Porokwa kupambana na Lowassa

Msharika

JF-Expert Member
May 15, 2009
947
69
MWENYEKITI wa zamani wa Jumuiya ya Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Arusha, Daniel Porokwa (37), ametangaza rasmi nia yake ya kuwania ubunge wa Jimbo la Monduli kupitia chama hicho katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika baadaye mwaka huu.

Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa ni Mbunge wa jimbo hilo tangu mwaka 1995.

Porokwa ametangaza nia hiyo jana nyumbani kwao katika Kijiji cha Monduli Juu.

Viongozi wa kimila wa jamii ya Wamasai (Laigwanan) zaidi ya 30 kutoka wilaya za Monduli na Simanjiro walimuombea dua.

“Ndugu zangu napenda kuwaarifu kuwa natarajia kuwania nafasi ya ubunge wa jimbo la Monduli kupitia chama changu cha CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu utakaofanyika baadaye mwezi Oktoba…kwa hiyo nawaomba wana Monduli na wenye nia njema na jimbo letu kuniunga mkono,” amesema Porokwa.

Amesema, lengo la kujitosa kuwania nafasi hiyo ni kuleta changamoto katika nafasi ya uongozi na kumpokea Mbunge wa sasa ambaye kwa kiasi kikubwa amesukuma mbele maendeleo ya jimbo hilo.

“Napenda kuchukua fursa hii kumpongeza mheshimiwa Lowassa amefanya kazi kubwa sana kupigania maendeleo ya jimbo letu…lakini kwa kuwa katika Taifa letu tumejenga utamaduni wa kupokezana uongozi, basi nafikiri ni muda muafaka sasa kumpokea na kumsaidia mheshimiwa Lowassa,” amesema Porokwa.

Amesema, muda wa kampeni uliopangwa na chama ukiwadia, atatangaza kaulimbiu yake atakayotumia katika kampeni zake na wanachama wa CCM watatumia nafasi yao kidemokrasia kuwapigia kura wagombea watakaokuwa wamejitokeza kuwania nafasi hiyo.

Porokwa alikuwa Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha kati ya mwaka 2003 hadi 2008, alimaliza muda wake na nafasi yake kuchukuliwa na Mwenyekiti wa sasa, James ole Millya.

Porokwa ni mwana CCM wa kwanza kutangaza nia ya kuwania ubunge katika jimbo hilo, wengi wanatarajia kuwa Lowassa atagombea tena.
 
Hata mimi ningeshauri EL asigombee, ajipumzikie kama ma ex pm wenzake kina Msuya, Sumaye, Warioba na Dr.Salim.

Ni kweli Monduli, CCM imetimiza ilani yake kwa asilimia 100 na EL kafanya mengi. Wazee wakimasai walishaamua kumuengua EL baada ya kupata siri kuwa kumbe jamaa sio Mmasai ni Mmeru aliyepose kama Masai.

Ile kesi ya Ole Sendeka na Ole-Milya ni battle ground ya EL na Porokwa. Mangi anamwaga fungu kwa Sendeka waing'oe ngome ya EL, huku RA akimwaga kwa Milya EL abaki. Monduli ni kipindi cha mavuno, maana vita vya mafahari huku wakimwaga fedha, nyika haziumii bali zinaneemeka.
 
Hata mimi ningeshauri EL asigombee, ajipumzikie kama ma ex pm wenzake kina Msuya, Sumaye, Warioba na Dr.Salim.

Ni kweli Monduli, CCM imetimiza ilani yake kwa asilimia 100 na EL kafanya mengi. Wazee wakimasai walishaamua kumuengua EL baada ya kupata siri kuwa kumbe jamaa sio Mmasai ni Mmeru aliyepose kama Masai.

Ile kesi ya Ole Sendeka na Ole-Milya ni battle ground ya EL na Porokwa. Mangi anamwaga fungu kwa Sendeka waing'oe ngome ya EL, huku RA akimwaga kwa Milya EL abaki. Monduli ni kipindi cha mavuno, maana vita vya mafahari huku wakimwaga fedha, nyika haziumii bali zinaneemeka.

