MJADALA/
1. Kamati ya ZITTO ikaagiza CAG akague utata wa malipo ya GES toka 2008. Magazeti yakaandika ufisadi huo na Mh. Mwanakijiji akamaliza kwa ripoti yake aliyoiweka humu JF
2. Uongozi wa PPF ukaanza vitisho kwa wafanyakazi hasa wale wanaodhaniwa kuwa ndio waliotoa siri hiyo nje. Wakawanyang'anya computer zao, wakazuia mtandao wa internet ndani ya PPF
3. Baadhi wakahojiwa na polisi
KUSIMAMISHWA KAZI.
Ijumaa iliyopita, uongozi wa PPF umewasimamisha kazi wale wote ambao computer zao zilinyang'anywa kwa tuhuma za;
a. Kuhisiwa kushiriki kwenye mijadara ya JAMII FORUMS
b. Kuhisiwa kutoa taarifa kwenye magazeti
c.Kupanga mapinduzi ya kuupindua uongozi wa PPF (?????????)
d. Kuhujumu mfuko eti wanazuia wanachama wasijiunge na PPF
Hivi niandikapo, LANDCRUISER VX, ya PPF imekwenda Mbeya na kumbeba staff mmoja ili kumpelekea barua aliyekuwa Mhasibu Mkuu aliyegoma kuwalipa GES.
WANA JF, WATANZANIA NA WAHESHIMIWA WABUNGE
1. Kamati ya Bunge imeagiza ukaguzi ufanyike, leo mtu mwenye taarifa muhimu za huu ufisadi anasimamishwa kazi ili wakaguzi wakija wao waliodokoa ndio watoe majibu.
Zitto na Kamati yake wanasemaje kuhusu hili?
CAG anakubali upuuzi huu?
2. Hivi katika hali ya uchumi wa nchi hii na mafao kidogo yanayotolewa na PPF, ni sahihi kupeleka barua moja tu kwa VX landcruser na kwalipa allowance dereva na mbeba barua? HII NAYO NI KASHFA. DG ajieleze VALUE FOR MONEY IKO WAPI? Mwezi March walifanya hivi hivi kwenda kumnyang'anya computer.
Haya tunawasaidiaje hata kama sio wana JF,
Mwanakijiji na Zitto Kabwe hebu liangalieni
Miezi ya January hadi March, kulikuwa na mjadala mrefu sana hapa jamvini juu ya tabia mbaya za uongozi wa PPF wa kutumia madaraka vibaya.
Tuhuma zilizo anikwa hapa ni pamoja na;
1. Wakurugenzi kujilipa zaidi shilingi milioni 220 kila mmoja za Group Endowment (GES) ambayo sio stahili yao mwaka 2008 na kurudia kujilipa tena mwaka huu mwezi wa tatu kiasi hicho hicho tena. Kwa utaratibu wa PPF kama mwajili, wafanyakazi wa mikataba hulipwa GRATUITY TU na imekuwa miaka yote na wafanyakazi wa kudumu wanapostaafu au kufa hulipwa group endowment. Cha kusikitisha na kwa kutumia madaraka vibaya, wakaamua na hiyo GES wajilipe walipo maliza mkataba. Mhasibu Mkuu wa PPF akakataa kuwa sio sahihi, wafanyakazi wakachachamaa kuzuia lakini wapi, wakachukua mwaka 2008 na wamelipwa tena 2011 licha ya kamati ya fedha ya Bunge kuzuia.
2. Mwaka 2010, Mkurugenzi Mkuu wa sasa baada ya kumaliza miaka mitatu akalipwa GES isivyo halali Milioni 520, hizi ni nje ya 25% ya mishahara yake kwa kipindi cha mkataba kama gratuity, na ni nje ya 15% anayochangiwa kwenye pension na PPF amabyo nayo ni kinyume na waraka wa Wizara ya utumishi unaokataza watumishi wa umma wanaolipwa gratuity kuchangiwa tena na mwajili michango ya pension
3. Mkurugenzi wa Fedha na Mkurugenzi wa ukaguzi wa ndani kujichukulia viwanja vya PPF Bahari Beach vilivyonunuliwa mwaka 1996 kwa milioni 56 lakini wao wakavichukua kwa milioni 16 tu mwaka 2004 kwa kisingizio kuwa vinalitia hasara shirika.
4. Uzinzi ndani ya mfuko uliokithiri. Mkurugenzi Mkuu akiongoza kwa ngono na wafanyakazi ( vibinti vidogo vilivyoajiliwa kama vibarua), Mkurugenzi wa utawala na Mkaguzi wa ndani wakimfuatia.
5. Uizi kupitia miradi ya uwekezaji, hasa ule wa Bunge na wa UDOM ( vyote vimeanza kuvuja na nyufa mmeziona)
6. Unyanyasaji wa wafanyakazi wenye msimamo tofauti nao hasa wakipinga udokozi na uzinzi.
YALIYOTOKEA BAADA YA MJADALA/
1. Kamati ya ZITTO ikaagiza CAG akague utata wa malipo ya GES toka 2008. Magazeti yakaandika ufisadi huo na Mh. Mwanakijiji akamaliza kwa ripoti yake aliyoiweka humu JF
2. Uongozi wa PPF ukaanza vitisho kwa wafanyakazi hasa wale wanaodhaniwa kuwa ndio waliotoa siri hiyo nje. Wakawanyang'anya computer zao, wakazuia mtandao wa internet ndani ya PPF
3. Baadhi wakahojiwa na polisi
KUSIMAMISHWA KAZI.
Ijumaa iliyopita, uongozi wa PPF umewasimamisha kazi wale wote ambao computer zao zilinyang'anywa kwa tuhuma za;
a. Kuhisiwa kushiriki kwenye mijadara ya JAMII FORUMS
b. Kuhisiwa kutoa taarifa kwenye magazeti
c.Kupanga mapinduzi ya kuupindua uongozi wa PPF (?????????)
d. Kuhujumu mfuko eti wanazuia wanachama wasijiunge na PPF
Hivi niandikapo, LANDCRUISER VX, ya PPF imekwenda Mbeya na kumbeba staff mmoja ili kumpelekea barua aliyekuwa Mhasibu Mkuu aliyegoma kuwalipa GES.
WANA JF, WATANZANIA NA WAHESHIMIWA WABUNGE
1. Kamati ya Bunge imeagiza ukaguzi ufanyike, leo mtu mwenye taarifa muhimu za huu ufisadi anasimamishwa kazi ili wakaguzi wakija wao waliodokoa ndio watoe majibu.
Zitto na Kamati yake wanasemaje kuhusu hili?
CAG anakubali upuuzi huu?
2. Hivi katika hali ya uchumi wa nchi hii na mafao kidogo yanayotolewa na PPF, ni sahihi kupeleka barua moja tu kwa VX landcruser na kwalipa allowance dereva na mbeba barua? HII NAYO NI KASHFA. DG ajieleze VALUE FOR MONEY IKO WAPI? Mwezi March walifanya hivi hivi kwenda kumnyang'anya computer.
Haya tunawasaidiaje hata kama sio wana JF,
Mwanakijiji na Zitto Kabwe hebu liangalieni