Tonge
JF-Expert Member
- May 7, 2010
- 695
- 12
Mtoto wa mkulima kwa hili la kutumia matrekta ya Tafe na Kubota linaniingia akilini lakini hili la Power tiller aghaaaaaaa. Ki ukweli power tiller ni mzigo kwa wakulima kwani hili linafaa sana kwenye maeneo ambayo ni soaked land na sio yenye dry/hard land kama dodoma nk na pia si mazuri kwenye milima kama lushoto.
Cha kushangaza sasa.
Wakurugenzi wa halmashauri wameyanunua bila kuomba ushauri wa maofisa kilimo wao wakisema ni agizo la waziri mkuu na bei ya power tiller moja ni kama tsh 5 mil ila limenunuliwa kwa 12mil na hizi halimashauri.
Matokeo yake sasa.
Wananchi wameshindwa kuyatumia baada ya kuona wenzao wanaoyatumia hayawasidii zaidi ya kuwaletea magonjwa kama kifua kikuu kutokana na vumbi na pia kuwanyong'onyeza kiafya kwani ili lilime linahitaji mkulima atumie nguvu nyingi, kama ukifika kwenye bohari au maeneo mengi ya ofisi za ujenzi Tanzania utayakuta haya matreka madogo yakiwa yamepark, ukiuliza utaambiwa kuwa wakulima hawaji kuyakopesha.
Maswali.
Je ilikuwa agizo toka kwa Waziri mkuu kuwa kila wilaya ni lazima inunue power tiller?
Je wataalamu wa kilimo na udongo walihusishwa kikamilifu kutoa ushauri wao kama power tiller zinunuliwe au la au wakurugenzi walinunua kisiasa zaidi?
Je azimio la kilimo kwanza litaleta mapinduzi ya kijani au litapindisha migongo wakulima?.
Ushauri.
Wataalamu wa kilimo wasikilizwe, serikali itenge hela ya kutosha uli kuweza kuagiza mbolea na matrekta kama kubota ambayo yana uwezo wa kulima hekta nyingi kwa siku bila kuadhili afya ya mkulima.
Swala la siasa lisiingie kwenye vitu muhimu kama kilimo nk.
Wakurugenzi waache nidhamu ya woga wafanye kazi kutokana na ushauri mzuri wa maofisa wao walio chini kama DALDO.
Waziri mkuu awachukulie hatua za kisheria wale wote ambao wamenunua mapoer tiller kwa bei za juu ikiwa hali bei zake si kubwa kivile kwani hapo kuna chembe chembe za rushwa na ufisadi.
Mwisho.
Haiwezekani kilimo kuwa kwanza kinadhalia tu, sio kivitendo wakati katika bajeti ya nchi kimepewa kipaumbele cha nne, ni vema kuwa makini kwa kila jambo sio kushika hili na lile baadae moja lazima lituponyoke tu.
Mkereketwa
Cha kushangaza sasa.
Wakurugenzi wa halmashauri wameyanunua bila kuomba ushauri wa maofisa kilimo wao wakisema ni agizo la waziri mkuu na bei ya power tiller moja ni kama tsh 5 mil ila limenunuliwa kwa 12mil na hizi halimashauri.
Matokeo yake sasa.
Wananchi wameshindwa kuyatumia baada ya kuona wenzao wanaoyatumia hayawasidii zaidi ya kuwaletea magonjwa kama kifua kikuu kutokana na vumbi na pia kuwanyong'onyeza kiafya kwani ili lilime linahitaji mkulima atumie nguvu nyingi, kama ukifika kwenye bohari au maeneo mengi ya ofisi za ujenzi Tanzania utayakuta haya matreka madogo yakiwa yamepark, ukiuliza utaambiwa kuwa wakulima hawaji kuyakopesha.
Maswali.
Je ilikuwa agizo toka kwa Waziri mkuu kuwa kila wilaya ni lazima inunue power tiller?
Je wataalamu wa kilimo na udongo walihusishwa kikamilifu kutoa ushauri wao kama power tiller zinunuliwe au la au wakurugenzi walinunua kisiasa zaidi?
Je azimio la kilimo kwanza litaleta mapinduzi ya kijani au litapindisha migongo wakulima?.
Ushauri.
Wataalamu wa kilimo wasikilizwe, serikali itenge hela ya kutosha uli kuweza kuagiza mbolea na matrekta kama kubota ambayo yana uwezo wa kulima hekta nyingi kwa siku bila kuadhili afya ya mkulima.
Swala la siasa lisiingie kwenye vitu muhimu kama kilimo nk.
Wakurugenzi waache nidhamu ya woga wafanye kazi kutokana na ushauri mzuri wa maofisa wao walio chini kama DALDO.
Waziri mkuu awachukulie hatua za kisheria wale wote ambao wamenunua mapoer tiller kwa bei za juu ikiwa hali bei zake si kubwa kivile kwani hapo kuna chembe chembe za rushwa na ufisadi.
Mwisho.
Haiwezekani kilimo kuwa kwanza kinadhalia tu, sio kivitendo wakati katika bajeti ya nchi kimepewa kipaumbele cha nne, ni vema kuwa makini kwa kila jambo sio kushika hili na lile baadae moja lazima lituponyoke tu.
Mkereketwa