Mwanzoni nilikuwa sielewi....Asante sana mkuu kwa hili,
 
Kila mtu ana haki ya kugombea uogozi na pia kila mtanzania anayo haki hivyo kuna haja ya watanzania kuacha kama wanaona amechoka na kutompa kura
 
Hata mimi ningeshauri EL asigombee, ajipumzikie kama ma ex pm wenzake kina Msuya, Sumaye, Warioba na Dr.Salim.

Ni kweli Monduli, CCM imetimiza ilani yake kwa asilimia 100 na EL kafanya mengi. Wazee wakimasai walishaamua kumuengua EL baada ya kupata siri kuwa kumbe jamaa sio Mmasai ni Mmeru aliyepose kama Masai.

Ile kesi ya Ole Sendeka na Ole-Milya ni battle ground ya EL na Porokwa. Mangi anamwaga fungu kwa Sendeka waing'oe ngome ya EL, huku RA akimwaga kwa Milya EL abaki. Monduli ni kipindi cha mavuno, maana vita vya mafahari huku wakimwaga fedha, nyika haziumii bali zinaneemeka.
Monduli labda Lowassa aamue kuacha kugombea mwenyewe. Lowassa na wafuasi wengi sana vijana na akina mama na hao ndiyo wapiga kura. Wazee mara nyingi mvua ikinyesha hawaendi na hata jua likiwa kali mno hawaendi. Ili kuwa mmasai siyo lazima kuzaliwa umasaini, siyo lazima uwe na baba mmasai au mama mmasai bali hata kama wewe ni mzungu na umekabili kufuata mila na desturi za kimasai utapewa heshima zote za kimasai na hautabaghuliwa kwa vyovyote vile. Ukiangalia Monduli wengi wa wakazi wake wamehamia na wengi wana orijin ya Meru, Rombo, Machame, na Kibosho na hata majina yao kwa kiasi fulani yanalandana. Kama EL akiamua kung'atuka ni vizuri zaidi kwake lakini nadhani hii itakuwa mapema sana kuisemea!!!
 
Hata mimi ningeshauri EL asigombee, ajipumzikie kama ma ex pm wenzake kina Msuya, Sumaye, Warioba na Dr.Salim.

Ni kweli Monduli, CCM imetimiza ilani yake kwa asilimia 100 na EL kafanya mengi. Wazee wakimasai walishaamua kumuengua EL baada ya kupata siri kuwa kumbe jamaa sio Mmasai ni Mmeru aliyepose kama Masai.

Ile kesi ya Ole Sendeka na Ole-Milya ni battle ground ya EL na Porokwa. Mangi anamwaga fungu kwa Sendeka waing'oe ngome ya EL, huku RA akimwaga kwa Milya EL abaki. Monduli ni kipindi cha mavuno, maana vita vya mafahari huku wakimwaga fedha, nyika haziumii bali zinaneemeka.

Heshima kwako Pasco,

Ni vigumu sana Bwana Lowassa kuachia ngazi hasa tukizingatia kwamba bado ana hamu ya kutaka kukamata madaraka makubwa ya kisiasa[urais].Ubunge,UNEC na CC ni nafasi nzuri zitakazo mwezesha kutimiza ndoto zake.Bwana Lowassa anajua kuachia ubunge ni hatari sana kwake kisiasa kurejea kileleni.

Bwana Parokwa anaungwa mkono na wamasai wengi ambao wanadhani Lowassa hastahili kuwa mwakilishi wao kwasababu asili yake ni Meru.Bwana Lowassa amekuwa akifanya juhudi kubwa tangu zamani kuhakikisha hakuna mmsai mwenye nguvu anachomoza kwenye anga za siasa Arusha.Walijaribu kina Lekule Laiser na Elisa Mollel kugombea uenyekiti wa mkoa na ujumbe wa halmashauri kuu ya taifa waliishia kuzushiwa kesi na kuondolewa katika kugombea nafasi hizo.kilichofuatia ni Bwana Lowassa kumweka Bwana
Onesmo Nangole kugombea uenyekiti na mmeru mwenzake Bwana Kaaya nafasi ya NEC.

Kuna wakati wananchi wa Monduli walitaka mtoto wa marehemu E Sokoine agombee lakini aliishia kupelekwa ubalozini,Bwana Lowassa ni mjanja sana kiasi kwamba mara nyingi karata zake anazicheza vyema.

