Bigirita
Platinum Member
- Feb 12, 2007
- 15,986
- 7,366
Siku ya Wanawake Duniani ni jumatatu 8/3/2010. Napenda kutoa wito kwa Jamii inapaswa kuondokana na na vitendo vya dhuluma na nyanyaso kwa wanawake na wasichana, vinavyodhoofisha afya zao na kuongeza umaskini, badala ya kuwawezesha na kuboresha maisha ya wanawake.
Idadi ya wanaume wanaokemea vitendo vya unyanyasi wa kijinsia inazidi kuongezeka kwa kubadili tabia, mila na desturi ambazo zimepitwa na wakati zinapaswa kukoma.
Serikali na vyombo vyake haina budi kusimama kidete kupinga dhuluma na nyanyaso dhidi ya wanawake, kwa kuweka sera nzuri za kiuchumi na kijamii kwa ajili ya maendeleo ya wanawake. Vyombo vya upashanaji habari havina budi kulinda na kuheshimu utu wa wanawake na kamwe wasiwageuze kuwa ni vichokoo vya matangazo yao ya biashara. Sheria ziwe wazi kwamba, nyanyaso la kijinsi kwa wanawake na wasichana ni kosa la jinai, wahusika wawajibishwe, ile sheria ya mahusiano ya kingono (Sexual Conduct Act of 1994) isiwe ni urembo -just another document.
Nakumbuka Hayati Baba Mtakatifu Yohane Paulo wa pili alisema hivi kuhusu utu wa mwanamke, "Mulieris Dignitatem" alisema kwamba, bado mfumo dume unaendelea kutawala na hivyo kuwafanya baadhi ya watu kushindwa kutambua kwamba watu wote, wameumbwa kwa sura na mfano wa Mungu.
NAWAPENDA NA KUWAHESHIMU WANAWAKE WOTE. na hii ndiyodeclaration yangu kuanzia leo.
Idadi ya wanaume wanaokemea vitendo vya unyanyasi wa kijinsia inazidi kuongezeka kwa kubadili tabia, mila na desturi ambazo zimepitwa na wakati zinapaswa kukoma.
Serikali na vyombo vyake haina budi kusimama kidete kupinga dhuluma na nyanyaso dhidi ya wanawake, kwa kuweka sera nzuri za kiuchumi na kijamii kwa ajili ya maendeleo ya wanawake. Vyombo vya upashanaji habari havina budi kulinda na kuheshimu utu wa wanawake na kamwe wasiwageuze kuwa ni vichokoo vya matangazo yao ya biashara. Sheria ziwe wazi kwamba, nyanyaso la kijinsi kwa wanawake na wasichana ni kosa la jinai, wahusika wawajibishwe, ile sheria ya mahusiano ya kingono (Sexual Conduct Act of 1994) isiwe ni urembo -just another document.
Nakumbuka Hayati Baba Mtakatifu Yohane Paulo wa pili alisema hivi kuhusu utu wa mwanamke, "Mulieris Dignitatem" alisema kwamba, bado mfumo dume unaendelea kutawala na hivyo kuwafanya baadhi ya watu kushindwa kutambua kwamba watu wote, wameumbwa kwa sura na mfano wa Mungu.
NAWAPENDA NA KUWAHESHIMU WANAWAKE WOTE. na hii ndiyodeclaration yangu kuanzia leo.