Elections 2010 Post-Mortem: Kwa Nini Dr. Slaa Na CHADEMA Wameshindwa

Superman

JF-Expert Member
Mar 31, 2007
5,695
1,696
Wana JF;

Katika Uchaguzi Mkuu 2010 Dr. Slaa na CHADEMA wametoa changamoto na upinzani mkali tofauti sana na miaka ya nyuma. Uchaguzi mwaka huu ulikuwa na msisimko mkubwa sana huku kukiwa na propaganda nyingi sana ambazo hazijawahi kusikika.

Kuna baadhi waliamini kabisa kuwa Dr.Slaa na CHADEMA wangeshinda katika Uchaguzi Mkuu 2010.

Kwa maoni yangu baadhi ya sababu zilizoifanya CHADEMA na Dr. Slaa washindwe ni pamoja na:

1. Kutokuwa na Mtandao mkubwa wa chama na wanachama na hivyo kukosa kuwafikia wapiga kura wa uhakika.
2. Maandalizi duni ya ki-organaizesheni katika kampeni
3. Ukosefu wa rasilimali za kutosha katika kampeni hasa fedha

Je kwa maoni na utafiti wako ni sababu gani zingine zilizofanya Dr.Slaa na CHADEMA wasishinde Uchaguzi Mkuu 2010?
 
Wizi pia umechangia kwa kiasi kikubwa.
Hofu ya vita ambayo CCM iliwajaza wananchi hasa wa vijijini
Uelewa mdogo kwa wapiga kura. Na mtaji mkubwa wa wananchi wasiojua haki zao na kuwaona wapinzani kama ni maadui
 
Asante Nicky,

Mpaka sasa tuna sababu hizi:

1. Kutokuwa na Mtandao mkubwa wa chama na wanachama na hivyo kukosa kuwafikia wapiga kura wa uhakika.
2. Maandalizi duni ya ki-organaizesheni katika kampeni
3. Ukosefu wa rasilimali za kutosha katika kampeni hasa fedha
4. Tuhuma za wizi wa kua umechangia kushindwa kwao
5. Hofu ya vita ambayo CCM iliwajaza wananchi hasa wa vijijini na kuogopa kuwapigia kura
6. Uelewa mdogo kwa wapiga kura juu ya mageuzi.
7. Ukosefu wa Elimu ya Uraia kuwafikia wengi na hivyo kusababisha wananchi kutokujua haki zao na kuwaona wapinzani kama ni maadui

Je kuna sababu zingine?
 
Superman... unamaana gani "wameshindwa"? maana ukiniuliza mimi nitakuambia walioshindwa ni CCM kulinganisha na matokeo ya 2005. Kwa kila kipimo.. hakuna mahali ambapo CCM imeongeza viti au kura. Lakini naweza kukuonesha mahali ambapo Chadema imeongeza viti na kura (ndio kushinda kwenyewe). Ama ushindi ni kuwa Rais tu ndio tunaweza kuuhesabu kuwa ni ushindi?
 
Wizi pia umechangia kwa kiasi kikubwa.
Hofu ya vita ambayo CCM iliwajaza wananchi hasa wa vijijini
Uelewa mdogo kwa wapiga kura. Na mtaji mkubwa wa wananchi wasiojua haki zao na kuwaona wapinzani kama ni maadui

Nicky, ni kwa vipi sababu hizo zimechangia Dr. Slaa na CHADEMA kushindwa? Haiko wazi bado.
 
