Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,391
- 39,484
Habari ambazo zinaingia mida hii kutoka Dar zinasema kuwa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Posta baada ya kukutana leo imeamua kuwatimua wakurugenzi wake watatu kwa kile kinachoaminika ni kuvujisha siri za shirika hilo hususan zihusiano na vitendo vya kifisadi.
Habari za ufisadi kwenye shirika hilo zilitemwa kwenye mtandao huu wa JF siku chache zilizopita. Hata hivyo kwa wale "wanaojua" habari hizi hazikutoka kwa afisa yeyote wa juu ndani ya shirika hilo isipokuwa baadhi ya Watanzania ambao wamechoshwa na hujuma na vitendo vya kifisadi.
Kama ufukuzwaji huo utathibitishwa hii itakuwa ni mara nyingine ambapo JF imetumiwa kisingizio cha kufukuza watu ili kutishia watumishi wa umma wasifichue uovu kwenye taasisi za umma na ambazo ni nyeti. Miezi michache iliyopita shirika la ndege la ATC nalo lilitimua watumishi wake watano kwa kisingio cha kuvujisha siri za ununuzi wa dege la Airbus na vitendo vya kifisadi ndani ya shirika hilo.
Wakati huo huo mojawapo ya Vyuo Vikuu vya Tanzania nacho kimemfuta kazi mmoja wa wahadhiri wake waandamizi kwa kile amacho viongozi wa chuo hicho wanadai kuwa ni "pressure" toka juu hasa baaada ya mhadhiri huyo mwishoni mwaka jana kujitokeza hadharani na kumnyoshea kidole cha ufisadi mmojawapo wa mawaziri na kumtaka ajiuzulu.
Kama tabia hii ya "kufukuza fukuza" itaendelea bila kukomeshwa mara moja, Taifa la Tanzania litakuwa limeanzisha utawala wa vitisho na utamaduni wa kuziba habari za vitendo vya kifisadi kwa kutishia retaliation kwa mtu yeyote yule.
Hadi hivi sasa haijajulikana ni kwa kiasi gani sheria ya "Whistleblowing" imefikia na ni lini sheria hiyo itaanza kuwalinda Watanzania ambao wanaibua vitendo vya kifisadi, kuhujumu uchumi, rushwa, na ukiukwaji wa maadili katika sehemu zao za kazi.
Habari za ufisadi kwenye shirika hilo zilitemwa kwenye mtandao huu wa JF siku chache zilizopita. Hata hivyo kwa wale "wanaojua" habari hizi hazikutoka kwa afisa yeyote wa juu ndani ya shirika hilo isipokuwa baadhi ya Watanzania ambao wamechoshwa na hujuma na vitendo vya kifisadi.
Kama ufukuzwaji huo utathibitishwa hii itakuwa ni mara nyingine ambapo JF imetumiwa kisingizio cha kufukuza watu ili kutishia watumishi wa umma wasifichue uovu kwenye taasisi za umma na ambazo ni nyeti. Miezi michache iliyopita shirika la ndege la ATC nalo lilitimua watumishi wake watano kwa kisingio cha kuvujisha siri za ununuzi wa dege la Airbus na vitendo vya kifisadi ndani ya shirika hilo.
Wakati huo huo mojawapo ya Vyuo Vikuu vya Tanzania nacho kimemfuta kazi mmoja wa wahadhiri wake waandamizi kwa kile amacho viongozi wa chuo hicho wanadai kuwa ni "pressure" toka juu hasa baaada ya mhadhiri huyo mwishoni mwaka jana kujitokeza hadharani na kumnyoshea kidole cha ufisadi mmojawapo wa mawaziri na kumtaka ajiuzulu.
Kama tabia hii ya "kufukuza fukuza" itaendelea bila kukomeshwa mara moja, Taifa la Tanzania litakuwa limeanzisha utawala wa vitisho na utamaduni wa kuziba habari za vitendo vya kifisadi kwa kutishia retaliation kwa mtu yeyote yule.
Hadi hivi sasa haijajulikana ni kwa kiasi gani sheria ya "Whistleblowing" imefikia na ni lini sheria hiyo itaanza kuwalinda Watanzania ambao wanaibua vitendo vya kifisadi, kuhujumu uchumi, rushwa, na ukiukwaji wa maadili katika sehemu zao za kazi.