Elections 2010 Post-Mortem: Kwa Nini JK Na CCM Wamepata Ushindi Mdogo

Superman

JF-Expert Member
Mar 31, 2007
5,695
1,696
Wana JF;

Tofauti na Uchaguzi Mkuu Wa 2005 katika Uchaguzi wa Mwaka huu 2010 JK amepata ushindi wa asilimia 61%+ ukilinganisha na 80%+ aliyopata 2005. Pia CCM imepoteza majimbo mengi kwa upinzani.

Je ni sababu zipi zilizopelekea kupata ushindi mdogo ukilinganisha na 2005?
 
Nadhani hapa swali sahihi ni kwanini "wameshindwa kufanya vizuri kama walivyofanya 2005"? Kwani mwaka huu ni CCM walioshindwa siyo upinzani.
 
Usisahau kuwa juzi tu wadau wamelalamikia wizi wa kura.Kifupi huo si ushindi ni kwamba ameshindwa kuchakachua zaidi kutokana na uelewa wa WATANZANIA KWA SASA.Hajashinda yule ameiba kura.Ushinndi wa wizi hata yeye ukimwangalia usoni unamuona roho yake inamsuta,tumuache atawale ili tumdhibiti kwa kuibua uporaji watakaofanya
 
kusoma hujui, hata picha uoni? nani kakwambia ccm wameshinda?
 
Back
Top Bottom