Posho za wabunge: Wamiliki hoteli Dodoma wamkana Makinda

EMT

Platinum Member
Jan 13, 2010
14,483
15,308
Chama cha Wamiliki wa Hoteli na Nyumba za Kulala Wageni mkoani Dodoma, kimekanusha madai ya kupanda kwa gharama za huduma za malazi zilizoongeza gharama za maisha kwa wabunge kama ilivyotangazwa na Spika wa Bunge, Anne Makinda. Mwishoni mwa mwaka jana, Makinda alitangaza kuwa posho za wabunge zimeongezwa kutoka Sh 70,000 mpaka Sh 200,000 kwa siku, kutokana na kupanda kwa gharama za maisha, kwa wawakilishi hao wawapo katika vikao vya Bunge. Alisema sehemu ya gharama hizo ni pamoja na malazi, kwa kuwa baadhi ya nyumba zilizokuwa zimekodiwa na wabunge wa Bunge la Tisa, bado wanazimiliki na hivyo kusababisha wabunge wapya kupanga hotelini, ambako gharama ni kubwa.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa chama hicho, Chavuma Taratibu, alisema uchunguzi uliofanywa na chama hicho wiki mbili zilizopita, umebaini kuwa kupanda kwa gharama za maisha mjini Dodoma hakulingani na majiji ya kibiashara ya Mwanza, Arusha, Mbeya, Morogoro na Dar es Salaam. Kwa mujibu wa taratibu, uchunguzi huo umebaini kuwa mkoa wa Dodoma una nyumba za kulala wageni 413 zenye vyumba 3,973 ambavyo gharama zake ni kati ya Sh 5,000 na Sh 45,000 kwa siku, kwa kuzingatia ubora wa vyumba na huduma zilizopo.

“Kwa nyumba za kulala wageni zenye vyumba vinavyounganisha huduma za vyoo na bafu, gharama yake ni kati ya Sh 10,000 na Sh 20,000 kwa kuzingatia ubora wa vyumba,’’ alisema Taratibu. Alisema mbali na vyumba hivyo, pia vipo vingine maalumu vyenye hadhi ya juu ambavyo kwa siku ni kati ya Sh 80,000 na Sh 150,000 lakini vyumba hivyo Dodoma viko 25 tu. Alisema wanafahamu kuwa hakuna mbunge anayeweza kupanga vyumba hivyo maalumu vyenye hadhi ambavyo pia vinatofautiana bei kulingana na umaarufu wa hoteli na ubora wa vyumba vya kulala wageni vilivyopo katika hoteli husika.

‘’Kwa tamko hili, tunapenda kufuta uvumi wa kisiasa kuhusu kuongezeka maradufu kwa gharama za maisha, hatua hiyo inalenga kuvuruga soko la huduma zetu mkoani hapa kwa kuwaogofya wageni na watalii na hivyo kuathiri biashara hizo na huenda hata mapato ya serikali yakapungua kutokana na kodi inayotoza,” alisema Taratibu.

Alisema kelele za kudai posho haziwezi kuthibitishwa kwa kauli zisizofanyiwa utafiti wa kina, licha ya kuwa hali ya uchumi imeyumba kwa nchi nzima, kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta, kushuka thamani ya sarafu na uzalishaji duni uliosababishwa na tatizo la umeme uliodumu kwa mwaka mzima uliopita. Wamiliki hao wa hoteli wanaungana na vyama vya siasa, asasi za kijamii, viongozi wa dini na baadhi ya wananchi, kupinga nyongeza hiyo ya posho.

Chanzo: HabariLeo
 
Nasubiri kwa hamu vipindi vya Bunge vutakapo anza maana sijui huyo mama atatueleza nini watanzania. sijui litaficha wapi sura yake kama nyani.
 
Mhhhhhhhhh! muda wote huo walikuwa wapi kutoa hayo maelezo?au ndo kusema akili zao zimeamka sasa!
 