Wizi pia umechangia kwa kiasi kikubwa.
Hofu ya vita ambayo CCM iliwajaza wananchi hasa wa vijijini[/COLOR]
Uelewa mdogo kwa wapiga kura. Na mtaji mkubwa wa wananchi wasiojua haki zao na kuwaona wapinzani kama ni maadui

hii hofu sio vijijini tu hata mjini, rafiki yangu mmoja dar aliombwa na bibi mmoja amsaidie kutia tick sehemu ya mgombea anaemtaka, bibi alikuwa anamwonyesha kwenye picha ya kikwete, jamaa yangu akamuuliza kwa nini unamchagua huyu na sio huyu hapa ( akimwonyesha Slaa), yule bibi akasema "sina miguu ya kukimbilia baba vita ikitokea", so ni kweli wananchi wametishwa na wakatishika
 
Wana JF;

Katika Uchaguzi Mkuu 2010 Dr. Slaa na CHADEMA wametoa changamoto na upinzani mkali tofauti sana na miaka ya nyuma. Uchaguzi mwaka huu ulikuwa na msisimko mkubwa sana huku kukiwa na propaganda nyingi sana ambazo hazijawahi kusikika.

Kuna baadhi waliamini kabisa kuwa Dr.Slaa na CHADEMA wangeshinda katika Uchaguzi Mkuu 2010.

Kwa maoni yangu baadhi ya sababu zilizoifanya CHADEMA na Dr. Slaa washindwe ni pamoja na:

1. Kutokuwa na Mtandao mkubwa wa chama na wanachama na hivyo kukosa kuwafikia wapiga kura wa uhakika.
2. Maandalizi duni ya ki-organaizesheni katika kampeni
3. Ukosefu wa rasilimali za kutosha katika kampeni hasa fedha

Je kwa maoni na utafiti wako ni sababu gani zingine zilizofanya Dr.Slaa na CHADEMA wasishinde Uchaguzi Mkuu 2010?

NEC na Usalama wa Taifa ndio sababu pekee ya DK Slaa kushindwa.
 
Superman... unamaana gani "wameshindwa"? maana ukiniuliza mimi nitakuambia walioshindwa ni CCM kulinganisha na matokeo ya 2005. Kwa kila kipimo.. hakuna mahali ambapo CCM imeongeza viti au kura. Lakini naweza kukuonesha mahali ambapo Chadema imeongeza viti na kura (ndio kushinda kwenyewe). Ama ushindi ni kuwa Rais tu ndio tunaweza kuuhesabu kuwa ni ushindi?

MKJJ, tunaweza kuanzisha thread nyingine ya kwa nini CCM safari hii Rais amepata kura kidogo kuliko 2005 au kwa nini wamepoteza majimbo mengi safari hii ukilinganisha na 2010.

katika thread hii ni kuangalia kwa nini CHADEMA hawakushinda na kuwafanya waunde serikali. Japo wameshinda kwa kuongeza majimbo na kura za Urais kuliko 2005 lakini bado hawajaweza kuunda Serikali. Tunapenda tuweke wazi sababu zote.
 
ABABU ILIYO KUBWA KABISA YA CHADEMA kushindwa ni kwasababu ya hujuma na njama za CCM . Njama na hujuma hizo ni pamoja na:
  1. NEC KUCHAKACHUA MATOKEO KWA KUIPENDELEA CCM.
  2. KUWATIA HOFU WAPIGA KURA KWA KUTUMIA JESHI.
  3. CCM KUCHELEWESHA KUBANDIKA MAJINA YA WAPIGA KURA KWENYE VITUO.
  4. CCM KUTUMIA USALAMA WA TAIFA KUIBA KURA.
  5. CCM KUTUMIA VIHIYO WA IT KWENYE KUHESABU KURA.
 
Wana JF;

Katika Uchaguzi Mkuu 2010 Dr. Slaa na CHADEMA wametoa changamoto na upinzani mkali tofauti sana na miaka ya nyuma. Uchaguzi mwaka huu ulikuwa na msisimko mkubwa sana huku kukiwa na propaganda nyingi sana ambazo hazijawahi kusikika.

Kuna baadhi waliamini kabisa kuwa Dr.Slaa na CHADEMA wangeshinda katika Uchaguzi Mkuu 2010.

Kwa maoni yangu baadhi ya sababu zilizoifanya CHADEMA na Dr. Slaa washindwe ni pamoja na:

1. Kutokuwa na Mtandao mkubwa wa chama na wanachama na hivyo kukosa kuwafikia wapiga kura wa uhakika.
2. Maandalizi duni ya ki-organaizesheni katika kampeni
3. Ukosefu wa rasilimali za kutosha katika kampeni hasa fedha

Je kwa maoni na utafiti wako ni sababu gani zingine zilizofanya Dr.Slaa na CHADEMA wasishinde Uchaguzi Mkuu 2010?


Ya kwanza nakubaliana na wewe. KWamba CHADEMA campaign was under staffed. Haikuwa na watu wengi wa kuweza kufika kila eneo la Tanzania kwa kipindi kifupi. Na CCM walijua hilo kuwa wao hata wakiwa na mwezi mmoja wa kampeni tayari ni head start.

Yapili si kweli. Ukiangalia kwa udani unaweza kuona CHADEMA imepata mafanikio makubwa sana kuliko uchaguzi uliopita. Angalia idadi ya ongezeko la wabunge wake bungeni ikilinganishwa na 2005. Sababu moja ni ni kuwa kuliwa na smart organisation ya wasomi na watendaji.

Tatizo kubwa la Chadema ni kuwa it is too honest and too clean. CCM wenzao wametumia njia zote ili kupata ushindi. Kutoa ahadi ambazo hazitekelezeki, ukiangalia kwa makini utaona kuwa CCM imepata kura nyingi kwa wanyonge(hohehahe na wasio na elimu) mtu akinunuliwa tu T-shirt, akipewa kofia au kitenge anachagua CCM. Hiyo kwa upande fulani ni kama kurubuni watu hawa wale wanyonge. Lakini CHADEMA haikufanya hivyo.

Lakini mkuu angalia kwanza takwimu za waliojiandikisha na waliopiga kura, kwanini ziko tofauti sana? ni bahati mbaya au watu wakutaka kupiga kura????, jaribu pia kuangalia pia uchakachuaji. Angalia pia role ya CUF, kampeni chafu za kukitaja CHADEMA kama chama cha kikristo. Ukiangalia hayo unaweza kujua ni kwanini CHADEMA haikupata ushindi. Otherwise naweza kusema CHADEMA hawajafanya vibaya, lakini they could do much better.
 
MKJJ, tunaweza kuanzisha thread nyingine ya kwa nini CCM safari hii Rais amepata kura kidogo kuliko 2005 au kwa nini wamepoteza majimbo mengi safari hii ukilinganisha na 2010.

katika thread hii ni kuangalia kwa nini CHADEMA hawakushinda na kuwafanya waunde serikali.

Basi swali lako hapa haliko sahihi - kwani halina qualification. Umeuliza kwanini wameshindwa? Kushindwa maana yake ni kutofanikiwa, kutofikia malengo n.k Kwa mfano, kwenye Halmashauri lengo ni kupata madiwani wengi na kuunda serikali ya Manispaa hapo - mwaka 2005 Chadema nadhani ilikuwa na Halmashauri nne tu inazoongoza (Tarime, Karatu, na Kigoma Mjini, Kigoma Kaskazini kama sikosei) Mwaka huu wameshika miji karibu yote mikubwa - kwanini huku kuwe ni kushindwa?

Kwa upande wa Wabunge Chadema ina wabunge wengi zaidi ikiwaangusha baadhi ya wabunge maarufu na hivyo kuongeza idadi ya wabunge wake kutoka sita wa kuchaguliwa kufikia 24 - Kwa maneno mengine wamefanikiwa kuwashawishi wananchi wengi zaidi kukuwakubali - kwanini huko kuwa ni "kushindwa"?

Japo wameshinda kwa kuongeza majimbo na kura za Urais kuliko 2005 lakini bado hawajaweza kuunda Serikali. Tunapenda tuweke wazi sababu zote.