Parokwa anaweza kumsumbua sana Lowassa ikiwa anapata sapoti ya Mzee Mengi,ikumbukwe Lowassa mara zote anahakikisha hapati mpinzani kwenye jimbo lake hii itakakuwa mtihana mkubwa sana ikiwa Parokwa ataendelea na msimamo wa kugombea ubunge Monduli.
 
Hata mimi ningeshauri EL asigombee, ajipumzikie kama ma ex pm wenzake kina Msuya, Sumaye, Warioba na Dr.Salim.

Ni kweli Monduli, CCM imetimiza ilani yake kwa asilimia 100 na EL kafanya mengi. Wazee wakimasai walishaamua kumuengua EL baada ya kupata siri kuwa kumbe jamaa sio Mmasai ni Mmeru aliyepose kama Masai.

Ile kesi ya Ole Sendeka na Ole-Milya ni battle ground ya EL na Porokwa. Mangi anamwaga fungu kwa Sendeka waing'oe ngome ya EL, huku RA akimwaga kwa Milya EL abaki. Monduli ni kipindi cha mavuno, maana vita vya mafahari huku wakimwaga fedha, nyika haziumii bali zinaneemeka.


Mzee Pasco, tunakuamini sana kwa michango yako humu. Lakini hii ya 100 % nina mashaka nayo mkuu!!!
 
Sidhani kama atamuweza.Lowassa ndio amesha safishwa.

Porokwa anaweza kumuangusha Lowassa kwasababu wamasai kwa utamaduni wao sio Mafisadi, ni watu wachapa kazi na wanajiheshimu, kuiba mali za watu wengine sio utamaduni wao; Sekoine kabla ya EL alikuwa kiongozi muadilifu lakini sasa EL amethibitika kuwa ni fisadi na mwizi kwahiyo wamasai hawapendezeshwi na sifa hizo na ndio maana hata hoja za kuwa EL sio mmasai zinapata nguvu!! Kwa mtaji huu Porokwa anaweza kuua tembo kwa ubua!!
 
Porokwa anaweza kumuangusha Lowassa kwasababu wamasai kwa utamaduni wao sio Mafisadi, ni watu wachapa kazi na wanajiheshimu, kuiba mali za watu wengine sio utamaduni wao; Sekoine kabla ya EL alikuwa kiongozi muadilifu lakini sasa EL amethibitika kuwa ni fisadi na mwizi kwahiyo wamasai hawapendezeshwi na sifa hizo na ndio maana hata hoja za kuwa EL sio mmasai zinapata nguvu!! Kwa mtaji huu Porokwa anaweza kuua tembo kwa ubua!!

Sishawishiki kuwa wamasai huko vijijini wanajua kama kuna kitu kama hicho.
 
Sishawishiki kuwa wamasai huko vijijini wanajua kama kuna kitu kama hicho.


Hiyo ndio itakuwa kazi ya Porokwa kuwaelimisha juu ya ufisadi wa EL; na kazi hii nadhani amekwishaianza na ndio maana hao wazee wa kimasai wamempa baraka zao!! Kazi ipo wajameni.
 
Ni vizuri wakati mwingine kukumbuka historia na kutambua nafasi za watu hasa kwenye uongozi wa kijamii na tusiishie kupiga kelele na kuwa wapayukaji kwenye jukwaa hili muhimu. Kwa watu wa Monduli na jamii ya wamasai Mhe Lowassa ni mtu wa muhimu kwao hata kama watanzania wote hawatomtambua,uthibitisho wa hilo ni kwa kumpatia cheo cha Uleiguanan na tena kumchagua kuwa mkuu wa "luiguanans" in East Africa,pili utekelezaji wake wa ilani ambao hata Porokwa anaukubali. Upande wa Porokwa,alipewa nafasi ya kuongoza Umoja wa vijana Arusha wa CCM kama Mwenyekiti kwa muda wa miaka mitano hakuna lolote alilofanya zaidi ya kuruhusu katibu wake ndugu Mfaume Kizigo kujiuzia nyumba ya umoja wa vijana,huu nao ni ufisadi wa hali ya juu. Pengine angeulizwa alishindwa kusimamia kanuni ya umoja wa vijana leo hii anataka kusimamia Ilani ya chama,Katiba ya chama na Katiba ya Nchi kama Mbunge ataweza kweli? Kama kweli wana Monduli wamemchoka Mhe Lowassa nadhani wanahitaji kiongozi makini zaidi ya Porokwa.
 
Porokwa hafai wala hataweza kumng'oa Edward. Yeye mwenyewe akiwa mwalimu wa shule anazo kashfa za udokozi wa mapesa. Na yeye anajua hamwezi. Kwa sababu ni mtu anayependa pesa bila shaka anataka kumtikisa Edward ili anunuliwe na amwachie. Na hilo ndilo atakalofanya. EL is very powerful. Hate him or Love him. Lowasa is there to stay na mwaka 2015 atarudi kama Rais a la Jacob Zuma.
 
Porokwa hafai wala hataweza kumng'oa Edward. Yeye mwenyewe akiwa mwalimu wa shule anazo kashfa za udokozi wa mapesa. Na yeye anajua hamwezi. Kwa sababu ni mtu anayependa pesa bila shaka anataka kumtikisa Edward ili anunuliwe na amwachie. Na hilo ndilo atakalofanya. EL is very powerful. Hate him or Love him. Lowasa is there to stay na mwaka 2015 atarudi kama Rais a la Jacob Zuma.



mmhh! watu bwana...yaani jamaa awe Rais!! Mchonga atafufuka walahi.....mimi simooooo....
 
Huyo pokorokwa anataka siasa ya kupokezana?

wanapokezana kitu gani?

yaani kama ana sababu ya kipuuzi ya namna hii basi hafai coz hataki kusema ukweli;

Bora angesema ana lengo la kuwaondoa wale wote wenye kashfa ya ufisadi
 
Hata mimi ningeshauri EL asigombee, ajipumzikie kama ma ex pm wenzake kina Msuya, Sumaye, Warioba na Dr.Salim.

Ni kweli Monduli, CCM imetimiza ilani yake kwa asilimia 100 na EL kafanya mengi. Wazee wakimasai walishaamua kumuengua EL baada ya kupata siri kuwa kumbe jamaa sio Mmasai ni Mmeru aliyepose kama Masai.

Ile kesi ya Ole Sendeka na Ole-Milya ni battle ground ya EL na Porokwa. Mangi anamwaga fungu kwa Sendeka waing'oe ngome ya EL, huku RA akimwaga kwa Milya EL abaki. Monduli ni kipindi cha mavuno, maana vita vya mafahari huku wakimwaga fedha, nyika haziumii bali zinaneemeka.

Porokwa anapoteza muda wake tu ni bora angefanya kitu kingine..anajua hashindi
 
Ni nzuri ila aangalie utasikia mara kapata ajali barabarani Mwache ashindane na huyo fisadi!
 
Porokwa anapoteza muda wake tu ni bora angefanya kitu kingine..anajua hashindi


Kugombea au kutogombea ni haki ya msingi na uamuzi wa kila mtu apendaye, msikatishe watu tamaa, wanajua wanachokifanya mpaka kutangaza nia zao....swala la atashinda au la ni wantanzania au wanamonduli ndio wenye majibu . After all hakuna hata mtu mmoja ambaye mwenye kujua dhahiri kama atashinda au la lakini pamoja na hayo wanaendelea kugombea na wataendelea kugombea tena sana tu .
 
Porokwa anaweza kumuangusha Lowassa kwasababu wamasai kwa utamaduni wao sio Mafisadi, ni watu wachapa kazi na wanajiheshimu, kuiba mali za watu wengine sio utamaduni wao; Sekoine kabla ya EL alikuwa kiongozi muadilifu lakini sasa EL amethibitika kuwa ni fisadi na mwizi kwahiyo wamasai hawapendezeshwi na sifa hizo na ndio maana hata hoja za kuwa EL sio mmasai zinapata nguvu!! Kwa mtaji huu Porokwa anaweza kuua tembo kwa ubua!!

andika hii meseji kwenye diary yako siku kura za maoni zinatangazwa ntaku PM mkuu.Porokwa nina uhakika atapatta namba za kiatu katika kura za maoni...EL hamuwezi hamuwezi hata afanyeje
 
Back
Top Bottom