BIBI WA JAZBA/PANIC hajawahi kuliongolea suala hilo tangu wampinge, kaamua kuwa silence. ipo siku atasema tu ili azomewe vizuri
 
Mhhhhhhhhh! muda wote huo walikuwa wapi kutoa hayo maelezo?au ndo kusema akili zao zimeamka sasa!

walihitaji kufanya utafiti na kuwa na collective voice, sio kila mtu kulipuka na ksema lote. mambo mazuri hayataki haraka
 
mambo ya bi kidude hayo.
kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake
 
Chama cha Wamiliki wa Hoteli na Nyumba za Kulala Wageni mkoani Dodoma, kimekanusha madai ya kupanda kwa gharama za huduma za malazi zilizoongeza gharama za maisha kwa wabunge kama ilivyotangazwa na Spika wa Bunge, Anne Makinda. Mwishoni mwa mwaka jana, Makinda alitangaza kuwa posho za wabunge zimeongezwa kutoka Sh 70,000 mpaka Sh 200,000 kwa siku, kutokana na kupanda kwa gharama za maisha, kwa wawakilishi hao wawapo katika vikao vya Bunge. Alisema sehemu ya gharama hizo ni pamoja na malazi, kwa kuwa baadhi ya nyumba zilizokuwa zimekodiwa na wabunge wa Bunge la Tisa, bado wanazimiliki na hivyo kusababisha wabunge wapya kupanga hotelini, ambako gharama ni kubwa.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa chama hicho, Chavuma Taratibu, alisema uchunguzi uliofanywa na chama hicho wiki mbili zilizopita, umebaini kuwa kupanda kwa gharama za maisha mjini Dodoma hakulingani na majiji ya kibiashara ya Mwanza, Arusha, Mbeya, Morogoro na Dar es Salaam. Kwa mujibu wa taratibu, uchunguzi huo umebaini kuwa mkoa wa Dodoma una nyumba za kulala wageni 413 zenye vyumba 3,973 ambavyo gharama zake ni kati ya Sh 5,000 na Sh 45,000 kwa siku, kwa kuzingatia ubora wa vyumba na huduma zilizopo.

"Kwa nyumba za kulala wageni zenye vyumba vinavyounganisha huduma za vyoo na bafu, gharama yake ni kati ya Sh 10,000 na Sh 20,000 kwa kuzingatia ubora wa vyumba,'' alisema Taratibu. Alisema mbali na vyumba hivyo, pia vipo vingine maalumu vyenye hadhi ya juu ambavyo kwa siku ni kati ya Sh 80,000 na Sh 150,000 lakini vyumba hivyo Dodoma viko 25 tu. Alisema wanafahamu kuwa hakuna mbunge anayeweza kupanga vyumba hivyo maalumu vyenye hadhi ambavyo pia vinatofautiana bei kulingana na umaarufu wa hoteli na ubora wa vyumba vya kulala wageni vilivyopo katika hoteli husika.

''Kwa tamko hili, tunapenda kufuta uvumi wa kisiasa kuhusu kuongezeka maradufu kwa gharama za maisha, hatua hiyo inalenga kuvuruga soko la huduma zetu mkoani hapa kwa kuwaogofya wageni na watalii na hivyo kuathiri biashara hizo na huenda hata mapato ya serikali yakapungua kutokana na kodi inayotoza," alisema Taratibu.

Alisema kelele za kudai posho haziwezi kuthibitishwa kwa kauli zisizofanyiwa utafiti wa kina, licha ya kuwa hali ya uchumi imeyumba kwa nchi nzima, kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta, kushuka thamani ya sarafu na uzalishaji duni uliosababishwa na tatizo la umeme uliodumu kwa mwaka mzima uliopita. Wamiliki hao wa hoteli wanaungana na vyama vya siasa, asasi za kijamii, viongozi wa dini na baadhi ya wananchi, kupinga nyongeza hiyo ya posho.

Chanzo: HabariLeo

The Citizen wameandika vizuri - kwamba kwa ufahamu wao, hakuna mbunge anayelala chumba kinachozidi Tsh.20,000/=
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Mhhhhhhhhh! muda wote huo walikuwa wapi kutoa hayo maelezo?au ndo kusema akili zao zimeamka sasa!

Watu hawakurupuki kama bi kiroboto wewe, wanafanya kwanza utafiti ili kuhakikisha kuwa watakachokisema ni sahihi.
 
Inakuwaje kiongozi mkubwa wa mhimili kama Bunge anatoa taarifa isiyotafitiwa. Hivi Bunge si lina kitengo cha utafiti na ukusanyaji wa habari na taarifa mbalimbali?
 