Mbunge ana majukumu ya Bunge na siyo kila mbunge lazima awe sehemu ya kuunda serikali. Huitaji kuunda serkali ili upime kufanikiwa kwa ubunge. Lakini mimi naamini swali sahihi lingekuwa "kwanini hawakufanya vizuri zaidi ya walivyofanya sasa"? Wouldn't you agree? Kwa sababu kusema wameshindwa ni kuashiria kuwa hawakuwa na mafanikio yoyote kitu ambacho naamini si kweli.
 
Hivi kikweli kweli CHADEMA wameshindwa au CCM wamechakachua matokeo na kuyafanya yawaonyeshe wao ndio washindi? Enthusiasm iliyokuwepo kwa Slaa hailingani kabisa na matokeo. Hayo ndiyo maoni yangu...
 
Asante Nicky,

Mpaka sasa tuna sababu hizi:

1. Kutokuwa na Mtandao mkubwa wa chama na wanachama na hivyo kukosa kuwafikia wapiga kura wa uhakika.
2. Maandalizi duni ya ki-organaizesheni katika kampeni
3. Ukosefu wa rasilimali za kutosha katika kampeni hasa fedha
4. Tuhuma za wizi wa kua umechangia kushindwa kwao
5. Hofu ya vita ambayo CCM iliwajaza wananchi hasa wa vijijini na kuogopa kuwapigia kura
6. Uelewa mdogo kwa wapiga kura juu ya mageuzi.
7. Ukosefu wa Elimu ya Uraia kuwafikia wengi na hivyo kusababisha wananchi kutokujua haki zao na kuwaona wapinzani kama ni maadui

Je kuna sababu zingine?
Chadema haikuwa na walinzi wa kura za Uraisi kama ilivyokuwa kwa wabunge.
Tumeshuhudia vijana wakilinda kura kwa ushujaa dhidi ya mbinu mbalimbali za kijizi katika majimbo karibu yote iliposhinda.
 
Hivi kikweli kweli CHADEMA wameshindwa au CCM wamechakachua matokeo na kuyafanya yawaonyeshe wao ndio washindi? Enthusiasm iliyokuwepo kwa Slaa hailingani kabisa na matokeo. Hayo ndiyo maoni yangu...

Dude you are damn right. I believe that there was a serious job in doctoring election results, no wonder why NEC was twitching it's hand in releasing results, there is a huge body of evidence pointing to that direction. Any person with working brains could easily see that, but unfortunately those who make decisions in this country have decided that the will of the people can not prevail. We just have to move on, but one door has just been opened.
 
Wana JF;

Katika Uchaguzi Mkuu 2010 Dr. Slaa na CHADEMA wametoa changamoto na upinzani mkali tofauti sana na miaka ya nyuma. Uchaguzi mwaka huu ulikuwa na msisimko mkubwa sana huku kukiwa na propaganda nyingi sana ambazo hazijawahi kusikika.

Kuna baadhi waliamini kabisa kuwa Dr.Slaa na CHADEMA wangeshinda katika Uchaguzi Mkuu 2010.

Kwa maoni yangu baadhi ya sababu zilizoifanya CHADEMA na Dr. Slaa washindwe ni pamoja na:

1. Kutokuwa na Mtandao mkubwa wa chama na wanachama na hivyo kukosa kuwafikia wapiga kura wa uhakika.
2. Maandalizi duni ya ki-organaizesheni katika kampeni
3. Ukosefu wa rasilimali za kutosha katika kampeni hasa fedha

Je kwa maoni na utafiti wako ni sababu gani zingine zilizofanya Dr.Slaa na CHADEMA wasishinde Uchaguzi Mkuu 2010?

katika sababu zako hizo tatu, mimi sizikubali hata moja,
mimi kwa mtazamo wangu, katiaka miaka yote ya vyama vya Upinzani ni mwaka huu pekee ndio chama cha upinzani kilionesha kufanya kampeni iliyokuwa well organized, na ilikuwa so focused na ilikuwa ina malengo maalumu,
Wapiga kura wengi wa Tanzania wako Mwanza, Dar, Mbeya,Shinyanga,Arusha, KLM na wanafuatiwa na Kagera na KIgoma na Chadema walilijua hilo na wakaweka nguvu zao huko muda mrefu ref-operation Sangara (Japo ilikuwa nchi nzima lakini kwewnye mikoa hiyo ndio ilikuwa zaidi),
sasa ukiangalia wapiga kura wa Lindi, mtwara hata wakiwa mara tatu hawawezi kuwafikia watu wa Shinyanga pekeyake, sasa uwezo ka kichama lazima uwe na target na malengo,
ni ukweli usiopingika Japo Chadema hakupata kura nying maeneo ya kusini, lakini walikuwa na kura za kutosha kuchukua madaraka, kwa sababu walikuwa na kura nyingi kutoka kwa maeneo yenye majority
hebu chukua mfano wa Mwanza-Nyamagana, Chadema kachukua viti 12 vya udiwani, Masha kapitwa kwa kura nyingi na Wenje, alafu JK kampita Slaa kwa kura, hivi inakuingia akilini hiyo?
Chadema walijipanga kwa resources zao ndogo walizo nazo na walishinda huu uchaguzi
 
ELIMU YAKUTOSHA KWA WAPIGA KURA. Mfano: Nilikuwa na vijana wa kitaa waliotoka kupiga kura wakielezea walicho fanya kwenye chumba cha kura kama kuchora vibaya picha za wagombea wengine wasio wapenda kwakufikiri ujumbe wao kwa wasio wapenda utafika na palepale chaguo lao likitimia kumbe sivyo wanaishia kuharibu kura.
Hivyo tuna hitaji elimu ya jinsi yakupiga kura itolewe kunusuru kuharibu kura
 
mikakati ielekezwe vijijini zaidi watu wajue umuhimu wa kulinda kura zao vituoni, na kupata mawakala wa ukweli wasio mapandikizi; hapo kitaeleweka

Sababu kuu ni Hujuma=Wizi wa kura; NEC kuwa chombo pandikizi/chakachuzi cha CCM;

Naamini nikakati kwa 90% ilifanikiwa.
 
hii hofu sio vijijini tu hata mjini, rafiki yangu mmoja dar aliombwa na bibi mmoja amsaidie kutia tick sehemu ya mgombea anaemtaka, bibi alikuwa anamwonyesha kwenye picha ya kikwete, jamaa yangu akamuuliza kwa nini unamchagua huyu na sio huyu hapa ( akimwonyesha Slaa), yule bibi akasema "sina miguu ya kukimbilia baba vita ikitokea", so ni kweli wananchi wametishwa na wakatishika
kiukweli ccm walikuwa wanatumia mno vitisho kwa wanachi hasa wa vijijini kuhusu upinzani, ndo maana watu wa vijijini waliowengi ukiongelea upinzani wanajua unaongelea vita, mi nafikiri kuna haja ya elimi kubwa ya uraia kwa watu hawa ambao akili zao zimedumaa kwa umaskini wao na ujinga ulioletwa na ccm
 
Msichanganye ushindi wa kura kidemokrasia na usimikwaji wa madaraka kibabe. Mpaka sasa hakuna ushahidi w kutosha kuonyesha kuwa Slaa kashindwa kwa kura hasa kutokana na rindi la uficho wa kuhesabu kura, tofauti za wazi baina ya namba ya kura zilizotangazwa na NEC na Zile za vituoni, na ukweli kuwa NEC haikutaka kusikiliza kabisa malalamiko ya CHADEMA huku ikitoa uzito wa ajabu kwenye malalamiko ya CCM kufikia kusaidia kubadilisha matokeo kama ilivyotokea KIBAHA, KIGOMA, TARIME, SEGEREA, MBOZI, Karatu, na nusura iwe hivyo pia kwa Ubungo na arusha mjini
 
Wana JF;

Katika Uchaguzi Mkuu 2010 Dr. Slaa na CHADEMA wametoa changamoto na upinzani mkali tofauti sana na miaka ya nyuma. Uchaguzi mwaka huu ulikuwa na msisimko mkubwa sana huku kukiwa na propaganda nyingi sana ambazo hazijawahi kusikika.

Kuna baadhi waliamini kabisa kuwa Dr.Slaa na CHADEMA wangeshinda katika Uchaguzi Mkuu 2010.

Kwa maoni yangu baadhi ya sababu zilizoifanya CHADEMA na Dr. Slaa washindwe ni pamoja na:

1. Kutokuwa na Mtandao mkubwa wa chama na wanachama na hivyo kukosa kuwafikia wapiga kura wa uhakika.
2. Maandalizi duni ya ki-organaizesheni katika kampeni
3. Ukosefu wa rasilimali za kutosha katika kampeni hasa fedha

Je kwa maoni na utafiti wako ni sababu gani zingine zilizofanya Dr.Slaa na CHADEMA wasishinde Uchaguzi Mkuu 2010?

Kwa mawazo yangu, nadhani mbinu ya kutisha watu imetumiwa kwenye chaguzi nyingi, mfano US wakati wa Bush watu walitishwa kuhusu kuvamiwa na magaidi kama hawatamchagua Bush etc. Cha msingi ni chama kinachotuhumiwa kucounter attach, nadhani machinery ya Chadema kwenye kampeni kupangua hoja haikuwa kali sana. CCM walijitahidi na mpuuzi wao kampeni Manager.

Nadhani pia Chadema kukosa VP (Mgombea mwenza) makini na mshambuliaji imechangia

Lakini lingine kubwa ni kukosa resources. Kama mtakumbuka Obama alimu outspent McCain kwenye election ads kwa mara tatu or so, na ililipa. CCM wamewaoutspent Chadema zaidi mara kumi etc.Chadema walikosa uwezo huo, especially kurudi sehemu ambayo wagombea wengine walimwaga sumu kwenda kuclear air. Ona jinsi alivyovuna Mbeya na Mwanza, kwani alirudi kuclear air, JK alifanya hivyo lakini it was too late Mwanza, Mbeya Silaa alifunga kampeni, akavuna sana.

CCM ilimtumia Mama Kikweche kusambaza fedha na kanga kwa kina mama. Chadema haikuwa na mkakati mzuri wa kuwapitia wapiga kura wakina mama- (simaanishi kuwapa rushwa noo), hata kwenye mikutano ya Slaa waliokuwa wanaonekana kwa wingi ni vijana na wana ume

Lakini kubwa ni idadi ya waliopiga kura, nadhani hiyo asilimia 42 si kweli, na si ajabu kura za wapinzani zilienguliwa na ili kuoanisha mahesabu, wanasema turnout ilikuwa ndogo. This time kulikuwa na stake kubwa kwenye huu uchaguzi, watu wengi walihamasika, ccm base na chadema base walikuwa fired up, so independets voters, kuliko mwaka 2005. 1995 watu walikuwa fired up but wengi walikuwa hawajajiandikisha kwani ujio wa Mrema ulikuja late.

Na la mwisho ni ile dhana potofu ambayo bado ipo kwenye akili za Watanzania kuwa mpinzani hawezi kushinda kiti cha uraisi. Kuna hilo jeraha alilotuachia Nyerere kuwa upinzani wa kweli utatoka ccm. That is very true, Slaa ni zao la CCM, alitoka CCM kwa kuwa alishindwa, Shibuda etc. Watanzania wenye kupenda vyama vya siasa wote walikuwa CCM, kabla ya mfumo wa vyama vingi, So tayari wameshameguka, sasa sijui Wtz wanangoja imeguke block kubwa ndio iishinde ccm.
 
Back
Top Bottom