Inakuwaje kiongozi mkubwa wa mhimili kama Bunge anatoa taarifa isiyotafitiwa. Hivi Bunge si lina kitengo cha utafiti na ukusanyaji wa habari na taarifa mbalimbali?

Kukusanya habari na taarifa gani?
 
Kama makinda akiwa amekalia kiti cha spika naongea vitu ambavyo haviko kwenye kanuni hadi anasomewa kanuni na makamanda wa CDM, mnashangaa nini akilopoka uongo akiwa mtaani?
 
Laiti ingewezekana hayo mahoteli kuweka rate maalum kwa Wabunge wapenda posho (shilingi 140 000 kwa chumba kwa siku) ningefurahi sana!
 
Chama cha Wamiliki wa Hoteli na Nyumba za Kulala Wageni mkoani Dodoma, kimekanusha madai ya kupanda kwa gharama za huduma za malazi zilizoongeza gharama za maisha kwa wabunge kama ilivyotangazwa na Spika wa Bunge, Anne Makinda. Mwishoni mwa mwaka jana, Makinda alitangaza kuwa posho za wabunge zimeongezwa kutoka Sh 70,000 mpaka Sh 200,000 kwa siku, kutokana na kupanda kwa gharama za maisha, kwa wawakilishi hao wawapo katika vikao vya Bunge. Alisema sehemu ya gharama hizo ni pamoja na malazi, kwa kuwa baadhi ya nyumba zilizokuwa zimekodiwa na wabunge wa Bunge la Tisa, bado wanazimiliki na hivyo kusababisha wabunge wapya kupanga hotelini, ambako gharama ni kubwa.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa chama hicho, Chavuma Taratibu, alisema uchunguzi uliofanywa na chama hicho wiki mbili zilizopita, umebaini kuwa kupanda kwa gharama za maisha mjini Dodoma hakulingani na majiji ya kibiashara ya Mwanza, Arusha, Mbeya, Morogoro na Dar es Salaam. Kwa mujibu wa taratibu, uchunguzi huo umebaini kuwa mkoa wa Dodoma una nyumba za kulala wageni 413 zenye vyumba 3,973 ambavyo gharama zake ni kati ya Sh 5,000 na Sh 45,000 kwa siku, kwa kuzingatia ubora wa vyumba na huduma zilizopo.

"Kwa nyumba za kulala wageni zenye vyumba vinavyounganisha huduma za vyoo na bafu, gharama yake ni kati ya Sh 10,000 na Sh 20,000 kwa kuzingatia ubora wa vyumba,'' alisema Taratibu. Alisema mbali na vyumba hivyo, pia vipo vingine maalumu vyenye hadhi ya juu ambavyo kwa siku ni kati ya Sh 80,000 na Sh 150,000 lakini vyumba hivyo Dodoma viko 25 tu. Alisema wanafahamu kuwa hakuna mbunge anayeweza kupanga vyumba hivyo maalumu vyenye hadhi ambavyo pia vinatofautiana bei kulingana na umaarufu wa hoteli na ubora wa vyumba vya kulala wageni vilivyopo katika hoteli husika.

''Kwa tamko hili, tunapenda kufuta uvumi wa kisiasa kuhusu kuongezeka maradufu kwa gharama za maisha, hatua hiyo inalenga kuvuruga soko la huduma zetu mkoani hapa kwa kuwaogofya wageni na watalii na hivyo kuathiri biashara hizo na huenda hata mapato ya serikali yakapungua kutokana na kodi inayotoza," alisema Taratibu.

Alisema kelele za kudai posho haziwezi kuthibitishwa kwa kauli zisizofanyiwa utafiti wa kina, licha ya kuwa hali ya uchumi imeyumba kwa nchi nzima, kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta, kushuka thamani ya sarafu na uzalishaji duni uliosababishwa na tatizo la umeme uliodumu kwa mwaka mzima uliopita. Wamiliki hao wa hoteli wanaungana na vyama vya siasa, asasi za kijamii, viongozi wa dini na baadhi ya wananchi, kupinga nyongeza hiyo ya posho.

Chanzo: HabariLeo

Duh, Kweli hawa ni wenye nyumba!

Alafu hawa wabunge na Mawaziri si wamenunua nyumba za srekali, nssf, ppf zote si zao?
pia wengi wamepanga mtaani ambapo wanalipa kodi kati ya 300,000 na 500,000 kwa mwezi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom